UONGOZI WA   Chuo cha Biblia cha Elam Christian Harvest
Seminary (ECHASE)   unayofuraha kuwatangazia  Watendakazi na Viongozi wa Kanisa Nafasi za
kujitolea kufundisha  katika chuo hiki.Tunaamini
kuwa  Wako watumishi wa Mungu  nchini wenye  elimu ya Huduma   na Theolojia wanaoweza kufundisha watumishi
wengine.
Elam Christian Harvest
Seminary ni Taasisi ya Kikristo  inayofanya kazi na madhehebu yote katika
kuwaanda watendakazi na Viongozi wa Kanisa 
kwaajili ya Mavuno ya nyakati za mwisho.
Tunaamini kuwa
Watendakazi wanapaswa kuandaliwa katika uwanja wa Mavuno, kama alivyofanya
Bwana wetu Yesu Kristo katika kuwaandaa wanafunzi wake kwaajili ya kazi ya
Mavuno 
Tunakusudia kuwaandaa
watendakzi na viongozi wa Kanisa wengi wenye kujaa maarifa ya Neno la Mungu na
Upako wa Roho Mtakatifu kwaajili ya kuingia katika  Mavuno ya Kiroho ili kuondoa changamoto ya
uhaba wa watendakazi  kama alivyosema
Bwana Wetu Yesu Kristo kwamba “Mavuno ni Mengi lakini Watendakazi ni Wachache
(Luka 10:2)
Tunakusudia kuanzisha  Vituo vya mafunzo katika  Maeneo mbalimbali katika mikoa na wilaya  Nchini Tanzania. Vituo hivyo vitaendesha
Mafunzo ya wiki  moja hadi wiki  mbili kwa  
mwezi. Hivyo tunahitaji kuwa na Wakufunzi wengi  ili kuweza kutimiza mkakati huu.
Biblia inasema  katika 2Timotheo 2:2
  Na
mambo yale uliyoyasikia kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu
waaminifu watakaofaa kuwafundisha na wengine
Tunatoa  ombi  la kujitolea kufundisha   katika vituo 
hivi  vitakavyoanzishwa   katika Maeneo mbalimbali nchini.
SIFA ZINAZOTAKIWA.
           Mwombaji anatakiwa kuwa na sifa  zifuatazo:-
1.     Awe
amezaliwa mara ya pili (awe ameokoka)
2.     Awe
na Huduma mojawapo ya zile huduma tano za Uongozi (Mtume,Nabii,Minjilisti,
mchungaji au mwalimu)
3.      Mhitimu wa Chuo cha Biblia  katika fani ya Theolojia, Huduma  au uongozi wa Kiroho ngazi ya   Shahada, Stashahada ya Uzamili au Shahada ya
Uzamili.
4.     Awe
Mshiriki  katika kanisa  la Mahali  Pamoja (a member of a local Church).
5.     Awe
anajua kuongea na kuandika vizuri Kiswahili au Kiingereza.
Jinsi
ya Kutuma Maombi
Mtumishi yeyote
aliyetayari  kujitolea kufundisha
katika  Seminari  hii awasiliane na   uongozi
wa Seminari  kwa simu namba 0762532121/0765992774
au kwa barua pepe elamseminary@gmail.com
Mwisho wa kupokea
maombi ni tarehe 25/
Tangazo hili limetolewa
na
Rev.Dr. Erick L Mponzi
MKURUGENZI
MKUU
