Saturday 10 January 2015

MWONGOZO WA KOZI. PITIO LA AGANO LA KALE II



CHUO CHA MAFUNZO YA HUDUMA PHILADELPHIA
KLPT PARISHI YA IWALA.
Kuwatarisha watendakazi kwaajili ya mavuno ya nyakati za mwisho.
KIHUNZI CHA KOZI.
SEMISTA YA PILI 2015

JINA LA KOZI : Pitio La Agano La Kale Ii.
UKUBWA WA KOZI: Krediti 3
MHADHIRI: Erick Mponzi


Kozi hii inatalii Agano la kale kwa kuanzia vitabu vya historia hadi vitabu vya manabii. Ni mwendelezo wa kozi iliyopita yaani Pitio la Agano la kale I. Kozi hii inachunguza kwa muhtasari tu mambo mbalimbali yanayopatikana katika Agano la kale kama vile Mwandishi wa kitabu, kusudi, muundo, mafundisho muhimu, watu muhimu,mitajo ya Kristo .n.k

II.              MALENGO YA KOZI.
Kozi hii inalenga kumpa mwanafunzi mtazamo wa jumla wa Agano la Kale ili awe na uwezo wa kujenga theologia ya Biblia. Baada ya kusoma kozi mwanafunzi anatakiwa awe na uwezo wa kutaja mwandish wa kila kitabu, kusudi la kitabu, mafundisho muhimu ya kitabu, watu muhimu, tarehe ya kitabu. Pia aweze kueleza uhusiano uliopo baina ya vitabu vilivyo katika fungu moja na aweze kuainisha viongozi na watumishi mbalimbali ambao Mungu aliwaita  na kuwaweka katika utumishi nyakati za Agano la kale na jinsi walivyoitikia na kuutumikia wito wao na namna anavyoweza kufaidika katika utumishi wake kutokana na kujifunza mafanikio na changamoto walizokutana nazo na jinsi walivyokabiliana nazo .


III.            MAUDHUI YA  ZA KOZI
Moduli Ya Kwanza: UTANGULIZI.
·       Maandalizi ya kujifunza Neno la Mungu.
·       1.Nani ?  2. Nini?,  3.Lini?   4.  Wapi?  5. Kwanini? 6. Namna gani   7.Ninajihusishaje?
Moduli ya pili:  VITABU VYA HISTORIA
Yoshua hadi Esta.
·       Dhana ya historia.
·       Dhana ya vitabu vya historia.
·       Umuhimu wa vitabu vya historia
·       Uhusiano wa vitabu vya historia na makundi mengine kama Pentatuki,Maandiko na manabii.
·       Mwandishi wa kitabu
·       Asili ya Jina la kitabu
·       Tarehe ya kuandikwa
·       Muundo wa kitabu
·       Mafundisho muhimu
·       Watu muhimu
·       Mitajo ya Kristo
Moduli ya tatu:  VITABU VYA MAANDIKO/HEKIMA
 Ayubu Hadi Wimbo uliobora.
·       Mwandishi wa kitabu
·       Asili ya Jina la kitabu
·       Tarehe ya kuandikwa
·       Muundo wa kitabu
·       Mafundisho muhimu
·       Watu muhimu
·       Mitajo ya Kristo

Moduli ya nne: VITABU VYA MANABI
Manabii wakubwa.
Isaya hadi Danieli.
·       Mwandishi wa kitabu
·       Asili ya Jina la kitabu
·       Tarehe ya kuandikwa
·       Muundo wa kitabu
·       Mafundisho muhimu
·       Watu muhimu.
·       Mitajo ya Kristo
Manabii wadogo.
Hosea hadi Malaki.
·       Mwandishi wa kitabu
·       Asili ya jina la kitabu
·       Tarehe ya kuandikwa
·       Muundo wa kitabu
·       Mafundisho muhimu
·       Watu muhimu
·       Mitajo ya Kristo

IV.            MFUMO WA UFUNDISHAJI
Kozi hii itafundishwa kwa kutumia njia na mbinu mbalimbali ili kuweza ufanisi wa mwanafunzi kuelewa zaidi. Kozi itafundishwa  kwa mbinu zifuatazo.
·       Mhadhara
·       Majadiliano na
·       Uwasilishaji
V.              TATHMINI NA UPIMAJI.
·       Jaribio  alama 20
·       Mahudurio alam 5
·       Uwasilishaji  alama 5
·       Mtihani alama 70
·       Jumla ya alama 100


BIBLIOGRAFIA TEULE
Crowhurst, E(3ed)(1998).Old Testament survey 3: Hillcrest 3650, South Africa
Mock,J.D.9(1990) Uchunguzi wa agano la Kale:Chuo cha Biblia kwa wachungaji na viongozi wa KanisaAtlanta GA.
Self,  J .L.(-)Old tesatemnt Survey:Notes on theMessage and Meaning of
Old Testament Literature
Smith,G. ISOM TRIMESTER B: International School ofministry. USA.
Tanzania Assemblies of God,(2011).Mapitio ya Biblia I (BIB1063): Idara ya elimu
VanBuskirk, T.E.(2002-2007).Old Testament Survey. Taylorsville, UT 84118.
Htpp: www.villageministries.com. (2001). Misingi inayojenga katika imani.




.