Saturday 10 January 2015

UCHUNGUZI WA AGANO LA KALE .II



MADA YA KWANZA. UTANGULIZI
I.                MAANDALIZI YA KUJIFUNZA NENO LA  MUNGU.
Kuna maswali kadhaa  ambayo  yanaweza kutusaidia katika kujifunza Neno la Mungu. Maswali haya ni moja ya mbinu muhimu ya kujifunza Biblia.  Mbinu hii ikifuatwa itakusaidia katika kuielewa Biblia na kuihusisha na maisha yako ya kila siku. Maswali hayo ni:

1.     Nani ? 
 Sawli hili ilnamtaka msomaji kutambua au kujua nani anazungumza katika andiko                                  alisomalo na nani anaambiwa katika andiko hilo.
Mfano katika Mwanzo 22:2 Mungu ndiye msemaji a Ibrwahimnu ndiye anaeambiwa.                                                                                                                   

2.     Nini ?
Swali hili linahusu msomaji kutambua  mada inayoongelewa katika  andiko husika analosoma
 Ni muhimu sana unaposoma andiko ujue mada inayoongolewa na andiko hilo. Hivyo kwa kujiuliza swali hili wweza kuja mada inayoongelewa  katika andiko husika.  Andiko hili linasema nini?
Mfano Yohana 3:16,  Luka 10:2 Yohana 4:35, Yohana 1:29.

3.     Lini ? 
Swali hili linalenga kumfanya msomaji kutambua wakati andiko lilipoandikwa na wakati wa utekelezaji wa andiko hilo. Kutambua wakati ujmbe huo ulipotolewa. Kutambua wakati uliohusika ni muhimu sana kwani kuna mambo kadha kaika vipindi fulani yaliruhusiwa lakani baadae Mungu aliyakataaa.
Kabla ya sheria kutolewa Sinai Haikuwa dhambi kuoa ndugu wa karibu, lakini sheria ilipotolewa jambo hili lilikatazwa kabisa. Kutokana na dhana ya wakati ndoa ya Ibrahimu na Sara ilikuwa halali kwani ilikuwa kabla ya kutolewa sheria.  Warumi 4:15. Matendo ya Mitume 17: 37
4.     Wapi ?
Swali hili linalenga kumfanya msomaji atambue mazingira na utamaduni   wa mahali husika andiko lilipotolewa.Kutambua eneo husika na utamaduni kutamfanya msomji kutambua namna andiko lilivyohusika na watu wailoandikiwa na namna linavyoweza kusika na watu wa nyakati hizi zetu.
5.     Kwanini?
Swali hili linalenga kumfanya msomaji atambue sababu ya andiko hilo kutolewa kwa watu walioandikiwa kwanza kabla ya kulihusisha na maisha yake binafsi.  Kwanini andiko hili linasema hiki linachosema. Kwa sababu gani andiko hili liasema hivi ?
Mfano tzama bikira atachunua mimba na kuzaa motto mwanamme nae atamwita jina lake Imanueli . Isaya 7:114
Kwanini ilikuwa ni lazima Yesu kuzaliwa na bikira ?
Warumi 5 inajibu swali hili.
6.     Kwa namna gani ? au kwa jinsi gani?
Swali hili linalenga kumfanya msomaji kutambua mbinu au njia zilizotumika katika kutekeleza kile andiko liachosema
Mfano  Yesu kutembea juu ya maji.
Kivuli cha Petro kuponya wagonjwa na leso za Paulo kuponya wagonjwa.

7.     Ninajihusishaje ?
Swali hili ni la kimatumizi zaidi. Fundhisho hili linahusikaje katika maisha yangu. Namna gani naweza kulifanyia kazi mimi binafsi?.
Kumbuka kwamba Mungu huzungumza na mtu binafsi.
·       Waweza kulihusisha Neno na Mungu unalosoma kwa kujiuliza maswali yafuatayo.
·       Tukokana na Andiko hili kuna dhambi ninayotakiwa kutubu na kuiacha ?
·       Je uhusiano wangu na mungu, wamini wzangu na watu wengine ukoje?
·       Kuna ahadi ninazoweza kuzidai kwa Mungu?
·       Kuna jamboi ninalowea kumshukuru Mungu kwalo ?
·       Weka katika matendo Kile ulichojifunza  katika  Neno la Mungu.
Kumbuka kujifunza bila kuyaishi yale unayojifuna haina maana na nikupoteza muda.
Yakobo 1:22 Lakini iweni watendaji wa neno wala siwasikiaji tu hali kijidanganya nafsi zenu.
MADA YA PILI. UTAFITI WA VITABU VYA HISTORIA.
Maana ya Historia
Historia ni  taaluma/elimu inayohhusu rekodi ya matukio yaliyotokea katika vipindi mbalimbali.
Ni Elimu ya matukio yaliyopita, yaliyopo na yajayo.
Maana ya vitabu vya Historia
Ni vitabu vinavyoeleza histoia ya taifa la Israeli  tangu kuiteka nchi ya kanani chini y uongozi wa Yoshua  mnano kama mwaka  1400 KK  mpaka waliporudi toka utumwani Babeli na mwisho wa Agano la Kale kama mnamo mwaka wa 430 KK.Hivyo kipindi hiki kinachukua muda wa karibu miaka 1000.
Vitabu hivi viko 12 kuanzia kitabu cha Yoshua hadi kitabu cha Esta.
Usuli wa vitabu vya histoia
Kwa mujibu wa Mock 1990 vitabu vya vya ushaili isipokuwa cha Ayubu huingiliana sana na  na nyakati za wafalme wakakati wa utawala ulioungana (1050-931KK) chini ya himaya ya Sauli, Daudi na Sulemani.
Jambo la kukumbuka unapojifunza vitabu vya historia ni  Agano ambalo Mungu aliweka kati yake na wana wa Israeli ambalo kwalo aliahidi kuwapa Baraka  kwa sababu ya utii na adhabu kwa kutokutii  kukaidi Soma Kumbukumbu la Torati 28.
Vitabu hivi vya historia vinaonesha  matkio ya dhambi katika taifa la Israeli mpaka  kukawa na miaka 70 ya utumwa Babeli (605-535 KK). Hueleza kufnikiwa na kushindwa kwa taifa hili teule la Mungu  Bwana wa majeshi.
vitabu hivi vinaonesha na kuelez jinsi Mungu alivyokkuwa mwaminifu katika kutimiza  agano lake kwa kutekelezza kila alichoahidi. Ni ni mwaminifu katika kutimiza ahadi zake japokuwa watu hwake(Israeli) hawakuwa waaminifu.
Vitabu hivi vinaonesha jinsi Mungualiuvyothibitisha uaminifu wake kwa kuwakomboa wale waliosalia  kuwarudisha  nchini  baada ya kuwahukumu  kwa dhambi zao.
vitabu hivi kumi na mbili vinaeleza habari ya kutekwa na kutawaliwa kwa nchi ya Kanani, utawala wa Waamuzi, Wafalme, mgawanyo wa Israeli wa kaskazini na kusini, kuanguka kwa utawala wa kaskazini mikononi mwa Waasria na uhamisho wa utawala wa kusini kwenda Babeli na kurudi Yerusalemu chini ya utawala wa watu kama Nehemia na Ezra.


 MUHTASARI WA VITABU VYA HISTORIA
Yoshua
Waamuzi
Ruthi
Umiliki wa nci kwa taifa na ukandaminzwaji wa taifa
Utawala na Mungu:
Vitabu hivi vinafunika kipindi cha Waisraeli walipokuwa wakitawaliwa na Mungu (1405-1043 K.K.).
 1 Samweli
2 Samweli
1 Wafalme 1-10
1 Wafalme 11-22
 2 Wafalme 1-17
 2 Wafalme 18-25
1 Nyakati
 2 Nyakati

Uimarisho wa taifa
Kuongezeka kwa taifa
Utukufu wa taifa
Mgawanyo wa taifa
 Kuharibiwa kwa ufalme wa kaskazini
Kuondolewa kwa ufalme wa Kusini
 Maandalizi ya Hekalu
Kuharibiwa kwa Hekalu


Ufalme:
Vitabu hivi vinaeleza historia ya ufalme wa Israeli tangu kusimamishwa kwake hadi kuharibiwa kwake 586 K.K.

Ezra
Nehemia
Esta

Kurejeshwa kwa Hekalu
Ujenzi wa Yerusalemu tena
 Ulinzi wa watu wa taifa
Kurejeshwa:
Vitabu hivi vinaeleza kurudi kwa wageni katika nchi baada ya miaka 70 kuwa mateka (605-536 K.K.).

Ujumbe mkuu wa vitabu vya Historia ni maandalizi ya Kristo.






II.              KITABU CHA YOSHUA. USHINDI KWA NJIA YA IMANI NA UTII
Kitabu hiki kinasimama kamadaraja kati ya  kitabu cha Pentatki a vitabu vya historia. Jina la kitabu kiki linatokana na jina la mhusika wake mkuuambaye ni Yoshua. Kitabu hiki cha Yoshua kinaeleza habari za kuiteka na kuimiliki nchi na mgawanyo wan chi hiyo kwa makabila 12 ya Israeli.
Katika kitabu hiki tunamwona Mungu akitimiza ahadi za alizowaahidi mababa(Ibrahimu, Isaka na Yakobo) na taifa l Israeli kwa ujmla  kama taifa lake takatifu.
Mwandishi wa kitabu.
Yoshua ndiye anaedhaniwa kuwa mwandishi wa kitabu hiki
 Because Joshua believed God would give Israel victory, regardless of the
strength of the nations in the Promised Land, Moses changed his name to
"Joshua" which means "Jehovah is salvation".
Jina la  halisi la Yoshua awali lilikuwa ni  Hoshea (Hesabu 13:80) lenye maana ya Wokovu

Kwa sababu Yoshua alimwamini Mungu kwamba angewapa Israeli ushindi  na kuimiliki nchi ya ahadi bila kujali nguvu ndogo walizokuwa nazo Israeli Musa alimbadilisha jina na kuwa Yoshua ambalo maana yake ni YEH OVA  ni wokovu.
Tarehe ya kitabu:      kitabu hiki kimeandikwa kama mwaka wa  kati ya 1400-1370 K.K
Kusudi/ Lengo  la kitabu.
·       Kuonesha kutimizwa kwa ahadi za Mungu kwa watu wake.
·       Kuonesha sababu za Israeli kushindqa kuimiliki nchi yote kikamilifu.
Kutokana na mapambano makali kati ya Israeli na vikosi vikuu 30 vya maadui zao, Israeli walijifunza somo kuu  ya kwamba ushind hupatikana kwa njia ya imani na utii kwa Mungu  na sio kwa Nguvu za.  Kijeshi
Zeka
Muundo wa kitabu.
Kitabu hiki kina sura tatu   24
Migawannyiko mitatu.
v Mgawanyo wa kwanza Kujitayarisha kwa ushindi.
 Sura ya 1-5  Jukumu la Yoshua.  Yos 1:1-9
Mungu anampa yoshu maagizo Kushusu kazi iliyo mbele yake.
Ø  Agizo la kwenda.(Ebr 4:8-11)
Ø  Kuwa shujaa.(Yn 16:33)
Ø  Kuwapa watu urithi. Efe 4.
Ø  Kuwa watendaji wa Neno Yak 1:22.

·       Taarifa ya wapelelezi kule yeriko. Yos 2
·       Rahabu Y os 2
·       Kuvuka mto Yordan Yos 3
·       Mawe ya ukumbusho 4.
·       Tohara    Yos 5
·       Amirijeshi wa majeshi ya Bwana. Yos 5:

v Mgawanyo wa pili:  Kuiteka nchi.
·       Sura ya 6 -12.
·       Uvamizi wa kijeshi                      Yos 6
·       Ushindi kule yeriko                       Yos 6
·       Dhambi na kushindwa kule Ai.   Yos7
·       Uvamizi wa Kusini.              Yo 9-10
·       Uvamizi wa Kasakazini         Yos 11
·       Ushindi . Bwana alipigana upande wa watu wake Israeli. Yos 11:23

v Mgawanyo wa tatu: Kugawanya nchi.

Baada ya kuiteka  nchi, Yoshua anaigawanya nchi hiyo kwa makabila 12 ya waisraeli.
Mahali pa katikati pakatengengwa kwaajili ya kuabudia kule Shilo.
Miji ya Makimbilio.
Miji ya Walawi.
Israeli wanashindwa kuwafukuza baadhi ya maadui zao.
Hotuba ya Mwisho ya Yoshua
Muhtasari wa mgao wa  nchi.
Kasakazi : Nchi ya upande huu ilichukuliwa na makabila ya  Reubeni, Gadi na Nusu ya kabila ya manase.
Kusini: Nchi ya upande huu ilichukuliwa  Yuda na ndiko mji wa Yesrusalemu ulikuapo. Karebu walipewa mji wa Hebroni.Kisha miji a kikimbiliua ikachaguliwa na walawi wakapewa miji 48 kw a sababu hawakupewa urithi wowote katika nchi yenyewe.
Mashariki  ya kaanani.  Nchi ya upande huu ilichukuliwa  na makabila mengine tisa yaliyobaki.




Jambo muhimu.
 Ilikuwa ni jukumu la kila kabila lenyewe kuwaondoa wakaanani waliokuwa wamebaki katika maeneo yao.  Lakini cha kusikitisha ni kwamba jambo hili halikutekelezwa kikamilifu kwani baadhi ya wakaanini waliachwa na hii ikawa ni mtego na kitanzi kwao kama tutakavyoona katika kitabu cha waamuzi.
Bwana aliwapa nchi yote Yoshua 21:43. Halikuanguka jambo  lolote lilikuwa ni jema ambalo Bwana alikuwa amelinena kwa habari ya nyumba ya Israeli; yalitima mambo yote. Yoshua 21:45.
Hii inamaana kwamba Mungu alitimiza Agano lake alilomwahidi Ibrahimu. Ahadi za Mungu ni za kweli akiahidi anatenda.

Watu muhimu
·       Yoshua
·       Rahabu
·       Akani
·       Amirijeshi wa majeshi ya Bwana.
Matukio muhimu
·       Kuanguka kwa Yeriko.
·       Kushindwa kwa Israeli mbele ya Ai
·       Kusimamishwakwa dunia (Jua).

Mafundisho Makuu.
Mungu ni mwaminifu kwa ahadi zake.
Mungu hutuwezesha kutimiza makusudi yake tukiwa watiifu.
Neno la mungu lapaswa kuyaongoza maisha yetu.
Dhambi huondoa uwepo wa Mungu a kutufanya  tushinde mapambano mbele ya maadui zetu.
Ni lazima kufanya uchaguzi wa kumtii Mungu au la na si kuwa katikati.

Mitajo ya Kristo.
Amirijeshi wa majeshi ya Bwana.  Huyu ni yesu mwenyewe aliyemtokea Yoshua na kumthibitishia kwamba Mbingu ilikuwa inapigana upande wake hivyo hakupaswa kuogopa aana vita ilikuwa ni ya Bwana.
Yoshua: Huyu ni kivuli cha kristo kuanzia jina lake na kazi yake aliyopewa ya kuwarithisha watu nchi. Yesu nae anakazi ya kutuithisha mbingu.
Kamba nyekundu ya Rahabu:Kamba hii ilikuwa ni kivuli ikiwakilisha damu ya
Yesu ambayo ilitakiwa kumwagika kwaajili ya ukombozi wa ulimwengu.
Kamba hii ilikuwa ni kielelezo kwamba ukombozi wa kweli ungepatikana kwa kumagwa kwa damu isiyona hatia  na watu wote wenywe kufunikwa na damu hiyo wangekuwa salama salimini.



III.             WAAMUZI. Kushindwa kwa sababu ya kuasi
Jina la kitabu:
Jina la kitabu hiki kwa Kiebrania ni Shophetim, ikiwa na maana ya Waamuzi, Watawala Wakombozi au Mwokozi. Shophet siyo tu kwamba inabeba maana ya kulinda haki na kutengeneza mashtaka lakini pia ilikuwa na maana ya “mapinduzi na kukomboa”. Kwanza kabisa Waamuzi waliwaokoa watu halafu walitawala na kulinda haki.

Kitabu kinapata jina lake kutoka kwa idadi ya viongozi wanaoitwa “Waamuzi” ambao Mungu aliwainua ili wapate kuwaokoa waisraeli kutoka katika kukandamizwa. Kichwa cha habari cha kitabu hiki kinaonekana vizuri 2:16, Kisha Bwana akawainua waamuzi waliowaokoa na mikono ya watu hao waliowateka nyara.”
Hata hivyo Mungu alikuwa mwamuzi wa Israeli na mwokozi kwa sababu alikuwa ni Mungu ambaye aliwaweka kakika Mateso kwa kuwa walikuwa wamekengeuka (waligeukia njia zao wenyewe na hivyo Mungu akainua Waamuzi ili walete ukombozi  baada ya taifa kuwa limetubu na kujuta likihitaji msaada) (11:27 ;823).
Waamuzi ni daraja kutoka nyakati za Yoshua hadi nyakati za Samweli na mwanzo wa utawala wa kifalme chini ya Sauli na Daudi. Kinatoa historia ya kushindwa kwao, ukandamizwaji, maombi, na hata wokovu pia. Kwa kufanya hivyo kinakuwa ni kitabu cha maelezo na cha sababu ya mahitaji ya ufalme katika Israeli. Kwa kuwa kila mtu alikuwa akifanya kitu kinachompendeza machoni pake (21:25) hivyo, hitaji la taifa lilikuwa ni kupata Mfalme atakayewaongoza katika haki.
Kimafundisho, Waamuzi kinatupa mambo mazuri yaliyo katika ukweli. Kama Mungu alivyotahadharisha katika kitabu cha Kumbukumbu la Torati kutii kunatupa baraka, lakini kutotii ni laana. Waamuzi wanatukumbusha kuwa ikiwa watu watamrudia Bwana wakamlilia na kutubu, Mungu ambaye anatuhangaikia sisi, mwingi wa neena atatusikia na kutuokoa. Waamuzii inatuonesha kusudi lake la jinsi walivyojifungua katika maelezo yao kwa kuonesha madhaifu na jinsi gani walivyofanya katika kutubu yote na Bwana akainua na kuokoa taifa lao.
Mwandishi wa kitabu. Mapokeo yanadai kuwa Samweli ndiy mwandishi wa kitabu hiki cha waamuzi.
Tarehe ya kuandikwa. Kitabu hiki  kiliandikwa mnamo kama mwaka wa 1000 K.K.
Kusudi/Lengo  la kitabu : 
·       Kuonesha kutangatanga kiroho kwa Wana wa Israeli katika nchi ya ahadi.
Tambua kwamba Wana wa Israeli walitangatanga kiwmili wakiwa jangwani, sasa wakiwa katika nchi ya ahadi walitangatanga kiroho( yaani uhusiano wao na Mungu).
·       Kuonesha kwamba  kuasi neno  la Mungu huleta kushindwa.

Ujumbe wa kitabu.
Tunapomwasi Mumgu na kutenda yale tunayoyaona kuwa sawa machoni petu  tunakuwa watumwa wa dhambi na ukomboi waweza kuonekana tu pindi tunapomgeukia Mungu na kutubu.

Mistari ya misingi
Waamuzi 2:1-3,      2:20-32,          21:25.

Watu Muhimu: Mwamuzi-Othniel, Ehudi, Shamga, Debora na Baraka, Gideon, Tola na Yairo, Yeftam, Ibzan, Elon, na Abdoni, na Samsoni. Waamuzi wazuri wanaojulikana ni Debora, Gideoni na Samsoni.
 Muundo wa kitabu.
Kitau hiki kin sura 21
Migawanyo mikuu 3.

Mgawo wa kwanza.Hali ya kiroho ( sura za 1& 2). mmomonyoko wa maadili.
Baada ya kifo cha Yoshua  Israeli  hawakumtii Mungu kikamilifu  katika zoezi la kuwaondoa watu waovu waliokuwa wakiishi  nchini. Makabila ya kaanani yalikkuwa na tabia ya kuabudu sanamu, tamaa  za kimwili, kukosa uadilifu na ukaidi na Israeli walibadilika na kujihusisha na matendo hayo ya wakaanani.
Watu hawa wapagani waliweza kuwa na ushawishi kwa waisraeli na kusababisha Israeli kuanza kuabudu Miungu mingine  na kujiingiza katika dhambi mbalimbali  .
 Mgawanyo wa pili. (3-16) Mizunguko saba ya dhambi – ukaidi/ukombozi.
Kwa kipindi cha muda wa miaka miatatu wana wa Israeli walinaswa katika mizunguko  isiyo na mwisho ya  dhambi- kukombolewa-dhambi. Habari inajirudia mara kwa mara.
Kuna mizunguko saba ya dhambi inayojitokeza katika kitabu hiki cha Waamuzi.  Watu walimuasi Mungu na kujiingiza katika dhambi kisha Mungu aliwacha waonewe na kuteswa na maadui zao, baada ya kukandamizwa na maaduikwa muda mrefu waliamua  kumgeukia Mungu kwa kutubu kisha Mungu alituma waamuzi kuwaokoa, baada ya Ukombozi huo Israeli walipata raha na baada ya muda si mrefu tena walianguka dhambini tena na kuanza kuteswa na kuonewa na maadaui zao. Mzunuko huo unajirudia mara saba.
Ungu aliendelea kuonesha hhuruma, rehema na uvumilivu mkubwa mno kila walipolilia msaada wake na kutubu. Mungu aliwapa Waamuzi ali wawaokoe katika mateso yao.Pamoja na kupewa waamuzi bado waliendelea kukengeuka na kurudi dhambini tena na tena zaidi.

Mgawanyo wa tatu.(sura ya 17 -21).  Kuvunjika kwa uadilifu na upotovu kukithili.
Sura tano za mwisho za kitabu cha waamuzi ni nyongeza kadhawakadha za mambo yaliyochaguliwa  ambayo yalitokea wakati wa waamuzi ambayo yanaonesha udhaifu mkubwa way a hali ya uadilifu ya wana wa Israeli. Yaani upotovu ulivyokuwa umekithiri.

Soma  sua ya 21:25. “Siku hizo hapakuwa na mfalme katika Israaeli; kila mtu alifanya yaliyokuwa ni mema machoni pake mwenyewe”
Israeli walikuwa na mfalme wa wafalme  ambaye ni Mungu  mwenyewe. Vivyo waliamua kumuasi na kila mtu akachagua lilikowa jema machoni pake mwenyewe na kwa sababu ya kutend dhambi kia mtu aliishi masiha ya pekee bila Mungu.  Soma Mwanzo 3: 1-4,  Warumi 1:25. Matokeo yake kukawa hakuna serikali , kuwa na mtapakoa wa dhambi na machafuko.  Kitabu hiki cha waamuzi kinaleta utangulizi wa vitabu vya Samweli, Wafalme na Mambo ya Nyakati.
Mafundisho makuu
·       Kutomtii Mungu huleta matokeo mabaya sana.
·       Rehema na subira za Mungu ni kuu.
·       Mungu huwaadhibu watu wake wanapotenda dhambi.
·       Mungu huwakoa watu wake kutoka katka vifungo vya dhambi wanapogeuka na kutubu.
·       Mungu daima huthibitisha mapenzi yake kwa dalili zionekanazo.
·       Iwapo Mungu si Bwana wa Maisha yetu basi sisi si kitu kabisa.
Muhtasari wa waamuzi
Mwamuzi
Othinieli
3:7-11
Ehudi/shamgari
3:12-31
Debora/Baraka
4:1-5:31
Gideoni
6:1-8”32
Tora/Jaili
8:3310:5
Jefta/Ibzani
Eloni, Abdoni
10:6- 12:15
Samsoni
13:116:31`
Adui
Wamesopotamia
wamoabu
Wakanani
Wamidiani
Wabimeleki
Waamori
Wafilisi
Miaka ya utumwa
8
18
20
7
3
18
40
Miaka ya amani
40
80
40
40
45
6,7,10,8
20










Mzunguko wa waamuzi
Oval: UtumwaOval: DhambiOval: Ukombozi                                                                                               Oval: AmaniBwana alighairi kwaajili ya kuugua kwao                  Kisha Bwana akawainusa waamuzi waliowaokoa
Oval:      Toba                                                                                                                                                                                      2:18                                                                                                     2:16                                  














                                                    KITABU CHA RUTH. 
I.                Usuli wa kitabu
Kitabu cha Ruthi ni mwangaza katika kipindi cha giza  katika  wakati wa waamuzi. Ni hadithi ya mwanamke wa kimoabu (Ruthi) mwenye upondo mkamilifu na mwenye kujitoa kikamilifu kwamama mke wake Naomi.Ni hadithi  inayoelezea thawabu ya Mungu kwa watu wanaojiyoka kikamilifu katika kutumikia kusudi lake takatifu.
Ruthu ni historia ya wanandoa wawili katika Israeli ambao wakati wa njaa walihamia Moabu. Huko mme wake na watoto walikufa wakamwacha mwanamke (Naomi ) peke yake akiwa na wakweze wa kike (Orpa na Ruthu). Naomi aliamua kurudi Israeli pamoja na Ruthu alimsihi arudi pamoja naye. Katika Israeli walirudi kwa ndugu yao Boazi ili awasaidie na Ruthu aliolewa na Boazi.
 Kama dhahabu ing’aayo Ruthu alionekana kung’aa katika siku za giza nene za kitabu cha Waamuzi. Ruthu ni kitabu cha uaminifu,utakatifu,na upendo katika siku za vurugu na shida. Ubinafsi na ukengeufu ndio ulikuwa unatawala siku hizo.
 Hivyo katika kitabu hiki Ruthu anatupa picha ya imani na utii katika matatizo na anaonyesha ni kwa jinsi gani imani yaweza kuleta baraka .
 Ruthu anatumika kama mtumishi mwaminifu kwa mfalme Daudi na kama ilivyokwisha kusemwa hapo juu kuwa yeye anamwakilisha Yesu. Kusudi jingine la Ruthu linaonesha ukweli katika ukombozi wa kinsmani, uwepo wa mabaki ya watakatifu hata katika zile nyakati za shida na uaminifu wa Mungu kwa wale wanaomtegemea na kutembea naye kwa imani. Kwa kuwa Ruthu alikuwa mtakatifu, kitabu kinaonesha shauku ya Mungu ya kuuleta ulimwengu katika familia yake.
 Inaweza kushangaza kuwa kwa yeyote yule anayemtumaini Mungu kwa hakika ni Moabu. Uaminifu wake katika familia ya Israeli ambako aliolewa (Ruthu) na kuomba kwake huko kwa wakweze inamthibitishia kuwa mtoto halisi wa Israeli na Mtumishi mwema wa Daudi mfalme. Anatoa mfano halisi katika ufalme ujao wa Mungu kuwa hii haitafanyika tu kwa sababu ya kuzaliwa au kwa sababu ya damu, hapana, ila ni kwa sababu ya kukiri katika mapenzi ya Mungu kwa njia ya kutii kwa imani (Warumi 1:5).Na sehemu yake katika ukoo wa Daudi inaonyesha kuwa mataifa yote yatamilikishwa katika ukoo wa Mwana wa Daudi.
Kitabu cha Ruth ni Miongoni mwa vitabu viwili vyenye majina ya wanawake,  kikiwemo na kitabu cha Esta. Kitabu cha Ruthi kikihusika na mwanamke mmataifa aliyeolewa na mwisraeli na kitabu cha EWsta kikihusika na mwanamke mwisraeli aliyeolewa na mmataifa.
 Uwakilishi wa kitabu cha Ruthu.  Kwa kuolewa katka ukoo wa Daudi (4,17,22) Ruthu  kinabii Ruthu anawaleta wamataifa wote kwa Masihi. Mathayo 1:5
 

Matukio ya kitabu hiki ni ya kipingi  cha waamuzi kulingana na ushaihdi wa kitabu chenyewe soma.Ruth 1:1
II.              Tarehe ya kuandikwa.        Kitabu hiki kinadhaniwa kuwa kimeandikwa kama mwaka wa
1050KK
III.            Mwandishi wa kitabu. Samweli ndiye anae dhaniw kuwa mwandishi wa kitabu cha Ruthu.

IV.            Ujumbe wa kitabu. Imani na utii huleta thawabu.

Mungu huheshimu wertu nye imani na watiifu wanaoshi maisha matakatifu  wakia katika  huku wakiwa katika wakati uliojaa na maovu na uchafu wa kila aina.

V.              Kusudi/lengo la kitabu.
Eileen Crowhurst, (2008,uk 8&9) anaainisha malengo makuu ya kiabu cha Ruth kama ifuatavyo:
      i.          Kuonesha picha ya Neema ya Mungu.
    ii.          Kuonesha mwanzo wa ukoo wa Daudi
   iii.          Kuthibitisha kwamba  wamataifa nao wanahusika katika mpango wa Wokovu Wa Mungu.
Hivyo tunaweza kusema kwamba kusudi au lengo la kitabu ni kuonesha kwamba Imani ndiyo njia kuu inayowaingiza watu katika mpango wa Mungu na si undugu wa kidamu Hili linathibitishwa kwa kuwaangalia wanawake wawili wa mataifa yaani Rahabu na Ruthu walivyoingizwa katika mpango wa wokovu wa Mungu kwa njia ya imani na utii. Wanawake hao wote wawili wapo katika orodha ya ukoo wa daudi ambao ndiko masihi  alitakiwa kutoka yaani Yresu Kristo.  Yesu anatoka katika nasaba mchanganyiko yaani myahudi na mmataifa. Hivyo na kazi yake ya ukombozi inahusu nasaba zote.

VI.            Muundo wa kitabu.
Kiabu hki kina sura 4 na
Migawo iine kulingana na sura za kitabu.
Magawo wa kwanza (sura ya 1) Kurudi kwa Ruthu.
Kiatbu kinaanza na habari ya uhamisho wa Elimeliki na familia yake kwenda katika nchi ya Moabu kwa sababu ya njaa iliyokuwa imeanguka katka nchi ya Israeli. Elimeliki alifikiri kwamba mambo yangekuwa mazuri huko Moabu hivyo akaamua kuhamia huko. Uamuzi huo alioufanya ulitoa hatima ya maisha yake kwani hakuweza kuiona tana nchi ya ahadi maana alifia ugenini katika nchi ya kipagani. Yeye na watto wake wawili walifia ugenini.
 Jambo hili linatufundisha kuwa wavumilivu katika kungoja ahadi za Mungu wetu tunapokuwa katika shida na matatizo. Kutafuta njia mbadala  isiyo ya ki Mungu katika kukabiliana natatizo huwqeza kuharibu  hatima ya maisha yetu na familia zetu.
HIi inatufundisha pia kwamba aamuzi tunayoyafanya hayatuathiri sis tu bali huathili mzunguko mkubwa sana, kuanza wewe mweyewe, familia yako, kanisa na jamii kwa ujmla. Hivyo tuwe makini n maamuzi tunayoyafanya. Kutokana na maamuzi ya elimeliki, Naomi alibaki mjane na mpeke kwani aliondokewa na watu watatuambao ni  mme na wana wawili.

Baada ya mkasa huo Naomi mke wa elimeluki aliamua kurudi  nchini kwao (Israeli) na akawaomba wake za watoto wake (Olpa na Ruthu) waliouwa wajane kama yeye kila mtu arudi kwao.   Olpa baada ya kulia kwa muda mrefu aliamua kurudi kwao lakini na kwa Mungu wake.(1:14-15)
Ruthu alikataa kumuacha mama mkwe wake kwani alikuwa na mtazamo wa mbali hivyo aliamua kujiunganisha na Mungu wa mama mkwe wake. Ruthu aliwezq kudhihirisha uelewa wake kwa mambo ya kiroho. Aliweza kuuuona mpango wa Mungu wa wokovu na akaamua kushikamana nao kwa gharama zozote zile.

Mgawo wa pili; (sura ya 2)Kuvuna.
Ili Naoni ajipatie riziki  Ruthu akafanya kazi ya kuvuna gano shambani kwa Boazi aliyekuwa mwisraeli aliyekuwa anahusiana na Elimeliki.Boazi aliiona bidii na kazi njema ya Ruthu hivyo akwa anamtunza.Naomi akatoa ushari kwamba Ruthi afanye kazi kwenye shamba la Boazi tu kwaani Boazi alikuwa jamaa yao na alikuwa ni mkombozi. Ruthu akatii agizo hilo.

Mgawo wa tatu. (sura ya 3) Kustarehe kwa Ruthu.
Naomi anatoa ushauri kwamba ruthu anatakiwa apate pumziko  kwa njia ya kuolewa. Naomi  Anatoa ushauri Ruthu amwombe Boazi avunje undugu ili amuoe Ruthu. Hili linafanyika baabda ya ndugu wa karibua lityekuwa jamaa ya mjane kukataa kumkomboa Ruthu. Boazi alikubali kumkomboa na akamwoa.Boazi alipoikomboa ardhi ya jamaa ya Elimeliki alikuwa akinunua haki za urithi za mwanae aliyefariki  aliyeitwqa Mahloni  na kwa kufanya hivyo alitakiwa kumuoa mjane wa mahloni ambaye ni Ruthu ili kuendelezajina la ukoo.

Mgawo wa nne(sura ya 4) Kutuzwa kwa Ruthu.
Mungu alibariki uaminifu wake na Ruthu akaolewa na Boazi na kwakbarikiwa kumpata motto aliyeitwa Obedi ambaye ndiye aliye mzaa Yese baba wa Daudi. Hivyo Daudi ni mjukuu wa Naomi Mmoabu.

IV.            Watu Muhimu. Naomi, Ruthu na Boazi.
V.              Mitajo ya Kristo: Ruthu na boazi.

VI.            Mafundisho muhimu.

§  Urafiki  uliojengwaq juu ya upendo una nguvu kuliko undugu.
§  Mungu hwabariki watu wake waliowaaminifu na kuwatukuza.
§  Mpango wa Mungu wa wokovu ni kwa watu wote wayahudi na wamataifa.
§  Inawezekana kuishi maisha matakatifu katikati ya uovu mwingi.
§  Subira na uvumilivu kwa ahadi za Mungu ni jambo la msingi sana.



                                                          KITABU CHA SAMWELI. I
I.                Usuli wa kitabu
Kitabu hiki kinajulikana kama kitabu cha mpito toka utawala wa Mungu hadi utawala wa mwanadamu.
kawaida kitabu cha Samweli wa 1 na 2 viliwekwa pamoja kama kitabu kimoja katika kitabu cha Kiyahudi. Vitabu hivi viwili vinatupa historia ya ufalme wa Israeli katika kipindi cha mwanzo kabisa cha utawala wa kifame. Hata hivyo 1Samweli inaeleza habari za mfalme Sauli na 2 Samweli inaeleza habari za mfalme Daudi.
Japokuwa kitabu hiki asili yake kilikuwa ni kitabu kimoja katika kitabu cha kiyahudi, lakini ilibidi kigawanywe katika vitabu viwili na mkarimani wake wa Septuagint (hii ni tafasiri ya kiyunani katika Agano la Kale). Mgawanyo huu baadaye ulifuatiwa na Yerome kwa kilatini ni Vulgate (tafasiri ya Biblia kwa Lilatini) na hata katika tafasiri zingine.

Kitabu hiki kinaeleza kipindi cha mpito toka katika utawala wa THEOCRACY kwenda katika utawala wa ki MONARCHY  yaani utawala  wa kifalme.
Kunaushusiana mkubwa katika vitabu vya 1&2 Samweli, 1&2 Wafalme na 1&2 Mambo ya nyakati. Vitabu vya Samweli na wafame vinaeleza historia ya  Samweli, Sauli,  Daudi, Sulemani na ufalme uliogawanyika katika mtazamo wa Kihistoria wakati (Historical point of view). Wakati vitabu vya Mambo ya Nyakati vinarudia kwa kiasi kikubwa yale yaliyoandikwa katika Samweli 1na II kwa mtazamo wa kiroho(spiritual point of view). 1Samweli 4:18

1&2 Samweli
1&2 Wafalme
1&2 Mambo ya nyakati                                                  Vinaelezea kuanguka na kuinuka kwa ufalme wa      Israeli wa kimonaki
Kitabu cha Isamweli kinachukua kipindi cha  muda wa miaka 115, kikanza na kuzaliwa kwa Samweli na kuishia na kifo cha Sauli.
Samweli ndiye aliyetumia na Mungu kuanzisha utawala wa kimonaki baada ya Israeli kutaka kuwa na mfalme juu yao kama mataifa mengine.  Pia Samweli alitumia na mungu kuanzisha huduna ya kinabii na kuanzisha shule ya manabii. Historia inatuambia kwamba Samweli alifungua shule katika mjiwa Rama alifundisha kusoma na kuandika na Neno la Mungu hivyo Samweli alichagngia sana katika kukua kwa mfumo wa elimu katika taifa la Israeli. 1 Samuel 10:5).
Wayahudi wanamchukulia Samweli kuwa ni nabii wa pili baada ya Musa. Zaburi 99:6. Na Nabii wa kwanza katika mpangilio mpya wa manabii. 1 Samweli  3:20; Matendo ya mitume 3:24; 13:20.
Si kwamba Mungu alianzisha huduma ya manabii  na shule ya manabii tu  kupitia Samweli bali pia Mungu  alianzisha matengenezo ya kurejesha ibada na maadili mema katika taifa la Israeli kwa kupitia mtumishi wake Samweli. Jambo hili lilifanyika kupitia mfumo wa elimu ambao aliuanzisha Samweli.
Mfumo huu wa elimu uliwafunza watu mafundisho sahihi ya kiungu ambayo waliwarejesha watu kuanza kuwa na ibada na  kurudi kwenye maadili ya kiM-ungu. Mfumo huu wa elimu ulipelekea kukua kwa ustaarabu wa taifa na kupatikana kwa viongozi waliokuwa wanauwezo wa kuwaongoza watu walioelimika, mfano wa  viongozi hao ni Daudi, Sulemani, Isaya na
Mungu pia alimtumia Samweli kuunda katiba ya kimonaki. Sauli alitakiwa kuwa mfalme  kwa utii wa sheria ya Mungu  lajkini haikutokea hadi wakati wa Daudi.Katiba iliyoandikwa na Samweli kuongoza ufalme iliitwa kitabu cha mambo ya wafalme 1Samweli 10:25. Kitabu hiki hakikuwa na maana yoyote kwa Sauli mtu ambaye  hakujua kusoma na kuandika. Katiba hii ilianza kujulikana wakati wa mfale Daudi mtu aliyekuwa amekulia katika mfumo wa elimu ulioanzishwa na Samweli. Malme ambaye angeisimamia sheria ya Mungu aliingia kwenye utawala.

Mwandhishi wa kitabu.  Mwandishi wa kitabu hiki ni Samweli.
kitabu hiki hakikuandikwa chote na Samweli kwa bababu kuna matukio yaliyofanyika baada ya kufo cha  Samweli yameandikwa katika kitabu hiki. Mfano kifo cha Samweli  mwenyewe katika  Sura ya 24. Baadhi ya Sehemu za vitabu hivi zinadhaniwa kwamba ziliandikwa na watu waliokuwa karibu sana na samweli kama vile, Gadi mwonaji na nabii Nathani. 1 Mambo ya nyakati 29:29.
Mistari ya msingi I Samwel 13:13-14 na 1 Samwel 15:22-23.
 Muundo wa kitabu .  
Kitabu hiki kina sura31 na migawo mitatu ambayo ni
Mgawo wa kwanza(sura ya 1-8) Sawmeli mwamuzi wa mwisho wa Israeli na nabii wa kwanza.
Kitabu hiki kinaziba pengo  lilipo la miaka 60  ya historia ya taifa la Israeli kati ya wakati wa waamuzi na wakati wa wafalme.Baada ya kushindwa kwa kuhani Eli na familia yake Mungu alimwinua Samweli kuwa mwamuzi wa mwisho na nabii wa kwanza katka taifa la Israeli. Wakati huu Israeli ilikuwa katika wakati mgumu kwani  ni kipindi ambacho Israeli ilikjuwa ikisumbuliwa sana na wafilisti wailokuwa wameliteka sanduku la agano  lilipopelekwa vitani na watoto wa Eli kuhani wawakati huo. Samweli aliwaongoza wana wa Israeli kuinuka  tena walipotubu na  kubadili mwnendo wao wa uovu.
Samweli alipokuwa anazeeka alidhihirika wazi kwamba watoto wake walikuwa na tabia kama za watoto wa Eli mtangulizi wake  na kuwakosesha sifa ya kuwa viongozi baada ya baba yao kufariki vivyo Israeli walimwomba Mungu kupitia kwa Samweli awape mfalme kama mataifa mengine. Kwa kufanya hivyo Israeli walikuwa wanamkataa Mungu asiewe mfalme wao.
Mgawo wa pili: (9-15) Sauli mfalme wa kwanz wa Israeli.
Mungu akamchagu a Sauli kuwa mfalme na akamwagiza Samweli amtawaze kuwa mfalme.  Sauli alikuwa ndiye aina ya mfalme ambao Israeli ilifikiri kumpata.
Sauli alistarehe katika ushindi wake wa mwanzomwanzo  katika himaya ya utawala wake ingawa alishindwa kuwa mwadilifu mbele za Mungu. Kutokana na Sauli kukosa uadilifu Mungu alimkataa asiew mfalme juu ya Israeli japokuwa alimruhusu kutawala kwa muda wa miaka 15 hadi wakati wa kifo chake.
Mgawo wa tatu.(16-31) Daudi, mfalme wa kwanza aliyechaguliwa na Mungu.
Baada ya utawala wa  kama miaka 25 hivi wa Sauli Mungu alimchagua Daudi kuwa mfalme wa Israeli. Daudi alichaguliwa kuwa mfalme akiwa na miaka 15 lakini alianza utawala wake akiwa na maika 30. Umaarufu wa Daudi ulianza wakati alipomuua  Goliathi.  Baad a ya Daudi kumuua Goliathi na kupewa sifda nyingi kuliko Sauli kulizusha wivu na sauli akataka kumuua Daudi kwani alipoteza usalama moyoni wa kiuongozi.
Daudi alianza kuwindwa na Sauli kama mnyama ili auawe lakin kwa msaada wa rafiki yake Yonathani kijana wa Sauli na mke wake Mikali Daudi aliponyoka na kuishi jangwani kama mtoro.
Daudi alipata fursa kadhaa za kujilipizia kisasi juu ya sauli pale Mungu alipomtia Sauli Mikononi mwake, lakin Daudi alikataa kumdhuru Sauli, aliheshimu mafuta ya kimasihi yaliyokuwa juu yake Sauli na akakataa kuimwaga dmu ya Masihi wa Bwana. Hakika Daudi alikuwa na moyo wewnye kumcha Mungu  kwani aliamni kwamba kisasi ni juub ya Bwana mwenyewe.
Hata Sauli alipokufa bado Daudi hakuingiwa kwenye utawala yeye mwneyewe, japokuwa alijua kuwa nafasi ya ufalme ilikuwa ni yake. Aliamua kusubiri mpaka atawzwe na Mungu mwenye. Wakati huu wa dhoruba kali juu ya maisha ya Daudi ndio wakati alioandika Zaburi nyingi.

Watu muhimu  ni , Hana, Eli, Samweli, Sauli, Daudi, Goliathi,  na Yonathani.
Mitajo ya Kristo. Daudi.
Mafundisho muhimu.
·       Mungu anatafuta watu watakao sikiliza sauti yake na kuitii kikamilifu.
·       Urejesho na uamsho huja kwa kupitia toba ya kweli.
·       Mungu wakati mwinhgine hutupa yale tunayoyafikiri kuwa ndiyo tunayoyataka ili kutuonesha kwamba  siyo tunayohitaji.
·       Mungu hutaka utii mtimilifu.
·       Imani hutuwezesha kuona mbali kupita mipaka ya maisha tuliyonayo.
·       Tunapaswa kufuata ushauri wa Mungu na wala sio wa wanadamu.
·       Ushindi hupatikana kwa uweza wa Bwana mwenyewe wala si kwa nguvu za mwili.
·       Mungu huwachagua watrumishi kutimiza kusudi lake na sio makusudi na nia za mioyo wao wenyewe.
·       Ukaidi daima huleta matokep mabaya sana.
·        
SAMWELI  II
Miaka 40 ya utawala wa Daudi.
I.                Usuli wa kitabu.
Kitabu hiki ni mwendelezo wa kitabu cha Samweli na kiachukua jina lake toka kwa mhusika wake mkuu ambae ni Samweli.
Bila makusudi yoyote ya kuharibu historia ya ufalme wa Waisraeli 2 Samweli anaendelea kueleza juu ya kuanzishwa kwa ufalme wa Waisraeli na hata mwanzo wa kifo cha Sauli na inaendelea na utawala wa Daudi. Na hii imechanganuliwa tangu miaka ya 40 ya utawala wa Daudi (5:4-5) na inaendeleza utawala huu kupitia ushindi na majonzi ya masikitiko yanayojumuisha dhambi zake, uuaji na hata matatizo katika jamaa yake na hata taifa. Kusudi katika 2 Samweli inaonesha utawala wake Daudi, na hii inaweza kufupishwa “kwa kiasi gani dhambi inabadili furaha hata mafanikio kuwa shida na huzuni” Taifa lilisimama chini ya Sauli na kupanuka wakati wa Daudi. Utawala wa Sauli uliimarisha Israeli tangu wakati wa Waamuzi lakini utawala wa Daudi ulileta kupanuka kwa taifa hili na hata kukua zaidi. Kwa hiyo tunaweza kusema kuwa hii inatueleza kabisa kibiblia jinsi gani utawala wake ulikuwa, 2 Samweli inaonesha uzuri na ubaya wa mfalme Daudi.
Baada ya kifo cha Sauli Abneri kamanda mkuu wa majeshi ya Sauli alimtawaza  mmojwapo wa watotowa Sauli kuwa mfalme ambaye ni Ithiboshethi  kutawala sehemu moja ya ufalme (Israeli) kwa miaka miwili. Yuda ilimkubali Daudi kuwa mfalme wao. Baada y kufa kwa Ithiboshethi utawala ulitakiwa kwenda kwa motto nojawapo wa Yonathani laki Israeli yote ilitambuwa kwamba Daudi ndiye aliyetakiwa kuwa mfalme juu yao baada ya kifo cha Sauli.

II.              Mwanndishi wa kitabu  Gadi na Nathani ndio wanaodhwaniiwa kuwa waandishi wa kitabu hiki. Rejea maelezo ya utangulizi wa uchunguzi wa kitabu cha 1Samweli.

III.            Tarehe ya kitabu . Kitabu hiki kinadhaniwa kuwa kimeandikwa kama mwaka wa 1010 KK.

IV.            Kusudi/lengo la kitabu.Kueleza miaka arobaini ya uawala wa Daudi.
V.              Ujumbe wa kitabu. Tunavuna tunchopanda. Kila mwanadamu akifanyacho ni mbegu na kitatoa mavuno kutokana na aina ya mbegu iliyopandwa.

VI.            Mistari ya msingi.
2Samweli  7:16 na (2Samweli 24:24).

VII.         Muundo wa kitabu.
·       Kitabu hik kina sura 24 na
·       Migwanyo mikuu mine 4.
Mgawanyo wa kwanza (1-10) Kuinuka kwa Daudi.
Baada ya kifo cha Ssauli daudi alitawazwa kuwa mfalme wa Yuda katika mji wa Hebroni ambako kulikuwa na makabila mawili ya kusini. Makabila kumi  ya Kaskazini hayakmtambua Daudi kuwa mfalme yalimfuata Ish bosheth  (mwana pekee wa Sauli aliyekuwa amesalia )kuwa mfalme .
 Kutokana na jambo hili kulikuwa navita ya wenyewe kwa wenyewe kwa muda wa miaka saba na nusu. Daudi na amiri jeshi wake Yoabu walimshinda Ish bosheth na amiri jeshi wake Abneri. Na wote wawili waliuawa.
Daudi aliendelea kumngoje Mungu aili amuweke kuwa mfalme na baada ya kutimiza miaka 30 Mungu alimuweka Daudi kuwa mfalme wan chi nzima. Daudi alitawala taifa zima kwa muda wa miaka 30, kipindi hiki kilikuwa ni kipndi cha furaha mno kwa kuwa Daudi
Daudi aliufanya mji wa Yesrusalemu kuwa mji mkuu wa kisiasa na kidini.
·       Alirudisha lile sanduku la agano yerusalemu.
·       Alifanuikiw kiuchumi, kisiasa na kivita
·       Alileta uadilifu na haki nchini.
·       Daudi alikuwa n nia ya kumjengea Bwana  hekalu lakini Bwana alimkataza na kumwambia mwanae Sulemani ndiye angehusika na ujenzi huo.
·       Mungu alimwahidi daudi kwamba mbali yake itaishi milele na kwamba kutakuwa na mfalme na kiti cha enzi kutoka kwenye ukoo wa Daudi.  Ahadi hii  hujulikana kama agano la Daudi na hatimae ilitimizwa katika Kristo Yesu Bwana wetu.  Soma 2Samweli 7:8-17 na Luka 1:26-33.

Mgawanyo wa pili (11-12) Kuanguka kwa Daudi.
Anguko la Daudi lilitokea wakati wa kipindi chake cha mafanikio makuu na ustawi. Anguko hilo lilitokana na sababu zifuatzo.
 Kukosa kazi kwa Daudi. Daudi hakuwa mahali alipotakiwa kuwa na hivyo akajihusisha na dhambi. Tunakuwa mawindo rahisi kwa shetani tunapokosa kujihuisisha  na kazi ya Mungu.
Kama Daudi angekwenda vitani na majeshi yake tkio hilo la dhambi lisingetokea.

Daudi aliacha kujali (unconern). Kwa hakika kipindi hiki kilikuwa ni kipindi cha vita na Daudi aliamua kutokwenda vitani na kukaimisha mtu mwingine nafasi yake. Kwa sababu kipindi hiki kilikuwa ni cha mafanikio hivo Daudi hakujisikia kuwajibika yeye mwwenyewe. Tusipokuwa waagalifu wakati wa  Mafanikio waweza kuwa ni wakati mzuri kwa adui kutuangusha katika dhambi.

Kutokana  na Daudi kutokuwa katika nafasi yake aliiruhusu dhambi kutafuna maisha yake. Daudi alizini na Bethsheba na kumpa mimba, kisha akajaribu kuificha dhambi yake kwa kumrububi uria ili alale na mkewe Betsheba ili ionekane kwamba ni mimba ya Uria, lakini mpango huo ukashindikana.  Baada ya kushindikana mpango huo Daudi akaamua kufanya dhambi ya maauaji. Akamwamuru amiri jeshi wake mkuu (Yoabu) kumuweka Uria kwenye mstari wa mbele vitani ili uria auawe, mpango huo ukafanikiwa  Uria asiye na hatia akauawa. Hayo yote Daudi anayanya ili kufunika dhami yake.Dhambi inazaa dhambi na kisha mauti. Kutokuwa kwenye nafasi+ Tamaa= uzinzi+ uongo= mauti.
Dhambi inabakiwa kuwa dhambi hata ipakwe rangi nzuri kiasi gani na dawa yake ni toba tu. Unapojaribu kuficha dhambi utajikuta unaongeza dhambi juu ya dhambi. Hivyo toba ndiyo dawa pekee ya dhambi.
Mungu hakukubaliana na kile Daudi alichokifanya aliamua kumkabili mfalme Daudi kwa kupitia nabii Nathani.Daudi baada ya kukabiliwa na Mungu akatubu na Mungu akamtangazia hukumu.  Mtoto wa kwanza wa kiume ambaye angezaliwa na Daudi kwa Betsheba angetakiwa kufa na upanga usingetoka katika nyumba ya Daudi kwani aliwapa Adui za Bwana nafasi ya kukufuru.

Baada ya Yule motto wa kwanza wakiume kufa Mungu alimjalia Daudi kupata mtot mwingine  wa kiume kwa Betsheba  mtot hyu aliitwa Sulemani ambaye ndiye aliyekuwa mrithi wa kiti cha ufalme cha Daudi baba yake.
Mgawanyo wa tatu (13-20)Maafa ya Daudi.
Mungu ni mwingi wa rehema alimrehemu na kumsamehe Daudi alipotubu, lakini sababu alikuwa amepanda kanuni ya kupanda na kuvuna ilikuwa haina budi kutenda kzi, hivyo Daudi aliiltete familia yake balaa badala ya Baraka.
Sura hizi zinaeleza kwa undani matokio ya dhambi ya Daudi  na hkumu zake. Japokuwa Mungu alimsamehe Daudi lakini Daudi alitakiwa kuyapokea matokeo ya dhambi yake.  Mikasa ilianza katika watoto wa daudi, Amnoni akambaka ndugye Tamari dada wa Absalomu, Absalomu anamuua Amnoni na kisha anampindua baba yake na kujitangazia utwala. Daudi anakimbia kama mkimbizi toka ikulu akiwa peku huku akilia, Absalomu anauawa na kisha Daudi anarejea tena Yerusalemu  kwenye utawala ingawa hakuwa na utukufu kama ule wa mwanzo.
Dhambi ilileta pigo kubwa katika maisha ya Daudi.

Mgawanyo wanne (21-24) Ujasiri wa Daudi.
Sura hizi zinafanya nyongeza ya kihistoria ya kitabu cha Samweli II. Zinatoa taaarifa maalumu ya mbambo yaliyotokea wakati wa utawala wa Daudi. Daudi alitenda dhambi nyingine machoni pa Mungu ya kuwahesabu askari wake katika kuonesha nguvu yake ya  kijeshi.   Mungu akaleta tauni lakini Daudi akaomba rehema na tauni ikakoma. Toba yake Daudi na dhabihu aliyoitoa katika mlia Moria kuliipoozesha tauni.  Daudi akanunua mahali ambapo hekalu lingejengwa na Kristo angetjioa dhabihu yeye mwenye miaka 1000 baadaye.

VIII.Watu muhimu  Daudi, Yoabu, Abneri, Ish boshethi, Mefibosheti, Betsheba, Uria, Nathani na Absalomu.
Mafundisho makuu  ya kitabu.
Dhambi huleta matukio mabaya
Dawa ya dhambi ni toba pekee.
Dhambi yoyte ile inamatokeo ambayo mtenda dhambi hana budi kuyavuna.
Mungu hana upendeleo na hukumu zake ni za haki.
Mungu ni lazima aiadhibu dhambi.
Mungu husamehe husamehe dhambi tunapotubu.
Dhabihu ya thamani mbele za Mungu ni ile inayogharimu.
Matokeo y dhambi yanaathili jamii nzima.













1 Wafalme.
Usuli wa kitabu.




1 na 2 Wafalme kwa asili yake ni kitabu kimoja kama vile Samweli na hata Mambo ya  Nyakati . Kiliitwa Wafalme kwa Kiyahudi (Melechim). Viliitwa hivyo tangu historia ya Wafalme wa Israeli na Yuda tangu zama za Sulemani na hata kuelekea kwa mateka wa Babeli. Na 1 Wafalme inaishia kwa kueleza mwanzo wa utawala wa Mfalme Ahazia 853 K.K.  Vitabu hivi vinaelezea historia ya kipindi cha miaka karibu 400






Muda wa Kuandikwa:
Ni kama 550 K.K. Kuachiliwa kwa Yehoakimu toka gerezani ilichukuliwa katika 2 Wafalme kama tukio la mwisho. Na hii ilifanyika miaka ya 37th kufungwa kwake (560 K.K.). Kwa hiyo 1 na 2 Wafalme yamkini ilikuwa bado haijaandikwa kabla ya tukio hilo. Inaonekana kabisa kuwa kurudi kwa mateka toka Babeli

No comments:

Post a Comment