Sunday 6 January 2019

Kanuni  ya biblia
Neno kanuni kietimolojia   ni neno   la kiarabu  lenye asili yaya kiebrania   lijulikanalo kama keneh .lekiwa na maana ya fimbo nyofu ya kupimia  .Katika kigiriki kanon  likiwa na maana ileile fimbo nyofu ya kupimia
Maana ya Ki biblia, ni kanuni zinazo tumika kupima vitabu vinavyo stahili  kuhesabiwa kama Neno la Mungu
1.      Sababu ya kuwa na kanuni ,
2.      Zinatusaidia kujua vitabu vinavyostahili kuwa katika Biblia.
3.      Zinatusaidia kutambua kati ya kitabu cha kweli na cha uongo .
4.      Zinatusaidia  kuwa na imani thabiti.
5.      Zinatusaidia kutambua mafundisho potofu
1.      Aina za vitabu vinavyo paswa kupimwa
2.       
3.      Vitabu vilivyo katika biblia yetu vya
4.      Vitabu vilivyopotea vinavyo tajwa katika agano la kale,
5.      Vitabu  vya apokrifa

Uingazaji wa vitabu kwenye orodha ya Biblia
Uingizaji wa kitabu kwenye orodha ya biblia ni kitendo  ambacho vitabu vya Biblia hupokea ibali cha mwisho na kupokelewa na viongozi wa kanisa.Njia nyingi zilitumika katika kutambua vitabu vinavyo stahili kupokelewana kuingizwa katika orodha ya maandiko matakatifu yaani Bilbia,Watu wa Mungu walilazimika kutafuta ishara Fulani za ki –Mungu

KANUNI ZILIZOTUMIKA

Mamlaka ya kitabu; Je kitabu kinadai kuwa ni Neno la Mungu? Kila kitabu katika Biblia hubeba dai la kuwa na mamlaka ya ki-Munguy.Maneno yafuatayo mara nyingi yalitumika.kuthibitisha ;Asema Bwana wa majeshi ,Neno la Bwana lilinijia kusema.Katika vitabu vya historia maonyo humaanisha zaidi na matangazo ya mamlaka i kuhusu kile Mungu amefanya katika historia ya watu wake.
Kama mamlaka ya ki Mungu ilikosekana katika kitabu ,hakikufikiliwa  kuwekwa kwenye orodha ya maandiko matakatifu na kilkataliwa kuingizwa  katika orodha ya maandiko.

Mamlaka ya kiuandashi ; Kitabu kiliandikwa kwa mkono wa mtu gani ? Nabii,Mtume ;au mtu alieagizwa na mungu au mtu alietembea na mitume kwa karibu sana kama Marko na Luka.
Kama vitabu hivyo havikuandikwa na watu waliotajwa hapo juu ilibidi vikataliwe. Kutokana na maonyo ya mtume Paulo ilbidi kutopokea kitabu toka  kwa mtu ambae kwa udandanyifu alijiita mtume.(2the 2 :2,  2kor 11 ;13  na 1Yoh 2 ;18-19 ;4 ;1-3) Hivyo ilikuwa ni muhimu kutambuamwandishi wa kitabu.ili kuamua kama kitabu kikubaliwe au kikataliwe.
Uhakika wa kitabu ;je kitabu kina ukweli ?kinasema ukweli kuhusu Mungu,mwanadamu,dhambi ,wokovu .nk.Alama nyingine maalumu ya uvuvio ni  ukweli au uhakika wa kitabu Kitabu chochote chenye makosa ya kukosa ukweli (kutokana na ufunuo uliopita)kisingevuviwa na Mungu.kwani Mungu hawezi kusema uongo.mungu na neno lake ni wamoja. Kutokana na kanuni hii Waberoya waliyapokea mafundisho ya paulo ya Paulo na kuchunguza maandiko ili kuona kama kile kilichofundishwa na mtume Paulo kilikuwa kweli na  kilikubaliana na ufunuo wa Mungu katika Agano la kale au la.  (Mdo 17 :11)Kuhitilafiana na ufunuo uliotangulia kungeonesha wazi kwamba fundisho halikuvuviwa.Sehemu kubwa ya mafundisho ya apokrifa yaliyo dhaniwa kuwa na uvuvio yalikataliwa kutokana na kanuni hii ya uhakika  kitabu.

Asili ya kitabu kuwa na nguvu ;Je kitabu kina nguvu ya Mungu ?kina nguvu inayo weza kubadilihsa  maisha ya mwanadavumu ? Kipimo hiki hakikuwa wazi kama baadhi ya vingine, kipimo hiki kilihusu uwezo wa kitabu adili maisha ya mtu.
   Mana Neno la Mungu li  hai tena lina ngu…Ebr 4 :12. kwa sabau hii  linaweza kutumika .
….kwa mafundisho,na kwa kuwaonya watu makosa yao na kwa kuwaongoza  na kwa kuwaadibisha katika haki….2Tim 3 ;16-17. Mtume Paulo anathibitisha kuwa uwezo wa maandiko yaliyovuviwa kubadili maisha ya watu ulihusika katika kupokelewa kwa maandiko yote.vitabu vingine vilikataliuwa kutokana na kukosa sifa hii.

Kupokelewa kwa kitabu ;je kitabu kimepokelewa n kukubaliwaa watu ambao kwanza kiliandikwa kwaajili yao ?walikitambua kwamba kilitoka kwa Mungu.Chapa na muhuri wa mwisho wa maandiko yewenye mamlaka ni   kukubaliwa kwake na watu wa Mungu ambao kwanza maandiko hayo yalitolewa kwao.Neno la Mungu lililotolewa kupitia nabii wake pamoja na ukweli wake lazima litambuliwe na watu wake walioandikiwa. Katika utaratibu wa kuviingiza vitabu kwenye orodha mababa wa kanisa walitumia kanuni hii.Kwa sababu kama kitabu kilipokelewa,kikakusanywa, na kikatumika kama Neno la Mungu na wale ambao kilitolewa kwao kwanza basi kiliingizwa katika orodha ya vitabu vya Biblia .

Rev.Dr.Erick L M Mponzi
Mkurugenzi  Mkuu
ELAM CHRISTIAN HARVEST SEMINARY
               

No comments:

Post a Comment