Monday 15 December 2014

KIONGOZI WA KIKRISTO

KIONGOZI WA KIKRISTO
KOZI KWANZA
KITABU KWANZA
LCF/HPCC
PO BOX 2407
ARUSHA, TANZANIA
HAKI ZOTE ZIMEHIFADHIWA
Kitabu hiki au sehemu ndogo yake hairihusiwi kutolewa nakala ya aina yeyote bila ya
idhini ya kimaandishi. Hiki kimakala, au sehemu yake hairuhusiwi kutolewa nakala,
kuburuza au kutoa kivuli bila ya idhini maalum ya kimaandishi.
KIONGOZI WA KIKRISTO - Kozi 1 kitabu cha 1
DIBAJI:
Mada ya, Masomo ya kawaida na xnsingi ya Elimu ya Uongozi wa Kikristo
imepuuzwa. Ni miaka ya hivi karibuni tu vyuo vya Kikristo, Seminari na vyuo vikuu
vimeanza kutoa Vitengo vya elimu ya ya uongozi wa Kikristo. Kujihusisha kwangu na
suala kama elimu ya msingi katika mada hii kulikuja nilipojiunga na kitengo cha
maendeleo ya uongozi. Masomo haya yalitolewa na kioneo cha Kikristo lakini
upatikanaji wa vitabu ulikuwa wa mzunguko hivyo ikanifanya nipoteze hamu ya
kusoma. maendeleo ya uongozi tangia nikiwa mtoto katika umisheni kwa
zaidi ya miaka kumi nab-ado nilikuwa na kitu halisi cha kuendeleza uongozi katika
ngazi ya chini.
Miaka michache baadaye nilifurahishwa na maandiko ya Dr. Mxwell. Vitabu vyake
vilikuwa vyenye uvuvio na kutia moyo. Vilikuwa rahisi kuelewa, na vilivyoandikwa
kibiblia. Ndipo nilipoanza kutoa semina kwa viongozi wa kanisa kuanzia ngazi ya
chini na kufuata misingi ya masomo ya kijitabu hiki. Watu waliitikia semina vizuri
sana na hatimaye zikawa sehemu ya mipango endelevu ya mwaka. Nilichukua vitabu
vya Kikristo kwa ajili ya kufundishia lakini nikajikuta navutiwa zaidi na makala za Dr.
John Maxwell.
Nilifurahi pia wakati “EQUIP” taasisi aliyoianzisha na Dr. John C. Maxwell ilianzisha
kinachojulikana kama “Amri ya viongozi Milioni”. Hawa alituma wahitimu
bora(watuwenye kisomo kizuri) kwenda Ulimwenguni kote kufundisha viongozi wa
makanisa. Hawa wakufunzi walitumia vijitabu sita vyenye masomo sita kila kimoja.
Maomo haya yaligusa vema upande wa kiroho na kiutendaji kwa viongozi wa kanisa.
Nasi punde tukaanza kuvijulia hivi vijitabuna kuanza kuvitumia kwa ajili ya mafunzo
ya semina za viongozi ya mwaka na kupanuka kwa nchi zote nne zinazo hudumiwa na
chuo chetu. Sehemu ya makala hiiimetolewa toka mhutasari wa EQUIP wa “Amri ya
viongozi Milioni”. EQUIP ilianzishwa na Dr. John C. Maxwell kusaidia jumuiya ya
Kikristo kukuza stadi za uongozi kwa kufundisha viongozi Uongozi wa Kibiblia. Kwa
maelezo zaidi juu ya “EQUIP” tazama: www.iequip.org
Kipo kijitabu kingine kilichonivutia nilipotazama kwa undani haja ya kutoa
mwongozo sahihi wa elimu ya uongozi wa Kikristo. Kitabu hicho ni “wananukia kama
Kondoo”. Kilichoandikwa na DR. Lynn Anderson. Maelezo yake ya hekima ya
“Uongozi wa Kichungaji” na umuhimu wake kwa Mungu ni mtiririko sahihi wa
maandishi ya Dr. John Maxwell. Anatazama katika moyo wa uongozi wa Kikristo
kama utumishi wa kiroho kwa wengine. Katika hivi vipengele viwili vya uongozi wa
Kikristo umejikita katika maeneo makuu matatu. Maandishi ya Dr. John Maxweel, na
kitabu cha Dr. Lynn Anderson (wananukia kama kondoo) na uzoefu wa miaka 30 wa
kuendeleza viongozi wa makanisa wa nchi za magharibi mwa Afrika toka ngazi ya
hini. Kisehemu cha kwanza mpaka cha nane ni mjumuisho “amaelezo toka kwa Dr.
John Maxwell na uzoefu wangu mwenyewe. Kisehemu cha tisa ni mjumuisho wa
maelezo toka kwa Dri lynn Anderson na uzoefu wangu mwenyewe. Kisehemu cha
kumi ni moja kwa moja toka moyoni mwangu kama ambavyo najitahidi kujua tizamo
wa dunia kwa uongozi wa kanisa ni wa ki-Biblia katika amani na mapenzi ya Mungu.
Ningependa kumshukuru Dr. John C. Maxwell na Dr. Lynn Anderson kwa hekima na
ubunifu wao katika kuandaa masomo yao. Natumai watanisaheme kwa kile
nilichofanya kijulikanacho kama (kunakili) kufanyia kazi mawazo ya mtu mwingine.
Na pia naamini watanisamehe kwa kuungaunga mawazo yao ili yakidhi mafunzo
haya. Ningependa kuwashukuru wafanyakazi wa chuo cha uongozi wa Kikristo kwa
kunisadia kutathimini masomo, kusahihisha makosa yalijitokeza na kukiboresha kwa
kukipitia kama wanafunzi wa kitengo na wafanyakazi wenzangu mnaohusika na
kuendeleza uongozi mzuri wa Kikristo kwa ajili ya ufalme wa Mungu.
Zaidi ya yote natoa shukrani zangu kwa Mungu. Namrudishia utukufu, heshima kwa
lolote na yote yatakayotokana na mwendelezo ya mafunzo ya uongozi wa Kikristo.
Yeye heshima na utukufu ni zake kwa ajili ya kozi hii.
Kwa ajili ya utukufu wake,
Bob Sheffler
Sehemu ya kwanza: JE MUNGU ANAKUITA KUWA KIONGOZI?
Somo la 1: Mungu anatuita kuongoza.
1. Kozi hii ya “Kiongozi wa Kikristo” itakusaidia kupata mäjibu ya maswali
yafuatayo:
Nitajuaje kama mimi ni kiongozi wa Kikristo? Wakristo je, wameitwa kuwa viongozi
au watumishi? Tunawezaje kuwa viongozi na watumishi kwa wakati momoja? Je
mungu anakuita kuwa kiongozi wa Kikristo? Nini ufanye ili kujenga kanisa? Majibu
ya maswali mawili ya mwisho yanatofautiana kwa kila mmoja Wetu- HaYa “a
tufikirie mambo ambayo unayofanya ili kuongoza.
Una nafasi gani ya uongozi kanisani kwa sasa? Labda wewe ni mwalimu wa Biblia,
Shemasi, mzee wa kanisa, kiongozi wa vikundi kama wababa, wamama, vijana wa
kanisa n.k. siyo lazima ushikilie "afasi Ya Uongozi ya juu kanisani, lakini unasadia
katika kazi za kanisa. Orodhesha kazi zote ufanyazo kanisani katika mistari ifuatayo
hapa chini ____________________________________________________________
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
*********************************************************************
2. Kwa hakika hakuna kosa jibu sahihi au kwa swali hapo juu. Kuna mambo mengi
yakufanya kanisani. Kanisa linahitaji misaada yote kadri inavyowezekana. Haijalishi
unafanya kazi moja au nyingi kwa ajili ya kanisa zoote ni njema na muhimu. Na tuna
mshukuru Mungu kwa ajili ya nia yako ya dhati ya kujitoa kusaidia.
Hata hivyo, kwa nini unajitoa kusaidia kanisa? Unasaidia kanisa kwa sababu unataka
kusaidia au ni kwa sababu unatakiwa kusaidia? Unasaidia kanisa kwa sababu
nafurahia kusaidia au kwa sababu unaona ni wajibu wako kufanya hivyo?. zinaweza
kuwepo sababu nyingi za wewe kusaidia kanisa. Hebu kuwa mkweli na andika katika
mistari hapo chini sababu zinazokufanya ulisaidie kanisa. Usiandike kitu ambacho
unafikiri ndilo jibu sahihi. Andika hisia za moyo wako. Kama hujui au huelewi sababu
za wewe kusaidia kanisa basi andika “sijui kinachonifanya kufanya hivyo". Usiogope
kusema ukweli. Hakuna mtu atakaye angalia majibu yako isipokuwa labda kiongozi
wa kikundi chako kuangalia kama umemaliza kazi uliyopewa kuifanya. Ameagizwa
kutokukuhukumu, kukosoa/kutoa mapendekezo au kuwaambia watu kile ulichoandika.
Baadaye katika kozi hii tutakuuliza kuona kama umebadilisha msimamo wako juu ya
kusaidia/kufanya kazi ya kanisa.
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
*********************************************************************
3. Kama kwa sababu fulani Fulani hujisikii vema au kufurahia kazi unayofanya
kulisaidia kanisa, tunaamini kuwa mwisho wa kozi hdii itakuwezesha kuwa na sababu
nzuri ya kufanya kazi unayoifanya, au kukuwezesha kutatua matatizo yanayokufanya
kukosa raha au labda kukuwezesha kupata kazi ya kufanya ili upate furaha katika
nafasi ya uongozi uliyonayo. Kama unafurahiya kazi hiiunayofanya sasa, kozi hii
itakuwezesha kuifanya vizuri kuliko hapo awali na yamkini utapata furaha na
utoshelevu tele katika huduma yako kanisani.
Kichwa cha somo letu la kwanza ni “Mungu anatuita kuongoza". Wakristo wamefanya
midahalo kwa miongo mingi juu kama tumeitwa kuwa watumishi au watawala. Je
uongozi ni wazo la kibiblia? Soma Mw. 1:26 na kcsha jibu swali linalofuata hapa
Chini.
Tuliumbwa kwa mfano na sura ya Mungu na akatupa ______________ dunia.
*********************************************************************
4. Sehemu tu ya mfanano wetu na mungu ni uwezo tuliopewa wa kutawala dunia.
Mungu ametupa wajibu/jukumu la kuwa waangalizi watunzaji wa viumbe vyote
alivyoviumba. Sisi ni zaidi ya mimea na wanyama. Tuna uwezo (stagdtza kazi)
tunaweza kuzitumia katika kutunza mimea na wanyama. Sisi ni waangalizi wa
uumbaji wa Mungu.tuko chini ya mamlaka ya Mungu na hivyo tuna mamlaka juu ya
dunia-yote.
Kama Mungu ametupa kutawala katika uumbaji wake basi hakuna shaka atakuwa
ametupa ________________________ wa kutawala.
*********************************************************************
5. Mungu ametupa mamlaka na uwezo wa kuvitawala uumbaji wake. Mungu
asingelitupa kazi ambayo kwa hakika anajua hatuiwezi. Sasa chukua Biblia yako na
usome Mathayo 5:13-16.
Yesu aliwaambia wanafunzi wake kuwa wao ni chumvi na nuru ya ulimwengu:
(a) chumvi ya itia ______________________ ya chakula.
(b) nuru/mwanga unatuwezesha kuona _________ tunapotembea tusije
tukajikwaa.
*********************************************************************
6. yesu alitumia chumvi na nuru kutufundisha namna ya kuishi. Kamavile ambavyo
chumvi hutia ladha chakula, hali kadhalika maisha yetu yanatia ubora wa kuishi.
Na kama vile nuru/mwanga unavyo mwezesha mtu kuona mahali anapokanyaga akati
wa giza nene, maisha yetu yanatakiwa kuwa nuru ya watu kuishi maisha mema. Soma
tena Mathayo 5:16.
Namna moja tu ya kuwa chumvi na nuru ya ulimwengu ni kwa kuwafanya watu kuona
____________ yetu na __________________ Mungu.
*********************************************************************
7. Wafuasi waaminifu wa Kristo watakuwa kama chumvi na nuru kwa ulimwengu.
watu wataona matendo yao mema na kumsifu Mungu kwa ubora wa maisha Yesu
aliyoletea walimwengu. Tutakuwa na ushawishi kwa ulimwengu kama tutauonyesha
kuwa kuna maisha bora zaidi Ya kuishi.
Yesu aliposema kuwa tunatakiwa kuwa kama csumvi na nuru kwa ulimwengu
alimaanisha kuwa tutakuwa na ____________________ kwa ulimwengu kwa njia ya
matendo mema.
*********************************************************************
8. Yesu alituita ili kuubadilisha ulimwengu kwa njia ya ushawishi wa matendo yetu
mema. Dr. John Maxwell anasema “uongozi ni ushawishi.” Tutajifunza mada hii
katika somo letu lijalo.
Hebu fikiria hili. Kama Yesu anataka wafuasi wake wawe na ushawishi kwa
ulimwengu je, angependa wawe pia viongozi katika ulimwengu huu?
___________________________________.
*********************************************************************
9. Yapo mengi ambayo yanaweza kusemwa katika kalijibu swali hapo juu, lakini
kimsingi tunaweza kusema kuwa, ushawishi ni moja ya funguo za uongozi wenye
mafanikio. Yesu amewaita wakristo wote kuwa ushawishi mzuri ambao unaweza
kupelekea fursa za kiuongozi.
Tunasoma katika Biblia takatifu kuwa, Mungu aliwaita watu Fulani Fulani ili
kuongoza watu wake. Na mara nyingi watu hawa walijihisi wasiofaa au wasioweza
kuongoza. Hata, hivyo Mungu hili halikumzuia Mungu kuwaita kuongoza watu wake.
Mfano mzuri ni Musa. Musa alikulia katika nyumba ya Farao kama mtoto wa binti
Farao. Alifahamu fika utamaduni wa kimisri. Alikuwa ameelimishwa vya kutosha
katika shule za wamisri. Hata na hivyo, alielewa fika kuwa wana wa Israeli ndio
ndugu zake na kabila lake. Siku moja alimuona mnyapara akimpiga vibaya sana
mmoja wa ndugu zake akafika kusaidia ndugu yake na kumpiga mmisri na hatimaye
kumuua. Musa akatoroka kwani alijua kuwa ataadhibiwa vibaya sana kwa kumuua
mmisri. Akaenda kuishi katika nchi ya wamidiani na akichunga kondoo na wachungaji
wengine.
Siku moja Mungu alimwita Musa ili kuwaongoza ndugu zake wana wa Israeli ambao
bado walikuwa watumwa katika nchi ya Misri. Wakati huo Musa alikuwa na umri wa
miaka 80. Alikuwa ameshaoa na kupata watoto. Alikuwa ameridhika na maisha ya
uchungaji wa kondoo. Alitoa sababu za kutotaka kuwaongoza wana wa Israeli. (kut.
3:11)
Musa alijihisi kuwa hana uwezo wa _____________________________________.
*********************************************************************
10. Musa alihisi kuwa Mungu amechagua mtu ambaye si sahihi. Hakuwa kiongozi
aliyetambulika alipokuwa Misri. Alikulia mbali nao na hata alipojaribu kumuokoa
mmoja wa ndugu zake akipigwa na mmisri hawakumheshimu kutokana na hilo (Kut.
2:13- 14) Soma jinsi ambavyo Mungu alimwambia Musa baada ya kulalamika kwake.
(Kut. 3:12)
Je, Musa lijidhania kuwa anastahili kuongoza? _____________________________
*********************************************************************
11. Mungu hakumwambia Musa kufanya kazi peke yake. Alimwahidi kuwa angekuwa
naye katika uongozi wake. Kusema kweli mafanlklo katika uongozi wetu hauji kwa
kutokana na bidii zetu wenyewe' bali Mungu katika kutimiza mapenzi yake
mwenyewe. Tutalielewa hili vema kadri tutakavyokuwa tukijifunza somo hili.
Musa akatoa sababu nyingine kwa nini hawezi kuongoza. Somo (Kut. 3:13).
Musa hakujua ________________________________________ la Mungu.
*********************************************************************
12. Musa hakumjua Mungu vya kutosha kivyo alishindwa kuwaambia jina lake. Musa
kajiona mwenyewe kama kiongozi wa kiroho aliye karibu na Mungu. Hakupata muda
wa kusomea mambo ya theolojia. Hakuwahi kupata muda wa kuomba na kutafakari
mbele za Mungu. Alikuwa mchunga kondoo wa kawaida tu, na mtu aliyeelimika
kutoka katika ukoo wa Yakobo. Somo (Kut. 3:14:15) uone jinsi ambavyo Mungu
alimwambia Musa kutokana na hili.
Mungu alimwambia Musa kuwa yeye ni __________________ Mungu alimwambia
Musa awaambie wana wa Israeli kuwa Mungu wa ____________________________
______________________ amenituma kwenu.
*********************************************************************
13. Jina la Mungu ni “Niko ambaye niko” ikiwa na maana ya kuwa bila ya mwanzo au
mwisho. Hakuna dini nyingine yeyote itakayothubutu kudai kuwa na Mungu kama
huyu. Musa hakuamua kuwa kiongozi wa wana wa Israeli kwa mamlaka yake yeye
mwenyewe, lakini alikuwa ametumwa, ameamuriwa na Mungu wa baba zao, Mungu
wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo. Musa alikuwa ametumwa na Mungu pekee Mungu wa
milele. Musa hakuwa ameshawishika vya kutosha kuwa kiongozi. Soma (Kut. 421-9)
Musa alihofia kuwa wana wa Israeli ______________________ au ______________
kwao na Mungu kuwaongoza. (Kut. 4:1)
********************************************************************
14. Kwa nini wana wa Israeli hawakusikiliza Musa? Kwa nini waamini kuwa Mungu
wa baba zao ndio aliyemtuma kwao? Hizi zilikuwa baadhi ya changamoto
zilizomkabili Musa alipofikiri kuwaongoza wana wa Israeli.
Hata hiVYO Mungu aliahidi kuwafanya waamini kile alichowaambia Musa kwa
kufanya ishara na ___________________ kupitia Musa. (Kut. 4:8-9)
********************************************************************
15. Mungu alimwezesha Musa Kufanya miujizamingi ambayo ilikuwa ishara ya
kuwafanya waisraieli waamini kuwa ametumwa kwao na Mungu. Kama Mungu
ametuita kuongoza basi atatupa na ishara ya kupitita kwetu kuwadhihishia watu kuwa
ametuita kuongoza. Si lazima ishara kii iwe miujiza. Ishara ya Mungu kwa watu
inaweza kuwa ni maamuzi yenye busara ya kiuongozi, mafundisho yenya nguvu au
mahubiri. Mungu anatumia miujiza tu pale ambapo anaone ni lazima au inabidi
kuwashawishi watu kuamini. Musa likuwa na mashaka tele juu ya uwezo wake katika
kuongoza. (Kut 4:10)
Musa alijua kuwa hakuwa na uwezo wa ___________________________________.
********************************************************************
16. Musa hakuweza kujieleza (uwezo wa kushawishi watu). Alikuwa na ulimi mzito
sana. Angewezaje kuongoza watu wakati hakuwa na uzoefu wa kufundisha na
kuhubiri. (Kut. 4:11-12)
Mungu alimwahidi Musa kuwa angemwezesha ku_______ na kwamba ange
_____________________ mambo ya kuzungumza mbele za watu.
********************************************************************
17. Mungu kamwe hatuiti kufanya jambo Fulani bila ya kutupa uwezo wa kulifanya.
Mungu alimwezesha Musa kuongeza/kuzungumza mbele za watu na pia alimfundisha
mambo ya kusema. Kawaida hatujui jambo la kufanya mpaka tumruhusu Mungu
atutumie. Musa alifanya jitihada moja ya kukataa wito wa Mungu. (Soma Kut. 4:13-
16)
Musa alitaka Mungu achague_________________________ wa kumtuma na si yeye.
********************************************************************
18. Mungu anajawabu la kila mwenye udhuru kama Musa. Siyo ajabu Musa hakutaka
kusumbuliwa na matatizo na mahitaji ya ndugu zake wana wa Israeli. Mara nyingi
tumekuwa kama Musa. Mwitikio wetu kwa Mungu anapotuita ni kuwa "mtu
mwingine anaweza kufanya hiyo kazi na si lazima mimi."
Mwitikio wa Mungu ulikuwaje baada ya malalamiko ya Musa? _________________
Nani angemsaidia Musa kuongoza watu wake? ______________________________
********************************************************************
19. Mungu alikuwa na hasira Kwa sababu ya hali aliyokuwa nayo Musa. Hata hivyo
Mungu akaamua kumwita Haruni ndugu yake Musa kumsaidia. Mungu alitenda kazi
kupitia kwa Musa na Haruni kama mkalimani wake. Kwanza wakawashawishi wana
waIsraeli kuwa ulikuwa mpango wa Mungu kwao kwenda katika nchi mpya. Kisha
Milioni wakamshawishi Farao awaruhusu kwenda. Waisraeli wapatao milioni 3
waliachiliwa kutoka katika utumwa wa Misri chini ya uongozi wa Musa.
MARUDIO
a. Yesu anataka sisi tuwe nuru na chumvi ya ulimwengu kwa kuwa na
______________________ juu ya ulimwengu.
b. Mungu anaweza kuwa anakuita kuwa kiongozi katika idara yeyote ile
kanisani.
(1) Kama tunahisi kuwa hatukidhi viwa go basi ni vema kukumbuka
kuwa Mungu amehidi __________ pamoja nasi katika uongozi
wetu siku zote.
(2) kama tunahisi kuwa hatumjui Mungu vyema, tukumbuke
kwamba ___________________ ndiye anayetutuma.
(3) kama tunahisi kuwa watu hawatatufuata, Mungu ameahidi kuwa
atawafanya kutufuata kwa kuwapa I_________________.
(4) kama tunahisi kuwa hatuna stadi za kufanya kile alichotuitia, ni
vema tukakumbua kuwa ________________ ndiye aliyetuumba.
(5) Kama tutakataa wito wake na kudhani kuwa yeyote aweza
kufanya/kuitikia huo wito, basi tujue kuwa tunam___________
Mungu.
Sehemu ya kwanza:
Somo la pili:
JE MUNGU ANAKUITA KUWA KIONGOZI?
Je Mungu anakuita?
1. Kuna tatizo nyeti sana katika kanisa. Watu wengi wamedai kuwa wanataka kuwa
wakristo. Hata hivyo haku makanisa ya kutosha kwa watu hawa wote kwenda
kuabudu. Kuna makanisa mengi Afrika lakini hakuna viongozi wa kutosha kufundisha
hawa watu.
Kutokana na tungo hiyo hapo juu, kanisa la Afrika linakabiliwa na upungufu wa ____
____________________________________________________________________.
*********************************************************************
2. Hitaji kubwa sana la kanisa hapa Afrika ni Uongozi. Ni rahisi kushawishi watu
kumfuata Yesu. Wengi wanataka kumfuata lakini hawajui wanatakiwa kufanya nini.
Wanapohudhuria ibada ya kuabudu, wanaimba, kucheza na kuomba, lakini mara
nyingi hapana anayewaonyesha namna ya kuishi. Wanasikiliza mafundisho na
mahubiri, lakini hapana anayewasaidia kuju namna ya kuyaishi au kuyafanyia kazi
katika maisha yao ya kila siku. Wengine wanavunjwa moyo na kuamua kamwe
kutorudi kanisani.
Kanisa haliwezi kukua na kupevuka mpaka pale watu watakapojitokeza kusaidia.
Unaweza kusema “lakini hakuna mtu aliniomba au kuniteua kufanya hiyo kazi.”
Umeshawahi kuacha kutojali kuwa labda Mungu ananiita nimtumikie? Kulikuwa na
kipindi katika historia ya wana wa Israeli hapakuwepo na mtu yeyote aliyeteuliwa au
kuchaguliwa kuwa kiongozi. (some Amuz 21:25).
Je, wana wa Israeli walifanya nini wakati hapakuwepo na uongozi?_______________
____________________________________________________________________.
*********************************************************************
3. Kila mtu hufanya atakacho ili mradi hapana uongozi. Tatizo kubwa hapa ni
inamwia rahisi adui kuingilia kati na kushika usukani. Wakati huo katika historia ya
wana wa Israeli, Mungu aliwaita baadhi ya whaume kuongoza. Hawakuchanguliwa
na watu. Hawakuwa na vyeo au kufanywa wafalme, lakini waliweza chaguliwa na
watu, kushughulikia matatizo ya watu. Pia waliongoza jeshi la Israeli kukabiliana na
maadui zao. Watu hawa waliitwa WAAMUZI kwa sababu waliweza pia kutatua
matatizo yaliyojitokeza ndani ya jamii nzima ya waisraeli. Kipindi hiki katika historia
kiliitwa kipindi cha waamuzi.
Jambo la kufurahisha kwa waamuzi hapa ni kuwa hawaku ____________ na watu bali
wali _________________ na Mungu.
*********************************************************************
4. Hawa waamuzi hawakuteuliwa na watu bali waliitwa na Munqu kusaidia watu
wake. Hapakuwa na nafasi yeyote ya kugombewa katika uongozi. Hawakuwa na
katiba, jeshi au idara za kiutawala katika kuendesha shughuli za kiserikali.
Hawakukusanya kodi au kutunga sheria. Hawakufuata hata sheria za Musa ambamo
ndani mwake mlikuwa na sheria za kijamii.
Sheria zao zilionekana pale tu kulipotokea tatizo au uhitaji. Mfalme wa Mesopotamia
aliwatesa sana Israeli kwa muda wa miaka nane. Mungu akamuita Othinieli. Othinieli
akaona kuna haja ya kuunda jeshi la kujitolea ndipo alipofanikiwa kukomesha
manyanyaso ya wana wa Israeli toka kwa maadui zao. Kwa muda wa miaka 40 Israeli
wakapata amani ya kudumu. (Amuz. 3:9-11). Othinieli alikuwa ni mwamuzi wa
kwanza,
Baadaye wamoabu wakainuka na kuwatesa wana wa Israeli kwa muda wa miaka 18.
Mungu akamuita Ehudi mtu aliyekuwa akitumia mkono wa kushoto kuifanya kazi
hiyo. Ehudi aliona kuna haja ya kumuua Eglon mfalme wa Moabu. Baada ya kumuua
Eglon aliona vema kuwaunganisha watu pamoja ili kuwafukuza na kuwanyang' anya
waamuzi waliona kuwa kuna _________________ ya kurudisha amani ambayo
ilikuwa imepotea kwa muda mrefu kwa Israeli.
*********************************************************************
5. Wito wetu wa kiuongozi unaweza kuanzia pale tunapoona kuwa kuna uhitaji.
Uhitaji utasabisha shauku mioyoni mwetu kwa ajili ya kufanya jambo. Tunapochukua
hatua ili kukabili uhitaji, wapo watu watakaojitokeza kutusaidia. Hapo ndipo
tupokuwa viongozi.
Kila aliyeitwa kuongoza katika kipindi cha waamuzi, alikuwa na kipawa maalumu
kilichomwezesha kutatua uhitaji wa watu kwa kipindi kile. Debora mwanamke pekee
mwamuzi alikuwa na hekima na uwezo wa kutengeneza mikakati endelevu. Debora
hakushinda vita lakini ulikuwa ni mpango mbinu wake ulishinda vita dhidi ya
wakanaani. Gideoni alikuwa na kipawa cha pekee katika uongozi ambacho alikuwa
hakitumii. Uhitaji ulipotkea aliwapanga watu wake na kuwaongoza vitani dhidi ya
wamidiani.
Kila mwamuzi alikuwa na ___________________________ cha pekee amacho
kilitumika kwa wakati husika.
*********************************************************************
6. Mungu hutuita kuongoza kwa sababu ametupa vipawa maalum kwa ajili ya
kuvitumia wakati wa uhitaji. Wakati mwingine hatujui kuwa tuna vipawa maalum.
Ndiyo maana Mungu anaweza kutoa changamoto kwetu kwa hitaji maalum mahali
ambapo vipawa vyetu vinahitajika. Ni lazima tugundue vipawa vyetu, tuviendeleze na
kutafuta mahali pazuri pa kuvitumia. Tukifanya jambo jema/zuri watu wengine
watatuunga mkono kile tunachofanya. Watajua tunafanya jambo jema na watataka
kusaidia. Kufanya mambo vizuri kunatoa ushawishi kwetu kukubalika kuongoza.
Ndipo tunapofanyika viongozi na kuongoza wengine.
Gideoni alijua fika kuwa Israeli wanashida na wamidiani na hakujisikia kuwa ameitwa
na Mungu kufanya lolote. Mungu alimwambia kuwa anakipawa na hivyo aokoe
jahazi. (soma Amuz 6:14) Baada ya kujaribu na kujua kuwa ujumbe huo ulitoka kwa
Mungu akapata shauku ya kuchukua hatua dhidi ya wamidiani. Shauku kiyo ilimpa
ujasiri wa kumtii Mungu kwa kuharibu vinyago ambavyo familia yake ilikuwa
inafuga. Na huo ukawa mwanzo wa kuongoza kwake.
Gideoni alikuwa na ________________________________ ndani mwake ya kusaidia
watu wa Mungu.
*********************************************************************
7. Tunapoona uhitaji. au tatizo linalohitaji kutatuliwa na tukijua kuwa vipawa tulivyo
navyo vinaweza kutumika katika utatuzi wake tunapata shauku ya ndani kulitatua.
Shauku inaweza kututia moyo katika kufanya maamuzi sahihi juu ya jambo Fulani na
kuchukua hatua. Shauku inaweza kutufanyakuchukua hatua hata kama hatuna
nyenzo/vitendea kazi vyote vinavyohitajika. Waamzi hawakuwa matajiri. Hawakuwa
na mamlaka juu ya watu. Hata hivyo, kila mwamuzi aliokoa taifa la Israeli wakati wa
kipindi chake kwa sababu alikuwa na shauku ya kusaidia.
Kiongozi anapoamua kuchukua hatua kukabili tatizo, huwavutia wengine wanaotiaka
kujiunga katika kusaidia. Wengi kati yaohujisikia shauku lakini wanatafuta kiongozi
ambaye wanaweza kumwamini, kiongozi ambaye anashauku kama wao na amabaye
anaonyesha uwezo wake katika kutatua tatizo. Vilevile kiongozi mzuri anatambua
kuwa hawezi kutatua tatizo mwenyewe hivyo hutafuta msaada wa shati
utakaojutokeza.
Gideoni Aliwavutia manaume na wakaunda jeshi baada ya kuchu hatua dhidi vinyago
vya wamidiani ambavyo familia yake ilikuwa imehodhi. Ehudi avutia watu nakupata
msaada wa kuwafukuza wamaoba baada ya kumuua mfalme wa moabu (Amuz. 3:27-
30)
Kila mwamuzi aliwa _____________________ wengi pale alipaomua kuchukua hatua
kukidhi uhitaji.
*********************************************************************
8. ni baada ya kuchukua hatua kukabili hitaji ndipo wengine huvutiwa (hushawishiwa)
na kujiunga kutoa masaada. Hatuwezi kuonyesha kuwa tunahitaji msaada toka kwa
watu wengine mpaka tuonyeshe kwa dhati (kivitendo) kuwa tunamaanisha. Dr. John
Maxwell anatamka kwa busara kwamba “kila linalozungumziwa hufanyika.”
Linalofundishwa hufanyika. Linalopimwa hufanyika. Linalokadiriwa huganyika.
Linalolengwa hufanyika. Linalotunukiwa hufanyika.
Haitoshi tu kuanzisha jambo, nilazimakulitimiza. Othiniel aliamua kutupilia mbali
mateso ya wakushi/wahabeshi na kudumisha amani iliyokuwa imetoweka kwa miaka
40. Ehudi aliamua kutupilia mbali mateso waliyopata wana wa Israeli toka kwa
wamoabu na kudumisha amani iliyokuwa imetoweka kwa miaka 80. Debora alitoa
mwongozo wa kivitadhidi ya wakanaani na kurudisha amani ya nchi kwa muda wa
kiaka 40. Kideoni hali kadhalika alidumisha amani ya Waisraeli kwa muda wa 40.
Uongozi wao haukuishia pale maadui zao waiposhindwa. Bado palikuwa na kazi
nyingine ya kufanya. Lengi loa lilienda zaidi ya kuwashinda tu maadui zao. Lengo
lao lilikuwa refu sana. Waliihifashi amani ya taida kwa miaka mingi.
Kila mwamuzi alikuwa na ______________________________________ la muda
mrefu kutimiza.
*********************************************************************
9. Tunaweza kuanza mkutano wa "uhitaji au kutatua matatizo", lakini katika uongozi
tunalo lengo refu, kutimiza lengo la muda mrefu. Mungu anatuita kutimiza kusudi au
lengo la muda mrefu kwa kuwa viongozi wa muda mrefu. Mungu anahitaji viongozi
wanaotambua malengo yao ni zaidi ya kukutana katika vikao vya dharura.
MARUDIO
Viongozi hawa hawakuteuliwa au kuchaguliwa na watu. Waliitwa na
Mungu. Tumejifunza mambo matano yanahusu hawa waamuzi.
a. Waliona kuna __________________________ ya kufanya jambo.
b. Walikuwa na ___________________________ vilivyowawezesha
kutatua uhitaji ulijitokeza
c. Waliibua __________________kali ndani ya mioyo yao ili
kutatua uhitaji uliojitokeza
d. Waliwa _____________________________ watu wengine ambao
wangelitoa msaada katika kukabiliana na uhitaji uliojitokeza.
e. Walikuwa na ____________________________ la muda mrefu kutimiza.
MAELEZO YA MTU MMOJA MMOJA KWA AJILI YA MAKUZI
Je, Mungu anakuita kwa ajili ya uhitaji Fulani? Jiulize mwenyewe maswali haya.
A. Ni uhitaji una uona karibu ako ambao hakuna mtu anaye uhangaikia?
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
B. Una kipawa/kipaji gani ambacho unaweza kukitumia kukabili huu uhitaku?
_____________________________________________________________________
Sehemu ya kwanza: JE MUNGU ANAKUITA KUWA KIONGOZI?
Somo la tatu: Je umegundua kipaji/kipawa chako cha msingi?
1. Mungu amempa kila mmoja wetu kipaji na uwezo maalum ambao unaweza
kutumiwa kwa ajili ya ujenzi wa ufalme wa Mungu. Ni muhimu tukatambau na
kufahamu ni mahali gani Mungu anataka tuvitumie hivi vipaji/nipawa mara
tunapocigundua. Lengo na madhumini ya somo hili na lijalo ni kukusaidia kutambua
au kugundua ni kipi kipaji cha msingi kati ya vipaji alivyo kirimiwa na Mungu.
Agano Jipya limeorodhesha vipawa ambavyo Mungu amekirimia/amewapa waty wake
kwa ajili ya kuujenga ufalme wa Mungu:
1 Kor 12:4-11 _________________________________________________________
Ef. 4:11-16 ___________________________________________________________
1 Pt. 4:10-11 __________________________________________________________
Rum. 12:3-8 __________________________________________________________
Unaweza ukawa na baadhi ya hizi karama/vipawa. Hata hivyo kutakuwa na moja
ambayo unaitumia sana katika utendaji wa kazi kuliko nyingine. Kwa lengo na
madhumuni ya masomo na mijadala yetu tunaita hivi/hizi vipawa/karama kipawa cha
msingi. Kipawa/kipaji chako cha msingi ndicho kinachoumua ni eneo gani amalo
Mungu amekuita kutumika. (soma rum. 12:6-8)
Mungu kwa rehema zake amekirimia kila mmoja wetu na ______________ cha
msingi abacho angependa tuvitumie katika Nyanja ya uogozi.
*********************************************************************
2. Kipawa chetu cha msingi ndicho kinachoamua ni eneo gani katika kanisa
tutakalotumika kama viongozi. Mtume Paulo anatumia mwili kama kielelezo cha
vipawa vingi washirika wa kanisa na jinsi ambvyo hivyo vipawa vinapelekea wapi
tutumike katika kanisa. (soma l Kor. 12:l2-16)
Je, tuondoke kanisani kwa kuwa haturuhusiwi kufanya kazi tuitakayo?_____________
_____________________________________________________________________
*********************************************************************
3. Kama vile ambvyo mguu hauwezi kufanya kazi ya mkono, na sikio haliwezi
kufanya kazi ya jicho, vivyo hivyo tusitegemee kufanya kutumika katika eneo ambalo
staidc na vipawa vyetu vya msingi havionekani. Tatizo linaweza kuwa' hatujagundua
vipaji vyetu vya msingi au hatutambui umuhimu wa vipawa vyetu vya msingi.
(soma Kor. l2:17-20)
Mungu amepangilia ndani yetu vipawa vyetu vya msingi _______________ ili
tuvitumie kwa kusudi la kiuongozi.
*********************************************************************
4. Mungu anataka tuchukue wajibu Fulani wa kiuongozi. Ametupa vipawa vyetu vya
msingi amavyo vitatuwezesha kuongoza katika eneo na kazi aliyo tupa. Yapo mambo
tufauti mengi sana ambayo yanahitaji kufanywa katika ufalme wake. Amegawa
vipawa na stadi kwa waumini ili kwamba kila mtu asaidie katika eneo fulani.
(soma 1 Kor. 21:21-26)
Tusifikiri kwamba eneo Fulani kanisani ni _______________________________ sana
kuliko jingine. Lazima tutoe kipaumbele ___________________ kwa kila eneo la
huduma kanisani. Kama eneo moja la huduma litaadhirika, ni dhahiri kuwa ________
mengine yote zitaadhirika. Kama eneo moja limepata heshima basi ni vema na maeneo
mengine yaka ______________ pia.
*********************************************************************
5. Kanisa ni shirika moja. Hivyo linahitaji huduma tofauti nyingi ili kukamilisha lengo
lake. Aina moja ya huduma si vema ikaheshimika sana kuliko nyingine. Lazima tutoe
kipaumbele sawa kwa kila eneo la huduma kanisani. Ni muhimi kama mazingira ya
kanisa yatakuwa safi kama ambavyo ni muhimu kwa mahubiri kuwa yenye nguvu na
msisimko mkubwa. Kama eneo moja la huduma litaadhirika, ni dhahiri kuwa maeneo
mengine yote zitaadhirika. Kama eneo moja limepata heshima ya kipekee basi ni
vema na maeneo mengine yakafurahia. Tunahitaji kuziheshimu na kutilia maanani
huduma nyingine ambazo zimeachwa au zimedharauliwa. Kanisa ni shirika moja
lenye lengo moja. Lengo la kanisa ni nini hasa? (soma Ef. 4:11-13)
Tumepewa karama/vipawa mbalimbali na wito mbalimbali ili kwamba
a. Kuwaandaa watu wa Mungu kwa ajili ya __________________________
b. Kufikia umoja wa _____________________ na _____________________
wa Kristo Yesu.
c. Kuwa _____________________ katika kumfuata Kristo _____________.
*********************************************************************
6. Siwezi kufikiri kazi ya muhimu kufanya kuliko kuwaandaa watu kwa ajili ya
huduma, kuwaleta katika umoja wa imani na maarifaya Yesu na kuwaleta katika kimo
(kukomaa) katika maisha yao ya ukristo. Inahitaji aina zote za vipawa, vipaji, karama
na stadi ili kukamilisha hili. Hakuna awezaye kufanya yote mwenyewe. Hakuna
mwenye vipaji vinavyo hitajika kukamilisha haya yote. Ndiyo maana ni vyema kila
mmoja wetu kudadisi kipawa/kipaji chake cha msingi na kumuuliza Mungu
akuonyeshe wapi anataka tuvitumie kumtumikia. Kila atakachotuitia Mungu kufanya
kitakuwa muhimu na cha maana kwa ajili ya kutimiza kusudi lake.
(soma Rum. 12:3-8)
Lazima tuwe waanglaifu tusije tukajiona sis wenyewe _______________ kuliko
wengine. Kila kipawa/kipaji kina kazi _________________ na kingine.
Vipawa/vipaji vytu vinatofautiana kwa ajili ya ___________________ ya Mungu.
*********************************************************************
7. Kiburi kinaweza kusababisha sisi kujiinua na tukajifikiria wenyewe. Lazima
tukumbuke kuwa kila mmoja wetu ana kipaji msingi cha tofauti ambacho Mungu
ametupa kwa ajili ya kutimiza kusudi lake. Lazima pia tukumbuke kuwa ni kwa
sababu ya neema/rehema za Mungu tumepata hivi vipaji/vipawa. Siyo kwamba
tumePata kwa sababu tunastahili, tumepewa tu.
Soma (Rum. 12:3-8) kisha malizia sentensi zifuatazo:
Kama nina karama ya unabii ninahitaji _______________ sawa na imani yako.
Kama nina karama ya kuhudumu basi ninahitaji _____________________
Kama nina karama ya kufundisha basi ninahitaji _______________________
Kama nina karama ya kutia moyo basi ninahitaji ______________________
Kama nina karama ya utoaji basi ninahitaji____________________________
Kama nina karama ya uognozi basi ninahitaji ______________________
Kama nina karama ya rehema basi ninahitaji _______________________ wengine
*********************************************************************
8. Kila karama ambayo tumepewa, ni vema tukaitumia. Yawezekana Mungu anatuita
kutumika, kufundisha, kutia moyo, kuongoza kwa moyo mkuu au kurehemu. Zipo
karama nyingine zaidi ya hizi. Kila karama ina kusudi tofauti maalum. Iwapao kila
karama itatimiza Kusudi Lake, basi kanisa litaweza kutimiza kusudi lake. Siyo kazi
yetu kuamua karama ipi ni bora, bali ni wajibu wetu kutimiza kusudi la karama ya
msingi ambayo Mungu ametupa kwa rehema.
Viongozi wengi wana karama au vipawa vingi. Tunaweza kuita seti ya vipawa au
karama. Hata hivyo haikosi kimoja kitakuwa na nguvu kuliko vingine. Hii karama au
kipawa cha msingi kinakuwa kama dira ya huduma au uongozi wetu. Hii seti ya
karama au vipawa itakuwa na ushawishi kulingana namna tunavyoongoza. Kwa mfano
kiongozi anaweza kuwa na kipawa au karama ya msingi ya kufundisha/ualimu.
Anaweza pia kuwa na karama ya kiutawala na karama ya kurehemu. Karama nyingine
zitashawishi jinsi anavyofundisha na mada anazofundisha. Haijalishi ana nafasi gani
ya uongozi, lazima kufundisha kuwemo.
Mungu anatuita kuongoza sambamba na kutumia ___________________ yetu ya
msingi.
*********************************************************************
9. Ni jambo la muhimu sana kwetu sisi kujua ni kipi kipwa au karama yetu ya msingi.
Kama hatuitumii katika nafasi ya uongozi tuliyonayo, tutakuwa hatutimizi kusudi la
Mungu la kutupa kipaji, kipawa au karama. (soma 1Pt. 4:8-ll) ili kugundua namna
nyingine za kutathmini kama tunatumia vema karama ya msingi ili kutimiza
kusudi la Mungu.
Karama tuliyopewa na Mungu itatimiza kusudi lake kama
tutaitumiakatika:
a. ____________________ wengine.
b. Kuongoz _________________________ la Mungu.
c. Kunena neno la ______________________.
d. Kumpa Mungu ______________________ kupitia Yesu Kristo.
*********************************************************************
10. kusudi la karma ya msingi ni kujenga kanisa la Mungu. Hii
ina maana kuwatumikia wengine, kuonyesha rehema za Mungu,
kulinena neon la Mungu na kumletea Mungu utukufu. Kama hii karama
haitumuki namna hii, John Maxweli anasema tunajiibia wenyewe kwa
kuwa kinyume na mapenzi ya Mungu. Tuliibia kanisa faida za karama
zake Mungu na utukufu anaostahili.
Yamkini hujui ipi ni karama yako ya msingi. Inaweza
kukuchukua muda kuja kutambua karama yako ya msingi. Yafuatayo
ni baadhi ya mambo yatakayokuwezesha kujua/kutambua karama yako
ya msingi.
a. Soma haya zifuatazo kama zinavyoorodhesha baadhi ya karama za msingi
na ujiulize kama unazijua vema au kuzitíçndea kazi. (lKor. 12:4-11, Ef.
4:11-16, 1Pt. 4:10-11, Rum. 12:3-8)
b. Tafuta nafasi ya kusaidia kanisani. Jaribu kufanya kazi kadha wa kadha
kanisani na ungalie zipi una zifanya vizuri.
c. Mambo gani umewahi kufanya kanisani na ukasikia kuridhika, burudiko la
moyo na furaha moyoni?
d. Kazi zipi ulizofanya kanisani na matokeo yake yakawa mazuri?
e. Mambo yapi ambayo wazee wa kanisa, viongozi, na watu wazima kiimani
wanasema unayafanya vizuri?
Nini kusudi la jumla kwa karama ya msingi atupayo Mungu? ____________________
_____________________________________________________________________
_____________________________________________________________________
Sehemu ya kwanza: JE MUNGU ANAKUITA KUWA KIONGOZI?
Somo la nne: Nyenzo ya kugundua vipaji/karama
Hili siyo jaribio. Hakuna kosa au jibi sahihi. Tunakuomba uonyeshe tu ukweli juu ya
uzoefu wako na mambo unayopendelea Hizi dhana zinazokuhusu zitakuonyesha
karama ulizonazo. Zipo tungo 72 katika kurasa mbili zifuatazo ambazo unatakiwa
uzijibu. Utatumia namba ‘0’ (sofuri) mpaka 4 kubainisha namna ambavyo kila moja
inakuelezea. Utaandika majibu yako katika sehemu ya majibu iliyo katika ukurasa wa
tatu baada ya hizi zifuatazo mbili. Pata hata dakika moja kuangalia kwa makini hiki
kisehemu cha majibu katika ukurasa unaofuata. Chunguza tungo ambazo zimepewa
namba 1 mpaka 72. hapa ndipo utakapo andika namba zako. Baada ya kuangalia hiyo
kazi katika ukurasa ufuatao, rudi tena ukurasa huu uendelee kusoma maelekezo haya.
Unatakiwa kutumia namba O hadi 4 kubainisha jinsi zinavyoelezea wasifu wako.
Kama tungo inakuelezea vizuri sana, utaandika namba 4 juu ya mstari katika hiyo
tungo. Kama tungo inakuelezea vizuri, utaandika namba 3 juu ya mstari katika hiyo
utaandika namba 1 juu ya nstaru wa tungo. Na kama tungo haikuelezei kwa vyocyote
unatakiwa kuandika namba 0 juu ya mstari katitka huyo tungo. Namba 4 inaonyesha
kuwa tungo inakuelezea vizuri sana wakati namba 0 inaonyesha kuwa tungo
kaikuelezei kwa vyovyote. Namba numingine 3 mpaka 1 zinaonyesha uko kati ya
“vizui sana na hakuna” kama inacyoonyesha hapo juu. Kama sehemu tu ya tungo
mjoa inakuelezea vizuri sana na nyingine ya tungi hiyi hiyo inakuele kwa liasi au
kidogo au hakuna kabisa basi unatakiwa ukuandikie namba ndogo ilimradi isiwe to 0.
Sofuri (0) siyo namba mabaya wala 4 siyo namba nzuri. Namba hizi zinaonyesha tu
karama/kipaji ambacho Mungu amekupa. Hatua ya kwanza katika ugunduzi wa huu
mtiririko ni kuandika namba juu ya karatasi ya kazi kwa kila moja ya hizi tungo 72
zifuatazo. baada ya kuandika namba kwa kila tungo, utakuta maelezo katika hatua ya
pili tatu, nne na tano chini kabisa mw kazi hii. Ni lazima uandike namba juu ya mstari
katika kila moja ya kizi tungo 72 kabla ya kwenda hatua ya pili, tatu, nne na tano.
Jitahidid utumie si chini ya saa moja kumaliza hatua zote tano.
Sasa fungua ukurasa unaofuata kufanya hatua ya kwanza.
TUNGO ZA KUGUNDUA VIPAJI/VIPAWA
__ 1. Najisikia vizuri kufanya kazi kinyume na sehemu ambayo inanihusu, mara
nyingi hujishughulisha na mambo madogomadogo.
__ 2. Mara nyingine najitokeza mbele ya kikundi na kuchukua uongozi pale
ninapoona hakuna kiongozi.
__ 3. Ninapokuwa katika kikundi mar azote nawatambua wale wanaojiona wapweke
nakuwasaidia ili wajisikie kama sehemu ya kikundi.
__ 4. Nina uwezo wa kugundua uhitaji na kuutafutia uvumbuzi bila ya kujali
ukubwa au udogo wake.
__ 5. Nina uwezo wa kugundua mawazo, watu na miradi kufidia lengo Fulani.
__ 6. Mara nyingi watu husema kuwa ninauwezo wa suluhu au maamuzi mazuri ya
kiroho.
__ 7. Ni ujasiri sana wa kufikia mambo makubwa kwa utufufu wa Mungu.
__ 8. Nafurahia kuwapa pesa wale wenya matatizo/uhitaji mkubwa.
__ 9. Nafurahia kuhudumia watu katika maeneo ya hospitalini, magareza ili kuwatia
moyo.
__ 10. Mara nyingi nina upeo mkubwa wa kutoa majawaby ya papo kwa hapo juu ya
matatizo magumu.
__ 11. Nafurahia kushauri na kutia moyo wale waliovunjwa/vunjika moyo.
__ 12. Nuna uwezo wa kusoma kwa makini kifungu cha maandiko na kushirikisha
wendine baada ya kusoma.
__ 13. Saa hivi nina simamia makuzi ya kiroho ya kijana/vijana wa kikristo.
__ 14. Watu wananiheshimu kama mtu mwenye mamlaka katika mambo ya kiroho.
__ 15. Nina uwezo wa kujifunza lugha nyingi.
__ 16. Mara nyingi Mungy ananifunulia mwelekeo ambao anataka mwili wa Kristo
uchukue.
__ 17. Napendelea kuanzisha mahusiano na wasio aminin kwa kusudi la kuwaambia
habari za Yesu.
__ 18. Nina sikia kwamba kuna uhutaki nasikia nasukumwa kuombea hali hiyo.
__ 19. Ningependa kuwasaidia viongozi wa kanisa ili mtizamo walenge katika kutoa
vipaumbele ysa huduma zao.
__ 20. Ninapowaomba watu wanisaidie katika huduma nyeti kanisani mar azote
hukubali.
__ 21. Nafurahia kupokea na kuhudumia wageni na kuwafanya wakisikie nyumbani
kila mara wanapotutembelea.
__ 22. Natafuta nafasi kutumika kanisani na nafurahia kuwatumikia wendine.
__ 23. Mimi ni mtu wa mipango, mwenye ketengeneza mikakati na ktimiza malengo.
__ 24. Niko makini katika kukosoa mwendendo na nina uwezo wa kuona hata tatizo
dogo la kiroho.
__ 25. Mara nyingi naweza kujitokeza na kuthubutu na kuanzisha mradi ambao wengi
hawawezi na kufanikiwa.
__ 26. Siku zote natoa kwa furaha pesa zangu zaidi ya zaka kanisani.
__ 27. naweonea huruma sana watu walioumizwa na wapweke, na ninapata muda wa
kutosha kuwa nao nikiwatia moyo.
__ 28. Mungu ameniwezesha kuchagua kwa makini mambo kadha wa kadha
yanayohitaji maamuzi makini wakati hapana mtu mwingine awezaye.
__ 29. Nijisikia kutoshelezwa ninapo watia moyo wengine mathalani inapokuwa ni
juu ya kukua kwao kiroho.
__ 30. nafarahia kujifunza juu ya maswala magumu yatokanayo na neno la Mungu.
__ 31. Nafurahia kujihusisha na maisha ya watu na kuwasaidia kukua kiroho.
__ 32. Napenda na nafurahia kuanzisha kanisa.
__ 33. Nina uwezo wa kujifunza utamaduni, lugha na mfumo wowote wa maisha
tofauti na ya kwangu na ningependa kutumia uwezo huo kuhudumia watu wa
makabila mengine.
__ 34. Siku zote nitazinena kanuni za Kikristo kwa nguvu hata kama hazija zoeleka.
__ 35. Naona rahiis kumwalika mtu yeyote kumbali Kristo kama Mwokozi.
__ 36. Nina shauku kubwa sana ya kuomba kwa ajili ya mambo muhimu ya ufalme
wa Mungu na mapenzi yake kwa wakristo.
__ 37. Napendelea kuwaapumzisha wengine ili wakamilishe shughuuli za miradi
vema.
__ 38. Naweza kuelekeza na kumotisha katika kukamilisha malengo Fulani.
__ 39. Napendelea kukutana na watu wageni na kuwatambulisha katika kikundi.
__ 40. Mimi ni wa kutegemewa sana kuhakikisha mambo yamefanyika kwa wakati
uliokusudiwa na sipendi kusifiwa au kushukuriwa.
__ 41. Ni mwepesi wa kugawa majukumu muhumu sana kwa wengine.
__ 42. Ninaweza kutofautisha kati ta jema na baya katika maswala magumu ya kiroho
wakati wengine hawajui hata wapi pa kaunzia.
__ 43. Ninamwamini Mungu kwa uaminifu kwa maisha mazuri mbeleni hata kama
ninakabiliana na matatizo magumu ya kiroho.
__ 44. Sijali kushusha hali yangu maisha kwa ajili ya kanisa na watu wengine wenye
uhitaji.
__ 45. ninataka kufanya kila niwezalo kwa ajili ya wenye uhitaji wanaonizunguka
hata kama nin kwa kutoa chochote.
__ 46. Mara nyingi watu huomba ushauri wangu wanapokuwa hawajui lakufanya
katika kukabiliana na matatizo.
__ 47. Ninajisidia vema kutoa changamoto kwa wengine ili kufanya bora kiviwango
hususani katika makuzi yao kiroho katika kuwatia na siyo kuwavunja moyo.
__ 48. Watu hupenda kusikiliza mafundisho yangu ya Biblia mara ninapofundisha.
__ 49. Najali sana wengine wanapokuwa kitaka vita vya kiroho na nashauri na kutoa
mwongozo wa maisha mazuri ya kimungu.
__ 50. Ninakubalika kama kiongozi wa kiroho sehemy mbalimbali nchini au duniani
kote.
__ 51. Ningependa kuihubiri injili kwa lugha isiyo yangu, nan chi za kigeni.
__ 52. Nasikia uhitaji wa kunena ujumbe wa kibiblia ili kwamba watu wanjue mambo
ambayo Mungu anataka kutoka kwao.
__ 53. Npenda kuwaambia wengine namna ya kuwa mkristo na kuwaalika kumkubali
Kriso kama mwokozi.
__ 54. Mengi kati ya maombi niliyomwomba Mungu kwa ajili yawengine
yamejibiwa.
__ 55. Nafurahia kuwasaidia wengine katika kukamilisha kazi zao na sihitaji
katambulika na watu kwa sababu hiyo.
__ 56. Watu wanaheshimu mawazo yangu na hufuata maelekezo yangu.
__ 57. ningependa kujitolea nymba yangu kutumika na wengi wanaokuja kwa ajili ya
kanisa.
__ 58. Napendelea kwasaidia watu bila kajali aina ya ugitaji na najisikia utoshelevu
katitka kufanya hivyo.
__ 59. Najisikia vema kufanya maamuzi muhimu kata katika shinikizo kubwa.
__ 60. Watu hunijia kwa ajili ya kuomba msaada wa kiroho katika kutofautisha kweli
na lisilo la kweli.
__ 61. Nafanyika kazi imani yangu kwa njia ya maombi na Mungu hunijibu kwa njia
ya ajabu.
__ 62. Ninapompa mtu pesa sitegemei kulipwa chochote, na huwa sitaki watu wajue
kuwa ni mimi niliyempa.
__ 63. Ninaposikia watu ambao hawana kazi na ambao hawawezi kulipia nahitaji
muhimi ya maisha nafanya namna kuwasaidia.
__ 64. Mungu huniwezesha kufanya matumizi sahihi ya kweli ya kibiblia katika
maisha halisi ya mwili.
__ 65. Mwitikio WA watu ninapowatia moyo kuwa sawa kwa ajili ya Mungu siku
zote huwa mzuri.
__ 66. Huwa Nina mwelekeo sahihi na makini wenye mtiririko mzuri
ninapowaandalia watu somo la Biblia.
__ 67. Nina wasaidia wakristo wanaotangatanga mbali na Mungu ili kumrudia Bwana
na kukuza uhusiano nye pamoja na washirika katika kanisa analoabudu.
__ 68. Ningefurahia kushiriki injili na kuunda vikundi vipya vya kikristo maeneo
ambayo hakuna makanisa mengi.
__ 69. Mimi sina ubaguzi wa rangi, kabila au urasimu na nina moyo wa shukrani kwa
watu wenye msimamo tafauti na mimi.
__ 70. Ninajisikia rahisa kuzikiri na kujitamkia ahadi zote za kibiblia na kuzitumia
kila inapoitwa leo na niko tayari kuzitafuta kwa moyo mkuu kama ikibidi.
__ 71. Ninashauku kubwa kusaidia wasio wakristo ili na wao waweze kupata wokovu
kwa njia ya Yesu Kristo.
__ 72. Maombi ndiyo huduma chaguo langu la kwanza kanisani na mara nyingi
Napata muda mwingi wa kuomba.
KARATASI LA KUGUNDULIA VIPAJI/KARAMA
HATUA YA KWANZA: Chagua namba tutoka ‘0’ hadi 4 kwa ajili ya kila moja ya
tungo zilizo katika ukurasa uliopita. Andika namba yako juu ya mstari katika kujibu
kila moja ya tungo zifuatazo.
0 = hainielezei
1 = inanielezea kidogo
2 = inanaielezea kwa kiasi
3 = inanielezea vizuri
4 = inanaielezea vizuri sana
KAULI JUMLA ZAWADI
1. ______ 19. _____ 37. _____ 55. _____ _____ A. ________
2. ______ 20. _____ 38. _____ 56. _____ _____ B. ________
3. ______ 21. _____ 39. _____ 57. _____ _____ C. ________
4. ______ 22. _____ 40. _____ 58. _____ _____ D. ________
5. ______ 23. _____ 41. _____ 59. _____ _____ E. ________
6. ______ 24. _____ 42. _____ 60. _____ _____ F. ________
7. ______ 25. _____ 43. _____ 61. _____ _____ G. ________
8. ______ 26. _____ 44. _____ 62. _____ _____ H. ________
9. ______ 27. _____ 45. _____ 63. _____ _____ I. ________
10. _____ 28. _____ 46. _____ 64. _____ _____ J. ________
11. _____ 29. _____ 47. _____ 65. _____ _____ K. ________
12. _____ 30. _____ 48. _____ 66. _____ _____ L. ________
13. _____ 31. _____ 49. _____ 67. _____ _____ M. ________
14. _____ 32. _____ 50. _____ 68. _____ _____ N. ________
15. _____ 33. _____ 51. _____ 69. _____ _____ O. ________
16. _____ 34. _____ 52. _____ 70. _____ _____ P. ________
17. _____ 35. _____ 53. _____ 71. _____ _____ Q. ________
18. _____ 19. _____ 54. _____ 72. _____ _____ R ________
HATUA YA PILI: Jumlisha safu ulalo zote na andika juby lake kwenya msafa ya
jamla. Mfano jumlisha namba zote ulizoandika kwenye tungo ya 1, 19, 37, na 55.
Hii tunaiita safu ‘a’ andika jibu ulilipata toka safu ‘A’ mbele ya heryfi ‘A’. Fanya
hivyo kwa safu mpaka ya ‘R’.
HATUA YA TATU: Tafuta alama zako za juu sana. Zungushia duara jerufi
iliyapembeni mwa alama zako za juu. Kama umepata alama 4 au 5 kama alama za juu
basi zungushia duara herufi zilizo karibu na alama zako. Usingushie zaidi ya mara
tano.
HATUA YA NNE: Angalia ukurasa unaofuata yaani 31 utaona vipawa/karama 18
ambazo zimbepewa herufi ‘A’ mpaka ‘R’ kama kwenye karatasi ya maswali hapo juu.
Angalia alama zako za juu za kwanza kasha linganisha na herufi kwenye ukurasa wa
31 na 32. Andika kiyo karama mbele ya herufi ya kwenye karatasi la majibu. Mfano
kama ‘A’ ndiyo mojawapo ya alama zako za juu, basi andika neno MISAADA juu ua
mstari baada ya herufi ‘A’.
Ugundizi wako: Alam zako za juu zinaonyesha karama.vipaji ulivyo navyo. Alama
ya juu zaidi kuliko nyingine bila shaka ndiyo karama yako ya msingi. hilo ndilo eneo
ambalo utakuwa na mafanikio zaidi katika uongozi. Unaweza ukawa na karama za
msingi mbili, lakini huwezi kuwa na tatu.
HATUA YA TANO: Sasa andika karam nyingine zilizobaki kwenye karatasi ya
majibu kila moja mahali pake.
Ugundizi wako: Alama zako za chini ni maeneo ambayo hatafanya vizuri katika
uongozi.
UFUNGUO WA KARAMA: (A-R) ufafanuzi wake na rejea ya maandiko matakatifu.
Hii orodha ya ufafanuzi na rejea za maandiko matakatifu ya kukusaidia, yanalandana
na kitabiea na tungo 72 zilizoelezewa hapo nyuma katika zoezi la kugundua vipaji. hii
sio orodha ya vipawa/karama hasa. Ni Njia mojawapo ya kafahamu karama/vipawa
tunavyoona kwenye biblie takatifu.
A. Misaaada – uwezo wa kiotendaji na kusaidia wengine katika jitihada zao
kiuongozi. Mk 15:40-41, Mdo 9:36, Rum 16:1-2, 1 Kor 12:28
B. Uongozi – uwezo wa kushawishi wengine ili wakuunge mkono katika kutimiza
lengo, kusudi au mkakati. Rum 12:8, 1 Tim 3:1-2, 1 Tim 5:17, Ebr 13:17
C. Ukarimu – uwezo wa kufanya watu wajisikie nyumbani, wanajaliwa, na sehemu
ya kundi. Mdo 16:14-15, Rum 12:13, Rum 16:23, Ebr 13:1-2, 1 Pt 4:9.
D. Huduma – uwezo katabua na kutatua kivitendo mahitaji ya wendine. Mdo 6:1-7,
Rum 12:7, Gal 6:10, 2 Tim 1:16-18, Tit 3:14
E. Utawala – uwezo wa kuratibu na kusimamia watu na miradi. Lk 14:28-30, Mdo
6:1-7, 1 Kor 12:28
F. Utambuzi – uwezo wa Kun’amua/ujuzi wa kuamua kama matendo ya mtu
yanatokana na mungu, shetani au wanadamu. Mt 16:21-23, Mdo 5:1-11, 16:16-
18, 1 Kor 12:10, 1 Yn 4:1-6
G. Imani – uwezo wa kumwamini Mungu kwa ujasiri wa vitu visivyoonekana kwa
macho ya nuama na kwa makuzi ya kiroho, kwa mapenzi ya Mungu. Mdo 11:22-
24, Rum 4:18-21, 1 Kor 12:9, Ebr sura ya 11.
H. Utoaji – uwezo wa mtu wa kutoa kwa moyo na ukarimu mali zake kwa ajili ya
kazi ya Mungu. Mk 12:41-44, Rum 12:8, 2 Kor 8:1-7, 9:2-7.
I. Rehema – uwezo wa dhati wa kuwa na rehema masamaha, huruma kwa namna
ambayo mtu anaweza kujisikia kufunguliwa kutokana na maumivu, uchungu na
masumbuko haraka. Mt 9:35-36, Mk 9:41, Rum 12:8, 1 Th 5:14.
J. Hekima – uwezo wa kutambua ufahamu wa Kristo no kutumia kweli ya
kimaandiko kwa ajili ya mazingira Fulani Fulani ili kufanya maamuzi sahihi na
kuwasaidia wengine kuchukua mwelekeo sahihi
K. Maonyo – uwezo wa mtu kutia moto, kukaripia, au kukemea bila kukwaza
wengine hata yamkini hao wanao karipiwa. Mdo 18:22, Rum 12:8, 1 Tim 4:13,
Ebr 10:24-25
L. Kufundisha – uwezo wa kutumia kweli ya kibiblia kwa kupandikiza maarifa yenye
mantiki Fulani aliyonayo mtu kwa njia na utaratibu fasaha. Mdo 18:24-28, 20:20-
21, 1 Kor 12:28, Ef 4:11-14.
M. Uchungaji – uwezo wa kuchukua na kusimamia makuzi yakiroho na pamoja na
Jumuiya ya kikristo ya waaminio. Yn. 10:1-18, Ef 4:11-14, 1 Tim 3:1-7,
1 Pt 5:1-3
N. Mpanzi wa Kanisa – uwezo wa Kuanzisha huduma, na kutoa uongozi wa kiroho
kwa makanisa yapatikanayo kama mazao ya kizi huduma. Mdo 15:22-35, 1 Kor
12:28, 2 Kor 12:2, Gal 2:7-10, Ef 4:11-14.
O. Umisheni – uwezo wa kuhudumu ipasavyo katika tamaduni nyingine zaidi yaw a
kwako ulio nao. Mdo 8:4, Mdo 13:2-3, Mdo 22:21, Rum 10:15.
P. Tahadhari – uwezo wa kiujasiri katika kunena/kutangaza kweli ya Mungu katika
kuwalita kwenye haki bila kujali kitakacho tokea. Mdo 2:37-40, 7:51-53, 26:24-
29, 1 Kor. 14:1-4, 1 Th 1:5.
Q. Uinjilisti – uwezo wa kushirikisha watu wengine habari njema za Yesu Kristo
kwa namna ambayo wesioamini hutubu na kuokoka/kuongoka. Mdo 8:5-6, 8:26-
40, 14:21, 21:8 na Ef 4:11-14.
R. Maombezi – uwezo wa kuomba/kuombea jambo kwa muda mrefu na kwa
malengo ukitengemea kupokea majibu yake. Kol 1:9-12, 4:12-13, Yak 5:14-16.
JIANDAE KWA MAJADILIANO
Angalia tena udhuru wa Musa alioutoka kwa Mungu katika (kut. Sura ya 3 na 4). Je,
ni udhuru gani unaoutoa kwa Mungu ili usichukue jukumu la uongozi na unafikiri
mwitikia wa Mungu utakuwa nini?

No comments:

Post a Comment