Friday 5 December 2014

KUJIZIDISHA KIROHO

STRATEGIC IMPACT
SHULE YA
KUZIDISHA VIONGOZI ©
Q1
Somo la 1-10
v1.2.0 (2012)
STRATEGIC IMPACT
S.L.P. 78640
DAR ES SALAAM, TANZANIA
© Copyright, Strategic Impact. Usifanye mabadiriko yoyote kwenye masomo haya
isipokuwa unaruhusiwa kutoa nakala na kuwagawia wengine.
STRATEGIC IMPACT
P.O. BOX 830337
RICHARDSON, TX 75083
WWW.TOUCHINGEVERYNATION.COM
© Copyright, Strategic Impact. No changes may be made to this manual, but you
may freely copy and distribute without making changes to content.
2
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI - SOMO LA 1-10
YALIYOMO
! Utangulizi! 4
! Mapitio ya SI ! 6
! Hatua 10 Za Kuanzisha Mtembeo Wa Wanafaunzi ili Kulifikia Taifa Lako ! 8
" Taarifa Za Vikundi Vidogo Vidogo ! 11
! Jedwari La Maandiko Ya Kusoma ! 12
! Fomu Ya Mahudhurio ! 14
! Maswali Ya Uwajibikaji ! 15
" Ushuhudiaji - Kumbukumbu Ya Watu Walioshuhudiwa Injili " 16
" Somo la 1 - Kujiendeleza Binafsi: “Msingi wa Neno la Mungu”! 20
" Somo la 2 - Kujiendeleza Katika Uongozi: “Uongozi Ni Nini?”! 22
" Somo la 3 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua ya 1: Badili Mtazamo Wako”! 24
" NYENZO: Kuanzisha Na Kusimamia Seli (kanisa la nyumbani)" 27
" Somo la 4 - Kujiendeleza Binafsi: “Maombi Ya Mfano”! 30
" Somo la 5 - Kujiendeleza Katika Uongozi: “Kiongozi Ni Nani”! 34
" Somo la 6 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua ya 2: Maombi”! 36
" Somo la 7 - Kujiendeleza Binafsi: “Kutembea Katika Roho”! 40
" Somo la 8 - Kujiendeleza Katika Uongozi: “Tabia: Sifa Muhimu Kwa Kiongozi”! 44
" Somo la 9 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua ya 3: Eleza Maono Ya Kuzidisha Wanafunzi”! 46
" Somo la 10 - Kujiendeleza Binafsi: “Timiza Wajibu Wako Katika Familia”! 50
" Q1 Kujikumbusha Dhana Muhimu" 56
" Q1 Mambo Ya kuzingatia Kwa Waliomaliza Mafunzo Hatua Ya 1 " 57
" Ramani ya Huduma “Ministry Map”" 58
" ZANA: SI Kiperperushi Cha Uinjilisti v4.0" 62
" Maelezo Ya Ukumbusho ! 66
" Strategic Impact Msimamo Wa Imani! 70
" Maelezo Ya Mwanzo na marekebisho Ya Sasa! 72
3
UTANGULIZI
Msukumo wa maono ya SI ni kuandaa viongozi watakofundisha viongozi wengine, ili
kuongeza wanafunzi ambao watapanda makanisa yatakayojaa wanafunzi
yatakayojizidisha, Injili inapohubiriwa kwa watu wote duniani kanuni na maadili ya
ufalme wa Mungu vinadhihirika kupitia maisha ya watu katika jamii.
Mafunzo ya kuandaa viongozi na wanafunzi endelevu havitokei kutokana na matukio.
Ili kuwa kiongozi wa Kiungu atakayeendeleza viongozi wengine ni mchakato wa muda
mrefu. Pia inahusisha kujifunza, maombi na utii kwa Mungu. Inahitaji nidhamu binafsi
na kumtegemea Roho Mtakatifu. Hali hii inatokea vizuri katika jamii kutokana na
mahusiano, kutiwa moyo na uwajibikaji wa pamoja.
Kitabu cha Matendo ya Mitume katika agano jipya kinaonyesha furaha ya kupanuka
kwa ufalme wa Mungu katika karne ya kwanza. Kitabu hiki kinafunua matendo ya
Roho Mtakatifu kupitia watu wa Mungu Yerusalemu, Yudea, Samaria na miisho ya nchi
(Matendo 1:18) Waamini hawa walipopeleka ujumbe wa Injili kwa ulimwengu tunaona
muundo wa kanisa linaloendelea. Kwanza, tunaona kanisa la Yerusalemu , Matendo
1-7, kisha kanisa la Antiokia (Matendo 11-13) hatimaye kanisa la wa mataifa ambalo
Paulo alilipanda (Matendo 14-20).
Moja ya makanisa yanayonifurahisha sana ni kanisa la Efeso. Wakati Paulo alipokuwa
Efeso, Matendo 19:9-10 Inaonyesha jinsi Paulo alivyowakusanya wanafunzi na
kuzungumza nao kila siku akiwafundisha kwenye ukumbi wa Tirano (Tyrannus).
Jambo hili liliendelea kwa muda wa miaka miwili na kupelekea Wayahudi wote na
Wayunani walioishi katika jimbo la Asia kusikia Neno la Bwana. Kupitia shule ya
Tirano, Paulo aliandaa wanafunzi wengi ambao walienda kupanda makanisa
yaliyojizidisha katika jimbo lote la Rumi huko Asia, matokeo yake ni kwamba kila mtu
aliyekaa katika eneo hilo alisikia Injili. Hili ni jambo la kufurahisha.
Mmoja wa wanafunzi waliokuwa wanajizidisha ni Epafra. Alikuwa Mkristo na
alifundishwa na Paulo kule Efeso. Baadae alisafiri kwenda mji wa Kolosai kule Asia
(Inasemekana huo ndio mji aliotoka). Alifanya uinjilisti na kufungua makanisa jirani na
miji ya Hierapolis na Laodekia (Wakolosai 1:6-7; 2:1; 4:12-13). Tunaelewa kutokana na
maandiko haya kwamba Paulo alikuwa bado hajafika kwenye hiyo miji (Wakolosai
2:11), hata hivyo makanisa yalikuwa yamepandwa kutokana na huduma yake kule
Efeso.
Maandiko pia yanaonyesha kwamba baadhi ya watu ambao waliamini na kulelewa
(kufundishwa) kupitia huduma ya Paulo kule Efeso walisafiri kwenda Rumi na
kuanzisha makanisa (Warumi 16:5 inamtaja Epaineto (Epenetus) ambaye alikuwa ni
muongofu wa kwanza ambaye Paulo alikuwa naye kule Asia)
4
Agizo kuu ambalo lilitolewa na Yesu na mfano wa Shule ya Tirano (Tyrannas) kule
Efeso ni msingi wa shule ya kuzidisha viongozi ambayo iko mikononi mwetu leo.
Vitendea kazi ulivyonavyo mkononi mwako ni matokeo ya kuhudhuria kongamano la
viongozi (Leadership Thrust). Tunaomba kwa Mungu kwamba atumie mafunzo haya
kukutia moyo unapokuwa kiroho na kujifunza ujuzi wa uongozi. Umesikia na kujifunza
hatua kumi (10) za kuzidisha viongozi ili kulifikia Taifa au Nchi yako kwa injili. Pia
tunaamini kwamba umemuona Mungu akikutumia wewe pamoja na watu wengine
katika kuwaleta wengine kwa Yesu na kuanzisha makanisa katika jamii.
Kukua na kuendelea kwako katika eneo hili bado hakujakamilika. Ni muhimu sote
tukajitoa na kuendelea ili kukua zaidi katika eneo hili. Kuhudhuria kongamano la
viongozi (LEADERSHIP THRUST) ilikuwa ni mwanzo tu. Ni muhimu sana kuendelea na
mchakato wa kukua na kuzidisha viongozi. Masomo nane yafuatayo yametengenezwa
ili kutia mkazo mafundisho uliyoyapata kwenye kongamano la viongozi (Leadership
Thrust), na kupanua masomo.
Masomo haya yametengenezwa kulenga maeneo makubwa matatu:
1. Kukua kiroho na kujiendeleza binafsi
2. Ujuzi katika uongozi
3. Upandaji wa makanisa
Kila somo linakamilika kwa muda wa wiki moja. Mafunzo ya masomo kumi
yametengenezwa ili kukamilika kwa muda wa robo mwaka. Ili kuweza kuhitimu hatua
ya kwanza na kuweza kuruhusiwa kuendelea na hatua inayofuata, unapaswa kutimiza
mambo yafuatayo.
1. Kukutana kila wiki na wanafunzi wengine kwenye kikundi kitakachobadiri
maisha yako ili kujadiliana juu ya maswali 10 ya uwajibikaji.
2. Kukamirisha mambo ya kufanya kila wiki kwa muda wako kulingana na
mikutano ya kikundi chako.
3. Washirikishe injili watu 10 hadi 30 wasiomjua Kristo
4. Anzisha kanisa la nyumbani (seli) kuanzia na watu 2 hadi 10.
Mungu akubariki kwa kadri unavyoendelea kufuatilia masomo haya na kumtumikia
Mungu kwa kutimiza Agizo Kuu.
Wako, Timu ya Uongozi - Strategic Impact
5
“Kuwawezesha Wazawa kuyafikia Mataifa Yao”
MAONO (VISION):
Maono ya Strategic Impact ni kushirikiana na Mungu Roho Mtakatifu
ili kuwapa nafasi watu wote Billion 7 waliiopo hai dunuaini leo ili
kusikia injili ya Yesu kristo, kwa kuanzisha mtembeo wa upandaji
wa makanisa yatakayojizidisha katika kila jamii iliyopo duniani
kupitia nyenzo ya Kuandaa viongozi watakaojizidisha..
LENGO (MISSION):
Ni kuandaa viongozi watakaozidisha wanafunzi
watakaoanzisha mtembeo wa upandaji wa makanisa
kwa kila kundi la watu ili kutimiza Agizo Kuu.
“Yesu akaja kwao, akasema nao, akawaambia, nimepewa mamlaka yote
Mbinguni na Duniani. Basi, enendeni, mkawafanye Mataifa yote kuwa
wanafunzi mkiwabatiza kwa jina la Baba na Mwana na Roho Mtakatifu;
na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; natazama, mimi
nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”.
" " " " " " " " " Mathayo 28:18-20
MKAKATI (STRATEGY):
Kuandaa wanafunzi watakaopanda makanisa yatakayojizidisha
katika kila Miji Mikuu katika nchi 12 kubwa Duniani.
“Lakini wengine wakakaidi, wakakataa kuamini, wakiitukana ile Njia
mbele ya mkutano; basi, akaondoka akawaacha, akawatenga wanafunzi,
akahojiana na watu kila siku katika darasa ya mtu mmoja, jina lake
Tirano. Mambo haya yakaendelea kwa muda wa miaka miwili, hata wote
waliokaa Asia wakalisikia neno la Bwana, Wayahudi kwa Wayunani.
! ! ! ! ! ! ! ! ! Matendo 19:9-10
6
MCHAKATO (PROCESS):
I. SEMINA YA KUELEZEA MAONO (VISION SEMINAR VS): - Ni semina ya siku
moja inayotolewa kwa wachungaji na viongozi wa kikristo katika eneo. Semina hii
itambulisha huduma ya Strategic Impact na kutoa mfano wa mafunzo yanayotolewa
katika maeneo matatu yenye msisitizo:
" " 1. Kujiendeleza kiroho kwa mtu binafsi
" " 2. Ujuzi wa uongozi
" " 3. Mkakati wa upandaji wa makanisa
II. KONGAMANO LA VIONGOZI (LEADERSHIP THRUST - LT) - Ni mafunzo ya
wiki moja yanayotolewa kwa viongozi 50 wanaoalikwa. Hawa ni viongozi na
wachungaji waliojitoa kutimiza Agizo Kuu. Mafundisho yanatolewa kwa kina kwa
kugusa maeneo matatu yenye msisistizo yakiambatana na maelekezo mengine
yanayotokana na uzoefu wa mchakato wa upandaji wa makanisa.
III. SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI (SML) - Ni mafunzo ya miaka miwili , ya
kibiblia yanayotekelezeka na yanayotoa fursa ya kujiendeleza katika maeneo matatu
yenye msisitizo. Yanayomuwezesha kiongozi kuwajibika na kuzidisha viongozi.
• Mahusiano - Kila mshiriki anakutana na watu wengine katika kikundi cha
watu watatu au wanne kwa ajili ya kuwajibika na kutiana moyo.
• Unaweza kujifunza mwenyewe - Kama unaweza kusoma, unaweza
kuongoza ingawa kila eneo litakuwa na mratibu atakayehakikisha
kwamba mambo yanakwenda.
• Uinjlisti - Mara moja kwa wiki kila mshiriki anawajibika kuipeleka injili
• Muhimu - Mshiriki hatakiwi kwenda hatua nyingine kabla ya kumaliza
mafunzo ya hatua ya kwanza (ya robo mwaka) na kuyatekeleza.
• Kitakachoendelea - Mafunzo yameandaliwa kwa ajili ya kujifunza, kwa
vipindi vya robo mwaka (Miaka miwili, miezi mitatu), kwa kutoa vipindi 10
kwa kila robo mwaka, jumla viitakuwa vipindi 90.
• Kujizidisha - Washiriki wanapoendelea kwenda hatua ya pili ya robo
mwaka ya mafunzo, kila kiongozi anatakiwa atafute watu angalau wawili ili
kuanza mafunzo ya muhura wa kwanza. Kila kiongozi anayeandaliwa
anatakiwa kutimiza sifa hizo ili kuendelea na mafunzo ya kipindi cha pili.
• Expansion - Wakati mchakato huu unaendelea viongozi wanaodaka
maono haya watakwenda katika miji mingine ili kuendeleza mkakati
IV. KONGAMANO LA KUCHOCHEANA (FAN THE FLAME- FTFC) - Huu ni
mkutano wa mwaka wa watenda kazi wa SI, viongozi wengine wanaojizidisha kwa ajili
ya kutoa taarifa, kujadiliana, kutiana moyo, kuwezeshwa na kupanga mikakati ya kila
nchi kuufikia ulimwengu.
7
HATUA 10 ZA KUANZISHA MTEMBEO WA
KUZIDISHA WANAFUNZI ILI KUFIKIA TAIFA LAKO (V2.1)
! HATUA YA 1: BADILISHA MTAZAMO WAKO
! BADILI MTAZAMO WAKO kutoka lengo la kujenga kanisa
! langu, waza juu ya kuifikia jamii iliyopotea → nchi
! →ulimwengu.”
! (Mathayo 28:18-20; Matendo 1:8; Matendo 20:24)
! HATUA YA 2: MAOMBI!
! OMBA kwa ajili ya watenda kazi kwa ajili ya mavuno!
! (Luka 10:2; Matendo 13:1-3)
! HATUA YA 3: ELEZA MAONO!
! Washirikishe maono watu wa Mungu ili kulifikia eneo lako.
kwa maombi ! (Matendo 1:8; 13:1-3)
! HATUA YA 4: KUSANYA NA ANDAA TIMU
! Tambua, chagua, kusanya na andaa timu ya watu wawili
! watakaojizidisha kila mwaka. (Matendo 14:21-28;
! 19:9-10; Wakolosai 1:7; 2 Timotheo 2:2)
! HATUA YA 5: SELECT A SITE
! Kwa njia ya maombi chagua eneo au watu utakaowafikia
! kwa injili. (Matendo 16:6-40)
! ! ! A. Tafuta kujua Roho Mtakatifu anakuongoza
! ! ! ! wapi ili kuanzisha kanisa
! ! ! B. Fanya utafiti wa mahitaji, ngome na
! ! ! ! shughuli zinazoendelea katika eneo
! ! ! ! zinazoweza kuathiri kanisa jipya.
8
! HATUA YA 6: UINJILISTI
! Fanya uinjilisti katika eneo ulilolichagua.
! (Matendo 5:42; 14:21,25; 20:20)
! HATUA YA 7: WAFUNDISHE WAAMINI WAPYA
! Wafundishe waongofu wapya kwenye kikundi cha watu
! wawili au watatu. ! ! (Matendo 14:22; 20:20)
" HATUA YA 8: WAKUSANYE WAONGOFU WAPYA
! Wakusanye waongofu wapya pamoja kwa ajilli ya:
! ! ! A. Ukaribisho na ushirika,
! ! ! B. Kuabudu na maombi,
! ! ! C. Kujifunza Neno la Mungu,
! ! ! D. Kufanya kazi na kushuhudia.
! (Matendo 2:42,46; 12:12; 16:40; Warumi 16:15;
! 1 Wakorintho 16:19, Walosai 4:15)
! HATUA YA 9: KUZIDISHA WANAFUNZI
! Kuzidisha wanafunzi Katika kanisa jipya kwa kurudia
! hatua nane za kwanza. (1 Wathesalonike 1:7-8)
! HATUA YA 10: KUUNGANISHA MIKONO
! ! ! PAMOJA NA KUZINDUA MTEMBEO
! Unganisha mikono pamoja na wachungaji/ viongozi ili
! kuzindua mtembeo wa kuzidisha wanafunzi ili kutimiza.
Agizo Kuu
9
10
MRATIBU WA SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI
JINA: ______________________________________ SIMU: ______________________
MAJINA YA WANAFUNZI WENZANGU KWENYE KIKUNDI
JINA: ______________________________________ SIMU: ______________________
JINA: ______________________________________ SIMU: ______________________
JINA: ______________________________________ SIMU: ______________________
JINA: ______________________________________ SIMU: ______________________
MIKUTANO YETU INAFANYIKA:
MAHALI: ________________________________________________________________
SIKU: ______________________________ MUDA: ______________________
MAANDIKO YA KUSOMA KILA SIKU:
Chapters of Scripture each day: __________________
Starting in (book of Scripture): _________________________________________
11
KUMBUKUMBU YA MAANDIKO NINAYOSOMA KILA SIKU:
TAREHE Maandiko TAREHE Maandiko
12
TAREHE Maandiko TAREHE Maandiko
13
TAARIFA YA MAHUDHURIO YA WANAKIKUNDI:
TAREHE WALIOHUDHURIA
14
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
MASWALI YA UWAJIBIKAJI*
MASWALI HAYA YANALENGA KUSAIDIA WANAKIKUNDI KUKUA KATIKA TABIA NA KUUNGAMA
DHAMBI. YANATAKIWA YAULIZWE NA KUJIBIWA KWA UAMNIFU, KWA NEEMA NA USIRI. JAMBO
LOLOTE LITAKALOZUNGUMZWA KWENYE KIKUNDI NI SIRI LISITOKE NJE.
1. Je umekuwa katika upendo na ushirika na Kristo wiki hili? Kwa namna
gani?
2. Je umekamilisha kusoma mafungu ya maandiko uliyotakiwa kusoma wiki
hili? Mungu amesema nini na wewe? (mkubaliane maandiko ya kusoma
wiki ijayo, msichague mafungu mengine ya kusoma hadi kila mmoja
wenu awe amemaliza kusoma mafungu mliyokubaliana mwanzo)
3. Je umemsikiliza, umemtii na kumtegemea Roho Mtakatifu wiki hii ili
kufanya mambo ambayo Mungu anataka ufanye? Kwa namna gani?
4. Je umesoma ama kutazama picha za ngono wiki hili?
5. Je umekosa uaminifu katika eneo la fedha wiki hili au umetamani kitu
kisicho chako?
6. Je umetembea katika upendo kwenye mahusiano yako na watu wengine
katika familia, marafiki, majirani na washirika wenzako?
7. Je umekuwa na hasira na kutosamehe? Je kuna mtu yeyote uliyemdhuru
(kumuumiza) Kwa maneno yako wiki hili?
8. Je umekuwa shahidi mzuri wiki hii juu ya ukuu wa Yesu Kristo kwa njia
ya maneno yako na matendo, je nani umeongea naye habari za Yesu?
9. Je umetimiza kipengele cha mambo ya kufanya wiki hii? Je ni kitu gani
kikubwa ulichojifunza? Je ni changamoto gani kubwa uliyokabiliana
nayo? Kwa nini?
10.Je umekuwa mkweli katika maelezo uliyoyatoa?
*ADAPTED FROM “LIFE TRANSFORMATION GROUPS”, PUBLISHED BY CHURCH MULTIPLICATION ASSOCIATES
15
USHUHUDIAJI - KUMBUKUMBU YA WATU WALIOSHUHUDIWA INJILI
Tarehe Jina Matokeo Kifuatacho
1
2
3
4
5
6
7
8
9
10
11
12
13
14
15
16
Tarehe Jina Matokeo Kifuatacho
16
17
18
19
20
21
22
23
24
25
26
27
28
28
29
30
17
18
SOMO
19
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 1 - KUJIENDELEZA BINAFSI
“MSINGI WA NENO LA MUNGU”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Katika maisha kuna maamuzi machache yatakayoamua namna utakavyoyatoa maisha
yako na muda wa kuwa na Mungu pekee yako kila siku, ili kukutana naye kupitia Neno
lake. Daudi ambaye aliupendeza moyo wa Mungu alikuwa na shauku na ushirika na
Neno la Mungu. Zaburi 119 inaeleza kujitoa kwake na mahusiano yake na maandiko.
Angalia mahusiano ya Mfalme Daudi na Neno la Mungu
Soma mistari ifuatayo na kwa maneno yako mwenyewe jibu maswali yanayofuata:
" “Kwa moyo wangu wote nimekutafuta,
! usiniache nipotee mbali na maaagizo yako” [Zaburi 119:10]
“Roho yangu imepondeka kwa kutamani
! hukumu zako kila wakati.” [Zaburi 119:20]
“Sheria yako naipenda mno ajabu!
! ndiyo kutafajkari kwangu mchana kutwa.” [Zaburi 119:97]
SWALI LA KUJADILIANA: Ni kwa njia zipi Daudi alionyesha kuwa na NJAA ya Neno la
! Mungu?
Someni maandiko yafuatayo kwa pamoja:
! “Kama sheria yako isingalikuwa furaha yangu,
! hapo ningalipotea katika taabu zangu.” [Zaburi 119:92]
“Sheria ya kinywa chako ni njema kwangu,
! kuliko maelfu ya dhahabu na fedha.” [Zaburi 119:72]
“Na mikono yangu nitayainulia maagizo yako niliyoyapenda,
! nami nitazitafakari amri zako.” [Zaburi 119:48]
SWALI LA KUJADILIANA: Daudi alikuwa na mtazamo gani juu ya Neno la Mungu?
Someni tena mistari ifuatayo kwa pamoja:
! “Wana amani nyingi waipendao sheria yako,
! wala hawana la kuwakwaza.” [Zaburi 119:165]
20
“Moyoni mwangu nimeliweka neno llako,
! nisije nikakutenda dhambi.” [Zaburi 119:11]
“Hii ndiyo faraja yangu katika tabu yangu,
! ya kwamba ahadi yako imenihuisha.” [Zaburi 119:50]
SWALI LA KUJADILIANA: Ni faida zipi ambazo daudi alizipata kutoka kwenye Neno la
! Mungu?
" Washirikishe wengine kwenye kikundi faida uliyoipata kutoka kwenye Neno la
! Mungu katika maisha yako.
DHANA MUHIMU: VIONGOZI WA KIKRISTO LAZIMA WAJITOE KILA SIKU
! KUMTAFUTA BWANA KWENYE NENO LAKE.
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Je unaweza kujitoa leo kwa asilimia mia moja kutenga muda wa kusoma
" Neno la Mungu kila siku? Andika namna utakavyojitoa kwa Bwana:
Siku ya 2: Lini utatenga muda kila siku wa kumtafuta Bwana katika Neno lake?
" Panga muda huo kwenye ratiba yako ya kila siku.
Siku ya 3: Ni muda gani ambao umeupanga kumtafuta Bwana kila siku kwenye
" Neno lake? Mahali pa kila siku, nyumbani, ofisini au mahali pengine popote
" patakapokusaidia kujenga tabia hii.
Siku ya 4: Ni jinsi gani utatumia muda wako kila siku kumtafuta Bwana katika Neno
" lake? Utatafuta utaratibu gani au mpango gani wa kusoma na kujifunza Biblia?
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
21
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 2 - KUJIENDELEZA KIUONGOZI
“UONGOZI NI NINI?”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Wanawake na wanaume wengi wamepewa kipawa na Mungu cha kuongoza lakini
hawautendei kazi ule uwezo wa kuongoza. Kama unataka kutimiza makusudi ya
Mungu katika maisha yako, unatakiwa ukuze uwezo wako wa uongozi. Hebu
tuchukue muda sasa tujifunze asili ya uongozi. Swali muhimu ni hili:
UONGOZI NI NINI?
Tafsiri rahisi ni hii: Uongozi ni Kuhamasisha watu ili kutimiza malengo. Kuna
Nyanja tatu za uongozi. Ya kwanza, uongozi ni uhamasishaji. Ya pili uongozi
unahusisha kuhamasisha watu. Ya tatu, uongozi unahusisha kusudi. Uongozi ni
kuhamasisha watu kwa ajili ya kutimiza lengo lililo wazi.
SWALI LA KUJADILIANA: Mwelezee kiongozi ambaye amekuhamasisha wewe. Ni jinsi
! gani amekuhamasisha? Ni kitu gani alichosema ama alichotenda
! kilichokuhamasisha?
Kama huwezi kuwahamasisha wengine kukufuata, hivyo wewe siyo kiongozi! Lakini
uongozi sio tu kuhamasisha watu. Kuna watu wengi wanaoweza kuhamasisha
wengine. Pia kumekuwa na viongozi wengi katika historia ambao wamewashawishi
watu kwa mambo maovu.
SWALI LA KUJADILIANA: Je unaweza kutoa mifano ya viongozi katika historia ambao
! wamewashawishi watu kwa ubinafsi au kwa mambo maovu? Je unaweza kutoa
! mifano ya viongozi ambao wamewashawishi watu kwa mambo mazuri na ya
! Kiungu?
Kama kiongozi wa Kiungu, unatakiwa pia uwe na lengo lililo wazi kwenye akili ambalo
linatoka kwa Mungu na linatimiza mapenzi ya Mungu duniani. Lengo hili linakuja
kutokana na maono yaliyo wazi ambayo Mungu amekuitia kutimiza. Kwa namna
nyingine, kila kiongozi wa Kiungu ana lengo kama hili- Kutimiza Agizo Kuu. Hata hivyo,
maono yako na lengo lako vitakuwa ni njia maalumu ya kutimiza wito wako hapa
duniani. Ili Kutimiza lengo hili kunahitaji malengo, muda na kutafakari kwa umakini.
22
SWALI LA KUJADILIANA: Je ni lengo gani ambalo Mungu anakuitia kutimiza wakati huu
! ! katika eneo lako? Je lengo hili linalingana na mpango mzima wa Mungu wa
! kutimiza Agizo Kuu? [Mathayo 28:18-20]
DHANA MUHIMU:
" Kama huwezi KUHAMASISHA watu wewe huna UONGOZI..
" Kama huna WAFUASI ama watu huna UONGOZI.
" Kama huwezi KUTIMIZA LENGO huna UONGOZI ndani yako.
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Fikiri juu ya mambo ambayo viongozi wamekuhamasisha wewe ili
" kutenda. Andika sifa mbalimbali za muhamasishaji mzuri:
Je ni mambo gani unategemea kufanya ili kukuza sifa hizi kwa ajili ya kukusaidia
kuhamasisha wengine?
Siku ya 2: Je ni aina gani ya watu ambao Mungu amekuita wewe kuwaongoza?
Kwa nini wewe uwe kiongozi wao?
Tathmini kama hao watu wanakufuata kwa hiyari au la. Je ni namna gani
utawahamasisha zaidi ili kukufuata?
Siku ya 3 and 4: Tumia siku mbili zijazo kwa ajili ya kuomba na kumuuliza Mungu
" ili akupe lengo la wazi kutoka kwake ambalo anataka kulitimiza kwa muda huu
" mahali hapa. Andika kwa kifupi, na kwa uwazi malengo yako: _______________
" ________________________________________________________________
" ________________________________________________________________
" Tathmini lengo hili. Je liko kwenye mstari wa Mungu wa kutimiza Agizo Kuu?
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
23
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 3 - UPANDAJI WA MAKANISA
“HATUA YA 1: BADILI MTAZAMO WAKO”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Ukisoma kwa uangalifu tena kwa kurudia na kujifunza Agano Jipya, hutaona mahali
ambapo kuna maagizo ya mambo ambayo Wachungaji na viongozi katika makanisa
wanayoyafanya. Ingawa baadhi ya wachungaji wana shauku ya kutimiza mambo fulani
lakini siyo yale ambayo Bwana ameyaagiza. Je ni shauku gani ambayo viongozi
wanayo? Ni kujenga kanisa kubwa. Lakini Yesu hajawahi kumuita mtu yeyote
kujenga kanisa kubwa kwa ajili ya Mungu. Ukweli ni kwamba hakuna hata agizo la
kupanda kanisa. Je si kweli kwamba wengi tunaomtumikia Mungu tunatafuta kufanya
mambo haya? Tumepokea malengo yasiyo sahihi. Mara nyingi tumetafsiri mtu kuwa
na kanisa kubwa ni kuwa na watu wengi, labda kuwa na ratiba nyingi, bajeti kubwa,
kuwa na sifa kubwa katika jamii. Hebu tuwe wazi katika jambo hili, kanisa la namna hii
ndiyo laweza kuonekana kuwa kubwa machoni pa Mungu au la. Vivyo hivyo kanisa
dogo lenye programu chache linaweza lisionekane kubwa pia machoni pa Mungu.
Jambo muhimu hapa si ukubwa wa jengo au ukubwa wa programu nzuri. Bali ni
kanisa kutimiza kusudi la msingi la kimungu. Msukumo wa kutafuta kuwa na kanisa
kubwa kwa kujilinganisha na makanisa mengine si jambo ambalo Bwana alilikusudia.
Kaka zangu na dada zangu, lazima tubadilishe mtazamo wetu juu ya mambo ambayo
Mungu ametuita kutimiza.
SWALI LA KUJADILIANA: Je ni mkandamizo gani uliojisikia wa kutaka kujenga kanisa
! kubwa kwa ajili ya Mungu?
Kama Yesu hakutuita kujenga kanisa kubwa ama kupanda kanisa, sasa tumeitwa
kufanya nini? Yesu ametoa agizo lililo wazi “tunatakiwa kwenda kuwafanya mataifa
kuwa wanafunzi wake . . .” Mathayo 28:19. Hili ndilo Agizo Kuu kutoka kwa Yesu
lengo letu la msingi ni kuipeleka injili kwa jirani zetu, vijijini, kwenye miji, kwa mataifa
na ulimwengu, ili kuwapata wengi katika imani ya kristo, kuwafundisha na kuwalea
kisha kuwatuma kwenda kuuzidisha ufalme wa Mungu. Huu ndiyo mfano tunaouona
kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume. Mitume na wanafunzi walieneza injili
ulimwenguni kote. Matokeo yake makanisa yalianzishwa, yalikua na yakajizidisha
(Matendo 6:1, 7; 9:31; 19:10). Kwa hiyo mkazo haukuwa kupanda makanisa bali
kuwafanya mataifa kuwa wanafunzi. Walipofanya hivyo kuzidishwa kwa makanisa
24
kulikuja kama matokeo ya kutii Agizo Kuu. Hii ndiyo tofauti muhimu. Malengo yetu sio
kujenga makanisa makubwa lakini wanafunzi watakao jizidisha. Tunapotunza lengo hili
kwenye akili, makanisa mazuri na yenye afya yatajizidisha.
SWALI LA KUJADILIANA: Je ni mabadiliko gani unayoweza kufanya kwenye huduma
! yako ili kutia mkazo wa kutengeneza wanafunzi wataojizidisha (badala) ya
! kujenga kanisa kubwa?
Unaposoma Agano Jipya tunakuta kanisa rahisi. Muundo wake ulikuwa rahisi,
uliotengeneza mazingira ya kujizidisha. Kanisa liliongozwa na viongozi waliokomaa
(1Timotheo 3, Tito 4:2-6) na liliongozwa na viongoz waliokomaa na walifanya ibada
rahisi, walihudumiana na kushuhudia wengine (angalia 1 Wakorintho 14, Wakolosai
3:15-17; 4:2-6). Kiongozi mmoja wa kanisa anasema kwamba Makanisa katika Agano
Jipya yalitia mkazo katika maeneo matatu:
" " 1) Ushirika wa kweli na Mungu ,
" " 2) Kuwapenda na kuwatumikia wengine katika makanisa,
" " 3) Kushuhudia ulimwengu.1
Lakini kanisa la leo limejaa mkanganyiko. Miundo yetu na utendaji kazi wetu unaathiri
kuwaendeleza waamini ili kuwa wanafunzi wanaojizidisha jambo ambalo ndilo lengo
kuu la kanisa. Tuwekeze nguvu zetu kwa watu wengine kwa ajili ya yale wanayoweza
kutenda.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni mambo gani tunayoweza kufanya ili kuyafanya makanisa
! yetu yawe rahisi na kutekeleza mambo matatu yaliyopo juu?
Kwa hiyo, fursa na mtazamo wetu lazima ubadilike kutoka kujenga kanisa kubwa na
iwe kuzidisha wanafunzi. Ni lazima tumaanishe katika kutengeneza wanafunzi ambao
hawataridhika kuona tu watu wanahudhuria ibada bali wazae na matunda na
kujizidisha. Kanuni ya shughuli za kanisa ni hii kama jambo mnalotaka kufanya
halilengi kuzidisha wanafunzi usilifanye.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni mambo gani yanayofanyika kwenye kanisa, huduma
! ambayo yanamsababisha mshirika wa kawaida kushindwa kuzaa matunda? Kwa
! nini unadhani jambo hilo ni kizuizi cha kuzidisha wanafunzi?
25
DHANA MUHIMU: WITO WETU SIYO KUJENGA KANISA KUBWA BALI NI
! KUWAFANYA WANAFUNZI KUWA WENGI..
Unapofikiri na kupitia somo hili, tathmini huduma ya kanisa lako na ujibu maswali
yafuatayo.
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Pitia shughuli za huduma yako za mwezi mmoja uliopita na ujibu
" maswali yafuatayo kwa uaminifu. Je waweza kueleza lengo la msingi na juhudi
" yako kama mchungaji/kiongozi ni:
" " Kujenga kanisa kubwa?" " Kuzidisha wanafunzi?
" Kwa nini umetoa jibu ulilotoa?
Siku ya 2: Je kuna mambo gani au ratiba gani inayoendelea kanisani kwako
" inayokuzuia wewe kutumia fursa ya kuandaa wanafunzi watakao jizidisha?
Siku ya 3: Je ni ratiba gani au shughuli gani ambazo Bwana anakuongoza
" kuziondoa au kuzibadilisha katika kanisa lako ili kutengeneza muundo wa kanisa
" utakaotimiza Agizo Kuu?
Siku ya 4: Soma Nyenzo ya kuanzisha Seli Mpya. Ni nani ambaye umekuwa
" ukimshuhudia habari za Yesu ambaye unaweza kuanza naye seli? Mtaanza
" kukutana lini? Na wapi?
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
1Neil Cole, Organic Church, Chapter 8.
26
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
NYENZO: NAMNA YA KUANZISHA NA KUONGOZA CELL
(KANISA LA NYUMBANI) V1.2
Tukibadili mtazamo wetu juu ya huduma, malengo yetu sasa yanakuwa kuzidisha
wanafunzi ambao nao watasababisha makanisa kuongezeka.
Hitaji letu katika hatua ya kwanza ya shule ya kuzidisha viongozi ni kuanzisha seli
(Kanisa la Nyumbani) kwa kuanzia na watu wawili (2) na wasiozidi kumi (10). Seli hii
ihusishe mambo muhimu yanayohitajika kwenye ibada katika kanisa:
Waamini huwa wanakutana pamoja kwa ajili ya:
" A. Kuleana na kujifunza pamoja katika imani (UKARIBISHO)
" B. Kukua katika maarifa ya Mungu na Neno lake. (KUABUDU/NENO)
" C. Kutumika na kuwashirikisha wengine juu ya imani. (KAZI/USHUHUDIAJI)
Katika Muhula huu utakapofanya uinjilisti, wengine wataikubali Injili ya Kristo wengine
watakuwa na shauku ya kutaka Kujua zaidi habari za Kristo kabla hawajachukua
hatua ya kumwamini ili kupokea wokovu. Wengine watasema ndiyo na kumwamini
kama Mwokozi wao na kupokea uzima wa milele. Utakutana na wengine ambao ni
wakristo tayari lakini hawaendi kuabudu mahali popote na wala hawakui katika
uongozi.
Haijalishi watu utakaokutana nao wako kiwango gani katika uhusiano wao na Kristo
waombe uanze nao seli (Kanisa la nyumbani). Nyenzo zifuatazo zitakusaidia
kuongoza seli mtakapoanza kukutana na unapowasaidia waamini wapya kukua katika
imani ndani ya Kristo.
Panga muda na mahali ambapo mtakuwa mnakutana kama SelI. Inaweza ikawa
kwenye nyumba ya mtu, ofisini, kwenye maegesho ya magari, shuleni au sehemu
yoyote mtakayoona inawafaa. Fanyeni mawasiliano na makubaliano ya siku na muda
wa kukutana.
A. Watu wakiisha kusanyika kwenye Seli, wakaribishe ili kila mmoja aweze kujieleza
" anaendeleaje.
1. Kama una watu wapya kwenye Seli waombe wajitambulishe. Uliza maswali
" ambayo yatasaidia watu kufahamiana vizuri.
2. Baada ya kusanyiko la kwanza, hakikisha kwamba unauliza maswali mfano
" " “Je umemwona Mungu akifanya kazi kwenye maisha yako na kukutumia
" " kwa ajili ya wengine wiki iliyopita? Waulize kila mmoja wametimizaje
" " maswali namba 5 na namba 6 yaliyopo hapo chini.
3. Hakikisheni kwamba mnaombeana.
27
MUHIMU: Msiende kwenye mafungu mengine ya maandiko mpaka kila mmoja
ametii kutenda yale mliyokubaliana wiki iliyopita. Usiwafundishe watu ili tu
wapate maarifa bali wafundishe kwa sababu wanatii maelekezo.
B. Tumieni Muda wa kutosha kumwabudu Mungu.
" Ombeni na kumshukuru Bwana kwa jinsi alivyo na kwa yale aliyoyafanya. Kama
" " ikiwezekana imbeni nyimbo rahisi za kusifu na kuabudu. Mpiga vyombo vya
" " muziki apige ili watu wajifunze na kushiriki.
C. Mjadili sura ya kwenye Biblia (Maandiko yaliyo orodheshwa hapo chini kwenye
" kipengele D). Maneno ya Mungu, kwa kutumia maswali sita:
Mmoja asome kwa sauti wakati wengine wanasikiliza huku wakifuatilia kwenye
Biblia zao. Uliza maswali mawili kisha waruhusu watu wayajadili.:
" 1. Ni kitu gani ulicho kipenda kwenye habari hii tuliyosoma?
2. Ni kitu gani ambacho hukukipenda au kilikuchanganya kwenye habari hii?
Baada ya majadiliano mtu mmoja asome maandiko kwa sauti kisha jadilianeni
maswali mawili yanayofuata:
3. Ni kitu gani ulicho jifunza kuhusu watu walioko kwenye habari hii?
4. Umejifunza nini kuhusu Mungu?
Baada ya muda wa majadiliano, mtu mmoja asome maandiko kwa mara ya tatu
kisha jadilianeni maswali mawili yanayofuata:
5. Kutokana na mwangaza wa habari hii maisha yako yatakuaje wiki hii?
! ! (Weka kumbukumbu ya majibu ya watu na waulize maswali kwenye
" " kipindi cha majadiliano kitakachofuata wiki ijayo wakati wa ukaribisho).
6. Je kuna mtu unaye mfahamu anaye taka kujua mambo haya uliyojifunza?
! ! Andika jina la huyo mtu pia eleza lini utamwambia mambo haya.
" " Andika maelezo ya kila mmoja kwa ajili ya kumbukumbu ya maswali
" " kipindi kinacho kuja wakati wa ukaribisho.
D. Katika Swali namba 5 na 6 sisitiza KAZI na USHUHUDIAJI
" Unapoanza seli mpya, ni muhimu kushughulikia msingi wa Imani. Habari katika
" maandiko yafuatayo ni mapendekezo yatakayo faa kwa wiki 10 mtakazo kutana
" pamoja. Wiki nne za kwanza zina wafaa sana hasa wale ambao sio wakristo
" itawasaidia kumjua kristo ni nani, hata hivyo unaweza kuanza na yeyote kwa
" juma la kwanza.
28
MAANDIKO TUNAYOPENDEKEZA KUSOMA
! Yesu Ni Nani?
" " Wiki ya kwanza - Yohana 4:1-26
" " Wiki ya pili - Yohana 11:17- 46
" " Wiki ya tatu – Yohana 14:1-11
" " Wiki ya nne – Yohana 3:1-18. Kumwamini Kristo kwa ajili ya wokovu
" " " " " " " " wa milele
"
" " Wiki ya tano – Efeso 2:1-10. Maisha mapya ndani ya Kristo.
" " Wiki ya sita – Yohana 10:1-30 Usalama ndani ya kristo
" " Wiki ya saba – 1 Yohana 1:5-2:2 kushughulikia dhambi na uwajibikaji
" " Wiki ya nane - Zaburi 1:1 Neno la Mungu
" " Wiki ya tisa - Wagalatia 5:16-26. Kutembea katika Roho
" " Wiki ya kumi - Matendo 1:1-11. Kushuhudia wengine.
Hatimaye kutokana na kazi yenu ya ushuhudiaji katika seli watu wapya wataongezeka.
Hata hivyo seli yenu isizidi watu kumi. Seli inatakiwa iwe na watu 6 hadi 10 watu
wakiongezeka seli igawanyike. Watu wengine katika seli hiyo waanzishe seli zingine.
Tumia nyenzo hii kuwasaidia wanaoanza seli mpya.
Watie moyo washiriki ili seli zijizidishe badala ya watu kujazana kwenya seli
moja. Watu wanatakiwa watembee kwenda kwenye seli kila mahali kwenye kijiji,
mjini, kwenye Taifa mpaka ukanda.
29
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 4 - KUJIENDELEZA BINAFSI
“MAOMBI YA MFANO”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
SOMA : Mathayo 6:5-15
Maombi ni mawasiliano ya moja kwa moja na Mungu. Kama mwamini umepewa haki,
fursa na amri ya kuja mbele za muumba wa vitu vyote, Mungu mwenyezi na mtawala
mkuu wa duniani yote. Mmiliki na muumba wa vitu. Kwa vile maandiko yahusisha
maelekezo ya namna ya kuomba, kuna njia sahihi na isiyo sahihi ya kumwendea
Mungu katika maombi. Yesu anatufundisha namna ya kuomba. Katika mathayo 6:5-8
anatupa maelekezo ya namna ya kuomba. Katika mathayo 6:9-13 anatuonyesha
mfano wa kuomba/maombi, wakati katika mathayo 6:14-15 anatupatia maarifa ya
namna ambavyo maombi ya kweli yanavyotakiwa kuwa.
MAELEKEZO KABLA YA MAOMBI
Mathayo 6:5-6 inasema tusiombe kama wanafiki wanavyofanya. Haitakiwi kuomba
kwa kujielekeza wenyewe.Hatuombi ili kuwafurahisha watu kwa maneno mazuri
yaliyopambwa kwa werevu fulani. Watu wengi wamekuwa na hatia hii kutafuta fursa ya
kuomba mbele za watu ili kuwavutia kwa sala zilizopambwa kwa maneno ili
kuonekana ni watu wa kiroho. Wakati huo mioyo yetu ikitafuta utukufu binafsi, huu ni
udhihirisho wa mtu asiye wa rohoni.
Biblia inaagiza kuomba mahali pa siri. Mungu anasikia hata kama upo mahali pa siri.
Je hii inamaanisha kwamba usiombe mbele za watu wengine? Maombii haya ya
mfano katika mistari 7-13 yalifanywa mbele za watu ambao Yesu alikuwa
anawafundisha. Kuna matukio mbalimbali ya maombi yaliyofanywa hadharani katika
Agano Jipya. Siyo dhambi kuomba mbele ya hadhara, lakini ni dhambi kuomba kama
wanafiki wafanyavyo ili kutaka kuonekana. Kama huwezi kuomba kwenye hadhara bila
kushinda vishawishi vya kutaka kuonekana basi nenda kaombe mahali pa siri.
SWALI LA KUJADILIANA: Tunaweza kujizuia namna gani ili tusiombe katika hali ya
! kutaka kuonekana au kuwafurahisha watu?
30
Jambo la pili. Hatutakiwi kuomba kama “mataifa” wafanyavyo – sala ndefu zenye
maneno matupu. Maombi ya namna hii hayotoki moyoni pia hayana muunganiko,
maombi ya namna hii ni ya mazoea tena ni ya kukariri. Hayana ujazo wa maneno ya
msingi. Jambo la kusikitikisha ni kwamba sala ya Bwana imekuwa ikikaririwa na watu
na kuombwa kwa mazoea. Maneno ya sala ya Bwana yamekosa maana kwa watu
wengi. Wakristo hatutakiwi kuomba kama vile tunanuwiza ili kumvuta Mungu atusikie
Mstari wa 8 unasema kwamba Bwana anajua tunachokihitaji kabla hatujaomba kwake.
Mungu anajua kila kitu kwa hiyo tunapoomba hakuna jambo jipya asilolijua
tunalopeleka kwake.
SWALI LA KUJADILIANA: Tunawezaje kujizuia na maombi ya mapokeo ya kujirudia rudia
! ambayo Yesu alituonya tusiyafanye?
Kwa kuwa Mungu anajua mahitaji yetu sasa kwa nini tunaomba? Kuna sababu nyingi
zinazotufanya tuombe. 1). Tumeagizwa kuomba - kwa hiyo tunatakiwa kutii maagizo.
2). Maombi yanafuunua fursa zetu - kwa vile tukiomba na mambo ambayo tunaomba
yanafunua fursa ya mambo yaliyoko mioyoni mwetu basi maombi yana umuhimu. 3).
Yanaonyesha kumtegemea Mungu - tunapoenda mbele za Mungu na kupeleka
mahitaji yetu inaonyesha kumtegemea Mungu. 4). Maombi yanakuza mahusiano yetu
na Mungu. Kwa kadri tunavyotumia muda mwingi kuwasiliana na Mungu kwa njia ya
kusoma Neno lake, ndivyo tunavyokuwa karibu naye na ndivyo tunavyomjua zaidi.
SWALI LA KUJADILIANA: Maombi yamekusaidiaje kukuza uhusiano wako na Mungu?
MAOMBI YA MFANO.
Katika Mathayo 6:7-13, Yesu ametupa sala ya mfano, tunajifunza mambo mengi na
kupata maarifa ya NAMNA na JINSI Yesu alivyoomba. Hebu tuone JINSI alivyoomba,
Jambo la kwanza maombi yake yanaonyesha mahusiano ya karibu katika utatu
mtakatifu, anamkiri muumba, na Baba na siyo tu Baba bali Baba wa Mbinguni. Jambo
la pili, anaomba kwa kuzingatia jamii, anatumia wingi, “Baba yetu” Anaomba kwa ajili
yake na kwa ajili ya watu wengine kwa wakati huohuo. Katika maombi haya
anajiunganisha na watoto wa Mungu. Jambo la tatu, ameomba mambo makubwa!
Kwa sababu mambo ambayo aliyaomba yanaweza tu kujibiwa na Mungu.
NAMNA GANI, Yesu aliomba mambo 6 katika sala yake, Mambo matatu
yanamwelekea Mungu (Jina la Mungu liabudiwe kwa utakatifu, Ufalme wa Mungu uje,
31
mapenzi ya Mungu yatimizwe duniani). Na maombi matatu ni ya mwanadamu
(Chakula cha kila siku, kusamehewa kama tunavyosamehe wengine, ulinzi na
kufunguliwa). Unaona katika sala hii mambo yanayomhusisha Mungu ndiyo
yaliyopewa kipaumbele. Utakatifu wa jina la Mungu ndiyo jambo lililopewa kipaumbele
katika maombi haya. Jambo la pili lililopewa kipaumbele ni kuendeleza ufalme wa
Mungu – jambo hili linahusisha kuwakuza waamini kufikia hatua ya kufanana na Kristo
na kuipeleka injili kwa watu ambao hawajaisikia. Jamba la tatu ni mapenzi ya Mungu
yatimizwe katika ulimwengu huu wa dhambi kama yatimizwavyo huko mbinguni. Ili
kwamba kila mtu amtii Mungu na makusudi yake yatimizwe hapa duniani sasa kama
huko mbinguni. Kisha Yesu anatuonyesha mambo yanayofuata – mahitaji ya kila siku.
Pia anatuonyesha msamaha kama tunavyosamehe wengine. Hii inafafanua juu ya
umuhimu wa kutembea katika umoja. Kristo anatuonyesha namna ya kutafuta ushirika
na Mungu usiovunjika kwa njia ya toba. Na pia inatuonyesha umuhimu wa kutafuta
ushirika wa kindugu katika Kristo usiovunjika kwa kuwasamehe wengine
wanapotukosea. Mwisho Yesu anaomba kwa ajili ya ulinzi, na kuokolewa toka kwenye
majaribu na uovu, amabo ni halisi na hatari kutoka kwa adui.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni jinsi gani tunaweza kutumia sala hii ya mfano kama kiongozi
! katika sala zetu na kuepuka maombi ya marudio marudio yasiyo na maana?
Jambo la mwisho na muhimu kulitazama ni kwamba Yesu alikuwa mwombaji kweli.
Haongelei tu suala la maombi, hatoi tu maelekezo ya namna ya kuomba YEYE
MWENYEWE ALIKUWA NI MWOMBAJI, NA KWELI ALIOMBA. Hii ni changamoto kwa
wachungaji na viongozi kutoa maagizo na maelekezo kwa watu kuomba wakati wao
wenyewe hawaombi. Tusiwe wanafiki. Haitoshi tu kuongelea suala la maombi.
Tunatakiwa kuomba. Kama tunataka kumfuata Kristo, maombi ni jambo muhimu kila
siku.
SWALI LA KUJADILIANA: Washirikishe watu wengine mambo ambayo yamekusaidia
! wewe kuwa na ufanisi katika maisha ya maombi.
DHANA MUHIMU: TUNATAKIWA KUOMBA KWA BABA BILA KUACHA KWA KUFUATA
! MWONGOZO AMBAO YESU ALITUPATIA.
32
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Yachunguze maisha yako.
" Je ni mara ngapi unaomba?
" Mkazo wa maombi yako ni nini?
" Je baadhi ya maneno au misemo imekuwa tupu kwa sababu nya kuitumika mara
" kwa mara ?
Siku ya 2: Wiki hii yafanye maombi kuwa jambo muhimu, omba asubuhi, mchana
" na jioni. Utatekelezaje jambo hili?
Siku ya 3: Katika maombi, maombi yako yamwelekee Mungu na pia ombea juu ya
" mahitaji ya kibinadamu. Omba katika roho na kwa akili pia (1 Wakorintho 14:15).
Siku ya 4: Omba kila siku kwa ajili ya “watenda kazi kwa ajili ya mavuno” (Luka
" 10:2) na fursa ya kuipeleka injili yenye matumaini na kuwafanya mataifa kuwa
" wanafunzi. Timu ya Strategic Impact imetegesha kengele ya saa kila siku saa
" 4:02 asubuhi kuomba ili Bwana apeleke watenda kazi katika mavuno. Tegesha
" kengele yako ya saa au simu ili kuungana nasi katika kila siku kwa ajili ya
" maombi haya.
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
33
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 5 - KUJIENDELEZA KIUONGOZI
“KIONGOZI NI NANI?”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Katika somo la 2, uongozi umetafsiriwa kama kuhamasisha watu ili kutimiza lengo lililo
wazi. Kutokana na mwanga wa tafsiri hii, katika somo hili tutazungumzia mambo
yanayomfanya mtu kuwa kiongozi.
Kiongozi Ni NANI?
Kiongozi ni mtu anayejua kweli tatu za msingi:
1) Kujua mahali anakotakiwa kwenda (WAPI - WHERE),
2) Kujua namna ya kufika huko (JINSI - HOW),
3) Kujua jinsi ya kuhamasisha watu wengine kwenda pamoja na yeye (MOTIVATE)
Jambo la kwanza, kiongozi anatakiwa awe na mwelekeo, lengo, au kusudi lililo wazi.
Kiongozi anatakiwa awe na picha ya namna ya kukamilisha maono hayo. Zaidi ya
hapo, kiongozi hajui tu anapokwenda, lakini anajua pia hatua maalumu
zitakazomsaidia kukamilisha malengo. Kwa maneno mengine, kionngozi ana ramani
ya kukamilisha malengo. Mwisho, kiongozi anajua namna ya kuwahamasisha wengine
ili waweze kushirikiana naye kukamilisha lengo. Kama mtu hawezi kuwahamasisha
watu wengine kumsaidia kufikia malengo huyo mtu siyo kiongozi.
SWALI LA KUJADILIANA: Kwa nini unadhani kanuni hizi tatu ni muhimu kwa kiongozi?
! Unadhani upungufu wa moja wapo utamuathiri vipi kiongozi?
DHANA MUHIMU: KWA HIYO, SIFA TATU ZA KIONGOZI NI:
" " 1) Kuwa na MAONO: Kujua unakokwenda
" " 2) Kuwa na MKAKATI: Kujua namna ya kufika unakokwenda
" " 3) UHAMASISHAJI: Jinsi ya kuibua shauku ndani ya watu wengine ili
" " " washirikI hayo maono.
"
SWALI LA KUJADILIANA: Je ni jinsi gani tunaweza kukuza mambo haya matatu katika
! maisha yetu ili tuwe viongozi bora?
34
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Katika somo la 2, tulikuomba ueleze malengo yako, maono unayodhani
" kwamba Mungu amekuita kuyatimiza (Ukurasa 23) Tafadhali pitia mambo
" uliyoyaandika ili kuyatazama kwa upya maono yako. Tathimini maono yako, Je
" unaweza ukayatamka maono yako katika sentensi moja? Je yanaeleweka Kwa
" watu wengine? Je mtu mwingine anaweza kuyafafanua baada ya kuyasikia mara
" moja?
Siku ya 2: Tengeneza mkakati wa mwaka mmoja utakaokusaidia kutimiza maono
" yako. Ni hatua zipi utakazozichukua ili kutimiza maono yako?
Siku ya 3: Je ni mambo gani muhimu unayotarajia kuyafanya ndani ya siku 30
" zijazo yatakayokusaidia kutimiza maono? Lini utayafanya? Kwa namna gani?
Siku ya 4: Je ni watu gani ambao ungependa kuwashirikisha maono na mikakati
" yako? Lini utafanya hivyo? Je utazungumza na mtu mmoja mmoja au kikundi?
" Anza kupanga hiyo mikutano sasa.
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
35
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 6 - UPANDAJI WA MAKANISA
“HATUA YA 2: MAOMBI”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
SOMA: Matendo 2:42; Wakolosai 4:2-4; Warumi 12:12; 1 Yohana 5:14-15 &
! Luka 10:2-3
Ukianza kubadirisha mtazamo wako kutoka kujenga ufalme wako (Kanisa lako/
Ratiba / bajeti n.k) na kujenga Ufalme wa Mungu, ndipo utakapoanza kuona uzito wa
wajibu ulionao. Wajibu tuliopewa ni kutimiza Agizo Kuu (kwenda kuwafanya mataifa
kuwa wanafunzi (Mathayo 28:18-20; Matendo 1:8). Lakini kuwafanya watu kuwa
wanafunzi ni kazi ya Roho (Yohana 6:65; Yohana 3:27). Nyongeza ni kwamba, Agizo
Kuu linahusisha kuufikia ulimwengu. Hakuna jinsi ambayo mtu mmoja anaweza kufikia
miji yote ya ulimwengu.
Mungu ametuagiza kufanya kazi ambayo ni zaidi ya uwezo wa kibinadamu. Kwa nini
sasa tunasahau sehemu ya Agizo Kuu. Yesu alisema “Mamlaka yote ya mbiguni na
duniani nimepewa mimi.” Pia alisema, kwamba “Mtapokea nguvu Roho akiisha
wajilia juu yenu.” Kama Mungu ametoa agizo, tunaamini kwamba atatupa kila
tunachohitaji ili kutii na kutimiza agizo - kama kwa imani. Katika 1 Yohana 5:14-15,
maandiko yanasema “Na huu ndiyo ujasiri tulionao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu
sawa sawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia,
tuombacho chote, twajua kwamba tunazozile haja tulizomwomba” Napenda
nikuulize swali, je kutimiza Agizo Kuu ni mapenzi ya Mungu? NDIYO! NDIYO!
NDIYO!!! Je Yesu anazo nguvu za kutimiza Agizo Kuu? NDIYO! NDIYO! NDIYO!!! Je
atatimizaje? Kwa nguvu zake kupitia kazi yako.
SWALI LA KUJADILIANA: Kwa nini mara nyingi tunategemea nguvu, vipawa na ujuzi wetu
! kufanya kazi ya Mungu aliyotuitia?
Maombi, ni zana yenye nguvu. Maombi yanafunua unyenyekevu na utegemezi wetu
wa nguvu za Mungu. Maombi yanafunua utegemezi wetu wa utukufu na nguvu zake ili
kutimiza makusudi yake. Kupitia maombi, tunaonyesha shukrani zetu kwa kazi ya
msalaba, mahitaji ya kila siku na utendaji kazi wake katika maisha yetu, na maongozi
36
ya namna ya kumtukuza yeye kwa kuwatia moyo wanafunzi wenzetu na kutengeneza
wanafunzi wapya.
Kila eneo la maisha yetu na huduma linatakiwa lizamishwe kwenye maombi.
Tumejitoa kuomba, lakini haina maana ya kwamba tunafanya maombi tu. Tusichukue
hatua ya kufanya jambo lolote la Kimungu bila kulipeleka mbele za Bwana kwa njia ya
maombi. Tukisha mkabidhi Mungu mipango yetu, tuamini kwamba Mungu ataziongoza
hatua zetu.
SWALI LA KUJADILIANA: Je ni shughuli gani ambazo mnajihusisha nazo sasa ambazo
! mnadhani mnahitaji kuongeza maombi zaidi?
Moja ya maombi muhimu tunayotakiwa kuomba ni kuombea watenda kazi. Katika
Luka 10:2-3 Yesu aliwaambia wanafunzi wake kwamba, mavuno ni mengi, lakini
watenda kazi ni wachache; basi mwombeni Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi
katika mavuno yake. Enendeni, angalieni, nawatuma kama wana kondoo kati ya
mbwa mwitu. Aliwaambia wafuasi wake kuomba kwa ajili ya watenda kazi zaidi, na pia
ili aweze kuwatuma SASA. Tunapoomba kwa ajili ya watenda kazi, hatusubiri waje na
sisi wenyewe tunaingia shambani. Ukweli ni kwamba, ili Agizo Kuu litimizwe, watenda
kazi wengi watatoka kwenye mavuno. Tafakari juu ya jambo hili watenda kazi wengi
watakaoshiriki katika kutimiza Agizo Kuu bado hawajapokea wokovu. Kwa hiyo
tunapomwomba Mungu kwa ajili ya watenda kazi, maana yake tunaomba roho za
watu ziokolewe – ili kuwapata wanafunzi lazima tuombe ili kupata maelekezo kutoka
kwa Mungu. Ni lazima tufanye kazi kwa kutegemea nguvu zake na sio nguvu zetu.
Tunatakiwa tujitoe katika maombi na kuwakusanya watu kwa ajili ya kuomba. Wengi
wetu tumeweka kengele (alarm) kwenye simu zetu ili kutukumbusha kuomba kila siku
saa 10:02 asubuhi kwa ajili ya kuombea watenda kazi Luka 10:2.
SWALI LA KUJADILIANA: Tulia kidogo saa hizi angalia kengele (alarm) ya simu yako.
! Omba kwa ajili ya watenda kazi waje kwenye mavuno.
Yesu ana mamlaka yote Mbiguni na duniani. Tumeagizwa na yeye kutimiza Agizo Kuu.
Mwombe Bwana wa mavuno apeleke watenda kazi kwenye shamba lake. Ukweli kwa
Mungu mambo yote yanawezekana. (Mathayo 19:26).
DHANA MUHIMU: MAOMBI LAZIMA YAPENYE KWENYE HUDUMA ZETU ZA
! KUZIDISHA WANA.
37
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Wiki hili, omba kila siku saa 10:02 Kwa Bwana ili alete watenda kazi
" katika mavuno. Kisha tiki kwenye kibox kifuatacho.
Jumapili Jumamosi Ijumaa Alhamisi Jumatano Jumanne Jumatatu
Siku ya 2: Weka ratiba ya muda ambao watu wako watakusanyika pamoja ili
" kuomba kwa ajili ya Ufalme wa Mungu kusonga mbele, kuombea watenda kazi
" katika mavuno, kuombea kutimia kwa Agizo Kuu, kuombea fursa za kuhubiri injili,
" kuwaombea watu waliopotea kwa majina yao, ombea ratiba ya uinjilisti iliyo
" mbele yenu.
" Mahali: _____________________ Tarehe: _____________ Muda:_________
Siku ya 3: Panga ratiba ya muda wa maombi ya kutembea yatakayofanywa na
" watu wako. Tembelea eneo mnalotaka kupanda kanisa na mwombe ili Bwana
" afungue mioyo ya watu na kukutana na mahitaji ya hiyo jamii au jumuiya.
" Mahali: _____________________ Tarehe: _____________ Muda:_________
Siku ya 4: Je ni njia gani utakazozitumia kuwafanya watu unaowaongoza kuwa
" waombaji?
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
38
39
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 7 - KUJIENDELEZA BINAFSI
“KUTEMBEA KATIKA ROHO”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Mungu amekusudia maisha ya mkristo yawe na mahusiano hai na Yesu Kristo kwa
njia ya uwepo wa Roho Mtakatifu ndani ya mwamini (Soma 8:9-14). Mungu
hajakukusudia wewe umfuate na kumtumikia kwa nguvu zako mwenyewe. Badala
yake Mungu amekupa Roho Mtakatifu ili uweze kumfahamu na kuwa na mahusiano
naye binafsi na kutembea katika nguvu zake ukimpendeza na kutimiza mapenzi yake.
KIla mtu aliyezaliwa mara ya pili katika roho anaye Roho Mtakatifu katika roho yake ya
kibinadamu (Warumi 9:9; Wagalatia 5:2-3). Roho Mtakatifu ana shauku ya kutaka
kukuhudumia na kukutumia unapotembea katika Roho (Wagalatia 5:16) Hii maana
yake nini?
MOJA: Anataka akufariji na kukutia moyo (Yohana 14:15-21). Bwana aliahidi
kwamba atamtuma Roho Mtakatifu kama mfariji. Tunaweza kutembea katika faraja
mioyoni mwetu na kwenye nia Zetu. Hata hivyo mstari wa 21 unasema tunatakiwa
kutii maagizo yake ili kuweza kufaidi huu ukaribu wetu na Bwana (soma Yohana
15:14-15). Tutakapotii kabisa tutakuwa na ushirika mkubwa, faraja na kutiwa moyo na
Bwana.
SWALI LA KUJADILIANA: Umetembeaje katika faraja ya Roho Mtakatifu wiki iliyopita? Je
! ni maagizo gani ambayo unadhani Roho Mtakatifu anakuongoza kutii leo?
MBILI: Roho Mtakatifu ameahidi kukuongoza kwenye kweli yote (Yohana 16: 12-15).
Matumizi ya kwanza ya maandiko haya ya Yesu yalikuwa kwa ajili ya mitume kuandika
maneno ya Mungu yaliyovuviwa ambayo tunayo katika agano jipya. Huu ndo unaitwa
uvuvio. Matumizi ya pili kwa ajili ya waamini wote ni kwamba Roho Mtakatifu
atatufundisha kupitia maandiko (Efeso 1:17-18). Huku ndo kutiwa nuru. Roho
Mtakatifu ana sauti na sauti yake ni “Biblia.” Kwa hiyo tusome Biblia tukiwa
tumefungua macho kwa Roho Mtakatifu. Unaposoma Biblia omba kwa kusema
kwamba “Bwana, sema nami.”
SWALI LA KUJADILIANA: Ni kweli gani kutoka kwenye maandiko ambayo Roho
! Mtakatifu ameweka moyoni mwako muda huu?
40
TATU: Roho Mtakatifu anashauku ya kuzalisha maisha ya Kristo ndani yako (Soma 2
Wakorintho 3:18; Wagalatia 5:16-17). Ulipozaliwa mara ya pili nafsi ya Roho Mtakatifu
ilikuja kukaa ndani yako (1Wakorithno 5:17). Hata hivyo, kuzaliwa mara ya pili
haimaanishi kwamba tumekomaa katika Kristo. Kazi ya Kristo ndani yetu ni kamilifu na
sahihi. Lakini, kazi ya Roho Mtakatifu ndani yetu bado haijakamilika. Roho Mtakatifu
ana shauku ya kuendelea kutubadilisha ili tufanane na Kristo. Hii imeelezwa kupitia
tunda la Roho (soma Galatia 5:22-23). Matunda haya yanachipushwa ndani yetu
tunapotembea katika Roho (soma Galatia 5:16). Tunatembea katika Roho kila siku
tunaposema ‘ndiyo’ kwake na ‘hapana’ kwa shauku za mwili (asili ya dhambi).
Ushindani wa shauku ya Roho na ya mwili utaendelea ndani mpaka utakapokutana na
Bwana mbiguni. Tunapoendelea kuchagua matakwa ya Roho, tabia ya Kristo inakua
na kuongezeka ndani yetu.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni shauku gani ya dhambi unayotaka kuiambia hapana muda
! huu? Ni tunda gani ambalo unahitaji msaada wa Roho Mtakatifu kulikuza muda
! huu?
NNE: Roho Mtakatifu ana shauku ya kukuongoza kufanya mambo fulani na kusema
mambo fulani (soma Warumi 8:14; Wagalatia 5:21; Wafilipi 2:12-13). Anatusukuma
kunia na kutenda makusudi mema. Sauti yake inaongea na moyo wako na akili yako.
Lakini, lazima tuwe waangalifu. Shetani na sauti za mapepo vinaweza kuwa na
ushawishi kwenye mawazo yako. Kwa hiyo hakikisha msukumo unaosikia ndani yako
unakubaliana na maandiko. Roho hawezi kukuongoza kufanya jambo lolote lililo
kinyume na Biblia. Tunatakiwa kuwa makini tunapopata msukumo wake hatua kwa
hatua na kumsikiliza.
SWALI LA KUJADILIANA: Je unasikia msukumo wowote wa Roho Mtakatifu kufanya
! jambo au kusema neno muda huo?
TANO: Roho Mtakatifu ana shauku ya kuwaleta wengine kwa Yesu na kuwafundisha
kupitia wewe (soma Yohana 15:26-27; Matendo 1:8; 1Petro 4:10-11). Anataka
akutumie wewe kuwasaidia wengine kumjua Yesu na kuwasaidia wanaomjua kukua
na kufanana naye. Kazi hii kubwa inakuhitaji wewe ushirikiane na Roho Mtakatifu.
Tunapowaeleza wengine habari za Yesu, atashuhudia pamoja na sisi na kuwavuta
wengi katika imani ndani ya Kristo. Hatuwezi kufanikiwa katika ushuhudiaji Roho
Mtakatifu asipofanya kazi ndani yetu na kupitia sisi. Kwa hiyo, shirikiana na Roho
Mtakatifu na anzisha mazungumzo juu ya Yesu na tarajia yeye kuwashawishi watu ili
wamwamini Kristo.
41
SWALI LA KUJADILIANA: Roho Mtakatifu anakusukuma kumwambia nani habari za
! Kristo na lini utaanzisha hayo mazungumzo?
Yesu aliahidi kwamba baada ya kuondoka duniani atamtuma Roho Mtakatifu akae
ndani yetu (Yohana 16:7). Yeye ni mfariji, mwalimu, anabadirisha maisha,
anatuongoza na anatutumia kuwaleta wengine kwa Yesu. Unaposhirikiana na
kutembea na Roho Mtakatifu kila siku utakuwa na maisha yenye furaha na matunda.
DHANA MUHIMU: MUNGU AMETUPA ROHO WAKE ILI ATUHUDUMIE NA
! KUTUTUMIA.
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Katika siku tano zijazo kila siku pitia moja ya kazi za Roho Mtakatifu ambazo
umejifunza katika somo hili.
Siku ya 1: Kariri Wagalatia 5:16. Sema kwa kurudia kila siku hii itakusaidia kushika.
Siku ya 2: Ni huduma gani kati ya huduma tano za Roho Mtakatifu ambayo ina
" maana kubwa kwako leo? Kwa nini? Andika jinsi gani unaweza kushirikiana
" vizuri na Roho Mtakatifu katika eneo hili.
42
Siku ya 3: Soma Yohana 15:26-27 na Matendo 1:8. Fafanua wajibu wa Roho
" Mtakatifu na wajibu wako unaposhuhudia wengine.
Siku ya 4: Andika nini maana ya maagizo haya katika maisha yako:
" " Waefeso 4:30:
" " Waefeso 5:18:
" " Wagalatia 5:16, 21:
" " 1 Wathesalonike 5:17:
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
43
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 8 - KUJIENDELEZA KIUONGOZI
“TABIA: SIFA MUHIMU KWA KIONGOZI”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Kiongozi anaweza akawa na maono makubwa, mkakati mkubwa na uwezo mkubwa
wa kuhamasisha wengine, lakini kuna kipengele kimoja ambacho ni muhimu kwa
kiongozi wa Kikristo. Kipengele hicho ni kuaminiwa. Haijalishi una maono ya namna
gani na uwezo mkubwa wa kuhamasisha, kama watu hawawezi kukuamini, hawawezi
kukufuata. Kama kiongozi akiharibu kuaminiwa na wengine, watu hawawezi
kuendelea kumfuata. Kwa hiyo ili kiongoozi aweze kushawishi wengine kutimiza
maono makubwa, ni lazima awe na sifa ya tabia njema.
Tabia ni nini? Tafsiri nzuri ya tabia ni kuaminiwa kunakotokana na udhihirisho wa
uaminifu katika miasha yako.
Mmoja wa viongozi wakubwa kwenye Biblia ni mfalme Daudi. Kwa nini Daudi alikuwa
ni kiongozi mkuu? Zaburi 78:72 inatupa ufafanuzi kwamba “[Daudi] akawalisha kwa
ukamilifu wa moyo wake, na kuwaongoza kwa busara ya mikono yake.” Daudi
sio tu kwamba alikuwa ni kiongozi mwenye ujuzi bali alidhihirisha pia uaminifu.
Uaminifu ni kuwa kamili na bila kugawanyika. Ni kuwa mwaminifu na mkweli wakati
wote. Mtu mwaminifu ana moyo safi alivyo hadharani ndivyo alivyo sirini. Ni mtu
anayetegemewa na kuaminiwa. Wanatenda walichosema na kutunza ahadi. Mtu
mwaminifu haimaanishi hana mapungufu au kwamba hawezi kutenda kosa au
dhambi, hii haiwezekani. Kiongozi mwaminifu ni mwepesi kukiri kosa na kutubu
dhambi. Kwa sababu hupenda kudhihirisha kuaminiwa, ili watu wengine wajifunze
kwake na kumtegemea.
SWALI LA KUJADILIANA:
1. Kwa nini unadhani ya kwamba tabia au uaminifu ni muhimu kwa kiongozi wa
Kiungu?
2. Kwa nini kushindwa kitabia ni tishio kwa viongozi wa Kikristo?
3. Ni maeneo gani ambayo kiongozi wa kikristo anatakiwa kuonyesha uaminifu?
DHANA MUHIMU: BILA TABIA YA MUNGU, KIONGOZI HANA SIFA.
44
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Ni maeneo gani katika maisha yako ambayo unafikiri unatakiwa
" kuyaendeleza katika tabia na uaminifu? Ni majaribu gani yanayotishia uaminifu
" wako?
Siku ya 2: Andaa mkakati wa kuleta mabadiliko ya tabia/uamnifu katika maisha
" yako. Mambo gani yatakayokusaidia?
Siku ya 3: Maeneo matatu ambayo viongozi wa kikristo wanashindwa katika
" maisha yao ni pesa, uzinzi, na matumizi mabaya ya mamlaka. Je kuna njia
" yoyote inayoweza kukuhakikishia kutoshindwa katika mojawapo ya maeneo
" haya? Je kuna kitu chochote unachohitaji ili kuacha kufanya haya? Je kuna kitu
" chochote unachohitaji ili uanze kuyafanya?
Siku ya 4: Moja ya njia zitakazokusaidia kuwa na tabia endelevu ni kuwa na mtu
" ‘partner’ ambaye unaweza ukamuamini na kumpa nafasi ya kuhoji na kufuatilia
" maisha yako kwa ajili ya ulinzi wa tabia yako. Kama huna mtu anayewajibika
" kwenye maisha yako je ungependa kumpata mmoja wapo? Ndiyo maana
" kushiriki kwenye kikundi ni muhimu na huu ndiyo moyo wa shule ya kuzidisha
" viongozi. Dhamiria kukutana na wana kikundi wenzio kila wiki. Kikundi chako ni
" kipi? Mnakutana wapi? Ni muda gani mnaokutana? Jaza taarifa hii kwenye
" ukurasa 11
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
45
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 9 - UPANDAJI WA MAKANISA
“HATUA YA 3: ELEZA MAONO YA KUANDAA WANAFUNZI”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Kiongozi yoyote wa Kikristo mwenye mguso mkubwa duniani anakuwa hivyo kwa
msaada na kushirikiana na watu wengine. Hata Bwana wetu Yesu Kristo alikuwa na
timu ya watu kumi na mbili ambao aliwafundisha na kuwatuma ulimwenguni. Msisitizo
mkubwa wa maisha yake alipokuwa ulimwenguni ilikuwa ni kuchagua na kuandaa
watu watakaoendeleza kazi ya Mungu baada ya kufa, kuzikwa na kufufuka kwake.
Mtume Paulo wakati wote aliandaa wanafunzi, alifundisha na kutuma timu ya
kuzidisha wanafunzi. Hakufanya huduma peke yake. Kazi yake yote inaweza
ikaelezwa kupitia maneno aliyomwandikia Timotheo, “Na mambo yale uliyoyasikia
kwangu mbele ya mashahidi wengi, hayo uwakabidhi watu waaminifu
watakaofaa kuwafundisha na wengine” (2 Timotheo 2:2). Paulo alimfundisha
Timotheo (kizazi cha 1). Alimwelekeza Timotheo kuwakabidhi watu waaminifu
alichomfundisha (kizazi cha 2). Hawa watu waaminifu waliwafundisha wengine (kizazi
cha 3). Kuzidishwa kwa wanafunzi hakukuishia hapo! Hii huduma ya kujizidisha
inafafanua jinsi injili ilivyoenea kwa kasi katika karne ya kwanza. Kama unataka
kutimiza wito wa Kiungu kuwafikia jirani zako, miji, taifa na ulimwengu kwa injili,
itawezekana tu kwa kuandaa timu ya wanafunzi waaminifu.
[Muhimu: Neno waamininifu katika mstari huu haimaanishi jinsia fulani linamuhusu
mwananmke au mwanaume. SML inawahusu wote wanaume na wanawake. Hata
hivyo, ni nzuri watu wa jinsia moja wakae kwenye kikundi kimoja. Kwenye vikundi na
makanisani wanawake na wanaume wanatakiwa kuwepo wote. Lakini kwenye vikundi
vidogo vidogo (SML) wanaume wawafundishe wanaume wenzao, wanawake
wawafundishe wanawake wenzao. Vikundi vidogo vidogo vimeundwa ili kufundisha
viongozi watakao jizidisha ambao nao watafundisha wanafunzi watakojizidisha,
wanafunzi hawa watapanda makanisa yatakayojizidisha na kuufikia ulimwengu kwa
injili.]
Ushiriki wako katika shule hii sio tu kupata maarifa bali kukupatia mafunzo na nyenzo
zitakazokusaidia kufikia malengo. Ushiriki wako katika shule unakuhitaji kutekeleza
mambo ya kufanya kila wiki, kuwashirikisha wengine injili, kuanzisha seli mpya/
kanisa na kuwafundisha viongozi wapya. Ili kupata wanafunzi na viongozi
watakaojizisha, unatakiwa utafute watu wawili ama watatu ambao utawapitisha
46
kwenye mafunzo. Kisha timu hiyo ya viongozi/wanafunzi wape changamoto nao ya
kutafuta watu wawili ama watatu ambao nao watawafundisha kupitia shule.
Unaombwa kujaza ‘ramani ya huduma’ ili kufuatilia watu unaowafundisha mpaka kizazi
cha tatu na kuwasaidia kukua na kufundisha wengine. Hatimaye utaona kwamba
wajibu wako sio tu kwa wale wa kizazi cha kwanza ama cha pili, bali ni pale
utakapoona kizazi cha tatu kinajizidisha na kuendelea.
Kwa wakati huu anza kuomba kwa ajili ya kufundisha viongozi wa kizazi kinachofuata.
Mwombe Mungu akupe watu waaminifu wawili au watatu ambao utawapitisha kwenye
shule ya kuzidisha viongozi. Wakati wote pandikiza maono haya kwa wale
unaowafundisha na wale ambao wako kwenye seli (kanisa la nyumbani).
Unapowashirikisha wengine injili anza kuwakusanya wanafunzi uwaweke kwenye
kikundi ama seli. Omba ili Mungu aweze kuinua viongozi ambao utawashirikisha haya
maono na kuwaomba wajiunge na wewe. Viongozi wa mavuno wanakuja kutokana na
mavuno.
Utaendelea kuongoza seli (kainsa la nyumbani) na kuwafundisha wanafunzi wapya
mpaka muhura wa pili wa shule. Kabla ya kuingia muhula wa tatu wa shule, unatakiwa
uwe na viongozi wapya wawili au watatu ambao unaweza kuanza nao muhura wa
kwanza. Sasa huu ni wakati wa kumuomba Mungu akuongoze kufundisha kizazi
kinachofuata.
SWALI LA KUJADILIANA: Kwa nini unadhani ni muhimu kwa kila kiongozi kuwa na watu
! wawili au watatu ambao unatakiwa kuwaongoza kwenye shule ya kuzidisha
! viongozi kabla ya kwenda muhura mwingine wa shule?
Unapokusanya timu ili kutimiza agizo kuu zinganitia mambo yafuatayo:
1. MAOMBI:- Mwombe Mungu ainue timu itakayokusaidia kutimiza maono.
" Soma Luka 6:12-13. Katika mistari hii Yesu alitumia usiku mzima kuomba kabla
" ya kuchagua mitume kumi na mbili kati ya wanafunzi wake. Alimuomba Mungu
" ampe watu kabla ya kuwaomba watu wamfuate!
SWALI LA KUJADILIANA: Je umekuwa ukiomba kila siku ili Mungu ainue watenda kazi
! kwenye mavuno? (Luka 10:2) Ni watu gani ambao Mungu anakusukuma
! uwashirikishe kuanza nao shule?
47
2. Washirikishe maono watu ambao Mungu anakuongoza kuongea nao:
" Ili kupandikiza maono haya kwa watu wengine kuna hatua mbalimbali
" unazopaswa kuzichukua.
• Andika orodha ya wanaume na wanawake ambao unadhani Mungu
anakuongoza kufanya nao kazi, kisha baada ya wiki kadhaa panga muda
ambao utawaomba kuungana na wewe ili kutimiza Agizo Kuu katika maisha
yako yote.
• Ni vizuri ukutane nao mmoja mmoja ili kuwashirikisha maono na kuwaomba
waungane na wewe.
• Waeleze maono ya kuufikia ulimwengu kwa injili na kuzidisha wanafunzi.
Waonyeshe mkakati wa kufundisha viongozi wapya watakao jizidisha na
kuwafundisha kupitia shuke ya kuzidisha viongozi.
• Washirikishe faida ulizozipata baaada ya kupitia shule ya huduma muhula
huu.
• Kisha waombe wajiunge na wewe kwenye timu. Waambie lini na wapi
mtakuwa mnakutana na mtakuwa mkifanya nini mnapokutana (maswali ya
uwajibikaji, masomo na mambo ya kufanya)
" Usitegemee kwamba watakupa majibu kwenye mkutano huu. Wape muda
" kuombea na wafuatilie ili upate maamuzi yao.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni jinsi gani unaweza ukaelezea maono ya kuzidisha wanafunzi na
! kuanzisha seli/kanisa la nyumbani na wengine?
! Mji wako unawezaje kubadilika kama utaanza kufundisha wanafunzi
! watakaojizidisha kila baada ya wiki 10?
DHANA MUHIMU: OMBEA, ELEZA MAONO NA WAOMBE WENGINE WAJIUNGE NA
! WEWE KWENYE TIMU YA KUZIDISHA VIONGOZI.
48
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Kwa muda huu ni watu gani unaowafikiria kuwakaribisha kwenye timu ili
" wakusaidie kutimiza maono na mikakati ya kuufikia mji, na taifa kupitia mafunzo
" ya viongozi ambao watazidisha wanafunzi ambao wataanzisha seli/kanisa la
" nyumbani? Andika orodha ya watu ambao unawafikiria kama bado huna kisha
" mwombe Mungu akupe watu ambao utafanya nao kazi.
" " 1. _________________________________________________________
" " " 2. _________________________________________________________
" " " 3. _________________________________________________________
Siku ya 2: Panga muda utakaokutana na washiriki wote katika timu hii katika
" kipindi cha wiki kadhaa zijazo ili kupanda maono ya kuufikia ulimwengu kwa injili
" na kuzidisha wanafunzi. Kwa uwazi fikiria juu ya mambo ambayo utaongea nao.
" Andika mawazo yako hapa:
Siku ya 3: Wasiliana na mchungaji wako ama mratibu wa shule ya kuzidisha
" viongozi ili kujua lini kongamano la viongozi litaendeshwa na Strategic Impact ili
" uweze kualika baadhi ya viongozi kwenye timu yako waweze kuhudhuria.
" Lini: ______________________________________________________
" Wapi: ______________________________________________________
Siku ya 4: Ni maeneo gani ya mji au ni aina gani ya watu ambao umeitwa
" kuwafikia kwa injili?
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
49
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
SOMO LA 10 - KUJIENDELEZA BINAFSI
“TIMIZA WAJIBU WAKO KWENYE FAMILIA”
Mnapoanza kukutana, gawanyikeni katika makundi ya watu wanne au chini ya wanne
kwa dakika thelathini. Ombeaneni na kuulizana maswali yaliyopo ukurasa wa 15 au
kutoka kwenye kadi za uwajibikaji. Kisha kusanyikeni Kama kikundi mpitie somo
linalofuata, mjadiliane maswali kwa pamoja.
Mungu anapotafuta kiongozi ndani ya kanisa, anaanza kuangalia mahusiano ya mtu
na familia yake. 1Timotheo 3 na Tito 1 inatupa sifa zinazotakiwa kwa kiongozi ndani ya
kanisa. Mwanzo wa kiongozi ni namna anavyohusiana na familia yake (soma 1
Timothheo 3:1-2, 4-5; Tito 1:5-6). Kanuni iko hivi, kama mtu hawezi kuongoza familia
yake vizuri basi hawezi kuongoza kanisa vizuri (soma 1Timotheo 3:5). Familia siyo
huduma ya kwanza tu kwa kiongozi bali ni kipaumbele cha huduma yake.
Mungu ni muasisi wa ndoa na familia. Ametupa wenzi ili kukutana na mahitaji na
shauku zetu kwa ajili ya utukufu wake. Ameitengeneza ndoa ili iwe na mahusiano ya
ajabu ambayo yataleta Baraka kwetu (soma Zaburi 128). Ametupa watoto ili tuwalee
kwa ajili ya utukufu wake na pia anabariki maisha yetu (soma Zaburi 127:3-5). Ili
tufurahie mahusiano na wenzi wetu na watoto, Mungu ametuelekeza namna
tunavyotakiwa kuhusiana kama mume, mke au wazazi. Kila mmoja wetu
anapotekeleza wajibu wa kipekee katika familia Mungu atatubariki na tutafurahia ndoa
na familia kama alivyotukusudia. Somo hili litazingatia wajibu maalumu wa
mwananume na mwanamke. Kama upo kwenye ndoa, tathmini maisha yako uone
unavyotimiza kipaumbele cha huduma yako katika ndoa.
(MUHIMU: Wanaume na wanawake wagawanyike
kwenye makundi mawili tofauti ili kujadili wajibu wao
katika somo hili.)
50
WAJIBU WA MWANAUME
Soma Waefeso 5:25-33. Wajibu wa mwanaume kwa mkewe umejumuishwa kwa neno
moja upendo. Kiwango cha mwanaume kumpenda mke wake ni kama kile cha Kristo
alivyolipenda kanisa. Mwanaume anatakiwa kujidhabihu kwa ajili ya mke wake (Mstari
25). Hii inamaanisha mwanaume asiwe mbinafsi. Wakati wote ajiulize je maamuzi
yangu na matendo yangu yanamuathiri mke wangu. Namna ambavyo mume
anatakiwa amtendee mke wake ni vile vile anavyojitendea mwenyewe (mstari 29).
Kuna agizo la Mungu linalohusiana na wajibu wa wanaume katika Wakolosai 3:19
“Ninyi wanaume, wapendeni wake zenu msiwe na uchungu nao”. Kinyume cha
upendo ni chuki, wanaume hawatakiwi kuwatenda vibaya wake zao kimwili, kihisia au
kwa maneno. Badala yake tunatakiwa kuwa wapole kuwafurahia na kuwatunza kama
Yesu anavyofanya kwa kila mmoja wetu (Waefeso 5:29).
SWALI LA KUJADILIANA: Ni njia gani za matendo unazoweza kuonyesha upendo wa
! kidhabihu kwa mke wako? Je unaweza kutoa mfano wa wanaume
! wanaowatenda vibaya wake zao? Je tunaweza kuzuiaje hali hiyo?
Wajibu mwingine wa wanaume unapatikana katika 1Petro 3:7: “Vivyo hivyo ninyi
wanaume, kaeni na wake zenu kwa akili, nanyi wapeni heshima mkitambua ya
kuwa wao ni wenzi wenu waliodhaifu kama warithi pamoja nanyi wa kipawa cha
thamani cha uzima, ili kusiwepo na chochote cha kuzuia maombi yenu” (Tafsiri
ya Neno). Wanaume wameamuliwa kuwaelewa wake zao. Tunatakiwa tuwe wanafunzi
wa kujifunza kuwaelewa wanawake ambao Mungu ametupa, hivyo tutaelewa mahitaji
yao, shauku zao na mipaka. Mungu hajatuita kuwaelewa wanawake wote isipokuwa
mwanamke mmoja ambaye ni mke. Hii inamaanisha kwamba unatakiwa
kumuonyesha upendo yeye tu na kukutana na shauku zake na mahitaji yake.
Mheshimu kama mrithi pamoja na wewe wa uzima wa milele ambao Mungu
ametupatia usimpeleke zaidi ya uwezo wake kimwili kwa kuwa yeye ni chombo dhaifu.
SWALI LA KUJADILIANA: Jadilianeni jinsi wanawake walivyotofauti na wanaume na
! mahitaji yao maalumu waliyonayo. Kama upo kwenye ndoa, washirikishe
! wengine jambo moja ambalo umejifunza kutoka kwa mke wako linalokufanya
! umpende kipekee? Ni onyo gani ambalo tumepewa katika mstari wa 7 mwishoni
! kama hatutawaelewa na kuwashimu wake zetu?
Wajibu wa tatu wa mwananume katika maandiko unapatika katika 1 Wathesalonike
4:11-12; 2 Wathesalonike 3:6-10 na 1 Timotheo 5:6 (tafadhali soma). Katika utaratibu
wa uumbaji wa Mungu, mwanaume ndiye anayetakiwa kuitunza ama kuleta mahitaji
ya familia. Hii inamaanisha kwamba anatakiwa kufanya kazi ili alete chakula, nguo,
malazi na mahitaji mengine ya kimwili na ya watoto. Hii haimaanishi mwanamke
hawezi kufanya kazi ya kuingiza pesa lakini wajibu wake wa msingi ni kufanya kazi
51
nyumbani hasa kulea watoto wanapokuwa wadogo (soma 1Timotheo 2:3-5). Katika
tamaduni zingine wanaume huwatwisha mizigo wake zao ya kutafuta pesa na kuleta
mahitaji muhimu ya kifamilia. Hii ni hatari kwa wachungaji na viongozi wa kanisa.
Wakati mwingine wanaume wanatoa muda wao mwingi na nguvu zao kwenye huduma
huku wakijisahau kutimiza mahitaji muhimu ya familia. Ukweli ni kwamba wachungaji
wengi na viongozi wa kanisa wanajihusisha na shughuli zingine za kujiongezea kipato.
Ingawa kanisa linawajibika kutimiza mahitaji ya kimwili ya wachungaji. Lakini makanisa
mengi yanashindwa kufanya hivyo (SOMA 1 Wakoritho 9:7-14; Wagalatia 6:6; 1
Timotheo 5:17-19). Ikiwa kanisa ama huduma itashindwa kuwalipa wachungaji
wanaume watatafuta njia za kuingiza kipato ili kutimiza mahitaji ya familia, Kama
Mtume Paulo alivyofanya kazi ya kutengeneza mahema (soma Matendo 18:1-2; 2
Wathesalonike 3:7-9).
Mwanamke anaweza kusaidia kuongeza mapato ya familia. Anaweza akawa na ujuzi
mzuri wa biashara (soma Mithali 31), lakini ni muhimu ieleweke kwamba mzigo wa
kuhudumia familia usiwekwe juu yake. Wajibu wa kuhudumia familia ni wa
mwananume huo ndiyo mpango wa Mungu.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni njia gani ambazo wachungaji na viongozi wanaweza
! kuzitumia kutimiza mahitaji ya familia zao wakati huo huo wakiendelea kuongoza
! kanisa la Mungu? Tulielimisheje kanisa ili kusaidia mahitaji ya viongozi wao?
Wajibu wa nne wa mwanaume upo katika 1Wakorintho 7:1-7 (tafadhali soma). Wajibu
huu unahusiana na tendo la ndoa na mke wake. Jambo la kwanza mwanaume
anatakiwa aelekeze hisia zake na hitaji la kindoa kwa mke wake tu! (mstari 2). Awe
mume wa mke mmoja (soma 1Timotheo 3:2). Asiwe na mahusiano ya kindoa na
wanawake wengine. Hata hivyo katika mahusiano ya kindoa atangulize mahitaji ya
mke wake kwanza (mstari 3-4). Hii inamaanisha kuwa makini katika mahitaji ya
mwanamke na kuwa tayari kumpa utoshelevu.Usilazimishe ama kutumia nguvu
kufanya tendo la ndoa na mke wako. Wajibu wako wa kwanza kama mwanaume ni
kutimiza mahitaji yake. Kama wenzi wote mkiwa na mtazamo huu basi mtatimiziana
mahitaji na kutoshelezana.
SWALI LA KUJADILIANA: Tunawezaje kujilinda dhidi ya majaribu ya ngono na
! mahusiano nje ya ndoa? Unawezaje kuweka uwiano wa kutimiziwa mahitaji yako
! ya tendo ya ndoa na agizo la maandiko la kutimiza mahitaji ya mke wako?
HITIMISHO: Mungu amewapa wanaume maelekezo yaliyo wazi wazi ya namna ya
kutimiza wajibu kwa wake zao. Tafadhali kumbuka kwamba Mungu hajakupa wewe
uhuru au wajibu wa kumlazimisha mke wako kutimiza wajibu wake kwako! Wewe
timiza wajibu wako kama mume ambao Mungu anataka utimize na mwache mke wako
awajibike kwa Bwana kama anavyomtaka kutenda.
52
WAJIBU WA MWANAMKE:
Soma Mwanzo 2:15-25. Mungu alimuumba Adam mtu wa kwanza ili amwabudu na
kufanya kazi yake duniani. Hata hivyo Mungu alitamka kwamba si vyema Adam awe
peke yake. Kwa hiyo, Mungu alimuumba Hawa kuwa ‘msaidizi anayemfaa’ Adam.
Katika utaratibu wa Mungu wa uumbaji, mwannaume anapewa mke kuwa msaidizi
anayefaa (mstari 18). Huu ndiyo wajibu wa msingi wa mwanamke. Mke anatakiwa
kuwa mwenzi na anayejaza nafasi kwa mume wake. Anatakiwa awe mfariji, amtie
moyo, amuunge mkono na kumsaidia anapomwabudu na kumtumikia Mungu katika
maisha yake. Mke anamfanya mume kuwa bora kuliko ambavyo angekuwa peke yake
na anamsaidia kutimiza mambo mengi kuliko ambavyo angekuwa peke yake. Matokeo
yake ni kwamba wawili wanakuwa mwili mmoja (mstari 24) na kwa pamoja
wanatakiwa waakisi utukufu na heshima ya Mungu duniani. Hii ni fursa na wito mkuu.
Mke asiwe peke yake na kutafuta mambo yake, bali awe pamoja na mume wake na
kutafuta kumsaidia mume wake kutimiza wito alionao.
SWALI LA KUJADILIANA: Unajisikiaje kuitwa msaidizi wa kumfaa mume wako? Ni kwa
! njia zipi unaweza kumsaidia mume wako kumwabudu Mungu na kutimiza wito
! wake katika maisha?
Ili kutimiza wajibu wake kama msaidizi anyamfaa mume, Bwana amempa mwanamke
wajibu wa kufanya. Soma Waefeso 5:22-24. Mke anatakiwa kutii na kunyenyekea kwa
mume wake. Anatakiwa afanye hivi kama vile kanisa linavyotakiwa kumtii na
kumnyenyekea Kristo. Kutii haimaanishi kwamba mwanamke ni duni kwa mume wake
(soma Wagalatia 3:29-29; 1Petro 5:7) pia haimaanishi kwamba hana akili au vipawa
ukilinganisha na mume wake. Utii unahusisha mamlaka katika familia. Mungu
amempa mwanaume wajibu wa kuwa kiongozi wa mke wake na familia. Hii ina maana
kwamba mwanamke anatakiwa kukubaliana na maamuzi na maongozi ya mume
wake. Kunyenyekea haimaanishi kwamba mwanamke asitoe mawazo yake kuhusiana
na maamuzi lakini inamaanisha kwamba kumpa mume wako nafasi ya uongozi kama
Mungu alivyomuumba kuwa kiongozi. Kutii haina maana kila wakati unakubaliana na
mume wako, bali ina maanisha kukubalina na maamuzi yake kama kiongozi. Jambo
lingine linalofanana na hili ni kwamba, mwanamke anatakiwa kumheshimu mume
wake, Waefeso 5:33. Unaheshimu wajibu wake kama kiongozi wa familia. Mweleze
kwamba una thamini na kuheshimu uongozi wake katika familia.
SWALI LA KUJADILIANA: Ni hofu gani inayokujia unapofikiria kumtii mume wako kama
! kiongozi wa familia? Ni jinsi gani unaweza kushinda hofu hii (soma 1 Petro
! 3:1-6). Washirikishe wengine njia unazoweza kuzitumia ili kuonyesha heshima
! kwa mume wako.
53
Wajibu wa tatu wa mke kwa mume unapatikana katika 1Wakorintho 7:1-7 (tafadhali
soma). Ni wajibu katika tendo la ndoa na mume wake. Jambo la kwanza, mke
anatakiwa ajitoe kwa mume wake tu kihisia na tendo la ndoa! (mstari 2). Asiwe na
mahusiano nje ya ndoa. Katika mahusiano ya kindoa na mume wake aweke mahitaji
ya mume wake mbele. Kwa kuwa mwili wake sio wa kwake peke yake ni wa mume
wake pia, mwanamke atafute kumtosheleza mume wake mahitaji (mstari 3-4). Hii
inamaanisha kwamba mwanamke asitumie tendo la ndoa kama adhabu au zawadi.
Anatakiwa apatikane kwa ajili ya kutimiza mahitaji ya kindoa ya mume wake. Mtazo
wako wa kindoa kwa mume wako usiwe wa kujitosheleza kibinafsi. Usilazimishe tendo
la ndoa au kumnyima mume wako. Badala yake fursa yako ya kwanza ni kutimiza
mahitaji yake. Wenzi wawili wanakiwa kuwa na mtazamo wa namna hii mahitaji yao
yatatimizwa na watatoshelezana.
SWALI LA KUJADILIANA: Unafanyaje kutimiza hitaji la mume wako la kindoa wakati siku
! hiyo hujisikii kufanya hivyo? Kuna hatari gani unapotumia tendo la ndoa kama
! adhabu au zawadi kwa mume wako?
HITIMISHO: Mungu amewapa wake maelekezo yaliyo wazi ya kutimiza kwa waume
zao. Tafadhali kumbuka kwamba Mungu hajakupa uhuru au wajibu wa kulazimisha
mume wako atimize wajibu wake! Mungu anataka utimize wajibu wako kama mke na
mwache mume wako awajibike kwa Mungu anapotimiza wajibu wake.
DHANA MUHIMU: MUNGU AMEWEKA WAJIBU MAALUMU WA MWANAMKE NA
! MWANAUME KUTIMIZA KATIKA NDOA ILI KULETA UTUKUFU NA HESHIMA
! KWAKE.
54
MAMBO YA KUFANYA WIKI HILI:
Siku ya 1: Jikumbusheni wajibu wa mwanaume na mwanamke kutoka kwenye
" somo hili.Tathmini unavyofanya katika maeneo yote. Uwe mkweli. Ni eneo gani
" unatakiwa kuboresha?
Siku ya 2: Tenga muda wewe na mume wako au mke wako na muulize maswali
" yafuatayo. Sikiliza kwa makini na usijaribu kujikinga utakaposikiliza majibu.
" Swali kwa mke: “Ni njia zipi zinazokufanya ushukuru kwa namna
" ninvyokuonyesha upendo? Ni kwa namna gani ungependa nikuonyeshe upendo
" zaidi?”
" Swali kwa mume: “Ni kwa njia ipi unaweza kusema nakuonyesha heshina na
" adabu? Ni jinsi gani ungependa nikuonye heshima zaidi?”
Siku ya 3: Kutokana na majibu ya mwenzi wako andika mpango mkakati wa
" kuboresha wajibu wako kwake.
Siku ya 4: Panga tarehe au muda mrefu wa kumwonyesha mwezi wako mapenzi.
" Usiwe mtoko wa gharama. Mwombeni mtu awaangalizie watoto wenu. Pangeni
" mtoko ambao hautaingiliwa na kitu ili muweze kuufurahia
Uinjilisti: Wiki hii mshuhudie angalau mtu mmoja ambaye hamjui Kristo kisha jaza
" kwenye kumbukumbu ya watu walioshuhudiwa ukurasa wa 16-17.
55
Q1 KUJIKUMBUSHA DHANA MUHIMU
Somo la 1 - Kujiendeleza Binafsi: “Msingi wa Neno la Mungu”
! DHANA MUHIMU: Viongozi wa kikristo wanatakiwa kujitoa kumtafuta Bwana kila siku
! ! kwenye Neno lake.
Somo la 2 - Kujiendeleza Kiuongozi: “Uongozi ni Nini?”
! DHANA MUHIMU: !
! ! Kama huwezi KUHAMASISHA watu wewe huna UONGOZI.
! ! Kama huna WAFUASI ama watu huna UONGOZI.
! ! Kama huwezi KUTIMIZA LENGO huna UONGOZI ndani yako.
Somo la 3 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua 1: Badili Mtazamo Wako”
! DHANA MUHIMU: Wito wetu sio kujenga kanisa kubwa bali ni kuzidisha wanafunzi.
Somo la 4 - Kujiendeleza Binafsi: “Maombi ya Mfano”
" DHANA MUHIMU: Tunatakiwa kuomba kwa Baba bila kuacha kwa kufuata mwongozo
! ! ambao Yesu alitupatia.
Somo la 5 - Kujiendeleza Kiuongozi: “Kiongozi ni Nani?”
! DHANA MUHIMU: Mambo matatu muhimu katika uongozi:
! ! 1. MAONO: Kujua unakokwenda
! ! 2. MKAKATI: Kujua namna ya kufika unakokwenda
! ! 3. UHAMASISHAJI: Jinsi ya kuibua shauku ndani ya watu wengine ili washirikI
! ! ! hayo maono
Somo la 6 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua 3: Maombi”
! DHANA MUHIMU: Maombi lazima yapenye kwenye huduma zetu za kuzidisha
! ! wanafunzi.
Somo la 7 - Kujiendeleza Binafsi: “Kutembea katika Roho”
! DHANA MUHIMU: Mungu ametupa Roho wake ili atuhudumie na kututumia.
Somo la 8 - Kujiendeleza Kiuongozi: “Tabia: Sifa Muhimu kwa Kiongozi”
! DHANA MUHIMU: Bila tabia ya Mungu, kiongozi hana sifa.
Somo la 9 - Upandaji Wa Makanisa: “Hatua 3: Shirikisha wengine maono ya kuzidisha
" " " " " " " wanafunzi”
" DHANA MUHIMU: Ombea, eleza maono na waombe wengine wajiunge na wewe kwenye
! ! timu ya kuzidisha viongozi.
Somo la 10 - Kujiendeleza Binafsi: “Timiza wajibu wako kwenye familia”
! DHANA MUHIMU: Mungu ameweka wajibu maalumu wa mwanamke na mwanaume
! ! kutimiza katika ndoa ili kuleta utukufu na heshima kwake.
56
Q1 MAMBO YA KUZINGATIA
Ili kuendelea na mafunzo ya hatua ya pili (Q2), unatakiwa kutimiza mahitaji
yafuatayo:
1. Kukutana kila wiki kwenye kikundi chako kidogo kwa ajili ya kujibu maswali ya uajibikaji na
kujadiliana masomo ya shule ya kuzidisha viongozi na kutimiza mambo ya kufanya baada
ya kila somo. (Tafadali pitia upya kablasha hili na weka alama ya tick kwenye kijisanduku
kuonyesha jambo ulilokamilisha au kufanya)
" " Mahudhurio" Somo" Hatua
" " & Uwajibikaji" Ulilomaliza" Ulilomaliza
" Somo 1" " "
" Somo 2" " "
" Somo 3" " "
" Somo 4" " "
" Somo 5" " "
" Somo 6" " "
" Somo 7" " "
" Somo 8" " "
" Somo 9" " "
" Somo 10" " "
2. Washuhudie watu 10-30 (kiwango cha chini 10) unapokuwa katika mafunzo ya hatua ya 1
(Q1) (angalia ukurasa 14): "
" " 1" " " 2" " " 3" " " 4" " " 5
" " 6" " " 7" " " 8" " " 9" " " 10
3. Je umeanzisha seli (kanisa ka nyumbani) watu 2-10. Saa ngapi na wapi mnapokutaba?
" Lini: ______________________________________________________
" Wapi: ______________________________________________________
4. Kamilisha kujaza ramani ya huduma katika ukurasa unaofuata. Anzia na muhula wa
kwanza.
Kama umekamirisha mahitaji ya hapo juuau ya hatua ya kwanza, ili kwenda
hatua nyingine tafadhari tembelea tovuti yetu kwa anwani hiyo hapo chini.
WWW.TOUCHINGEVERYNATION.COM/MATERIALS.HTML
Chukua somo linalofuata na endelea na mafunzo.
57
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
RAMANI YA HUDUMA
Muhula 1 Kupitia huduma ya uinjilisti na darasa la uanafunzi anzisha seli kuanzia watu 2 hadi 10:
1._________________________________ 2._________________________________
3._________________________________ 4._________________________________
5._________________________________ 6._________________________________
7._________________________________ 8._________________________________
9._________________________________ 10.________________________________
Muhula 2 Waandikishe wanafunzi 2 (K2) (“wanafunzi”) ili kuanza Q1 SML:
1._________________________________ (K1)
Mimi
2._________________________________ (K1)
Muhula 3 Kupitia uinjilisti na darasa la uanafunzi wasaidie viongozi wako 2 “wanafunzi”
kuanzisha kanisa la nyumbani:
1._________________________________ (K1)
1.______________________________ 2.______________________________
3.______________________________ 4.______________________________
5.______________________________ 6.______________________________
7.______________________________ 8.______________________________
9.______________________________ 10._____________________________
2._________________________________ (K1)
1.______________________________ 2.______________________________
3.______________________________ 4.______________________________
5.______________________________ 6.______________________________
7.______________________________ 8.______________________________
9.______________________________ 10._____________________________
Muhula 4 Wasaidie wanafunzi wako 2 (K1)kuandisha viongozi 2 (K2) ili kila mmoja aanze Q1 SML:
3._____________________________ (K2)
1._____________________________ (K1)
4._____________________________ (K2)
Mimi 5._____________________________ (K2)
2._____________________________ (K1)
6._____________________________ (K2)
58
Muhula 5 Kanisa lako la nyumbani(seli) lijizidishe :
A. Wanafunzi wako 2 (K1) waendelee kuongoza seli/ kanisa la nyumbani.
B. Wasidie viongozi wako wa kizazi cha pili (K2) kuanzisha seli/ makanisa ya nyumbani.
Muhula 6 Hakikisha kizazi cha pili (K2) wanaandikisha viongozi wapya 2 kuanza Q1 SML
pamoja nao. (kamilisha kujaza ramani ya uduma kizazi cha 3 (K3) 2 Timotheo 2:2)
7._____________________ (K3)
3._____________________ (K2)
8._____________________ (K3)
1._____________________ (K1)
9._____________________ (K3)
4._____________________ (K2)
10.____________________ (K3)
Mimi
11.____________________ (K3)
5._____________________ (K2)
12.____________________ (K3)
2._____________________ (K1)
13.____________________ (K3)
6._____________________ (K2)
14.____________________ (K3)
Muhula 7 Hakikisha wanafunzi wa kizazi cha 3 (K3) wanaanzisha seli/makanisa ya nyumbani
Muhula 8 Hakikisha wanafunzi wa kizazi cha 3 (K3) wanaandikisha viongozi 2 wapya (K4) ili
kuanza Q1 SML. Kwa muda utakaomaliza SML, unatakiwa ukamilishe ramani ya huduma
(Angalia ukulasa unafuata).
Muhula 9 Endelea kuweka mikakati ya ramani ya huduma na viongozi wako [hadi kizazi cha 4
(K4)] ili kutengeneza mkakati wa kufikia mji, mkoa, taifa na ulimwengu kwa njia ya
injili.
59
RAMANI YA HUDUMA kufikia kizazi (K) cha 4 - 2 Timotheo 2:2
Kizazi 1 ! Kizazi 2 ! Kizazi 3 Kizazi 4
15._________________(K4)
7._____________________(K3)
16._________________(K4)
3._____________________(K2)
17._________________(K4)
8._____________________(K3)
18._________________(K4)
1._____________________(K1)
19._________________(K4)
9._____________________(K3)
20._________________(K4)
4._____________________(K2)
21._________________(K4)
10.____________________(K3)
22._________________(K4)
Mimi
23._________________(K4)
11.____________________(K3)
24._________________(K4)
5._____________________(K2)
25._________________(K4)
12.____________________(K3)
26._________________(K4)
2._____________________(K1)
27._________________(K4)
13.____________________(K3)
28._________________(K4)
6._____________________(K2)
29._________________(K4)
14.____________________(K3)
30._________________(K4)
Tunachotakiwa kukifanya ili kutimiza Agizo Kuu ni kuhakikisha kwamba kila
mwanafunzi anajizidisha hadi kufikia kizazi cha 4! MUHIMU: (K) inamaanisha kizazi
60
61
STRATEGIC IMPACT SHULE YA KUZIDISHA VIONGOZI [SML]
ZANA: KIPEPERUSHI CHA UINJILISTI V4.0
๏ Tunapokwenda kushuhudia kwa majirani au vijijini, tutakwenda katika timu ya watu 2 au 3
nyumba kwa nyumba, sokoni, au sehemu maalumu iliyoandaliwa. Tunapoenda kwenye
ushuhudiaji tunataka kutimiza mambo 5 kwa kila tunayekutana naye.
MAMBO MATANO MUHIMU YA KUTIMIZA TUNAPOENDA KUFANYA UINJILISTI
1. Toa ushuhuda wako binafsi.
‣ Jitambulishe kisha eleza kwamba tumewatembelea ili kuwaeleza mambo ambayo Yesu
Kristo amefanya katika maisha yetu.
‣ Washirikishe mambo ambayo Mungu ametenda katika maisha yako.
‣ Tumia dakika chache sana kutoa ushuhida wa maisha yako kabla ya kumpokea Kristo
na tofauti iliyopo baada kumpokea kuwa Bwana na mwokozi wako.
‣ Mwisho wa ushuhuda wako waulize kama wanapenda kufahamu namna ya kuwa na
uhusiano na Mungu na kupata uzima wa milele. ”
2. Washuhudie injili kwa kutumia kipeperushi cha ushuhudiaji cha SI kipo ukurasa
unaofuata.
3. Mkaribishe huyo mtu sehemu mnayokutana kwa ajili ya mafundisho andika muda
na mahali mnapokutana kwenye hicho kipeperushi kisha mwachie.
‣ Watie moyo wawakaribishe wenzao.
4. Weka miadi nao kuwatembelea tena kwa ajili ya ufuatiliaji na kuwafundisha Biblia
siku inayofuata.
‣ Andika maamuzi yao kwenye kipeperushi cha SI ile sehemu itakayochanwa, Andika
jina, anwani, namba ya simu.
‣ Chana hicho kipande cha karatasi zenye kumbukumbu baki nacho kisha waachie wao
kipeperushi.
5. Mwombee huyo mtu na familia yake Baraka za Mungu.
‣ Waulize kama sasa wanauhakika kwamba wamepata uzima wa milele.
‣ Waulize pia kama kuna jambo lolote wangependa uwaombee.
‣ Waombee ili waweze kukua katika imani pamoja na hitaji walilokueleza.
62
JINSI YA KUTUMIA KIPEPERUSHI CHA KWENYE USHUHUDIAJI
๏ Baada ya kutoa ushuhuda wako onyesha sehemu ya mbele ya kipeperushi na waulize kama wana
hakika ya uzima wa milele.
Unaweza ukasema hivi:
“Naomba nikuulize maswali machache ya namna
unavyoamini na nikuonyeshe kwenye Biblia jinsi
unavyoweza kuwa na hakika ya kupokea uzima
wa milele?”
1.Waonyeshe umbo la pembe tatu kwamba
inawakilisha Mungu. Uliza, “Je unamwamini
Mungu? Je unaamini kwamba anakupenda?”
Subiri jibu lake. Maswali haya yatakusaidia
kuwa na mazungumzo na huyo mtu badala ya
wewe kuongea tu.
2.Ni muhimu kusoma andiko kwenye Biblia. Anza
na Yohana 3:16.
• Muulize huyo mtu kama ana Biblia. Kama
anayo msaidie kwa kumwonyesha hilo
andiko mahali lilipo.
• Ni vizuri asome mwenyewe. Hata hivyo,
uwe makini kama ana tatizo la macho na
hana miwani, basi soma mwenyewe
3.Waonyeshe picha ya mtu. Waulize, “Unadhani
picha hii inawakilisha nini?” Wanaweza
kusema “watu” au “ibilisi”. Waambie kwamba
picha hii inawakilisha kila mtu duniani.
Waonyeshe ukanda mweusi unaowakilisha
kutengwa kwa mwanadamu na Mungu. Soma
Warumi 3:23 kisha waulize, “Biblia inasema
tumetengwa na Mungu kwa sababu tumenda
dhambi je unaamini kwamba wewe ni mwenye
dhambi?”
4.Soma Warumi 6:23 iliyotiwa kivuli cheusi
kuonyesha kutengwa kwa mwanadamu na
Mungu. “Je unaamini kwamba dhambi zako
zitasababisha kifo – yaani kutengwa na Mungu
milele?”
63
Yohana 3:16
Warumi 3:23
Warumi 6:23
5.Geuza upande unaofuata unaoonyesha
msalaba soma Warumi 5:8 kisha sema,
“Mungu anatupenda sote na amefanya njia ya
kumjua yeye kupitia mwanae, Yesu Kristo,
ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya malipo
ya dhambi zetu. Je unaamini kwamba Yesu
alikufa msalabani kwa ajili yako?”
6.Soma Yohana 14:6 kisha uliza swali, “Je
unaamini kwamba Yesu Kristo ni njia pekee ya
kupata uzima wa milele?”
7.Soma 1 Wakorintho 15:3-8 kisha uliza, “Je
unaamini kwamba Mungu alimfufua Yesu
kutoka kwa wafu?”
8.Geuza kipeperushi sehemu ya tatu onyesha
picha ya zawadi kisha waambie, “Mungu
anataka wewe upokee uzima wa milele na
anakupa bure.” Kisha soma Efeso 2:8-9 na
uliza swali, “Ukipokea zawadi kwa imani,
Mungu anakupa uzima wa milele (1 Yohana
5:11-12). Ukikataa zawadi hii Mungu anasema
utaishi Jehanam milele (2 Wathesalonike
1:8-10) Je ungependa kupokea zawadi ya
uzima wa milele zawadi ya kumwamini Yesu
Kristo leo?”
9.Kama jibu ni ‘ndiyo’ basi soma Yohana 1:12.
“Ukimpokea na kumwamini Yesu leo utakuwa
mtoto wake.” Leo unaweza kumpokea Yesu
kwa imani kwa njia ya Maombi. Maombi
hayakuokoi wewe. Lakini maneno ya maombi
yako yanaidhihirisha imani. Mfano wa sala ya
kumpokea Yesu: “Bwana Yesu, Nakuhitaji.
Nakiri kwamba mimi ni mwenye dhambi
naomba unisamehe dhambi zangu, nakupokea
kama zawadi ya milele kwa imani kuanzia leo.
Kwa jina la Yesu. Amina.”
10.Baada ya mtu kumkubali Mungu kama zawadi
ya Milele kwa imani leo, muulize swali, “Je
umeamini kuwa Yesu amekusamehe dhambi
zako na kukupa uzima wa milele?” Soma 1
Yohana 5:11-12, kisha uliza, “Kulingana na
maandiko haya Mungu anaahidi nini kwako
leo?”
64
Warumi 5:8
1 Wakorintho 15:3-8
Yohana 14:6
1 Yohana 5:11-12
Yohana 1:12
Efeso 2:8-9
2 Wathesalonike 1:8-10
MUHIMU:
• Usibishane na mtu kutokana na imani yake.
• Kama mtu anataka kubisha au ana hasira, washukuru kukupa muda wa kuzungumza
nao kisha nenda nyumba nyingine au kwa mtu mwingine. Kwa sababu kuna watu wengi
ambao wangependa kusikiliza injili
Hakikisha kwamba Waefeso 2:8-9 inaeleweka vizuri kwa watu.
• Watu wengi duniani wanadhani wanatakiwa kufanya kitu fulani ili kupata uzima wa
milele.
• Wahakikishie kwamba wokovu ni kwa neema na ni kipawa kinachotolewa bure na
Mungu kulingana na Waefeso 2:8-9
MUHIMU: Ukikutana na mtu ambaye ana shauku ya kukusikiliza, muulize kama kuna mtu
mwingine katika familai yake ama marafiki ambao wangependa kujadiliana maswali haya.
Wakisema ‘Ndiyo’, basi waombe wakusanye familia zao ama marafiki pamoja Kisha
mjadiliane maswali haya kama kikundi na washirikishe injili. Huu utakuwa ni mwanzo wa
kanisa jipya. mtu huyu anaweza akawa ni ‘mtu wa amani’ ambaye Yesu alimzungumzia
(Soma Yohana 4:1-42 na Luka 10:1-6).
Mtu wa amani ni mtu ambaye:
1) Anaonyesha urafiki kwako, mwinjilisti,
2) Yuko tayari kupokea mambo ya kiroho,
3) Ni mtu mwenye ushawishi katika jamii,
4) Anaweza kukusanya watu wengine waweze kusikiliza.
11.Chukua mawasiliano au anwani yake kwa ajili
ya ufuatiliaji.
12.Chana hicho kipeperushi, tunza maneno ya
chini
13.Mwachie hicho kipeperushi mtu aliyempokea
Yesu.
14.Mpe mchungaji mawasiliano ya huyo mtu.
"
65
Jina
Anwani
Leo nampokea Yesu kuwa Bwana na Mwokozi.
Nataka kujua jinsi ninavyoweza kukua kiroho
Katika imani ndani ya Kristo.
Simu
Tarehe
Siku Muda
Ninapenda kujifunza Biblia na watu
Wengine/majirani
Mwinjilisti/Mshuhudiaji:
MAELEZO YA UKUMBUSHO
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
66
MAELEZO YA UKUMBUSHO
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
67
MAELEZO YA UKUMBUSHO
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
68
MAELEZO YA UKUMBUSHO
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
_____________________________________________
69
MSIMAMO WA IMANI
MUNGU
Mwanzo 1:1; Kumbu 6:4; Mathayo 28:19; Yohana 4:24; 10:30:2 Wakorintho 13:14.
Tunaamini ya kwamba kuna Mungu mmoja wa kweli, Mungu Mtakatifu, anayeishi milele katika nafsi
tatu - Baba, Mwana na Roho Mtakatifu - kila nafsi inasifa au tabia za kiungu. Tunaamini kwamba
hapo mwanzo Mungu aliumba ulimwengu na vyote vilivyomo ndani yake kutoka mahali pasipo na
kitu, Ili kuudhihirisha utukufu wa uweza wake, hekima na wema wake. Kwa uweza wa Uungu wake
anaendelea kuutegemeza uumbaji. Katika historia yote ametenda kama mtoaji ili kutimiza malengo
ya ukombozi.
YESU KRISTO
Mathayo 20:28; Matendo 4:12; Warumi 5:10; Wakiorintho 5:18 -19; Yohana 2:2
Tunaamini kwamba Yesu Kristo ni nafsi ya pili katika Utatu Mtakatifu ambaye alikuwa
ameunganishwa na asili ya kibinadamu kimuujiza kwa njia ya kutungiwa mimba na kuzaliwa na
bikira. Aliishi maisha makamilifu na utii kwa Baba na kwa hiari yake alijitoa kuwa fidia ya dhambi
kwa kufa msalabani badala yetu, kwa kufanya hivyo alitimiza haki ya malipo ya wokovu na uzima
wa milele kwa kila atakaye mwamini. Alifufuka katika mwili na kutukuzwa. Alipaa kwenda mbinguni
Na ameketi mkono wa kuume wa Baba, mahali ambapo yuko kama mpatanishi kati ya Mungu na
wanadamu, na anadumu katika kutuombea. Atarudi tena duniani katika mwili ili kuukamilisha wakati
na mpango wa Mungu wa milele.
ROHO MTAKATIFU NA MAISHA YA KIKRISTO
Yohana 15:26; 16:8 - 11
Asili ya maisha ya kweli yenye uhusiano na Yesu Kristo baada ya kuokoka ni maisha matakatifu na
utii, anayo yapata mwamini baada ya kujinyenyekesha kwa Roho Mtakatifu, ambaye ni nafsi ya tatu.
Alitumwa ulimwenguni na Mungu Baba pamoja na mwana ili kusaidia kazi ya Kristo ya ukombozi.
Huangazia akili ya waovu, huamsha utambuzi wa umuhimu wa wokovu ndani ya maisha ya mtu na
kumpa maisha mapya. Wakati mtu anapopokea wokovu huingia ndani ya mwamini na kufanya
makao, Yeye ndiye chanzo cha nguvu, hakika ya wokovu na hekima, na kwa namna ya kipekee
Roho Mtakatifu humpa kila mwamini vipawa kwa ajili ya kuujenga mwili wa Kristo. Roho Mtakatifu
humuongoza mwamini kuelewa na kutumia maandiko. Nguvu na maongozi yake vinapatikana kwa
imani, Roho Mtakatifu ndiye anaye mwezesha mwamini kuishi maisha ya mfano wa Kristo na kuzaa
matunda kwa utukufu wa Baba.
BIBLIA
2 Timotheo 3:16; 2 Petro 1:21
Chanzo cha kuamini kwetu ni Biblia yenye vitabu sitini na sita vya Agano la kale na Agano jipya.
Tunaamini kwamba chanzo cha maandiko yote ni Mungu. Tulipewa maandiko haya kupitia
wanadamu walio chaguliwa na Mungu. Maandiko yanaongea kwa mamlaka ya Mungu wakati huo
huo mazingira, muundo wake na kamusi ya maneno ni ya mwandishi mwanadamu. Tunaamini
kwamba maandiko hayawezi kubadirika na kwamba hayana makosa tangu asili. Tunaamini kwamba
maandiko ni ya kipekee yenye mamlaka ya mwisho katika maswala yote ya imani, tabia na
mwenendo, na hakuna maandiko mengine yoyote yaliyovuviwa na Mungu zaidi ya haya.
70
WOKOVU
Warumi 3:23; 5:8; Waefeso 2:1,8-9
Kusudi la msingi la ufunuo wa Mungu katika Maandiko ni kuwaita watu wote katika ushirika pamoja
naye. kimsingi tuliumbwa ili kuwa na ushirika na Mungu lakini mwanadamu aliasi na kuchagua njia
yake mwenyewe, na hapo ndipo alipotengwa na Mungu na kuteseka kwa sababu ya uharibifu wa
asili, na hivyo kupelekea kushindwa kumpendeza Mungu. Anguko la mwanadamu limetokea tangu
mwanzo wa historia ya mwanadamu na tangia hapo wanadamu wote tumeathiriwa na madhara ya
anguko, hivyo kila mtu anahitaji neema ya wokovu wa Mungu, wokovu wa wanadamu wote ni kazi
ya neema ya Mungu, hautokani na matendo mema ya mwanadamu, wokovu unapokelewa kwa
neema kwa kila mtu anayemwamini Yesu. Mungu anapoanza kazi ya wokovu kwenye moyo wa mtu,
ametupa uhakika kupitia neno lake kwamba kazi hii itaendelea hadi ukamilifu wake.
HATIMA YA MWANADAMU
1 Wathesalonike 4:16-17; Waebrania 9:27
Tunaamini kwamba kifo kinakamilisha hatima ya kila mtu. Tunaamini kwamba wanadamu wote
watafufuliwa katika mwili ili kusimama kwenye hukumu itakayoamua maisha ya mtu kulingana na
alivyoishi. Kuna hukumu ya milele kwa watu ambao hawajaokoka na kuna Baraka ya milele kwa ajili
ya watu waliokoka. Wale waliomwamini Kristo watapokelewa na kuwa na ushirika na Mungu milele
na kupewa thawabu kutokana na kazi walizo fanya katika maisha yao.
KANISA
Matendo 2:42; Warumi 12:1- 6
Matokeo ya kuunganishwa na Yesu Kristo ni kwamba waamini wote wanakuwa washirika wa mwili
wake, yaani kanisa. Kuna kanisa moja la uhakika ulimwenguni linalo jumuisha watu wote
waliomwani Yesu Kristo kuwa Bwana na mwokozi wa maisha yao. Maandiko yanahimiza kwamba
waamini wote tukusanyike pamoja kwa ajili ya kuabudu, kuomba, kujifunza Neno, kubatizwa,
kushiriki meza ya Bwana na kutunza maagizo ya Kristo, ushirika, ibada katika mwili wa Kristo,
kuendeleza na kutumia vipawa na karama na kuufikia ulimwengu. Mahali popote ambapo watu wa
Mungu wanakutana kwa sababu ya utii wa maagizo yake kunakuwa na udhihirisho wa kanisa. Chini
ya uangalizi wa wazee na viongozi wengine washirika wanafanya kazi pamoja kwa upendo na
umoja kwa lengo la kumuinua Kristo kwa utukufu wa Mungu na kwa utimilifu wa Agizo kuu.
IMANI NA MATENDO
1 Wakorintho 10:24, 31; 2 Timotheo 3: 16-17
Maandiko ni mamlaka ya mwisho ya mambo yote yanayohusu imani na mwenendo. Tunaamini
kwamba akili ya mwanadamu haiwezi kufungika katika maeneo ambayo maandiko yamenyamaza
kimya. Hata hivyo kila mwamini ataongozwa na Bwana katika maeneo hayo kwa kuwa sote
tunawajibika kwake.
71
MAELEZO YA MWANZO NA MAREKEBISHO YA SASA:
v1.0 (2009)
" - Toleo la kwanza lenye masomo 24
v1.1 (2010)
" - Mgawanyo wa masomo yakawa 10. Soma moja kwa kila muhula wa mwaka.
" - Kulekebisha maneno.
" - Kuongeza vikundi vya majadiliano na maswari katikati ya somo.
" - Tafsiri kwa lugha ya kuanzishwa spanishi.
" - Mabadiriko ya jina kuwa shule ya kuzidisha viongozi (SML)
" - Kuongeza maswali ya uwajibikaji
v1.1.1 (February 2011)
" - Mwendelezo wa kufomati kazi hii
- Kupitia mifano kwenye somo la 4
" - Kubadilisha kulasa
" - Kuboresha maswali ya uwajibikaji
" - Kuongeza mapitio ya SI
" - Kuongeza majedwari ya SML ya kujidizidisha.
" - Kuongeza mifano ya hatua kumi
v1.1.2 (April 2011)
" - Kupanua mifano ya hatua 10 za mifano
" - Kuongeza ukubwa wa “Q1” kwenye jarad
" - Kuongeza anuani ya mratibu, majina ya wana kikundi, na mahali pa kukutana
" - Muda na siku, ukubwa wa maandiko na mahali pa kusoma
- Kuongeza recodi ya mahudhurio na jedwali la maandiko ya kusoma.
v1.2 (2012)
" - Marekebisho makubwa ya mtiriko wa SML
" - Nyongeza ya maeneo ya kujaza kwa mtu aliyemaliza muhula.
" - Kuboresha maswali ya uwajibikaji
" - Kuongeza mti wa uongozi wa familia na upandaji wa makanisa ya nyumbani.
" - Kuongeza nyenzo ya kipeperushi cha SI
STRATEGIC IMPACT
P.O. BOX 830337
RICHARDSON, TX 75083
WWW.TOUCHINGEVERYNATION.COM
© Copyright, Strategic Impact. No changes may be made to this manual, but you
may freely copy and distribute without making changes to content.
© Copyright, Strategic Impact. Usifanye mabadiriko yoyote kwenye masomo haya
isipokuwa unaruhusiwa kutoa nakala na kuwagawia wengine.
72

No comments:

Post a Comment