Friday 5 December 2014

KUFUASA

MAKABILI YA MWANAFUNZI
na
Jerry pamoja na Nancy Reed
MAKABILI YA MWANAFUNZI
na
Jerry na Nancy Reed
KIMETAFUSIRIWA NA PASTOR KINGORI
PAMOJA NA
PASTOR MANYARA WANAFUNZI WA
NORTH PARK THEOLOGICAL SEMINARY
Copyright 2002 Kiswahili na Pastor Kingori Pamoja na
Pastor Manyara
Kijabe Printing Press
P.O. Box 40
Kijabe
UTARATIBU WA YALIYOMO
Mwanzo i
Utangulizi iv
Mpango wa Makabili
Hatua ya Kwanza Mambo manne ya uhakika wa kuwa mkristo 1
Hatua ya Pili Nguzo ya mwanafunzi 2
Hatua ya Tatu Ngurundumu 4
Hatua ya nne U Bwana wa Kristo 5
Hatua ya Tano Roho Mtakatifu 7
Hatua ya Sita Neno 10
Hatua ya Saba Maombi 12
Hatua ya Nane Ushuhuda 14
Hatua ya Tisa Ushirika 16
Hatua ya Kumi Muumini Mtiifu 18
Nyongeza ya Mafundisho
Usaidizi wayanayo kupasa kufanya 20
Hatua unazoweza kufanya nazo
Biblia, Mungu na Watu 23
Mfano wa Daraja 26
Makaratasi ya kuweka maendeleo ya kila makabili ya mafanikio (karatasi tayari)27
Utaratibu wa maombi (karatasi tayari) 29
Mkutasari wa mistari ya Biblia kwa moyo 30
Vifungu via Biblia ambazo 31
Kusoma Maandiko 32
MWANZO WA MAKABILI YA UWANAFUNZI
Subiri! Usisome tena hadi utakaposoma utangulizi wa Makabili haya ya uwanafunzi. Onyo katika utangulizi inahimiza kwamba kujua tuu sio maana hasa yakuwa na uwanafunzi bora.
Tafadhali weka alama katika saduku ukisha soma utangulizi.
Shukurani kwa kusoma utangulizi. Hapa kuna yale unayoweza kufikiria ya kusaidie unapo endelea katika njia hii ya uwanafunzi:
1) Rudia mambo ya kufanya ya kukusaidia kwa uwanafunzi inayo patikana katika
ukurasa wa 24 ya nyongesa ya mafundisho.
Tafadhali weka alama katika saduku ukisha soma usaidizi wa mambo ya
kufanya.
2) Sasa angalia ukurasa 27 na 29 . Haya yanajulikana kama Biblia, Mungu na watu na inasimamia Mahali Pengine ambapo unaweza kuanzia katika njia ya uwanafunzi. Unaweza kuona katika utaratibu wa yaliomo ya kwamba hatua hii inaanzisha mazungumzo kuhusu Mungu ni nani, Biblia ni nini na Vile Mungu amefanya ndani ya Kristo ili watu Waweze Kumjua. Tazama Ukurasa 30 . Haya ni maelezo ya mfano wa daraja ambao wengi wamefaidika kwa kuweza kumwongoza mtu katika uhusiano wa kibinafsi na yesu Kristo.
Tafadhali weka alama katika sanduku ukisha soma ukurasa 27 , 29 , na 30 .
3) Sasa tazama katika karatasi ya maendeleo ukurasa 31 na 33 . Tengeneza makaratasi kadhaa ya kurasa hizi mbili za kila kudi ya makabili uliyo nayo. Halafu andika jina au majina ya mwanafunzi au wanafunzi wako katika nafasi ambayo umepewa juu ya ukurasa. Katika mwisho wa kila makabili ya uwanafunzi weka alama ya cho chote kile mmefanya (wakati mwingine hamtafanya yale yote yalio katika utaratibu kwasababu utakuwa ukifanya mambo mengine muhimu). Andika tarehe ya makibili mengine kado ya mahali mnapo tarajia kuanzia.
Tafadhali weka alama katika sanduku ukiisha tengeneza makaratasi ya
maendeleo.
4) Kumbuka umuhimu wa kuuliza swali. Swali ni rafiki yako. Yatumie unapo wafundisha wanafunzi wengine. Maswali huwezesha mwanafunzi au wanafunzi wako kuzungumza na kushirikiana kimawazo na kujua na wakati mwingine itaongoza maongezi yasio tarajiwa lakini ni maongozi ya muhimu.
5) Unapo anza, kubalianeni pamoja mda mtakao tumia kwa kukutana pamoja. Mnaweza kushauriana kukutana wiki mbili au tatu halafu mjadiliane juu ya wakati mrefu ikiwa wewe na
mwanafunzi au wanafunzi wako mtakubaliana. Njia nyingine ya mkondo wa kwanza na mtu fulani ni kutengeneza karatasi ya hatua ya kwanzi isio na laini ya juu inayosema Hatua ya Kwanza na kurasa -1-. Katika jia hii hatua ya kwanza anasimama peke yake na haishauri yakwamba kuna mengine yanayo fuata. Kwa hivyo ina kuwa rahisi kuwa na mwisho wa mapema ikiwa utagudua ya kwamba kikundi hakiendelei vizuri.
Jihadhari na “kulegea” kwa uhusiano wenu kabla ya mwisho wa somo. Zaidia wale wanao fanyika wanafunzi kuwa na nia ya kuendelea, kidogo kidogo mnapo endelea kukua pamoja. Unapomaliza hakikisha unamalizia kwa nguvu. Usififie tu.
6) Jambo la mwisho la kufidilia kabla hujaanza kufanya mwanafunzi yeyote ni la mzingi na linachukuliwa kwa mzaha. Nini madhumuni au matarajio yako ya kufanya mtu au watu wanafunzi uliyo nayo fikivani sasa? Kuna njia tofauti ya kujibu swali hili.
Majibu yanayo wezekana yanaweza kujumuishwa na vitu kama mzingi wa kuelewa vile maisha ya mkristo yalivyo, uwezo wa kufundisha wakristo wapya, fafunzo ya uongozi ya vikundi, vichanga, kujitayarisha kwanzisha kanisa jipya, kufundisha watu wanaoweza kusaidia kazi ya uchuugaji, kuwatayarisha wale ambao wanaweza kufunza shule ya jumabili au na kuwauezesha wale ambao wanaweza kuongoza lbada ya kuabudu. Madhumuni ya yale yote yametajwa hapo juu ni kuinua kizazi kingine cha wanafunzi. Tumia mawazo yako kufikivia juu ya mengi mengine yanayowezekana kwa kutoa mwelekeo halisi kwa njia ya uwanafunzi.
Tena ni nini lengo lako la kumfudisha mtu wakati huu?
Andika lengo au malengo yako hapa kwa kumaliza mstari huu.
Lengo langu wakati huu la kuwa pamoja na (jaza njina au majina ya Watu 1, 2, au 3 hapa).
__________________________,__________________________
__________________________
ni ya: ____________________________________________________
Weka alama saduku hii wakati utakapo andika lengo au malengo yako.
Kumbuka wasiwasi utakao kukumba wakati utawakalibia wale ambao unataka muwe pamoja na mkue unatoka kwa adui wetu wa kiroho. Hataki mpango huu wenye nguvu na ulio wa maana uazishwe. Lakani tuna ushindi ndani ya yesu. Kwa hivyo omba na Uende, ukimuuliza Roho Mtakatifu akujaze na akutumie.
UTANGULIZI
Hadithi inayo Kua
Labda hakuna kitu kingine ambacho huridhisha kama kujua kwamba Mungu anakutumia kutia moyo mtu mwingine ili akuwe kama mkristo. Miaka ishirini iliopita ma mia ya watu wamegundua maana ya furaha na kuridhika kutokana na kumsaidia mtu mwingine kukua katika maisha yake ya ukristo kwa kutumia
Makabili ya uwanafuzi.
Marvin Ladner, mfanyi biashara ambaye alikua wa kwanza kunifanya mwananfuzi katika chuo kikuu, alipanda mbegu ambayo inaendelea kukua. Kwanza huko Equador, halafu zaidi huko Mexico, njia rahizi lakini ya maana katika taratibu ya uwananfunzi ambayo imeonyeshwa hapa ilionekana wazi wakati tulipo wafundisha viongozi ili waazishe makanisa na kuyahudumia. Taratibu hii inaendelea. Iliaza kwa kihispaniola halafu kiingeraza halafu sasa mpango huu wa uwanafuzi umeedelea hadi Spanish, English, French (Europe), French (Democratic of Republican Cango), Japanese, Korean, Liugala, Swedish, Tagalog (Philippians), Russian, Tenyidie (Angami), Bulgaria, Paite, Burmese (Swahili), Ufarasa Ujapani, Korea, Lingala na utafusiri wa Lugha Kule Urusi.
Tunapo tazama taratibu za makambiri ya uwanafuzi katika mbango huu tumegundua watu wanaotumia nja hii ya makabiri ya uwanafuzi katika njia tofauti. Kurasa zinasofuata zimebuniwa kumsaidia kiiongozi wa wanafuzi awe na uhakika wakujua kuwatalisha wanafuzi.
Njia Nyembamba Na NJia Pana Ya Uwanafunzi
Neno uwanafunzi kwavikundi vingine imekuwa sawa sawa na mafundisho au elimu ya ukristo. Maana ya uwanafunzi la makabiri haya ya uwanafuzi ni nyembamba au ya umuhimu wa uhusiano mbaina wa mtu anayejua na mmoja, wawili au watatu wengine. Hii inaweza pia kuitwa mwangozo wa uhusiano ambayo hekima, ufahamu, kujua na maono imepatiwa mtu moja hadi mwingine.
Kuzidisha Viongozi
Aina hii ya uwanafunzi hufanya kazi vizuri katika sehemu yoyote ya maisha ya kanisa na ukasisi. Pia aina hii ya uwanafuzi inaweza kutumika kwa walimu wa shule ya Jumapili, Kwa viongozi wa lbada na waanzishi wa kanisa au yeyote aliye na ono ya kuzidisha aina yake.
Umoja na Utunzaji Ndani ya Kanisa
Nilipo wahoji walimu walio na ujuzi wa zaidi ya miaka kumi na miwili nilishangaa kuona ya kwamba uwanafunzi huleta matokeo muhimu ya mazao ya kuwaleta watu pamoja katika kanisa na kuwafanya marafiki wa kweli. Mchungaji Roberto Gonzalez mmoja wa wale waliokua na ujuzi wa walimu alisema kwamba katika kanisa lake ukasisi wa uwanafunzi ulileta hamu ya kuntunsana kati ya washiriki. Aliongea juu ya mshiriki ambae_ alimujua mwingine saidi ya miaka kumi na sita, lakini hakuwa rafiki hasa. Sasa (kwa sababu ya uwanafuzi) wamekua marafiki wa karibu na wakutunzana moja kwa mwingine.
Zaidi Ya Moja Kwa Moja
Watu hukosea wanaposema juu ya nguvu za elimu zinazoendesha kamanjia ya kumfikia uwanafunzi mmoja kwa mmoja. Kama vile-ilivyo kweli hua tunakutana na uwanafunzi mmoja kwa mmoja, hii ni lazima ionekane ni njia nzuri ya kuridhisha. Kwa kweli watu wawili, watatu au zaidi katika kidu hupeana motokeo mazuri ya elimu ya nguvu inazo endesha kwa uwanafunzi. Panapo wawili au watatu pamoja mapatano ya kuwa kiugo cha mwili wa Kristo huonyesha kujua zaidi. Maisha ya mwili wa Kristo inaweza kueleweka kwa urahisi katika tangulizi hii. Kunakufunga-mana vilevile kwa kupasishwa inayo onekana wakati kuna zaidi ya mwanafunzi mmjo kwa makabili.
Uwalimu Au Kufundisha? (Kukutana Au Darasa?
Neno la muhimu kwa wale ambao wanatumia vifaa hivi kabla hujaanzisha "Kufundisha' watu unapaswa kukata kauli. Kauli hii ni lengo mmoja. Una mpango wa kufundisha mambo yaliomo katika makabili ya uwanafunzi au utawafundisha watu wachache ukitumia maneno machache ya kukusaidia katika taratibu ya uwalimu? Kama lengo lako ni lakufundisha mambo yaliomo ndani ya vifaa hivi ninakuhimiza ufanye hivyo bila kuita taratibu hii uwanafunzi. Uwanafunzi ni zaidi ya kufundisha mambo yaliomo. Kama unatafuta jina lakutumia unapofundisha kwakutumia vifaa hivi unaweza kuliita kufundisha mzingi wa Ukristo. Katika jia hii utakuwa na "madarasa" lakini si "kukutana" mnapo kuwa pamoja. "Kukutana" ni mkutano mbaina yako na mwanafunzi au wanafunzi pamoja na Bwana Kwa Kukuwa kupitia maombi, ushirika unao tia nguvu, na kwifunza Biblia ukitumia maisha ya kila siku.
Kufanyiza au habari?
Ni njia hii maalum ya uwanafunzi ambayo inatiliwa mkazo na taratibu hizi. Lengo ni kukua kwa mkristo kuwa kama kristo. Kusudi ni kumfanya mtu awe na maisha ya kiungu na tabia nzuri sambamba na msingi wa elimu ya Biblia. Ukilinganisha mafundisho ndani ya darasa, elimu au habari ndiyo lengo; wakati katika uwanafunzi kufanyika (kwamfano) kanuni thamini, maono, na kusudi, pamoja na elimu huwa lengo. Kwa upande mmoja, njia ya kufundisha hutuambia kuwa Yesu ni Bwana. Kwa upande mwingine njia ya uwanafunzi hutusaidia kuwa na maarifa ya ubwana wa kristo katika maisha yetu ya kila siku.
Njia hii ya uwanafunzi ina kielelezo kuwa maisha hugawanywa pamoja na wengine. Kuna kukua pamoja. Maono na kazi zote hushirikishwa na kufunzwa. Kumtegemea bwana yesu huongezeka na tunda huzaliwa. Kwa hivyo uwanafunzi unaweza kushirikisha kulea, uwinjilisti, kuanzisha kanisa, maombi, kusujudu, na haki na amani zote pamoja wakati mmoja.
Wakati mzuri wa kuonyesha maono (vision)
Viongozi nilazima wawe na maono -- picha ya mawazo ya vile kesho kutakua. Viongozi hao huona miaka ya kesho ya kazi ya bwana na mambo mazuri ambayo yanaweza kutendeka. Hata hivyo, wengi wa wale wanaonyesha maono wamegundua kuwa wanafunzi wao (disciples) huenda wakasahau maono (vision) baada ya mda wa miezi kadhaa kama maono hayo hayatarudiwa mara kwa mara kwa njia nyingine. Makabili haya hupeana nafasi ya kuonyesha maono na kutia nguvu maono hayo kwa mda wa miezi kadhaa.
Maisha ya mmoja kushawishi maisha ya mwingine
Mfano unaweza kusaidia kuonyesha uhusiano wa ndani wa mtu mmoja kushawishi mwingine kwa njia ya kulea wanafunzi. Kama vile Susana alivyo mwangalia mama yake akishona kamba ya makonge, naye alikata nyasi akaanza kufanya kamba yake na kuangalia kazi nzuri aliofanya. Kwa mshangao ilikua sawa na ya mama yake. Wakati mama yake alipotazama, aligundua kuwa Susana alitengeneza kamba na nyazi.
Susana alifanya yote yaliyo takikana, lakini matokeo yalikuwa tofauti. Alikosea kitu kimmoja -- hakutumia makonge. Na hivyo ndivyo ilivyo kwa uwanafunzi. Kutumia taratibu kama vifaa vya kufundisha nisawa na kutengeneza kamba ya nyazi. Kwa uwanafunzi wa kweli kutendeka nilazima tugawane makonge ya maisha yetu. Makonge yetu nikama maono yetu, juhudi ya roho, taamaa ya kumjua mungu, unyonge wetu na, kumtegemea Bwana, kutafuta kujazwa na roho mtakatifu, uadilifu wetu,lutakatifu wetu -- haya yote na mengine. Mambo haya nirahisi kushikwa kuliko kufundishwa. Hiyo ndiyo sababu tunasema yakwamba taratibu ya makabili ndiyo sababu ya kukutana pamoja.
Wakati na Kuzidisha
Tunda la uwanafunzi huonekana baada ya kutenga wakati wa uhusiano na Uonyeshe makonge ya maisha yako kwa kushawishi wanafunzi wako (unapoendelea kumtegemea Roho Mtakatifu aendelee kukujaza). Hakuna njia ya mkato. Hii ni kazi ya zaidi ya wiki kumi. Miezi sita hadi miaka miwili ni hali ya ukweli. Nimegundua miezi tisa inatosha kwa uhusiano wa uwanafunzi ambao wamefika hatua ya tano ndani ya somo, wanapaswa kuchagua watu ambao watakuwa wakikutana nao kwa kawaida kwa “makabili yao ya Uwanafunzi”.
Hii inamaanisha yakuwa utapatikana wiki baada ya wiki kuwatia nguvu na kuwasaidia wanafunzi wako wawe na uhakika na ushawishi wa kudumu kwa kizazi kijacho cha wanafunzi. Kimawazo wakati utamaliza hatua ya kumi na zinginezo ?kujifinza mandiko matakatifu? somo la Biblia, wanafunzi wako wanapaswa kufanya vyema katika makabili yao na unaweza kuanza tena na kundi lingine ndogo la watu wawili au watatu.
Nimekuwa na kutofaulu katika uwanafunzi. Wakati mwingine mwanzoni wa njia hii na wakati mwingine baadaye, mtu mmoja huwacha kuendelea. Nimefanya kazi na wale ambao hawafanyi wanafunzi mara ya pili. Hali kama hii hunirudisha kwa Bwana katika kumtumainia na unyonge. Hata hivyo ushindi huzidi mara nyingi kutofaulu. Uwanafunzi unathamani kuliko kutofaulu katika mwenedo huu. Tunajifunza kila wakati.
Utangulizi huu nilazima utumike kama uongozi lakini sio kanuni. Lakini kuna kanuni mmoja inayopasa kuendelea kutumiwa kwa njia ya mafundisho ya uwanafunzi: Je kile ninacho fundisha, kinaonyesha, na kudhibitishwa kwa urahisi kukabidhi na kupatiwa “mtu mwingine”? Sisi husikia mahubiri mengi mazuri, na kuna semiinar nyingi nzuri na madarasa yanayopatikana amboyo husaidia kujenga maarifa yetu. Lakini mengi hayakufanywa yaweze kupitishwa kwa urahisi kwa wengine. Fanya iwe rahisi.
Sababu ya Kukutana Pamoja
Kwa vile njia ya elimu ya Uwanafunzi hutegemea mambo kadhaa yaliyo tajwa hapo awali, tunapaswa kujitahidi kuepuka mitego ambayo inaweza kuifanya iwe darasa lingine au njia ya kutumia wakati tu. Kwahivyo taratibu ya makabili ya uwanafunzi huwa sababu ya kukutana pammoja na kukua pammoja. Watu wote waliohusika katika njia hii hukua pammoja.
Ninani nitakaye fanya kuwa mwanafunzi?
Swali linatokea kila mara “Ninani nitakaye fanya kuwa mwanafunzi”? Kuna hiari tano ambazo nitataja hapa:
1. Wakristo wapya. Hapo mwanzoni makabili yaliandikwa kwa wakristo wapya iliwaweze maramoja kushuhudia imani yao mpya ndani ya Yesu Kristo kwa jamii zao na marafiki. Mzingi wa njia hii ilikua ono ambalo wakristo hawa wapya wataanza kufanya wanafunzi marafiki zao wenyewe na jamaa mara tu wanapo mwamini Yesu Kristo.
2. Wakristo wenye moyo wa bidii. Bila mwelekeo wa wazi na lengo, wakristo wachanga wenye mioyo ya bidii kwa urahisi hupoteza ubichi katika mienendo yao na Bwana Yesu. Makabili hutoa maneno yalio tangulia na lengo la kuendelea kukua na maana halisi ya kazi ya Bwana.
3. Wakristo wa wakati fulani. Makabili hutoa mjengo wa kusaidia wakristo wa wakati kutengeneza akili zao ili waweze kuwapatia wengine -- hasaa kwa wale wakristo wapya abao wamekua wakiwaombea. Vile vile utaratibu hutoa nafasi ya kuwezesha kufanyika upya kati ya wale wanaotamani wingi wa Mungu katika maisha yao. Katika uwanafunzi sisi hukua pamoja -- zote mwanafunzi na pia mwalimu.
4. Wale abao si wakristo. Makabili yanaweza kutumiwa kwa kusaidia wale bado kuwa wakristo kupeleleza maana yakuwa mkristo. Kama hivi ndivyo ilivyo taratibu ya yaliyomo itawaongoza kwenye hoja mbali mbali au mahali pakuanzia ili waweze kufaidika katika makabili yao pamoja.
Shukrani
Mwalimu tayari atatabua kwamba taratibu hizi zina machache sana yalio ya mwanzo . Bibi yangu Nancy, nami tulitunga utaratibu wa kwanza kule Ecuador, Marikani ya kusini. Tulitumia mfano wa gurudumu wa Navigator’s ili kuelewa mambo muhimu ya masomo. Baadaye kufuatia mageuzo ya gurudumu ya Dale Bishop’s na Keith Tungseth’s tukaongeza kitovu cha gurudumu Kusimamia Roho Mtakatifu. Wanafunzi wengi, waalimu na marafiki walio katika kazi ya Bwana wamesaidia maendeleo ya kitabu hiki. Tunataka kumshukuru Tim ek kwa kusaidia katika utaratibu wa kujielewa katika maisha ya Ukristo. Shukurani ya namna yake inaenda kwa Jerry na Vicky Lave, Wa missionary marafiki Zetu Kule Mexico, Kwa kusaidia na kujaribu kazi hii na Kufanya marekebisho ya taratibu na kwa maendeleo na kutimiliza somo linalo patikana katika nyongeza ya mafundisho. Pia tunashukurani kwa Carl Racine, Mimishonari wa muda mfupi kule Ecuador na Mexico, werevu wake na mashauri yake. Shukurani zetu ni kwa maendeleo mapya werefu na mawazo ya marekebisho inaenda kwa aliyekua mishonari wa muda mfupi kule Mexico na Mchungaji wa vijana alieko sasa,
Keith Hamilton. Shukurani zingine ni kwa wanafunzi wa seminari ya North Park Chicago Wachungaji Simon Kingori Muhota Pamoja na Paul Manyara kwa kuisaidia na utafsiri kwa lugha ya kiswahili na mpiga Chapa Bi Michelle D. Bynum.
Hata baada ya kurudi Marikani, Mimi (Jerry) na Fudisha Uinjilisti, Kukua kwa Kanisa na Uwanafunzi katika Shule ya Theologia ya North Park. Nancy hufanya Kazi Katika Ofisi ya Kanisa letu ya Latin American Ministries. Tunaendelea kuhusika katika njia ya uwanafunzi. Tumetumia mwisho wa juma mwingi tukifanya kazi na wachungaji na watumishi wengine wa kanisa katika semina za uwanafunzi katika marekani, Canada, Asia, Europa, na Latin America. Werevu na majibu ya wanafunzi yaliyopatikana Kutokana na Semina na hata kutoka kwangu, wanafunzi na ujuzi wa kibinafsi yameonyeshwa katika jadala la wakati huu la Makabili ya Uwanafunzi. Pia tumeendeleza mwongozo kwa walimu itumiwe sambamba na makabili. Mwongozo uko ndani ya karatasi wazi na niusaidizi kwa wale ambao wanaanza kazi ya uwanafunzi ilio na matokeo ya furaha.
Chicago, Julei, 1999 Jerry pamoja na Nancy Reed
HATUA YA KWANZA -1-
MAMBO MANNE YA UHAKIKA WA WOKOVU
1. Kama mtu akikuliza njia ya Kuwa MKristo unaweza Kumjibu Namna gani?
2. Wokovu unatokana na Kumwamini Yesu Kristo Peke yake. Kitabu Kama mambo manne ya Kiroho inatusaidia kueleza wengine vile wanaweza kumkubali yesu na Kuwa WaKristo.
2.1 Kuwa MKristo Kutokana na Kitabu cha warumi
A. Shida ya mwanadamu: Dhambi - Warumi 3:23
B. Mshahara wa dhambi na zawadi: ya Mungu - Warumi 6:23
C. Upendo wa mungu hata nikiwa mwenye dhambi - Warumi 5:8
D. Imani na Kunyenyekea Kwa u Bwana wa Yesu – Warumi 10:9
2.2 Wokovu ni zawadi ya mungu - Waefeso 2:8-10
2.3 Mpango Pamoja na njia ya Wokovu -
Ufu 3:20, Yn 1;12 na Warumi 10:9. *
3. Njia nne za uhakika
Shetani anawashambulia wakristo wachanga kwa njia inne. Tunajikinga na neno la mungu kama vile yesu alifanya -Matayo 4:4,7,10
3.1 Uhakika wa wokovu
I Yohana 5:11, 12 
3.2 Uhakika wa ushindi
I Wakorintho 10:13 
3.3 Uhakika wa Kusamehewa
I Yohana 1:9 
3.4 Uhakika wa Mungu wa kutupatia
Yohana 16:24 
Kazi ya nyumbani: Jifunze kwa moyo Ufu 3:20 na Yn 1:12. Kwa wiki zinazofuata utajifunza kwa moyo mandiko haya ya Biblia.
Warumi 10:9 I Yohana 1:9
I Yohana 5:11,12 Yohana 16:24
I Wakorintho 10:13
*  Kisaduku husimamia kazi ya nyumbani.
HATUA YA PILI -2-
MSINGI WA UWANAFUNZI
Warumi 1:11,12 "kwa maana ninatamani sana kuwaona, nipate kuwapa karama ya rohoni, ili mfanywe imara. Yaani, tufarijiane mimi na ninyi, kila mtu kwa imani ya mwenzake, yenu na yangu".
1. Kufanya Mwanafunzi
1.1 A. Vizazi vinne - mfano wa biblia wa kujumlisha wanafunzi. Injili na maisha ya ukristo hugawiwa wengine ili waweze kupitisha kutoka kwa kizazi cha kwanza hadi cha nne. II Timotheo 2:2
Kizazi cha kwanza: Paul 
Kizazi cha pili: Timotheo
Kizazi cha tatu: Watu waaminifu
Kizazi cha nne: Wengine
B. Maana ya kwanza ya Agano la kale ya kufanya wanafunzi - Zaburi 78:5,6
1.2 Mfano wa ziwa mbili
A. Bahari ya Chumvi haisaidii uhai kwa sababu haina uhai ndani yake. (Wakristo ambao hupokea habari njema lakini hawashuhudii wengine kwa maisha yao.)
B. Bahari ya Galilaya huzaidia uhai kwa sababu maji huingia na kutoka nje. (Wakristo ambao hushuhudia kristo kwa wengine).
1.3 Mifano:
A. Anderea akamuita Simoni Petro - Yoane 1:40-42
B. Filipo na Natanieli - Yoane 1:43-45
C. Yesu na wanafunzi wake - Marko 3:14
Aliwachagua kwanza kuwa Pamoja naye badaye Akawatuma
2. Ni mambo gani yanayo kupasa kujua yanayo husu uwanafunzi
Luka 14:25-33? (Huu ni mfano ambao hutumika sana kwa waebrania.) Linganisha Matayo 10:37-39, 15:3,4.
3. Ni mambo gani ya muhimu ambayo inamuhusu mwanafunzi yanayopatikana Katika Yohana 15:7-16?
-3-
4. Tunatayarisha msingi wa uwanafunzi usife moyo kwa kutoona yale yote ambayo yanamhusu mwanafunzi mwanzoni. Tunajifunza na kukua.
4.1 Mifano ya mtu binafsi ambayo inatokana na maisha ya mwanafunzi.
A. Kuchukua hatua Wakorintho wakwanza 16:13,14
B. Kukomaa. Kukua ndani ya kristo Waefeso 4:14,15
C. Ujitoe Kabisa: Uwe na hamu ya kujifunza na ujitoe kuyafanya yale ambao umejifunza. Timotheo 1, 4:15
D. Uwaminifu. Jitahidi kujuana mtu na yule mwingine. Eneza kutegemeana I Kor 4:2, Mez 20:6, Muh 5:4-6a
E. Mfano wa wengine kufuata I Tim 4:12
F. Huwaweka moyo wengine ili waweze kuendelea katika hali yote ya maisha Wafilipi 2:3,4; Luka 22:24-26; Warumi 12:3
G. Hujitayarisha katika hali yote - I WaKorintho 9:24,25
4.2 Uhusiano na wengine.
A. Urafiki unahitaji bidii - Mithali 17:17; Yohana 15:12-14
B. Uongozi hujielekeza katika kutumika - Mairko 10:43-45. Mkristo kiongozi ni mtumishi. Hii siyo desturi yetu, lakini ni mfano wa kristo ambao tumepewa.
C. Unyenyekevu ni mpango wa Mungu. - Waefeso 5:21;
I Petro 5:5 na umoja na matokeo ya kuunganishwa pamoja kwa mwili mmoja - Waefeso 4:16
D. Uwezo wa kiroho huja kutokana na kufanya kazi kwa kujitolea chini ya wengine. Hebu tazama vile Tito Ameamurishwa na Paulo - Tito 1:5 - Atende na uwezo - Tito 2:15. Vile vile angalia vile Paulo alivyo mnyenyekevu kwa wanafunzi wa yesu - Matendo ya Mitume 15:1,2; 16:4 na Wagalatia 2:9,10. Tunatambua na kunyenyekea kwa uwezo wa kiroho. hatulazimishwi.
Kazi ya Nyumbani: Mstali wa Moyo II Timotheo 2:2 
Angalia tabia kadhaa za mwanafunzi: 
Yohana 13:34,35__________________________
Yohana 8:31______________________________
Waefeso 6:18_____________________________
I Petro 3:15_____________________________
Yohana 15:8_____________________________
Mariko 10:43-45___________________________
Matendo ya Mitume 1:8______________________
HATUA YA TATU -4-
MFANO WA GURUDUMU
1. Mafundisho ya Kibinafsi ya neno la Mungu ya kila siku.
1.1 Mfano wa Kristo Mariko 1:32-35
1.2 Anza na dakika 7 kila siku.
Dakika 2 omba, uliza Mungu akuongoze
Dakika 3 soma neno la Mungu
Dakika 2 omba uwezeshwe kufanya yale umejifunza
1.3 Yanayo hitajika: Wakati, Mahali, Mpango na Bibilia (Kalamu na Kitabu)
2. Mfano wa gurudumu *(unaonyesha uhusiano wa jambo linalo Fundishwa Katika kila hatua inayofuata ndani ya mistari ya kuonyesha mambo yanayo fundishwa katika makabili ya uwanafunzi)
2.1 KRISTO - Chuma cha katikati ya gurudumu, katikati ya maisha - Wafulipi 2:9-11
2.2 ROHO MTAKATIFU - Kitovu cha gurudumu - Waefeso 5:18; Yohana 16:13,14; Luka 3:16
2.3 Wima wa chuma cha gurudumu (Mungu huzungumza nasi kupitia neno lake nasi huzungumza naye kwa maombi)
NENO - Zaburi 119:9,11; Mathayo 4:4
MAOMBI - Wafilipi 4:6,7; Yohana 15:7
2.4 Chuma cha gurudumu inayo lala (Tunawafikia wakristo ndani ya ushirika na kwa wasio wakristo - kupitia ushuhuda wetu)
USHIRIKA - I Yohana 1:7
USHUHUDA - I Yohana 1:3
2.5 UTIIFU - Yohana 14:21; Luka 6:46-49 - tairi au Ukingo wa gurudumu, Mkristo kuishi maisha ya utiifu kwa kristo.
Kazi ya nyumbani:
Anza au endeleza wakati
wa mafundisho ya kibinafsi. 
Kariri Yohana 15:5 na
sehemu za gurudumu. 
HATUA YA NNE -5-
KRISTO NDIYE KATIKATI
UBWANA WA KRISTO
1. Biblia husema yesu ni Bwana*. Anataka kuwa Bwana wa maisha ya kila muumini. Ufafanusi wa neno Bwana ni: mwenyewe chifu, liwari, Mwenye watumwa, Mamlaka ya juu, Mfalme. Neno hili linaonyesha: hali, Uzuifu kamili, Mamlaka Makuu, Bwana mkubwa. Kwa hivyo, inatupasa kujibu swali linalo ulizwa katika Luka 6:46.
2. Ni lazima tuamue kumtumikia Bwana moja au mwingine Luka 16:13.
3. Chagua sehemu Mbili au tatu sinazo fanya Mambo kuwa magumu kwako kuishi chini ya maongozi mapya ya yesu au kumruhusu awe Bwana wa maisha yako.
3.1 >Kuwa Kwanza - Mathayo 6:33
3.2 >Mambo - mavazi, mifugo, na kadhalika - Luka 12:15
3.3 >Mambo yapasayo watu wote - Mathayo 20:26-28
3.4 >Mamlaka - I Petero 5:5,6
3.5 >Kiburi - Warumi 12:3
3.6 >Jamii - Luka 14:26; Mathayo 10:37
3.7 >Anasa za dunia - Madawa ya kulevia, Mvinyo Waefeso 5:18
3.8 >Raha - Mariko 4:19
3.9 >Kujipenda - Wafilipi 2:3,4
3.10 >Pesa - Muhubiri 5:10,11; Zaburi 62:10
3.11 >Mapensi - I Wakorintho 6:18-20; Mathayo 5:27,29
3.12 >Mashaka - Warumi 8:28; Wafilipi 4:6
3.13 >Matendo Mema - Warumi 4:4,5; Waefeso 2;8-10
3.14 >Sehemu ya Kumi (zaka) kumuibia mungu - Malaki 3:8-10;
II Wakorintho 8:1-5, 9:6-8
3.15 >Uoga - IITimotheo 1:7; I Yohana 4:4,18
3.16 >Maisha ya fikira - Wafilipi 4:8; Wakolosai 3:2
3.17 >Roho wa uhafivu wa mambo - Mathayo 7:1-3
3.18 >Uchungu - Waebrania 12:14,15
3.19 >Ulimi - Yakobo 3:2; Mithali 26:20-22
3.20 >Wivu - Mithali 14:30
3.21 >Nia mbaya - Mithali 16:32; II Timotheo 1;7
3.22 >Kutojali - I Wakorintho 4:2; Mathayo 25:14-30
3.23 >Utunzaji wa Mwili - I Wakorintho 6:19,20
3.24 >Uongo - Mambo ya Walawi 19:11; Waefeso 4:25
3.25 >Chuki - Mithali 10:12; I Petro 3:9
3.26 >Kusameheana - Mariko 11:25,26
3.27 >Mengine - (kwa mfano: Ubaguzi wa rangi, Kumkana Kristo,
-6-
Kutowakubali wengine, hila, kudanganya, Kuwatumia Wengine kwa ajili ya Kupata faida, hatia, na Kadhalika)
*Katika agano jipya neno Mwokozi linaonekana mara 24 tu na neno Bwana zaidi ya mara 600 kwa hivyo kuonyesha maana ya ubwana wa Kristo.
4. Chagua kwa moyo wako na kusudi lako kutoa maisha yako kama dhabihu ilio hai - Warumi 12:1,2
4.1 Fikiria wazo la kutoa haki zako zote kwa Mungu. Hua anatulinda wakati wote na hutunza kilicho chake. Sasa hakuna haja ya mabishano au nia mbaya kuelekeza kwa wengine, kwasababu sasa wewe sio mwenye kitu chochote wanacho weza kudhuru.
4.2 Fikiria wazo la kutoa mali yako yote kwa Mungu - Mwanzo 22:1-18
- Abrahamu alimtolea Mungu nini?
- Mungu alifanya nini na dhabihu hii?
- Unaweza kumwamini Mungu kufanya yalio mema na maisha yako na mali yako ukizitoa kwake?
4.3 Jitahidi kushukuru Mungu kwa yote yanayotendeka -
I Wathesolonike 5:18; Waefeso 5:20. Huu ndiyo ufunguo wakujua kama kweli umetoa haki zako zote kwa Mungu.
4.4 Endelea kutafuta mafundisho kutoka kwa kristo kila siku. Ni tendo la kuendelea - Luka 9:23.
A. Jikane mwenyewe
B. Chukua msalaba wako kila siku
C. Mfuate Kristo
KAZI YA NYUMBANI:
Jifunze kwa moyo Wafilipi 2:9-11 
Soma kijitabu "Je umesha pata kugundua maisha yalio jazwa na Roho?" 
HATUA YA TANO -7-
ROHO MTAKATIFU
1. Kila muumini ana Roho mtakatifu
1.1 Wamepigwa mhuri wa Roho Mtakatifu - Waefeso 1:23
1.2 Roho mtakatifu hushuhudia pamoja na Roho zetu - Warumi 8:16
2. Maneno ya yohana mbatizaji
2.1 ‘yeye atawabatiza kwa Roho mtakatifu na kwa moto’ - Mt 3:11; Mariko 1:8; Luka 3:16
2.2 Kutimiza ahadi - Matendo ya mitume 1:5; 2:4
3. Mafundisho ya Yesu
3.1 Baba huwapatia Roho mtakatifu wale waomboa - Luka 11:9-13
3.2 Mifano ya Roho mtakatifu: mito ya maji yaliyo hai -
Yohana 7:37-39; "Kama" njiwa - Mt 3:13-17; Upepo - Mitume 2:2; Moto - Mitume 2:3
3.3 Kazi ya Roho mtakatifu
A. Yohana 14:26
1. Msaidizi - Baba atampeleka kwa jina la Yesu Kristo
2. Hufundisha mambo yote
3. Hutukumbusha yale yesu alisema
B. Yohana 15:26 - 16:15
1. Msaidizi - Yohana 15:26
2. Roho wa kweli
3. Atashuhudia Kristo
4. Atauhakikishia ulimwengu juu ya;
- Dhambi
- Haki
- Hukumu
5. Huongoza katika kweli yote Yohana 16:13
Hunena aliyoyasikia
6. Hupasha mambo yajayo
7. Hutukuza Kristo - Yohana 16:14
C. Matendo 1:1-9 - Hupeana nguvu za Kushuhudia -
Matendo 1:8
D. Hupeana ushuhuda wa Kutangaza - Warumi 15:18,19; Waebrania 2:4
-8-
4. Wanafunzi walikua na Roho mtakatifu kabla ya pentekoste - Yohana 20:22 - lakini walijazwa kwa Roho mtakatifu baada ya pentekoste (tazama ukuraza ufuatao)
5. Biblia huongea juu ya kujazwa na Roho - Mitume 1:8; Waefeso 5:18 Kuna maarifa mbali mbali. (Matendo 2:1-4; 8:14-17; 9:17-18; 10:44-48;
19:1-6) linganisha Matendo 2:1-4 na Matendo 4:31 - marifa yanayo endelea.
6. Ni amri ya Bwana - ?mjazwe na Roho mtakatifu? - Waefeso 5:18
7. Nimfiringo kamili wa pahali tulipo anzia (laini 3:1) - Luka 11:13
Baba atawapa Roho mtakatifu wale waombao. Kwa hivyo nilazima tuombe na kupokea kwa imani. Wagalatia 3:2-5
8. Roho mtakatifu na watu.
8.1 Roho mtakatifu nilazima atujaze na atuongoze
maishani mwetu - Waefeso 5:18 
Muongozo huu huhusisha mwili, moyo na Roho
I Wathesalonike 5:23
A. Roho yetu - huhusishwa na Roho mtakatifu -
Warumi 8:10, 16 
B. Mwili wetu - sehemu ya mwili Warumi 12:1, I Wakorintho 9:27
C. Moyo wetu - Elimu ya sehemu ya akili Warumi 12:2
8.2 Roho mtakatifu hupeana vipawa kulingana na kusudi na madhumuni ya kila mmoja wetu. Kwa kawaida hupeanwa kwa kuwabariki wengine. Warumi 12:4-8; I Wakorintho 12:1-11; na 27-31; Waefeso 4:11; na I Petero 4:10, 11
8.3 Tunahusika katika vita vya kiroho (II Wakorintho 10:3-5):
A. Kupambana na dunia - I Yohana 2:15-21; Yohana 16:33
B. Kupambana na mwili (umbo la mwanadamu - Wagalatia 5:16-17; Warumi 8:9,13
C. Kupambana na ibilisi I Petro 5:7-9; Waefeso 6:10-13
8.4 Lazima tuongozwe na Roho. Lazima tuenende ndani ya Roho - Wagalatia 5:16, 28, 25. Tunaanza kutembea na imani na:
A. Kupokea kujazwa kamili na Roho matakatifu kwa imani (saba yaliyo juu)
B. Kumtii mungu - Waeberania 12:9; Yakobo 4:7; Wagalatia 2:20; Zekaria 1:3
-9-
C. Kumpatia masumbuko na haja zetu - I Petro 5:7
D. Kumpinga shetani naye atawakimbia - Yakobo 4:7,8; Mt 16:23; Waefeso 4:27, 6:11; na 16; I Petero 5:8,9 na Ufunuo 12;11
E. Kuzaa tunda litokalo kwa Roho - Wagalatia 5:22,23
F. Kusulubisha umbo la dhambi mawazo na tamaa za mwili - Wagalatia 5:24
G. Ushirika na Roho Mtakatifu kuwa wa kuendelea
2 Wakorintho 13:14
9. Roho Mtakatifu hukaa ndani ya mkristo
A. Tazama I Wakorintho 3:16, II Wakorintho 6:16 Mahali neno hekalu ni wewe (kwa wingi)
B. Roho Mtakatifu huongoza kanisa katika umoja wa maamuzi-Matendo ya mitume 15:28
C. Mungu hufanya maskani ndani ya knaisa kupitia katika Toho Mtakatifu -Waefeso 2:22
KAZI YA NYUMBANI:
Kariri
Waefeso 5:18 
Warumi 8:16 
Rudia kijitabu "Je umeshagundua maajabu ya maisha
ya kujazwa na Roho mtakatifu?" 
HATUA YA SITA -10-
NENO LA MUNGU
1. Kwa nini tunatumia Biblia kama msingi wa maisha ya mkristo?
2 Timotheo 3:16,17; 2 Petro 1:20,21
2. Kwa mkristo, Biblia ni:
2.1 Nineno la milele na lakudumu la mungu
A. Lina mwanzo kutoka kwa mungu kupitia kwa roho mtakatifu -
2 Petro 1:20,21
B. Linadumu milele - 1 Petro 1:23-25
2.2 Chakula cha kiroho - Jer. 15:16; Matayo. 4:4
A. Miili yetu inahitaji chakula, nafsi zetu hulishwa kwa kusoma na roho zetu huhitaji kulishwa kunatokana na neno la mungu -
Heb. 5:12-14
B. Maziwa inapaswa kutamaniwa na kuhitajiwa - 1 Petro. 2:2
2.3 Silaha yetu muhimu - Waefeso. 6:12-17
A. Yesu alilitumia kumpinga shetani Matayo.4:4,7,10
B. Ni upanga wa kiroho -Waefeso. 6:17
C. Lina nguvu ndani ya maisha ya bin-adam - Heb. 4:12
2.4 Ni mwanga wa njia yetu - Zabari. 119:105
A. Linatuonyesha namna yakumfikia mungu:
1. Kupitia yesu kwa wokovu - Yohana. 14:6
2. Nihakikisho kupitia kwa Yesu kuhani wetu mkuu -
Heb 4:14,16
3. Katika jina la Yesu tunapoomba - Yohana. 14:13,14
B. Linatuonyesha hamu na kusudi ya Mungu:
1. Agizo la uinjilisti: (agizo kuu) - Yohana. 3:16,
Matayo. 28:18-20
2. Agizo asili - kutunza ulimwengu - Gen 1:26
3. Sheria ya upendo - Matayo 5:43-47; Yohana. 13:34-35
3. Mambo ambayo Biblia hutenda kwa Mkristo
3.1 hupambanua mafikira na mawazo ya roho - Wab 4:12
3.2 Kinga ya dhambi - Zab. 119:11
3.3 Hupeana Hekima - Zab. 19:7; II Tim. 3:15
3.4 Hufurahisha roho - Zab. 119:8; Yeremia 15:16
-11-
3.5 Hutumika kwa kufundisha ukweli, kuonya, kuwaongoza na kuwaadibisha katika haki II Timotheo 3:16,17
3.6 Hutuhakikishia yafuatayo
A. Kusamehewa dhambi I Yohana 1:9, Mitume 26:18
B. Kiumbe kipya II Wakorintho 5:17, II Petro 1:4
C. Kuongozwa na Bwana Zabu 32:8, Mitume 16:6-10
D. Bwana yu pamoja nasi Mathayo 28:20
E. Ushindi wa majaribu I Wakorintho 10:13
F. Atatutimizia haja zetu zote Yohana16:24, Waf 4:19
G. Uzima wa milele I Yohana 5:11,12, Yohana 5:24
H. Kuja kwa Yesu mara ya pili I Wakor 15: 52, I Wathe 4:16,17
4. Njia tano za kukua katika elimu yetu ya neno la Mungu ili tuweze kulitumia
katika maisha yetu ya kila siku.
KAZI YA NYUMBANI:
Kariri vitabu vya Biblia 
Kariri Zab 119:9,11 
Kariri mfano wa mkono 
-12-
HATUA YA SABA
MAOMBI
Maombi ni kuzungumza ma Mungu, ni njia mbili maongezi na kujipeana kwake na kumsikiliza. Unaweza kuomba wakati wowote mahali popote.
1. Mifano ya Maombi:
1.1 Kukiri -I Yohana 1:9; Zaburi 66:18; Mithali 28:13
1.2 Kusifu - Zaburi 86:12; Waebrania 13:15
1.3 Kushukuru - Waefeso 5:20; I Wathesalonike 5:18; Wafilipi 4:6,7 
1.4 Maombi ya haja
A. Kwa wengine - Kuwaombea - Wakolosai 4:12; Waefeso 6:18,19; Kutowaombea Wakristo wengine ni dhambi) - I Samweli 12:23
B. Kwa Mungu apele ke watneda kazi katika mavuno yake -Mathayo 9:37
C. Sisi kwa sisi - Maombi ya dua - Mathayo 6:11; 7:7,8
2. Madhumuni ya Maombi
2.1 Ni amri ya Mungu - Luka 18:1-7
"Omba kwa uthabiti" - I Wathesalonike 5:17 natunayahitaji-Wafilipi 4:6,7
2.2 Mfano wa Kristo - Marko 1:35
"Alienda peke yake mahali pasipokuwa na watu na hapo akaomba"
2.3 Mfano wa Paulo
"Kuomba Kila Wakati" - Wakolosai 1:3; I Wathesalonike 3:10
"Fuata mfano wangu, kama nilivyo mfuata Kristo"- I Wakorintho 11:1
2.4 Kupitia maombi tunapata ushindi wa kiroho juu nguvu za falme na mamlaka - Waefeso 6:12,13,18
3. Pingamizi ya maombi yenye nguvu
3.1 Dhambi - Isaya 59:1,2
3.2 Shaka - Yakobo 1:6; Marko 11:24
3.3 Kusudi mbaya - Yokobo 4:3
3.4 Undugu wa jamii - I Petro 3:7
3.5 Kutosameheana - Marko 11:25,26; Mathayo 6:15
3.6 Kiburi - I Petro 5:5
3.7 Mamlaka ya Kiroho, Shetani - Waefeso 6:12; Danieli 10:2, 12-14
-13-
4. Tunawejaze kufanya maombi yawe ya kufaa?
4.1 Kutii amri zake na kufanya yanayo mpendeza - I Yohana 3:22
4.2 Omba kulingana na mapenzi ya mungu - I Yohana 5:14
4.3 Omba ukiamini - Mathayo 21:22
4.4 Dumu katika neno - Yohana 15:7
4.5 Samehe - Marko 11:25
4.6 Nyenyekea - I Petro 5:5
4.7 Hifadhi yaliyo muhimu - Mathoya 6:33
4.8 Omba ukisema wazi - Marko 10:51
5. Matokeo ya maombi nini?
5.1 Pokea Roho Mtakatifu - Luka 11:9,13
5.2 Amani - Wafilipe 4:6,7
5.3 Furaha - Yohana 16:24
5.4 Upendo wa kujishughulisha - I Petro 5:7
5.5 Hekima - Yakobo 1:5
5.6 Kuponya - Yakobo 5:13-15
5.7 Kukua katika imani, kwa mfano Abrahamu - Mwanzo 18:16-33
5.8 Ufufuo - II Mambo ya Nyakati 7:14
6. Jumla au Umoja katika Maombi - Matendo 2:42; 4:31; Mathayo 18:19-20
KAZI YA NYUMBANI:
Kujifunza kwa moyo Wafilipe 4:6, 7 
Tayalisha talatibu ya. 
Maombi ya kila siku na uitumie. Anza kusoma zaburi, na Pia nyimbo na itikiyo (choruses), tayarisha taratibu ya majina yanayo eleza maana ya jina la Mungu ili itumiwe katika kusifu na kuomba. 
MAMBO YA KUFANYA:
Je Mungu hujibu maombi yetu kila mara "Ndio"? Angalia vifungu hivi vya Biblia uone vile Mungu hujibu maombi chora mstari kutoka kila kifungu kuonyesha mfano wa maombi yaliyo jibiwa: 
A. I Yohana 5:14,15 1. Majibu yaliyo cheleweshwa "Ngoja"
B. II Wakorintho 12:7-9 2. Majibu tafauti
C. Yohana 11:1-44 3. Majibu halisi "Ndio"
D. Matendo 16;1-10 4. Maombi yaliyo gawanyika
E. Kumbukumbu La Torati7:22 5. Maobi ya Kunyima "Hakuna"
HATUA YA NANE -14-
USHUHUDA WETU
1. Njia za Kushuhudia
1.1 Maisha yako - Yakobo 1:22; Wakolosai 4:5,6; I Petro 3:16 "Jinsi ulivyo husema kwa sauti kuu hata siwezi kusikia unavyo sema." Emerson
1.2 Neno lako - I Yohana 1:3; I Petor 3:15
A. Ushuhuda mwelekevu/uinjilisti - Kwa mfano kwa kutumia sheria nne za kiroho - II Timotheo 1:8
B. Ushuhuda usio wazi - shuhudia nguvu za Mungu katika maisha yako
1.3 Maombi ya kufikiria marafiki na shida zao - Matendo 28:8
2. Ninani anayehusika kuwaokoa watu?
2.1 Yesu Kristo - I Timotheo 1:15
2.2 Tu mabalosi wa Kristo - II Wakorintho 5:19,20
2.3 Injili - Nguvu za Mungu za kuokoa - Warumi 1:16; Eleza neno injili vile unavyo lielewa - I Wakorintho 15:3,4
3. Mfano wa kushuhudia; Filipo na mtu wa kushi, towashi - Matendo 8:26-40
3.1 Alijulisha kwa kinywa - akanene - Matendo 8:35
3.2 Katika kutensa akatumia mandiko napia - Matendo 8:35. Mpango wa wokovu kutoka Biblia utatusaidia kufanya vile vile.
(Mpango huu wa wokovu unapatikana katika Hatua ya Kwanza)
MPANGO WA WOKOVU
A. Wote wamefanya dhambi - Warumi 3:23
B. Mshahara wa dhambi ni mauti - Warumi 6:23
C. Kristo alikufa kwa ajili yetu - Warumi 5:8
D. Wokovu ni kipawa cha mungu - Waefeso 2:8,9
E. Kuna haja ya kupokea - Ufunuo 3:20; Yohana 1:12
F. Lazima umpokee kama Bwana - Warumi 10:9
G. Hakikisho la wokovu - I Yohana 5:11,12
3.3 Filipo alikua amejitayarisha na alijua maandiko - I Petro 3:15,16
-15-
4. Ushuhuda wako
4.1 Ushuhuda wako wa kibinafsi ni nini? I Yohana 1:3; Matendo 4:20
4.2 Ushuhuda wa Paulo - Matendo 26:4-23; 22:1-21 Ushuhuda huu unaweza kugawanywa katika sehemu tatu:
A. K.K. Vile maisha yalivyo kua kabla ya kumjua Kristo - Matendo 26:4-11
B. W.K. Wakati Paulo alimjua Kristo - Matendo 26:12-18
C. V.K. Vile maisha yalivyo baada ya kumjua Kristo - Matendo 26:19-23
5. Umoja wa Wakristo - shuhudio lenye nguvu - Yohana 17:21,23; I Wakorintho 12:20,25
6. Njia moja muhimu ya ushuhuda ni ile iliyo amriwa na Bwana katika maneno yake ya mwisho inayo julikana kama agizo kuu - Mathayo 28:19,20. Umuhimu wake inaonekana tuna pokubuka maneno yake yakwanzo kwa wanafunzi - Mathayo 4:19. Kumbuka amri yake ya kuomba - Mathayo 4:37,38. Ushuhuda huu unaanza nyumbani na kuenea nnje kwa miviringo mikubwa inayohuzisha ulimwengu wote - Matendo 1:8
KAZI YA NYUMBANI:
Kariri kwa moyo I Yohana 1:3 
Andika ushuhuda wako mwenyewe ukitumia hatua zile tatu
zilizotajwa katika semu ya 4.2 
Kariri kwa moyo mpango wa wokovu katika sehemu 3:2 
Kuwa tayari kueleza mfano wa daraja (tazama ukurasa 26) 
- 16-
HATUA YA TISA
USHIRIKA
1. Ushirika ni umoja kati ya washiriki wa kundi inahusika na urafiki na upendo wa kusaidiana kimaarifa, matendo au moyo wa kupenda. Mambo yanayo tangulia ndani ya ushirika wa ukristo no umonja wa familia inayoishi Pamoja Chini ya kiongozi mmoja, Kristo. Wote humfuata wakiendelea kupendana wao kwa wao, wakisaidiana, na wa kijifunza wao kwa wao.
2. Mzingi wa ushirika
2.1 Watu wote wana, au hupenda ushirika ulio na
A. Hamu ya kuwa katika kitu fulani
B. Mambo ya kawainda yakupendeza
C. Kufanya watu wajisikie kuwa wamuhimu
D. Raha, Upendo wa raha
2.2 Ushirika Waukristo huongeza mambo yasiyo ya kawaida kwa
uhusiano
A. Ngunzo yake ni ushirika Pamoja na Baba na mwana -
I Yohana 1:3
B. Humaanisha kutembea katika nuru - I Yohana 1:7
C. Ni ya kundumu kwasababu yesu habadiliki -
Waebrania 13:8
D. Tu viungo kila mmoja kwa mwenzake - Warumi 12:5
3. Mfano wa kanisa ya Kwanza
3.1 Mambo manne ambayo waliendelea kutenda - Matendo ya mitume 2:42
A. Kujifunza kutoka kwa wanafunzi wa Yesu
B. Ushirika
C. Kuumega mkate
D. Kusali
3.2 "Nia moja...mkinia moja" Wafilipi 2:1,2. Kwa maneno yako mwenyewe, eleza hii ina maana gani kwako.
3.3 Wakristo walipendana moja kwa mwingine - I Wathesalonike 4:9,10; II Wathesalonike 1:3
4. Sababu ya ushirika wa wakristo kuwa wamuhimu.
4.1 Katika kanisa hutoa:
A. Kufaa kwa maombi - Mathayo 18:19,20
B. Kusaidiana - Mhubiri 4:9,10,12; Wagatia 6:10
C. Kupenda na kushikilia undugu - Wagalatia 5:6; 6:2
D. Kuonya na kufundisha - Wakolosai 3:16
E. Kukua kwa kukomaa - Waefeso 4:13-16
F. Kutia nguvu undugu wajamii - Waefeso 5:22-6:4
- 17-
4.2 Katika ulimwengu (au baina ya wasio wakristo) Ushirika wa ukristo
A. Huonyesha yakuwa tu wanafunzi wa Kristo - Yohana 13:34,35
B. Hudhibitisha umoja wetu ili wengine waamini kwamba Mungu alimtuma Yesu - Yoanan 17:21,23
C. Hufanya kazi ya umishonari na kuhumbiri (uinjilisti) iwezekane - Warumi 10:14,15
5. Mwili wa Kristo - Warumi 12:1-8
5.1 Jukumu ya kila mshiriki - Warumi 12:1-3
A. Kujitowa kama dhabihu iliyo hai - Warumi 12:1
B. Mgeuzwe - Warumi 12:2
C. Usinie makuu kupita inayokupasa kunia - Warumi 12:3
5.2 Jukumu ya mshiriki wa mwili wa Kristo kwa mtu na mweigine
A. Mpendane ninyi kwa ninyi - Yohana 13:34-35
B. Rejezaneni mtu na mwingine...Chukulianeni mzigo - Wagalatia 6:1-2
C. Chukulianeni na kusameheana mtu na mwingine - Wakolosai 3:13
D. Mjengane mtu na mwingine - I Wathesalonike 5:11
E. Kufajiriana na kuamini...zuianeni na undanganyifu wa dhambi - Wahibirania 3:12-14
F. Kuhimizana mtu na mwenzake katika upendo na kazi nzuri...Farijianeni kwa tumaini - Wahibirania 10:24-25
G. Ungameni dhambi mtu na mwenzake...na kuombeana - James 5:16
5.3 Tabia ya mwili wa Kristo yenyewe - Warumi 12:4-8
A. Viungo vingi - Warumi 12:4
B. Kuwa viongo vingi, ni mwili mmoja - Warumi 12:5; I Wakorintho 12:20
C. Sio viungo viote vilivyo na kazi sawa - I Wakorintho 12:7-11
D. Viote ni viungo kila mmoja na mwenzake - Warumi 12:5
E. Kiungo kimoja kikiumia, viongo viote huumia nacho -
I Wakorintho 12:26
6. Wakristo wana uhusiano wakipekee na Mungu. Wao ni:
6.1 Watoto wa Mungu - Yohana 1:12
6.2 Warithi wa mungu na warithio pamoja na Kristo - Warumi 8:17
6.3 Wenyeji wa nyumba ya mungu - Waefeso 2:1
6.4 Njamii ya waminio - Wagalatia 6:10
6.5 Ndugu na dada wa Yesu - Wahibirania 2:11-14
Kazi ya Nyumbani:
Kujifunza kwa moyo I Yohana 1:7 
Soma I Wakorintho 12. Kutoka mstari 11-13, ni tabia ya aina gani
inayo onekana wazi katika mwili wa Kristo. 
HATUA YA KUMI -18-
MUUMINI MTIIFU
1. Madhumi ya maisha
1.1 Kufanywa kua mfano wa Kristo - Warumi 8:29; I Yohana 3:2
1.2 Ukamilifu (Kukomaa) katika Kristo - Wakolosai 1:28
1.3 Tunda lenye kukaa - Yohana 15:16
2. Utiifu wa mkristo ni nini?
2.1 Kushika amri za Kristo - Yohana 14:15
2.2 Kufanya yale anatuagiza - Yohana 15:14
2.3 Kufanya mapenzi ya Baba - Mathayo 7:21
2.4 Kufuata mifano ya Biblia:
A. Kristo - Wafilipi 2:5-8
B. Mitume - I Wakorintho 11:1 - Paulo
C. Mashujaa wa imani - Wahibirania 12:1
2.5 Kumpenda Mungu na jirani - Yohana 13:34,35
A. Amri mpya...Mpendane kama awapendavyo
B. Amri mbili zilizo kuu - Luka 10:27
1. Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa Roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote.
2. Mpende jirani yako kama nafsi yako.
2.6 Jikane nafsi yako - Luka 9:23
2.7 Kufuata maagizo yale mawili:
A. Maagizo ya uinjilisti- Mathayo 28:19-20
B. Maagizo ya utamaduni (Kutunza Uumbaji wa Mungu) - Mwanzo 1:26, 28-30
3. Yale Mungu anawaahidi wamtiiyo:
3.1 Baraka - Kubukubu ya Tolati 28:1-14; Joshua 1:8
3.2 Kuwa rafiki wa Mungu - Yohana 15:14
3.3 Kupendwa na Mungu - Yohana 14:21
-19-
4. Uwangalizi wa utiifu
4.1 Utiifu ni bora kuliko dhabihu za kidini -I Samweli 15:22; Isaya 1:11-17
4.2 Kuna pingamizi katika maisha ambayo humzuia mtu kumtii Kristo
4.3 Yesu huhitaji utiifu wa kweli katika kufanya yale anayo niambia.
A. "Ni kwanini mwaniita Bwana..." Luka 6:46
B. "Hakuna awezaye kuwatumikia mabwana wawili..." Luka 16:13
4.4 Utiifu hutoka moyoni - Mithali 4:23; Zaburi 119:10,11. Kwa hivyo hili ni jambo la kujitolea. Wakati huu unaweza kuamua kumtii Kristo bila kulazimishwa. Ahadi yake ni kwamba atakupatia nguvu za kuendelea - Wafilipi 4:13
4.5 Mungu humsaidia mwamwinifu mtiifu - Wafilipi 1:6; 2:13 - Kujitolea na nguvu za kutii; Matthyo 11:28-30.
4.6 Utiifu unaweza kuleta kudhulumiwa na taabu II Timotheo 3:12, I Petro 4:12-16. Ibrahimu alitii na alipata taabu. Waebrania 11:8-10
5. Ni lazima tuwe watiifu katika maisha yetu.
5.1 Anaye jidhania kuwa amesimama na angalie asianguke -
I Wakorintho 10:12
5.2 Umuhimu wa uwaminifu--"unapoweka ahadi kwa Mungu, usiwe mpole kutimiza." Mhubiri 5:4,5
5.3 Mambo madogo ni yamuhimu - Mathayo 25:21; Yokobo 3:3-5; Wimbo uliobora 2:15 (Tazama ni mbweha wadogo walio nyemelea miti ya mizabibu bila kuonekana na wakala migomba, na wakaharibu mizabibu. Hivyo ndivyo ilivyo nasi, dhambi ndogo zaweza kutunyemelea na kutuangamiza.)
5.4 Ni lazima kuyatazama mambo na jicho la milele.
A. Munda unayoyoma, usiku waja - Yohana 9:4
B. Kristo atarudi hivi karibuni - I Wathesolonike 3:12,13. "Usiwe na hatia wakati wakuja kwake Kristo."
KAZI YA NYUMBANI:
Kujifunza kwa moyo Yohana 14:21 
M W I S H O
-20-
USAIDIZI WAKUTENDA WA UWANAFUNZI
1. Anza kwa mpango wa kusikisana kwa kukuta na mwanafunzi au wanafunzi wako kwa wiki mbili au nne. Badaye mtakuwa huru kukutana mpendavyio
2. Kata shauri ya mahali utaanzia - Hauta ya kwanza au mahali pengine pakuanzia ni ukurasa 21 au 23. Wengine hata hivyo, huanzia na jambo fulani kwamfano, maombi, au ushuhuda, kulingana na hali zao wenyewe. Jitayarishe mbele ya wakati kufika.
3. Kutana mara moja kwa wiki kwa makabili ya uwanafunzi.
4. Uwe na vyombo mkononi (?somo? kadi za mistari ya Biblia, vitabu vidogo, na kadhalika.)
5. Kwa kawaida, nenda mkutane nao badala ya kuwangojea waje kwako. Kama kuna wanafunzi kadhaa, chagua kikao cha yule ambae ana matatizo ya kukutana.
6. Patiana taratibu ya hatua kwa hatua kurasa mmoja wakati mmoja.
7. Uwe na utaratibu wa kujulisha kama mtu yeyote hawezi kuhudhuria.
8. Kutaneni mfiringo mezani ikiwezekana.
9. Tumia saa moja au moja na nusu.
10 Ruhusu wengine waongee.
11. Wanawake wakutane na wanawake na wanaume na wanaume.
12. Kama wawili au zaidi katika kundi na mmoja akose kuhudhuria makabili ya uwanafunzi, moja wa wale walio hudhuria amsaidie kufikia wengine.
13. Usichukue jambo lolote kwa mzaha hii ndiyo sababu taratibu inaanza na Ufunuo 3:20; Yohana 1:12, na Warumi 10:9. Uwe na uhakika yakuwa wanamjua bwana.
14. Usijaribu kukaza jambo fulani; ruhusu Roho mtakatifu kutenda kazi.
15. Nenda sawa sawa na kundi. Sio lazima kusoma vifungu vyote vya Biblia vilivyo tajwa. Mahitaji na saa nilazima yawekwe maanani uwe na wakati wa kuruhusu mtu au watu kuelewa vifaa, sio tu maelezo ya akili (theory) lakini mambo ya kufanya katika maisha.
-21-
16. Stawisha uhusiano wa kibinafsi, sio tu mwanafunzi kwa mwalimu. Lakini kama marafiki. Kusudia kufanya matendo ya kijamii pamoja.
17. Ongea juu ya shida vile inavyotokea. Omba na mwanafunzi au wanafunzi na kuwaongoza kuelekea kwa mambo ya utendaji wa suluhisho. Kama kuna shida fulani, kwanza suluhisha halafu uendelee na makabili. Usisitasite kuuliza usaidizi kutoka kwa mkristo ambae unaheshimu.
18. Shirikianeni wazi wazi na wao kuhusu mahitaji yako ya kiroho na shida za kibinafsi (zote tunazo).
19. Rudia maelezo wakati fulani. Fanya mwanafunzi aeleze au arudie maelezo pamoja nawe au vizuri zaidi, na mtu mwingine.
20. Kumbuka yakwamba “habari” ni muhimu, lakini lengo ni “ujenzi” wa mwanafunzi kwa Bwana.
21. Wakati na mwanafunzi unahusisha:
20.1 Mambo ya kufanya binafsi kutoka kwa neno (shiriki).
20.2 Tazama (kazi ya nyumbani, kariri nakadhalika).
20.3 Suluhisha shida vile zinavyotokea.
20.4 Maombi.
20.5 Endelea na taratibu.
22. Fanya wanafunzi katika kundi kuandika mistari ya kukariri kwenye kadi zao vile unavyo wamuru.
23. Kabla ya kuwacha makabili, kusudia lile lingine kwa kufanya mpango wa maendeleo ya mafundisho ya “somo”.
24. Kumbuka, kuhusika katika kazi ya Bwana hutupatia nia ya mwelekeo kwa kila mmoja aliye husika kwa uwanafunzi.
25. Usikumbari ushirikiano wenu kufifia kwa kuwakanya. Sherekea kwa yale mmetimiza pamoja.
-22-
MASWALI AMBAYO HUULIZWA MARA
NYINGI KUHUSIANA NA UWANAFUNZI
SWALI - Je ninafanya inayopasa? Baada ya miezi minne niko tu katika hatua ya nne. Inaonekana kwamba tunatumia mda mwingi tukiongea “mambo mengine”.
JIBU - Umelenga shabaha. Hakuna wakati ambao umepangwa. Watu wengi humaliza mwaka mmoja. Wengine mda mrefu na wengine mchache. Haifai ufanye ?mambo mengine? ikiwa huna utaratibu wa somo mbele yako iwe kama ?sababu? ya kukutana pamoja. Nyote munakua!
SWALI - Kwa vile sasa tunawalea wanafunzi kanisani, je nilazima tuwe na kamitii ya kuiendelesha?
JIBU - Uwanafunzi sio orodha nyingine, lakini ni uhusiano wakindani (kufanyiza kinyume cha habari). Sherehe ya kila - mwaka au nusu-mwaka kwa mda wa nusu mchana kuwatia nguvu na kujenga maono ya waanafunzi ni jambo bora. Kurudiarudia maneno ya kutiana nguvu katika matangazo inaweza kusaidia kuanzisha moyo wa kupenda katika uwanafunzi kwa kanisa lote. Mambo kama haya huhitaji utaratibu mdogo.
-23-
BIBLIA, MUNGU NA WATU
1. Biblia - ndiyo mamlaka ya imani yetu mafundisho ya dini na tabia.
1.1 Asili ya Biblia (II Timotheo 3:16; II Petero 1:21)
1.2 Kristo alitumia maandiko ya Biblia - Agano la Kale (Luka 24:27)
2. Biblia hufundisha ya kwamba Mungu ni:
2.1 Muumba (Mwanzo 1:1; Matendo ya mitume 17:24-31)
2.2 Mpeanaji - Hakuachilia mbali uumbaji Wake (Mwanzo 22:14; Yohana 16:24)
2.3 Alfa na omega, Mwanzo na Mwisho (Ufunuo wa Yohana 1:8; 21:6; 22:13)
2.4 Mimi ndimi (Kutoka 3:14; Yohana 8:58)
2.5 Mungu wa upendo wa milele (Yeremia 31:3)
2.6 Mungu wa Kusameheana na Kupatanisha (Nehemia 9:17; Yeremia 31:33,34)
2.7 Roho (Yohana 4:24; II Wakorinitho 3;17)
2.8 Utatu (Mwazo 1:26, 27; Mathayo 28:19; Yohana 8:58; I Petero 1:2; II Petero 1:1)
2.9 Haki (KumbuKumbu ya torati 32:4)
3. Biblia hufundisha yakwamba mimi:
3.1 Mimi ni kiumbe cha namna ya Pekee cha mungu (Zaburi 139:13-16)
3.2 Nimepotea Kwa Kuchagua mimi mwenyewe (Isaia 53:6)
3.3 Siwezi kupatana na Mungu (Warumi 3:23)
3.4 Mtu binafsi ana uhuru wa kuchagua (Warumi 6:23)
4. Mpango wa asili wa Mungu kwa Mwanaadamu (mfano #1)
4.1 Mungu alikua na mawazo gani alipowaumba wanaadamu? (Mwanzo 1:26, 27)
4.2 Je, mpango wa mungu ulibadilika wakati dhambi ilingia maishani mwao? (Warumi 8:29)
-24-
5. Vile Mungu huleta tumaini kwa watu - Mpango wake bado ni Kamili
5.1 Kama mungu hajabadili mpango wake kwa watu, hata baada ya kuanguaka, ni mabadiliko gani yanayo takiwa yaone-
5.2 kane ili wanaadamu waweze kushiriki katika mpango huo (Yohana 1:12, 13; Wakolosai 2:13; 3:9, 10)? Nilazima kuwe na mabadiliko ndani ya mtu binafsi. [Hili ni badiliko kutoka kuwa mpotevu na kuwa mfuasi wa Kristo.]
5.2 Vile watu wanavyo kuwa hai ndani ya Kristo: Ufunuo 3:20; Yohana 1:12; Warumi 10:9
6. Mpango wa mungu kwa wafuasi wa Yesu Kristo.
6.1 Kwa kawainda imekua na itakua mpango wa mungu tufanane na mfano wa yesu, mwana wake.
(Warumi 8:29; Wagalatia 4:19; Yakobo 1:18; I Yohana 3:2)
6.2 Vile tunavyo weza kushiriki katika njia hii.
A. Kila mtu amechukua mfano wa baba wetu, Adamu, Lakini anaweza kupokea mfano wa mtu kutoka mbinguni ambao ni mpango wa Mungu (I Wakorintho 15:49)
B. Haya ni mabadiliko ya kuendelea tukiweka lengo letu kwa Kristo (I Wakrointho 15:49)
C. Je, mwisho tutakua aje? (I Yohana 3:2)
7. Njia mbili ambazo wokovu unaweza kueleweka.
7.1 Ni njia moja ambayo inajulikana lakini si ya Biblia ni Kufikiria kwamba wokovu ni kuponyoka kutokana na mwisho usio na takikana (jehanamu).
A. Lakini je, iko wapi nia ya kuwa vile mungu ametupangia au mpenzi ya kutaka kukua?
B. Je mungu huishi tu kwa mema ya watu au watu huishi kwa ajili ya Mungu? (Wakolosai 1:15,16; Waefeso 1;5-6, 12)
7.2 Kueleweka kwa wakovu wa Biblia huonekana ndani ya uhusiano wetu na Kristo - Kunakubadilishana kwa maisha ( Wagalatia 2:20) ambayo:
A. Huleta kwa mkristo mapenzi ya kuonyesha mfano wa mungu (Warumi 8:8,9; Wafulipi 2:13-15; II Wakorintho 5:17)
-25-
B. Huleta mapenzi ya kukua na kukomaa (Warumi 8:9-14; Wagalatia 4:19)
C. Humuezesha mkristo kukabiliana na shida ya maisha (Wafulipi 4:12-13)
D. Hutusukuma tufanye kazi jema (Waefeso 2:10; Tito 3:8)
8. Kuelewa ukomavu (kukomaa) wa Mkristo.
8.1 Paulo alikua na mawazo gani alipo mfundisha Timotheo? (II Timotheo 2:2)
8.2 Je mtu anaweza kukua ndani ya kristo bila ya uwanafunzi? (I Petero 2:2)
8.3 Je tunafaidikaje kutokana na uwanafunzi? (Warumi 1:11-12)
8.4 Inamanisha nini kukua au kukomaa kama mkristo? (Waefeso 4:13)
8.5 Lengo kadhaa za mkristo:
A. Kuwa kama kristo mwenyewe (Warumi 8:29; II Wakorintho 3:18)
8.6 Ninani kielelezo chetu? (Waefeso 4:13)
Kazi ya nyumbani: Kariri Warumi 8:29 
-26-
MFANO WA DARAJA
Mungu aliwaumba watu ili awe na uhusiano kamili nawao. Uhusiano huo ilivunjika kwa sababu ya dhambi. Sasa kunauetengano baina ya watu na mungu.
1. Hali halisi ya mwana-adamu.
1.1 Wote wamefanya dhambi - Warumi 3:23
1.2 Mshahara wa dhambi - Warumi 6:23
1.3 Kutakua na hukumu - Wahibirania 9:27
2. Mungu anataka kuwa na uhusiano mwema na kila mtu.
2.1 Mungu alitupenda sana hata akatupatia mwanawe wapekee - Yohana 3:16e
2.2 Anataka kutupatia uzima tele - Yohana 10:10
2.3 Anatupenda ingawaje hatustahili upendo wake - Warumi 5:8
3. Watu wanajaribu kumfikia mungu kupitia dini, philosophia, matendo mema, raha, na kadhalika. Haya yanaonyeshwa na mfano nusu wa daraja ulio hapo chini. Waefeso 2:8,9 Mithali 14:12.
4. Mungu ametupatia njia ya Pekee ya kumfikia kupitia kwa yesu Kristo alie kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu - Yohana 14:6; I Petero 3:18
5. Ni lazima tumpokee kristo kama bwana wetu na mwokozi - Ufunuo 3:20; Yohana 1:12; Warumi 10:9
Uliza kama kuna kitu ambacho kinaweza kumzuia mtu kumpokeo kristo na kungojea majibu. Kama akisema hapana? basi muulize aombe kumpokea kristo. Mtu ana weza kuomba peke yake au arudie maombi nyuma yako. Wakati mwingine unaweza kumpatia mtu ?kazi ya nyumbani ya kufanya? ili eweze kuelewa yale ulio mfundisha. Mhakikishie yakua unahaja ya kujua ameelewa mafundisho kwa kiwango gani katika mawazo yake. Baada ya kumpokea yesu kristo katika maisha yoa ungetaka kutumia Hatua ya kwanza ili uwasaidie kuanza kukua.
Bila kuandika nambari katika mfano huu wa daraja unapozungumza, Chora mfano huu. (Namba hizi zinaleleza juu ya hatua zilizo hapo juu. Fanya mara kadhaa maelezo haya).
-27-
(Chapa makaratasi kadhaa ya maendeleo ya kila Makabili ya Uwanafunzi)
KARATASI YA MAENDELEO
(ya mwalimu)
Jina ya Mwanafunzi au wanafunzi: 1__________2__________3__________
_
____________________________________________________________
Mahali pengine pa kuanzia kurasa 27: Biblia, Mungu na Watu
kurasa 24 1.__􀀹__* 3._____ kurasa 25 5._____ 7._____
2._____ 4._____ 6._____ 8._____
Kazi ya nyumbani: Warumi 8:29 **
_
_____________________________________________________________
Hatua ya Kwanza - Mfano mdogo wa mpango wa wokovu na mambo manne ya uhakika
kurasa 1 1._____ Kazi ya nyumbani: I Yohana 5:11-12 
2._____ Ufunuo 3:20  I Wakorintho 10:13 
3._____ Yohana 1:12  I Yohana 1:9 
Warumi 10:9  Yohana 16:24 
_
_____________________________________________________________
Hatua ya Pili - Mzingi wa Uanafunzi
kurasa 2 1.1____ 2._____ 4.1_____ II Timotheo 2:2 
1.2____ 3._____ 4.2_____ Tabia 
1.3____karasa 3 4._____
_
_____________________________________________________________
Hatua ya Tatu - Mfano wa Gurudumu
kurasa 4 1._____ Wakati wa Kujitoa 
2._____ Yohana 15:5 
Gurudumu 
_
_____________________________________________________________
Hatua ya nne - Ubwana wa Kristo (Kristo Katikati) (Je mwanafunzi wako anaomba ⇐
juu ua wengine kuwafanya wanafunzi?)
kurasa 5 1._____kurasa 6 4._____ 4.3_____
2._____ 4.1____ 4.4_____ Wafilipi 2:9-11 
3._____ 4.2____ Soma kijitabu 
_
_____________________________________________________________
*Alama ulioweka ya mkono (􀀹) inakukumbusha ni wapi umefika.
**Masaduku  inaonyesha lazi ya nyumbani. Weka alama saduku ya
Kwanza  wati umepewa kazi ya kufanya na ya pili  wakati imemalizika.
Mkuki _ Unamaanisha  Tafadhali Angalia. Endelea karatasi ya pili.
-28-
Karatasi ya maendeleo (inaendelea)
Hatua ya Tano - Roho Mtakatifu
kurasa 7 1._____ 5._____ 8.2_____ Waefeso 5:18 
2._____ 6._____ 8.3_____ Warumi 8 :16 
3._____ 7._____ 8.4_____
kurasa 8 4._____ 8.1____ kurasa 9 9. _____ Rudia Kijitabu 
Andika majina ya wale mwanafunzi au wanafunzi wako wanataka kufundisha: _______________, ⇐
__________________,__________________,____________________
Hatua ya Sita - Neno la Mungu (Je wanafunzi wako wameanza kufunza? ⇐
Watie moyo.)
kurasa 10 1._____ 2.3____ kurasa 11 3.5____ Vitabu via Bibilia 
2.1____ 2.4____ 3.6____ Zaburi 119:9,11 
2.2____ 2.5____ 4._____ Mfano wa mkono 
Hatua ya Saba - Maombi (uone ya kwamba umeongea juu ya wanafunzi wa wanafunzi wako. Toa shauri ya nyote mkutane kwa maombi na kujifunza Biblia wakati mwingine) ⇐
kurasa 12 1._____ kurasa 13 4.____ Wafilipi 4:6,7 
2._____ 5.____ Mambo ya kuombea 
3._____ 6.____ Mambo ya kusifu 
Mambo ya kufanya 
Hatua ya Nane - Ushuhuda (Tia moyo wanafunzi wako kwa mambo ya kufanya ⇐
ya uwanafunzi.)
kurasa 14 1.1____ 3.____ I Yohana 1:3 
1.2____ kurasa 15 4.____ Ushuhuda wa kwadikwa 
1.3____ 5.____ Mpango wa Wokovu 
2._____ 6.____ kurasa 27 Mfano wa Daraja 
Hatua ya Tisa - Ushirika (Omba kwa ajili ya wanafunzi wako kwa mambo ya kufanya ⇐
ya uwanafunzi)
kurasa 16 1._____ 4.2____ 6._____
2._____ 5.1____ I Yohana 1:7 
3._____ 5.2____ Tabia ya mwili katika
kurasa 17 4._____ 5.3____ I Wakorinitho 12 
Hatua ya Kumi - Muumini mtiifu (Ongea juu ya wanafunzi wako wakifanya wanafunzi.) ⇐
kurasa 18 1._____ kurasa 19 4._____ Yohana 14:21 
2._____ 4.3.____
3._______ 5._____
-29-
(Chapa makaratasi ya maombi kwa kila makabili ya uwanafunzi)
MAOMBI YA MAKABILI YA UWANAFUNZI YAKO
Haja ya maombi Majibu ya maombi Tarehe
-30-
MTUMISHI WA KWELI KATIKA MAISHA YA MKRISTO
1. Utumishi wa kweli maishani huonyesha kujipeana kwa mungu katika:
1.1 Kutumaini - Mungu ametupatia chochote kile tunacho - I Wakorinitho 4:7, 10:26; Zaburi 24:1; 115:16; Kumbukumbu ya Torati 26:11
1.2 Wakati - Tunadhihirisha vile tutatumia wakati wetu - Waefeso 5;15-16
1.3 Talanta - Uwezo wetu na vipawa vyetu vya kiroho hutoka kwa mungu na zinapaswa kutumiwa kwa wengine - I Wakorintho 12:7
1.4 Shukurani - Majibu yetu tunapo kuja mbele za mungu ni ya shukurani - Zaburi 95:2
1.5 Takataka - Tunapaswa kuitawala nchi (Mwanzo 1:26) na kwa hivyo tuna jukumu kwa takataka zetu - Zaburi 24:1
1.6 Harambee - Tufanye kazi pamoja kwa sababu tu kiungo kimoja na mwingine kama jami ya familia moja - Waefeso 2:19
1.7 Fungu la Kumi - Tumechaguliwa kusimamia mia moja kwa mia ya mali ambayo Mungu ametukabidhi kwa mwenyewe ambaye ametupatia mwana wake kwetu sisi ni kitu kidogo. Hata kuongeza matoleo zaidi ya fungu la kumi ina maana zaidi. Malaki 3:10 inatupatia mwanzo mzuri wa matoleo - I Mambo ya Nyakati 29:14
1.8 Ushuhuda - Hadidhi Zetu za wema wa Mungu na uwaminifu husaidia wengine kuelewa ya kwamba mungu anawapenda watu kibinafsi - I Wakorintho 4:1
2. Majaribu ya utumishi wa kweli:
2.1 Zidi kwa neema ya matoleo - II Wakorinitho 8:7-8
2.2 Tutoe kulingana na vile tunavyo pata - I Wokorinitho 16:2
Kwa wale ambao mapato haitokani na mshahara wanaweza kutoa mazao kutoka kwa kumi kwa mia ya uuzaji wa mifugo na kadhalika.
A. Vile tunapaswa kutoa:
1. Kwa kawaida katika kanisa lako -- I Wakorintho 16:1-2
2. Kwa moyo chungufu - II Wakorinitho 9:7 
3. Mapendekezo kwa wale wanaotaka kutoa kwa miradi fulani watoe zaidi ya fungu wanalotoa kwa mwili wa Kristo.
B. Matokeo ya kutoa II Wakorinitho 9:6-15
1. Mtajaziwa katika mahitaji yenu - mst. 8
2. Utawezeshwa kuwa mkarimu - mst. 11 na 12
3. Shukurani zitatolewa kwa mungu - mst. 12
4. Mahitaji ya watu wa mungu ya tatimizwa - mst. 12
5. Mungu atasifiwa na kutukuzwa - mst. 13
Kazi ya nyumbani: Kariri II Wakorintho 9:7 
-31-
VIFUNGU VIA BIBLIA AMBAZO
ZIMEJIFUNZWA
HATUA YA KWANZA Mfano mdogo wa Ufunuo 3:20
Mpango wa wokovu Yohana 1:12
Warumi 10:9
Mambo manne ya I Yohana 5:11,12
Uhakika I Wakorinitho 10:13
I Yohana 1:8
Yohana 16:24
HATUA YA PILI Uwanafunzi II Timotheo 2:2
HATUA YA TATU Gurudumu Yohana 15:5
HATUA YA INNE Ubwana wa Kristo Wafilipi 2:9-11
HATUA YA TANO Roho Mtakatifu Waefeso 5:18
Warumi 8:16
HATUA YA SITA Neno Vitabu Vya Biblia
Zaburi 119:9,11
HATUA YA SABA Maombi Wafilipi 4:6,7
HATUA YA NANE Ushuhuda I Yohana 1:3
Mpango wa Wokovu Warumi 3:23, Waefeso 2:8-10
Warumi 6:23, Ufunuo 3:20
Warumi 5:8, Yohana 1:12
HATUA YA TISA Ushirika I Yohana 1:7
HATUA YA KUMI Utiifu wa Mkristo I Yohana 14:21
NENO LINGINE NA MISTARI YA KUKARIRI:
Biblia, Mungu na Watu Warumi 8:29
Utumishi II Wakorinitho 9:7
-32-
KUSOMA MAANDIKO
Jina Lako: Tarehe:
Kitabu na Mlango:____________________________________________
1. DOKEZO LA MUKTASARI
Mst. # |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
2. ANWANI:
3. Vigungo Vinavyokingana
Mst | Marejeleo | Wazo kuu
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
| |
4. Ungumu Wa Kifungu: (WA HAKIKA NA USIODHIHIRIKA)
Mst.# |
|
|
|
|
|
|
|
|
|
|
5. WELEKEVU WA MTU MWENYEWE:
Eleza vile mafundisho haya ya Bibilia yamekusaidia katika maisha yako leo.
Kikaratasi hiki kinaweza kutolewa kwawengine.

No comments:

Post a Comment