Monday 1 December 2014

KUKUZA VIONGOZI WA KANISA

Kuandaa viongozi makusudi
Mwili wa Kristo upate kujengwa
Mafundisho ya Uongozi
John E. Gore
————————————————————————
Imetafsiriwa katika Kiswahili na
Rev. Mwenembuka Lusungu By’ucinda
Tuna karama zilizo mbalimbali, kwa kadiri ya neema tuliyopewa, ikiwa karama ya mtu ni… uongozi, acha aongoze kwa uangalifu.
Warumi 12 :6,8
2
Mafundisho ya Uongozi
Copyright ©2008, John E.Gore
Haki yote ina setiriwa. Hakuna sehemu ya kazi hii ambayo itanakiliwa, kupigwa picha na kutafsiriwa au kutolewa au kupalekwa kwa namna yoyote ile au kwa njia yoyote ile bila ruhusa inayoandikwa ya haki ya mwenye aliyebuni kitabu; isipokuwa kwa madondoa fupi ya nayotumiwa katika marudio ya kupambanua au mambo fulani fulani.
Kila andiko inayotolewa katika BIBLIA TAKATIFU, NEW INTERNATIONAL VERSION. Copyright © 1973, 1978, 1984 international Bible Society. Inatumiwa kwa ruhusa ya Zondervan Bible Publishers.
Cover photo. Houses of Parliament, London.
Original photo by John E. Gore
November 2009
This version: 19 November 2013
Tafsiri ya Kiswahili: tarehe sahihi 2011
Chimbuko kwa tafsiri ya kingereza: 27 Aprili 2011
3
Yaliyomo
1. Uongozi ni nini? 4
2. Uongozi kwa kutumikia – njia ya Yesu 17
3. Mafundisho toka Kutoka 18 24
4. Maarifa mengine toka Musa 41
5. Kufanikiwa kunaleta mabadiriko 50
6. Mafundisho ya kipindi cha usimamizi 63
Bibliography 72
4
Sura ya 1
Uongozi ni Nini?
1.1. Utangulizi.
Mungu anapotaka kutumika kitu fulani mara kwa mara anafanya mtu fulani kuwa kiongozi wa kazi hiyo. Kwa mfano, wakati wa watu wake kutoka utumwani Misri ulipotimia alichagua Musa kuwa mkombozi wao. Nyuma ya kifo cha Musa, aliweka Yoshua na baadaye waamuzi kwa kuongoza watu wake. Nyuma ya utumwa wao Babiloni, Mungu alichukua hatua tena ya kukomboa watu wake na akachagua Sheshbazzer, Ezra na Nehemia kuwa watu ambao wangeliongoza kujenga tena Yerusalemu. Uongozi ni wa maana. Moja wapo ya tukiyo hizi haingetokea kamwe bila kiongozi.
Tunaona mfano sambamba katika Agano Jipya ambako Yesu aliweka na kufundisha wale kumi na wawili kuwa mitume na kuongoza kukua kwa jumla kwa kanisa lake. Katika Waefeso 4 :11, tunasoma kama Kristo aliweka vyeo mbalimbali vya uongozi katika kanisa kwa kuwa Mungu hataki kanisa la mahali, au dhehebu kwa jumla, kuwa bila uongozi thabiti wa kimungu.
Historia ya kanisa inaonyesha kuwa kila kuliko mvuto mkuu wa Mungu hao kwa kawaida kuna kiongozi mashuhuri kwenye usukani. Kwa mfano, Osteralia munamo 1930-40, Rév C.J Tinseley alikuwa mtu ambaye Mungu alitumia kwa kusababisha makanisa ya Baptist kushinda mengine yote kwa kukua kiesabu. Alitoa mfano na juhudi ambayo wachungaji wengine walishika na kwa hiyo kukua hakukuishia tu kwa kanisa lake pekee bali kulitawanyika katika dhehebu lote kwa jumla. Munamo 1970 Mungu aliinua John Wimber aliyeanza mfumo wa shamba la mizabibu Umarekani (USA) kwa kweli kishindo gani makanisa mengine mengi katika inchi iyo na kadhalika pande zote za dunia. Hali nyingine sawa na hiyo ilitokea Ostralia karibuni munamo wakati ule ule. Mungu alitumia watu kama vile Frank Huston na pia mwana wake Brian kwa kukuza kituo cha Maisha ya wakristo (Hillsong) na kusanyiko za kazi za Mungu Ostralia na kandokando. Clark Taylor pamoja na Christian Outreach Centre na Phil Pringle ya madhehebu ya Christian City Church ni mifano nyingine ya mafunzo haya.
Mmoja tu anaweza kuangalia hali ya kanisa ya mahali kuona tofauti gani anayo mchungaji kwanza anayefaa kimungu katika maisha na kukua kwa kanisa. Uongozi mzuri ni wa maana ikiwa kanisa na dhehebu zinakua.
Nina amini kama uongozi ni daraka muhimu ambalo mchungaji, anayesimamiya kanisa, analo la kutimiza. Anaweza kutumika kazi zingine nyingi, zikiwemo kuhubiri, enda kuamkia na kushauri, lakini wajibu wake kuu ni kuwa kiongozi anayefanikiwa kimungu.
1.2. Uongozi ni nini?
Acha niulize maswali kidogo ya kuwafanya kufikiri, ‘’Uongozi ni nini? Nini kinacho fanyiza kiongozi mzuri? Unaweza kusema nini ikiwa mtu akiwa kiongozi?’’
Kiongozi ni mtu ambaye watu wanataka kumfuata.
Kwangu mimi asili ya uongozi ni kwamba waru wanataka kufuata mtu huyo juu ya kusudi. Siyo tu eti wanataka kufuata lakini wanataka kwenda katika taabu kwa ajili ya kutimiza makusudi ya kiongozi. Yesu ni kiongozi mkuu wa wakati wote, kwa watu wa kila upande duniani na katika kila umri, walikuwa wakitaka kumfuata na kuendelea kumfuata; hata kwa kuuzwa kwa maisha yao binafsi. Aliko la Yesu kwa Petro, Andrea na wanafunzi wengine, lilikuwa la ‘’kuja, unifuate’’ (Mat 4:18-20); hii ni asili ya uongozi.
Usifikiri uko kiongozi tu sababu una jina la kiongozi; una weza kuwa na cheo lakini bila kuwa na yeyote anayetaka kukufuata kwa mfano, mtu mmoja anaweza kuwa na cheo wha ‘Mchungaji’ lakini
5
akiwa ndani ya kanisa linaloharibika kufuatana na umaskini wa uongozi. Anaweza kujaribu kuongoza kanisa katika mwelekeo unaopangiliwa lakini bila mafanikio kwa kupata wanamemba wakumfuata au, inawezekana, hajaribu hata kidogo kuongoza, akiwa na matokeo yakutokuwa nachochote cha kufuata. Kuwa na cheo haimfanye mtu kuwa kiongozi; unakuwa kiongozi mpaka pale watu wanakufuata. Ninapenda Methali inayosema, ‘’Anaye fikiri anaongoza lakini asiyekuwa na mtu anayemfuata, anajitembeza tu’’.
Unajuwa uko kiongozi ikiwa watu wana nia ya kutaka kukufuata na kuendelea kuvifanya, hasa ikiwa wanapaswa kutoa dhabihu katika njia. Siyo kawaida kusikia wachungaji wanalalamika kama hawaweze kufanya watu wao kuwa ndani ya mipango wanayo juu ya kanisa. Mara nyingi tatizo ni kwa mchungaji kuliko kwa watu juu haelewi ni nini kinachohitajika kwa kuwa kiongozi na, kama matokeo haweze pata watu wa kumfuata.
Usichanganye uongozi na kupana amri. Nilisikia habari moja juu ya kundi la watu waliokuwa wakitumia chakula ndani ya mkahawa mtu mmoja alipojigonga kwenye mtumisho matokeo ikawa ni chakula kumwangika juu ya meze na kwenye walikuwa wanakaa kandokando. Jibu la watu kwa hii ajali ilionekana kuonyesha karama mblimbali na ustadi wa akili wanazo. Mtu aliyeanza kupana amri kwa wengine yakutengeneza fujo hii alidhaniwa kuwa kiongozi.
Hakuna shaka kwamba kiongozi anachukua wajibu kwa hali Fulani na kwa kufanya hivo anatoa amri makusudi mambo yapate kutendeka. Walakini, uongozi ni zaidi ya hayo. Kwa mfano, niliwai kusikia juu ya biashara ndogo ambayo ilikuwa ikiongezeka na kwa hiyo msimamizi aliamua kama anahitaji kuingiza mtu mmoja katikia kundi la Usimamizi kuchukua mamlaka yote ya maamuzi nyingi ya siku kwa siku ambayo aliwai kuyafanya. Mtu aliyeweka hakuwa na magumu ya kupana amri kwa watu chini ya amri yake; kwa kifupi aliwasimamia kwa hatua ambayo walipaswa kufanya maamuzi madogo sana wao wenyewe. Kabisa ilikuwa ya kupita kiasi bna watu walichukizwa sana na tabiya hiyo timazi na Msimamizi alilazimika kugeuza usimamizi wake na kurudi kwenye muundo aliyokuwa naho mbele. Msimamizi huyo hakuwa na tatizo kwa kuchukua usimamizi na kutoa amri lakini hakuwa kiongozi sababu hakuna yeyote aliyetaka kumfuata.
Kiongozi anachukua watu mahali papya na panao zaidi
Rafiki yangu mmoja, aliye msimamizi katika umoja wa jamii ya watu duniani, anaeleza uongozi kama, ‘’Daraka muhimu la viongozi ni kuchukua watu mahali papya na panao faa zaidi’’. Ninafikiri hili ni elezo kubwa zaidi. Haya ndiyo Yesu anayoyafanya kwetu sisi wanao mfuata na ingekuwa ndivyo tunavyofanya kwa watu wanao tufuata.
Mkristo mzuri anapoongoza imempasa kuwa mwenye moyo wa kupenda sana na kutunza wanapaswa kuwa mbali zaidi kuliko hayo; wanapaswa kuchukua watu mahali papya na panao faa zaidi. Acha nieleze kwa mfano ninayomaanisha kwa kukumbuka nahodha wa meli. Tunatazamia mtu kama huyo kukaza mwendo na kuakikisha kuwa meli imefika salama kwenye badari. Ikiwa matatizo yanajiinua njiani tuna mtazamia kwa kuzishururikia katika hali inayofaa na kutunza.
Kumbuka jinsi tungelijisikia ikiwa tungegundua kwamba meli haikuwa na mwendo usiyofaa na ilikuwa ikienda kando ikizunguka zunguka. Kumbuka nini unaweza kusema ikiwa watu walijaribu kuachilia ukosefu huu wa mwelekeo wakituambia kama nahodha alikuwa mtu mwenye moyo wa upendo na kuwa alichukua muda mwingi akifanya kazi kubwa ya kuangalia watu wanaogonjwa kwenye baraza na kujaribu kufanya watu wajisikie vizuri wao wenyewe. Sehemu ya jibu letu inaweza kuwa, ‘’vema hayo ni nzuri, lakini hiyo siyo sababu halisi ya kuwa na nahodha. Tunataka yeye atumike kazi anayoitajika kutumika na kuakikisha kuwa tunaelekea kwenye anwani kamilifu.
Nelson Mandela ni mfano mkubwa wa kiongozi. Wachache wanaweza kutokubaliana na habari ya kwamba anatazama watu wa Afrika ya kusini kwa mahali papya na panapo faa zaidi. Kamawachungaji tupo viongozi na kama viongozi tuliitwa kuongoza kanisa kwenda mbele kwenye mahali pazuri zaidi kama Roho Mtakatifu anavyotuongoza. Si vema tubaki kitako kukiangalia mambo ikiendelea kama yalivyokuwa siku zote. Hatufanye kitu fulani sababu tunazoea kukifanya. Lazima tuchukue kanisa mahali papya na pazuri zaidi.
6
Kiongozi ni mtu anayo maono kwa kusudi fulani na anaweza kuyabadiri kuwa ukweli
Kama nilivyotaja hapo juu, daraka la kiongozi ni kupeleka watu kwenye mahali papya na pazuri zaidi lakini kwa kufanya hivi wanahitaji maono. Viongozi wazuri wana maono, ndoto.Ni watu wanayo shauku nyingi juu ya hiyo. Wanajuwa ni wapi wanataka kwenda ; wana kusudi katika maisha na wanajitolea kwa hiyo. Watu hawatafuata mtu tu sababu ana moyo wa upendo na mkarimu. Wanataka kufuata mtu anayejuwa ni wapi wanakwenda na aliye na uwezo wakuyageuza katika ukweli.
Fikiri juu ya viongozi wakuu wa wakati wetu na utaona kwamba ni watu waliyo na maono. Nelson Mandela alikuwa na ndoto ya kuwa Afrika ya kusini laiti ingekuwa Democracia ya asili nyingi na alikuwa na nguvu zinazotosha za tabia ya kufanya watu kumfuata ; bila kujali rangi ya ngozi zao. Ninaona shtuko la moyo linanifunika kabisa kila wakati ninafikiri juu ya Mandela na jinsi alivyokuwa na uwezo, alipofunguliwa toka gerezani, kuongoza kuweka mpito Afrika ya kusini bila taifa kumwanga damu. Mkazo wake kwenye haja ya kusamee kuliko kutafuta kulipisha kisasi ni ushuhuda kwa tabia yake na thamani ya mafundisho ya Ukristo ambayo alikuwa akifuata.
Nguvu za Rév. Martin Luther kwa kuondoa ubaguzi wa rangi katika Afrika ya kusini akitumia njia za amani bila fujo ni mfano ungine mkubwa wa yale mtu mmoja anaweza kutimiza ikiwa ana maono na anayafuatilia kwa makini. Ndoto yake ilikuwa kwamba ‘’Watoto wangu wane siku moja wataishi katika taifa ambamo hawataukumiwa kuusu rangi ya ngozi yao bali kwa kadiri ya tabia zao’’. November 2008 ndoto hiyo ulichukua hatua kubwa kwa kutimilika wakati watu walipochagua Rais mweusi. Viongozi wa kuu ni watu waliyo na maono.
Walakini, kuwa na maono inayo sindikizwa na juhudi, kikawaida hayakufanye kuwa kiongozi. Kiongozi ni mtu anayeweza kuchukua laono yake awe mwaume au mwanamke na kuyageuza kuwa ukweli. Niliwai kukutana na watu wengi waliyo na mipango mikubwa ya kufanya vitu vikubwa juu ya Mungu lakini kamwe hayafanane kuwa na uwezekano wa kuanzishwa. Hawaweze kuchukua maono yao na kuanza kuyaona yanafikia kufarahia.
Nilikuwa nikisogelewa na watu wengi wa Afrika wakiniomba pesa ili kwamba wapate kutekeleza maono yao lakini huko kuna mtu mmoja niliyemkubaliya kumkusanyia pesa kila mara. Nili sadiki kuwa maono yake ilikuwa kweli na kuwa ana uwezo wa kutekeleza ndoto yake. Sehemu ya shabaa iliyonipeleka kumsaidia ilikuwa kwamba alikuwa amekwisha hanza zamani na alikuwa akifanya kazi nzuri na nilijuwa kila pesa nitakazo kusanya laiti zitatumikishwa vipasavyo kwa kuendelesha yale aliyokwisha kuanza zamani.
Watu wengi wanaonisogelea wana maono ambayo ni ya jumla. Nina kumbuka mtu mmoja ambayo maono yake ilikuwa ya kuendelesha shule la biblia kwa kufunza wachungaji, kujenga shule la msingi na la secondary kwa watoto, nyumba ya kuhifadhi watoto mayatima kutokana na ukimwi pamoja na miradi mingine mingi ya muhimu. Ilikuwa kwa jumla isiyowezekana. Nilimpendekeza, na wengine kama nay eye, kuwa wanafinya maono yao kwa kitu kimoja wanachokitamani na ndipo wanakitoa inje na kuifanya kuwa.
Mchungaji mwengine aliniomba pesa wakati moja wa safari zangu ili kwamba atekeleze maono yake ya kukuza tabia ya maisha ya watu vijijini mwa Uganda. Nilijisikia kuwa alikuwa na maono mazuri na moja ambayo ilielekea kadiri ya kutosha ili kwamba ipate kufikia kuwa ukweli. Walakini, alitaka kiwango kikubwa wha pesa ili kwamba akodi ofisi kampala, kununua ma computers, photocopiers, kuajiri katibu na matumizi mengine. Nilimuambia kwamba hakuna kanisa wala mtu awezaye kumpa kazi wakati asipoonyesha atakavyo geuza maono yake kuwa ukweli. Nilichangia naye kuwa hangehitaji kuwa na ofisi kampala kwa kuanza nayo lakini ilihitajika kukuza utaratibu wa jinsi ya kusaidia watu, ndipo achagua mgine wakutia taratibu hiyo katika matendo na ndipo atakapo itia inje kwa kutengeneza kanuni za wale wanaoishi katika mgine ule.Wakati anapoweza kuonyesha kuwa nguvu zake hasa zilikuza maisha miongoni mwa watu wa vijijini hakika angeomba watu kumsaidia kiuchumi ili kwamba aweze kutawanyisha mabadiriko katika eneo lake. Watu wanataka kusaidia kiuchumi miradi ya thamani lakini kiongozi anapaswa kuonyesha kuwa ana maoni ya thamani kwa wakati ule na kuwa anaweza kuyabadiri kuwa ukweli.
7
Maono yangu ni, ‘’kuandaa viongozi wa kanisa ili Mwili wa Kristo upate kujengwa’’. Si jaribu kueneza injili duniani, wala kukuza hali ya afya ya watoto katika ulimwengu unao endelea au kusitisha udhalimu kwa wamaskini na wanao onewa; ijapo nina jisikia kuwa na nguvu sana kwa haya yote. Sijaribu hata kuelemisha wanamemba kawaida wa kanisa. Nina zingatia kwenye viongozi wa kanisa na kuwa andaa. Pengine Mungu anaweza kupanua huduma munamo miaka inayokuja mbele lakini kwa wakati huu, ni hii niliitiwa kufanya. Hii ndiyo ninayo tamani, hii ndiyo inayo chukua mda wangu wote nikifikiri juu ya hiyo na kutumika juu ya hiyo. Maono yako ni ipi? Unatamani nini? Nini unaweza kufanya kuwa ukweli?
Kwa haya kuna toleo nyingi ambazo mtu anahitaji ikiwa watabadiri maono yao kuwa ukweli lakini ninataka kuangazia zaidi moja hapa; kuwa na haja ya kutengeneza. Acha niamshe usikivu wenu kwa kubadili Mkondo, matazamo kwenye makanisa ya Baptist katika Britain kuu (Great Britain) ambayo ilikuwa na kusudi la kuhakikisha sababu zilizopelekea kanisa kukua. Ulizo lilitolewa kwa kila kanisa na walikuwa wakiuliza maulizo mengi kuhusu maisha na ibada ya kanisa zao. Moja ya maulizo yalielekea kwa nguvu za Mchungaji wa kwanza na watu wanao simamia ma kazi kanisani walikuwa wakiulizwa kutaja kwa kawaida nguvu za kipekee kubwa za mhudumu wao ilikuwa ni neon lake kuu ilikuwa akihubiri, utunzaji wa mchungaji, usimamizi, au maono/uongozi? Kila kanisa liliojiwa kuhakikisha ikiwa lilikuwa likikua au kupukunga na hapo nguvu g=hasa za mchungaji zililinganishwa kwa kadiri ya kukua au kupunguka.
Mtazamo uliona kuwa ambako nguvu zaidi za mchungaji zilipatikana na kuonekana kukua zaidi nikupilia usimamizi wa kanisa. Nyuma ya hayo kulikuwa maono baadaye kukaja tutunzaji wa mchungaji na mwisho wa yote mahubiri. Kitabu hakikuhamilisha kwa vile kilieleza usimamizi lakini ninaikamata kwa kumaanisha kwamba mchungaji alikuwa amejitengeneza nkufanyiza mambo kutendeka. Waandishi wa kitabu wanahitimisha, ‘’walakini, pale kulikuwa maelekeo kwa kibali cha makanisa kukua ambako usimamizi na uongozi/maono vilikuwa vimejulikana kama karama za kwanza.1 (Acha nipotoke na kusema nina amini kuwa mahubiri mazuri hayatakuza kamwe kanisa makini mahubiri fukaraitaiacha tupu. Mahubiri ni ya muhimu lakini siyo sehemu kubwa inayopelekea kanisa kukua).
Tangu nilipo chukua wakati wa kuongoza na viongozi wa makanisa kuhusu huu mtazamo na wanafanana kukubali kwamba wachungaji waliyo waharibifu wapo duni (wana kasoro) kwa kuwa na makanisa makubwa inayokua lakini wachungaji wanao jitengeneza huenda zaidi kanisa kuonekana kukua. Matengenezo ya kipekee na usimamizi wa wakati ni vya maana kwa kuwa kiongozi anayefaa na kuona maono yako inakuwa ukweli.
Mchungaji ni mtu anayepana mamlaka kwa watu wake ili kwamba wapate kufaulu vipasavyo kuliko vile wangekuwa.
Hili ni wazo langu pendelevu la uongozi. Lina niamsha sana. Ninapenda madondoa haya kwani yanakamale yale yanayohusu uongozi. ‘’Munatambua kiongozi namna gani ?... Wanakuja katika kimo zote, umri, umbo, na hali. Wamoja ni wasimamizi fukara, wakati wamoja hawapo wakunjufu…(lakini) kiongozi wa kweli anaweza kujulikana sababu ya vile watu wanavyopatana kwa kuonysha matendo makubwa’’.2 Hapa kuna siri ; kiongozi anapana mamlaka kwa watu wake ili kwamba waonyesha matendo makubwa kwa uthabiti ; hayo ni kwamba, wanawezesha watu wao ili kwamba wapate kufaulu vipasavyo kuliko vile wangekuwa.
Kiongozi ni mkubwa, siyo sababu ya mamlaka yake, lakini sababu ya uwezo anao wakupana mamlaka (kuwezesha) wengingi. Hii ina maana ya kwamba akiwa ni muhubiri mzuri, mwinjiliste anaye faa, aliye na upako wakuongoza maabudu au kiongozi mkuu ikiwa anawezesha wengine na kufungua wengine kuwa wahubiri wazuri, wainjiliste wanaofaa, walio na upako wakuongoza maabudu na viongozi wazuri wa kundi za nyumbani. Zaidi ya watu aliyowezesha wanafanya huduma ipasavyo, kubwa zaidi ya jinsi alivyo kama kiongozi.
1 Beasley-Murray and Wilkinson, Turning the Tide, 35-36
2 Maxwell, Devetoping the Leader within You, 9.
8
Kama kiongozi unaitwa kuwezesha na kuandaa watu makusudi wapate kufikia yanayowekana kwao katika Kristo. Hii inakuwemo maisha yao wenyewe kadhalika na huduma zao. Katika Waefeso 4 :11-13 Paulo anatuambia kama Mungu aliwapa viongozi katika kanisa kuandaa watakatifu kwa kazi ya huduma. ‘’Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa ma nabii ; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu ; 12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe ; 13 hata na sisi tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo’’. Hapatunaona wazo la mchungaji kuwezesha wengine kutenda kazi ya huduma makusudi sisi wote tupate kukomaa na kufikia yanayo wezekana kwetu. Wazo hili la kuwezesha watu makusudi wafikie yanayowezekana kwao katika Kristo ni ya maana kwa uongozi wa kibiblia. Wachungaji wamoja na mitume wanaingiwa na hofu ikiwa mtu mmoja chini yao anaanza kufanyiza mambo makuu. Kuliko kuwaimiza na kuwatolea njia za kushinda hata mbali na waliko kuwaimiza na kuwatolea njia za kushinda hata mbali na waliko anzia kwa kuwazuia, kuwachambua na hata kutoa madaraka yao. Tokeo la mwisho la kizuizi hiki ni kwamba mtu muelekevu mwenye msimamo anaondoka na kwenda mahali pengine. Mara unapo funga watu wenye karama wataondoka na utakuwa maskini kama tokeo la hiyo. Nita weka nafasi zaidi kwa jambo lenyewe baadaye lakini ninataka kutanguliza wazo hapa.
Sehemu muhimu ya kuwezesha watu ni kukuza tabia ya kuimizana kuliko kulaumu na kuchambua. Mwandisho kwa Waebrania anatupatia mashauri mamoja yenye mageuzi anapoandika, ‘’Tukaangaliane sisi kwa sisi na kuhimizana katika upendo na kazi nzuri, 25 Wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine ; bali tuonyane na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia’’ (Ebr 10 :24-25) Sehemu muhimu ya ‘kuchocheana’ mmoja na mwengine kwa upendo na matendo mazuri ni kuimizana mmoja na mwengine. Mchungaji, kumbuka jinsi ungejisikia ikiwa mtu moja angekuja kwako katikati ya jumaa kwa kupongeza juu ya moja ya hotuba zako za hivi karibuni.Waza jinsi utajisikia kupewa moyo anapokuwa akikuongelea jinsi alivyotia katika matendo yale uliyoyasema na kuwa Mungu alimubariki kama vile matokeo ya hayo. Ahina hii ya habari fupi, kuliko ile ya malaumu na machambuzi, ingekuchochea kwenye matendo makubwa. Kiongozi mwema anawapa moyo watu wake na anakuza tabia ya kupeana moyo katika shirika.
Sisi kama viongozi wajibu wetu ni kufundisha, kuandaa, kupeana moyo, kuwezesha na kufungua watu makusudi wafanye zaidi kuliko mengine wangekuwa nayo. Nina amini kuwa ikiwa kundi la waamini wapya linaingia katika kanisa ambalo lina mchungaji ambaye ni kiongozi fukara inwaezekana watakuwa na maendelao iliyo na mipaka zaidi katika maisha yao ya Ukristo na huenda wasijaribu hata kufanya kitu chochote kile kikubwa katika huduma. Walakini, ikiwa kundi hilo hilo linge ingia katika kanisa ambalo lina mchungaji ambaye ni kiongozi mkuu ninaamini kuwa matokeo ingekuwa tofauti kabisa. Huyu mchungaji angewaimiza na kuwawezesha ; angeona inayofaa kwao na kuwafundisha. Angewapa nafasi za kukuza huduma zao. Matokeo ya mwisho ingekuwa kwamba wangefanya mambo makuu katika maisha ya kanisa. Utofauti katika mambo yahani uwezo wa mchungaji wa kuwa kiongozi anayeandaa watu wake makusudi wafaulu zaidi kuliko vingine wange kuwa navyo.
Kiongozi anafanya mazingira ambako watu wanataka kukua.
Hii ni sambamba na neno la mwisho lakini ni ya muhimu zaidi ambalo nina taka kushughulikia moja moja. Ulizo ninalo ulizwa mara kwa mara na wachungaji ni, ‘’Jinsi gani naweza kushawishi watu wangu kubadirika ?’’. Jibu kwa ulizo hili ni kwamba tuna hitaji kufanya mazingira ambako watu wanataka kubadirika. Zaidi tunapoambia watu kuwa wanapaswa kuacha kutenda dhambi na kuwa wacha Mungu zaidi wanaendelea kukaa pale walipo.
Acha niwapeni ushuhuda wangu mwenyewe katika mtazamo huu. Kitambo tu baada ya kuoa, mimi na mke wangu tuliamia Canada na kuingia katika kanisa ambalo lilikuwa likionyesha mazingira haya. Walakini, kulikuwa mume na muke, na muke kwa upekee, aliyekuwa akiishi jinsi ya kuvutia ya Ukristo ambayo nilitaka kuwa kama yeye. Alikuwa missionari lakini alilazimishwa kurudi
9
nyumbani kwa ajili ya ugonjwa. Alikuwa na ushirika halisi na Mungu ambao wote wawili walikuwa na mvuto mkuu na wachochezi (waamushi) kwa wakati moja, upendo wa kweli kwa wengine, na furaha ya namna hii yenye wito kwa kuishi hayo nilihitaji kuendelea kumjua Mungu jinsi alivyokuwa akitenda. Mama huyo alikuwa zaidi ya yeyote ule ambaye nilikutana naye popote pale, kwa kweli aliishi maneno haya, ‘’penda Mungu, penda watu, penda maisha’’
Hii ndiyo ninayo maanisha kwa ‘’kufanya mazingira ambamo watu wanataka kukua’’. Maisha ambalo unaongoza, lingekuwa na kishindo dhahiri namna hii kwa watu wanaoingia kanisani mwako ili wahitaji kubadirika. Si lazima uwe mkamilifu, kwani hakuna aliye mkamilifu, lakini watu wangeona ukweli wa maisha ya Kristo katika maisha yako. Ninafikiri hayo kindani zaidi wengi wa wakristo wanataka kuwa washindi zaidi katika maisha yao ya Ukristo lakini wanahitaji mtu fulani kutoa mfan na kuwaonyesha jinsi ya kuwa mtu ambaye Mungu anahitaji wao kuwa.
Kukua kunakuja kwa urahisi tukiwa katika mazingira mazuri.
Acha niwapeni mifano miwili ya nyumbani. Wa kwanza unaelekea kwa sehemu za maisha ya Afrika ambako maharagwe ni ùavuno imara. Walimaji wanayoyafanya kwa kuakikisha mavuno mazuri ni kuandaa mazingira mazuri kwa mbegu za maharagwe kuota na anapofanya hivi, kwa kawaida anatumainia mavuno mazuri. Mlimaji anahitaji kuakikisha kuwa udongo unatayarishwa vizuri na kwamba magugu yaliondolewa, kuwa mbegu zimepandwa mahali ambapo zinapokea mwangaza wa jua na kupata liwango cha kutosha cha rutuba. Kadiri mimea inavyokomaa mlimaji anahitaji kuendelea kupalilia makusudi mimea isisongwe na magugu. Yale ninayo yaishi yanapendekeza kuwa wakati mbegu hazikuota vipasavyo kufuatana na yale unayo yafanya, nyingi zitaota na afya nzuri na kutoa mavuno mazuri ikiwa zilipewa mazingira mazuri ambamo zitakua.
Mfano wa unaelekea nyumbani kwangu binafsi pa Ostralia. Tulikuwa na nyumba yetu iliyojengwa juu yetu ambayo ilitaka kuonyesha kuwa tulipoamia ndani kweli humukukuwa sanamu yoyote iliyofanyika. Nilipendelea kupata miti mimoja ipandwe kandokando ya nyuma ya nyumba ili ipate kukua haraka na kutoa uvuli na maficho. Walakini, udongo ulikuwa mzito na unaonata sana na kwa ajili ya joto, kwa kawaida udongo ulikuwa mgumu na kavu ingalau nilichukua mda wa kuimiminia maji. Matokeo yalikuwa kwamba kwa kusubiri miti ilukua. Pamoja na hayo, yalikuwa yakishambuliwa na vidudu wengi na kupatwa na magonjwa mengi. Niliendelea kuya nyunyizia kwa kupiganisha haya na kuimiminia daima kwa kuharikisha kukua lakini yote yalifanyika tofauti kidogo.
Baada ya miaka miwili nilikuwa na wakati wakutosha wakujitoa nyuma ya nyumba na hivo kujilaza chini kwenye majani, kukata majani, kuikusanya na kuiweka mahali kuliko miti. Niliweka mtindo wa kumiminia majani hayo yote yakaoza na kuwa mbolea. Matokeo yalikuwa yakushangaza. Miti ilianza kukua ; kwa kasi kadiri haikuwa raisi kwangu kutambua jinsi ilikuwa ikikua kila usiku. Yaliyokuwa yakupendeza zaidi ilikuwa haya kapatwa na ugonjwa wowote ambayo yaliyashambuliya mbele. Utofauti ulikuwa kwamba niliyatolea mazingira ambamo yangekua na hii ikaipatia nguvu za kusitawi kwa kupambana na mashambulizi ambayo yalikuja kutoka magonjwa yaliyoletwa na vidudu.
Hayo yaliyo juu yanatumiwa hata kwetu kama viongozi. Ni Mungu anayetubadirisha na kutupa nguvu za kushinda dhambi lakini sisi, kama viongozi, lazima tuandae mazingira ambamo watu wanataka kukua na ambamo Mungu anaweza kufanya kazi yake ya mabadiriko.
Ninakumbuka nilienda katika semina ya kukua kwa kanisa wakati wa mwanzo wa miaka yangu ya huduma ya uchungaji wakati Mchungaji wa kwanza ambaye aliandaa kikao aliandika maneno haya ‘’Ukristo ni raisi zaidi kushika kuliko kufundisha’’. Hii inatuambia kuwa njia nzuri zaidi ya kufanya mtu kukua kuwa kama Kristo ni kuwazunguuka na mazingira mazuri ya Ukristo ambamo watu ‘’wanapenda Mungu, wanapenda watu na wanapenda maisha’’ na ambako wanaamini kwenye huduma ya Roho Mtakatifu kutokeza mabadiriko. Ikiwa mtu anapasiswa kwa hii, huenda ‘watashika’ ukweli wa imani na kukua na kufanana zaidi na Yesu. Walakini, uwe na uhakika kuwa unatolea haya maneno ya heshima na mafundisho mazuri makusudi wawe na msingi unaokomaa wa kibiblia kwa yale wanayo yaishi.
10
Acha nipane mfano, miaka mingi iliyopita mtu mmoja aliamia ndani ya mji wa inchi ambamo nilikuwa mchungaji na akaanja kushiriki kanisa. Alikiri kwa unyofu kuwa alikuwa kinyonga ; akibadili rangi kwa kisua kiti alichokalia. Anapokuwa na wakristo anatenda sawa mkristo lakini anapokuwa duniani anatenda kama moja wa dunia na, alipozaliwa mara ya pili, hakujitolea kwa maisha ya kanisa nilianza kumualika kuchangia naye chakula na laiti tuliongea juu ya mambo ya Ukristo kwa jumla. Sikum kamata katika mwenendo wa uongozi wa kawaida wala hatukifanya kitu chochote katika njia taratibu ; tulikuwa tukikaa na kuongea juu ya maisha. Baada ya karibuni mwaka hivi alifanya ombi la kazi na akapata kazi, amerudi mahali alipotoka na akarudi katika kanisa lake la zamani. Kadiri ya mwaka nyuma ya hayo, mchungaji wa kanisa ambamo huyo mtu alikuwa akihudumu, alinikuta katika mkutano mmoja na akaniuliza, ‘’Nini ulicho kifanya na ‘fulani’ (akitaja jina la huyp mtu), ni mtu tofauti kabisa ; ni mwenye bidii na anajitolea kwa kanisa, ni ya kushangaza ?’’ kwa nini haya yalitokea ? Ni Roho Mtakatifu aliyetubadirisha lakini tulitayarisha ‘udongo’ ambamo watu hawa wanaweza kukua.
Endeleza mazingira ya ‘’kupenda Mungu, kupenda watu na kupenda maisha’’.
Kabla niondoke katika jambo tunalozungumzia la kufanya mazingira ambamo watu wanataka kukua, Acha nirudiliye kuzungumzia maneno ya kuongoza maisha, ‘’Penda Mungu, penda watu, penda maisha’’. Ninajisikia kuwa ahina hii ya Ukristo ni ya kuvutia na, pamoja na msaada wa Roho Mtakatifu, ni vizuri kuandaa hali ambamo watu wanakua. Kisio mangu ni kwamba Wakristo wengi wangekubaliana na ‘’Penda Mungu na penda watu’’ lakini wamoja wangekuwa na matatizo na ‘’penda maisha’’. Wanaweza hojiana kuwa tuna jitoa katika vita zidi ya uovu na kwa hii hakuna wakati wa ‘’furahia maisha’’. Kwa ‘’furahia maisha’’ sina kumbukumbu kwa yale mara kwa mara ulimwengu unaeleza kama ‘kufurahia maisha’ ; ndiyo kwenda kwenye makundi makusudi upate kunywa kabisa. Hapana, nina sema juu ya watu ambao kiwazi wanafurahia kuishi na kupata furaha kwa yote ambayo Mungu aliyowapa. Acha nipane shairi tatu kwa kueleza ninayotaka kuonyesha.
 Wagalatia 5 :22-23 ; Lakini tunda la roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, 23upole, kiasi ; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria. Ni yakupendeza kujua kuwa mtu anayeonyesha matunda ya Roho atakuwa na furaha ; hawatakuwa watu wanaoenda pande zote wakinungunika juu ya jinsi mambo yalivyo magumu na jinsi tunapaswa kuyavumilia kama tunavyo ngoja kuja kwa pili. Hakuna ! Furaha, upendo wa maisha, ni tabia ya mtu anayeongozwa na Roho wa Mungu.
 Nehemia 8 :9-10, Naye Nehemia, ndiye aliyekuwa Tirshatha na Ezra kuhani, mwandishi, na Walawi waliowafundisha watu, wakawaambia watu wote, siku hii nitakatifu kwa Mungu wenu, msiomboleze wala msilie, Maana watu wote walilia, walipoyasikia maneno ya torati. 10kisha akawaambia, Enendeni zenu, mle kilichonona, na kunywa kilicho kitamu, tena mpelekeeni sehemu yeye asiyewekewa kitu ; maana siku hii ni takatifu kwa BWANA wetu ; wala msihuzunika ; kwa kuwa furaha ya BWANA ni nguvu zenu wote, wakasema, Nyamazeni, kwa maana siku hii ni takatifu ; wala msihuzunike. Jueni kwamba kama watu walivyosikikiza amri ya Mungu walikuwa katika shari na wingi wa dhambi zao na hivyo wakaanza kulia. Mara moja Nehemia na viongozi wengine wakaelewa kuwa walikuwa wametubu kweli wakaambia watu kuacha kulalamika na kusherekea na chakula nzuri na vinywaji vitamu. Hii ilikuwa siku ‘’takatifu kwa Bwana’’, kwa hii, jibu kamilifu ilikuwa kufurahi na kusherekea ; kula chakula kizuri na kufurahia maisha. Ni hali hii ambayo inapana msimamo kwenye shairi linalojulikana vizuri, ‘’furaha ya BWANA ni nguvu zenu’’.
Nilikomaa na mawazo potovu ambayo ikiwa siku ilikuwa ‘’takatifu kwa Bwana’’ ilitubidi kuwa wasiocheka hata kidogo na wapole na kutokuwa na mzaa wowote bila shaka.
Lakini hii siyo hali. Mara moja tulipoungana dhambi zetu inafaa kusherekea na kufurahia yote yale Mungu aliyotupatia. Kwa mfano, ninapenda kahawa nzuri, chakula kizuri, kutembea na kuangaliya kandanda (mchezo wa mpira).Nina ona hii kama zawadi kutoka Mungu na sehemu ya baraka ambayo aliyomimina katika maisha yangu.Fahamu kuwa Nehemia aliambia watu kwamba walikuwa wakituma sehemu ya chakula chao kizuri na vinywaji vitamu kwa wale ambao hawakuwa na kitu. Hii ni desturi ya muhimu na nitofauti kwa yale tunayoona mara kwa
11
mara kwa wamoja wamoja wa magharibi ambako wale walio na mengi mara nyingi wanazarau wale ambao hawana kitu.
 1 Timotheo 6 :17, Walio matajiri wa ulimwengu wa sasa uwaagize wasijivune, wala wasiutumaini utajiri usio yakini, bali wamtumaini Mungu atupaye vitu vyotr kwa wingi ili tuvitumie kwa furaha. Shairi hili linatuambia kama Mungu anatupatia kwa wengi kil akitu kwa furaha yetu. Lazima tufurahie maisha. Kama nilivyotaja juu, ninafurahia kahawa nzuri na chakula kizuri ; ninapenda kusafiri, ninapenda kucheza kandanda. Mungu alitupatia vitu vyote kwa wingi kwa kufurahi.
Walakini, furaha hii ya maisha ni matokeo ya kutubu na kutumikia Mungu ; hii inatokea kwanza. Ikiwa tunajaribu kuweka furaha kwanza tutaiona kuwa danganyifu na hatainayoharibu. Kwamfano, singeondoka kamwe kanisani na kwend a kukaa nyumbani kuangalia mchezo wa mpira, hata ikiwa ulikuwa ni mchezo wa mwisho wa kupana kombe la Dunia. Ikiwa nilivifanya ningekuwa nimebadili agizo la Mungu ‘’Penda Mungu, penda watu, penda maisha’’ ku ‘’penda maisha, penda Mungu, penda watu’’. Hii hailete mafanikio inayodumu na furaha.
Sikuona mwisho wa kombe la Dunia la 2010 katika Afrika ya kusini kwa sababu tofauti lakini, nilipokuwa Mauritius wakati niliposimama, njiani mwa kwenda kigali kwenye huduma, nilipofikia kwenda kwenye chumba changu mangharibi na kugeukia kwenye TV na kwa mshangao wangu na furaha sana, niligundua kuwa walikuwa karibu ya kuonyesha marudilio ya mwisho wa mchezo wa kombe la Dunia. Wakati wangu ulikuwa mzuri. Mungu ni mwema.
Kiongozi anajizugushia mwenyewe na timu nzuri
Nilitaja juu kuwa wachungaji wamoja wanatiwa woga na watu hodari chini yao na kuwaweka kando kwa kuwazuia (komesha). Tokeo la mwisho la kitendo hiki ni kwamba mtu hodari anajisikia kuwa hawana hiari lakini kuondoka na kwenda penginepo.Kuna sababu nyingi za kiongozi kutenda namna hii lakini moja ya hayo ni woga huo ikiwa hayapo afadhali kwa kila kitu basi watu hawata wafuata. Ikiwa mtu anainua aliye na karama ya unabii hiyo ni kubwa kuliko hiyo ya uchungaji au ikiwa ni kiongozi mzuri maabudu wala muhubiri mzuri kuliko kiongozi anashikwa na woga kuwa tena kumfuata. Njia hii ya mafikiri ni haribifu kwa hiyo sivyo inavyo tendeka. Kwa kifupi, ni mbalimbali kabisa; kiongozi mkuu siku zote anajizungushia mwenyewe na watu wakuu.
Acha nifananishe yale ninayomaanisha kwa kurejea kwa Rais wa inchi ambayo inaongozwa na mtindo wa urais, kama vile ule tunao Rwanda. Kiongozi kama huyo anahitaji kujizugushia mwenyewe na watu hodari; watu walio na ujunzi mwingi katika nafasi zao za kazi maahalum kuliko anayo. Hakuna anaye dhani Rais kuwa na zaidi ya elimu za juu kuliko yeyote ule ndani ya inchi wala hawamuhitaji kuwa aliye na ujuzi zaidi kwa ngambo ya afya, elimu au mambo ya unjenzi. Watu hawakati tama na kuacha kumfuata ikiwa kuna mtu Fulani katika inchi aliye na doctorates nyingi kuliko yeye au anajua mengi zaidi kuhusu mambo ya technology kuliko yeye. Watu wanayotuùaini kwa Rais ni kuwa anajizungushia mwenyewe na watu waliyo na maarifa mengi na ujuzi wa kutosha katika kazi zao makusudi apate kuchukua taifa katika mahali papya na pazuri. Ni hii wanahitaji kwake. Zaidi ya hayo, wanataka Rais kuwa na maono inayowekwa kwa kusudi Fulani juu ya inchi na kuwa na uwezo wa kuigeuza katika ukweli; wanamtumaini kuwezesha watu waliyo chini yao makusudi taifa kwa jumla lipate uwezo wa kutimiza zaidi ya vile ilivyokuwa navyo zamani. Haya ndiyo kiongozi anayoyafanya na haweze kutimiza hayo ikiwa wanajaribu kufanya kila kitu wao wenyewe au kuzuia watu wanao wazunguka ambao wana maarifa mengi katika kazi Fulani kuliko walivyo. Kiongozi anahitaji kumuzungusha na timu hodari makusudi wapate kuchukua watu mahali papya na pazuri. Si ya kushangaza kuwa Tony Blair, waziri mkuu wa Ungereza (uk) tangu May 1997 hadi June 2007 aliandika, ‘’…nguvu moja ninayo ni kuwa sitaki watu wakuu kandokando yangu’’.3
3 Blair, A Journay,114
12
1.3. Viongozi wanaenelea kadhalika kama kuzaliwa
Miaka ya kutosha iliyopita kijana wangu mkubwa kwa umri alikuwa amealikwa kushiriki baraza la vijana la uongozi, iliyotayarishwa na shirika la kidunia linalojulikana vizuri; ambayo ilianzisha wazo la kuwa mupo wala kujaliwa kiongozi au amupo. Ikiwa mupo ‘aliyezaliwa kiongozi’, na walewanao shiriki baraza walijijulishwa kuwa walialikwa sababu wanaonyesha tabia hizo, basi unaweza kuzifunza akili tofauti kwa kuongeza nguvu ya uongozi, ikiwa amukuwa ‘aliozaliwa kiongozi’, basi cha kwanza ilikuwa kwamba hakukuwa kitu wangefanya kwa kukufanya mmoja.
Je, hii ni kweli? Nilifika kwenye hilimisho ambayo sio. Hakuna shaka kuwa watu wamoja ‘wamezaliwa viongozi’ na wanaonekana kuelekea kiasili kwenye vyeo vya uongozi kwa umri wa chini. Mara kwa mara ni watu wanaochaguliwa kama nahodha wa shule au nahodha wa timu la michezo kutoka umri wa chini, nina sadiki pia kuwa watu wanaojitahidi sana kwa uongozi wanaweza kukuza huo uwezo juu ya wakati. Ninapenda yale John Maxwell anasema anapoandika, ‘’Uongozi unaendelezwa sio kuvumbuliwa. ‘Kiongozi wakizalikio’ wa kweli kwa kawaida wataibuka (wataonekana) lakini, kusema kwa kweli, tabia za kiongozi wa asili zinapashwa kuendelezwa au kukuzwa katikakutumika na maelfu ya watu wanaotamani kuwa viongozi, niligundua (kuwa) wao wote wanalingana kwa moja ya aina au (umbalimbali) au ngazi inne za uongozi’’
Basi anaenda kueleza aina hizo kama.4
 Kiongozi msimamizi. Huyu ni mtu ambaye ni ‘kiongozi wa kizalikio’ lakini anayekuza uwezo wake wa asili kwa kuwa kiongozi mkuu.
 Kiongozi aliyefundishwa. Huyu ni mtu ambaye hakuzaliwa na tabia za uongozi lakini alipasishwa kwenye uongozi mwema na aliye na maadili ya kipekee kwa kuwa kiongozi mkuu
 Kiongozi mwelekevu. Huyu mtu anafanana na ‘kiongozi aliyefundishwa’ lakini aliona tu hivi karibni kielelezo cha uongozi mzuri kwa mtu mwengine.
 Kiongozi wa kadiri. Huyu mtu alikuwa na uwazi ndogo au hkuwa na uwzi au mafundsho ya uongozi lakini ana haja ya kuwa kiongozi
Mara na mara Maxwell anadai kuwa tabia zote ambazo ni za muhimu kwa kiongozi zinaweza patwa ikiwa una hja yakuwa kiongozi. Hamuondolewe haki kweenye uongozi ikiwa hamupo ‘ kiongozi wa kizalikio’. Tabia tatu ni hizi:
 Kupasishwa ktika uongozi mwema
 Kujifunza yote ambayo unaweza juu ya uongozi
 Kukuza maadili ya kipekee inayofaa kwa kuwa kiongozi.
Nina ona pekeyangu kama ninkuwa katika aina ya kiongozi mwelekevu’ kwa vile sikuwa ‘kiongozi wa kizalikio’ au sikuonyesha tabia iwayo yote katika njia yoyote katika miaka yangu kwenye chuo. Nilikuwa kwa jumla siyafikiliza katika miaka hiyo lakini hayo yote yalibadirika wakati mke wangu na mimi tulipo hamia Canada nyuma kidogo ya kuoana kwetu. Tulienda kuishi katika ‘eneo la aina ya serkali’ na ilikuwa intolewa kwa watu ambao walikuwa viongozi katika kanisa, jamii na shirika za ulimwengu. Hii, pamoja na kupata daaaraja katika shughuli za dunia ilitufanya kuwa wenye kufaa katika huduma zetu za kanisa katika njia ambayo ilikuwa ya kigeni kwa yale tulikuwa tunayaishi ste wawili zamani. Sisi wawili tulipokea wito wa Mungu kwa huduma ya uchungaji kwa wakati wote na tuliliacha kanisa Canada na tukaenda kwenye shule la Biblia pa Ujerumani na kasha tukrudi Australia, ambapo nilimalizia mafunzo yangu ya theologia. Miaka ya baadaye katika hudum ya uchungaji ilionyesha kuwa ustadi wa uongozi unaweza kukuzwa hata wakati hatupo ‘viongozi wa kizalikio’.
Sababu yangu ya kufundisha ‘uongozi’ kwa wachungaji ni kwa sababu nina amini ni yamuhimu kuendelesha/kukuza eneo hili ikiw tunataka kufikia yote ambayo Mungu anayo kwa ajili yetu.
4 Maxwell, Developing the Leader within You, Introduction.
13
Wakati wa miaka yangu kama mwanafunzi wa kitheologia tulitumia masaa mengi tukizungumzia theologia, mengi ya ile ambayo ilikuw na thamani ndogo sana, lakini tulitoa mda mdogo kwa eneo lote la maendeleo ya uongozi. Tulikuwa tumetarajiwa kufundishwa kuwa viongozi katika kanisa lakini tulipewa uwazi mdgo kwenye jambo la uongozi. Mungu alikuita kuwa viongozi lakini tulikuwa hatukuwa tunafanywa kutambua umuhimu wa jambo hili.
Upo wapi katika hali inne za Maxwell? Je, unajiona mwenyewe kuwa ‘kiongozi wa kizalikio’? Ikiwa ni hivyo basi kuza yale Mungu aliyo kupatia. Ikiwa upo kiongozi aliyefundishwa au kiongozi mwelekevu bsi zifunze tabia ambazo zitakufanya kiongozi mkuu kweli. Ikiwa upo kiongozi wa kadiri sasa uwe na uhakika wa kuwa unaanza kukuza eneo hili la maisha yako sasa. Kuza haja yenye afya kwa kuwa kiongozi kadiri Mungu anavyotaka wewe kuwa. Jifunze kwa wale ambao ni vingozi wazuri na jitoa mwenyewe kwenye mafunzo mazuri ya uongozi. Usidharau umuhimu wa huduma yako kwa kukataa kukuza uwezo wako wa uongozi.
1.4. Ujikuze mwenyewe
Ingekuwa wazi nyuma ya kusoma yaliyo juu kwamba sura muhimu zaidi ya uongozi ni kujikuza mwenyewe. Ni ya maana kuwa tunasikia mafundisho na ufundi wa uongozi lakini baadaye mutainuka au kuanguka kwa vile mulivyo. Ikiwa mupo tayari kuwa kiongozi kadiri Mungu anavyotaka wewe kuwa basi kitu muhimu unacho weeza kukifanya ni kujikuza mwenyewe, au ninaweza nikaseme, shirikiana na Mungu katika hatua hii. Unapaswa kukua kama mtu ikiwa unataka kuwa kiongozi mkuu. Uongozi ni kwa ajili ya kushawishi wengine wakufuata na atu watafuata mtu wa maana; mtu ambaye ana maono thabiti n aliye na uwezo wa kutimiza malengo yake. Nelson Mandela, mmoja wa viongozi wakuu zaidi duniani katika karne ya makumi mbili, ni mfano wa ukweli huu.
Nina amini kuwa eneo inne muhimu ambazo tunahitaji kueleza. Ni zifuatazo:
 Uwezo wa asili. Kwa mfano, ikiwa upo muhubiri basi kuza uwezo wako kwa kupanga vema hotuba makusudi watu wapate kusikia vizuri yale unayoyasema. Jifunze jinsi ya kuongea na watu, jifunze jinsi ya kupata usikizi wao na jinsi ya kumaliza kusema. Mafunzo haya yanatumiwa n mchungaji kama vile kwa mfanya siasa wa serkali ya nchi na kwa yeyote anayetaka ujumbe wao upenye vipasavo. Ikiwa mupo katika hatua ya uongozi; jifunze kwa wingi kadiri uwezavyo juu ya kila kitu unayoitwa kufanya.
Mimi ni mtu anayeamini katika kujifunza kutoka kwa wengine na nitauliza maulizo yakufaa ya watu ninaokutana nao makusudi nipate kujifunza na kukua. Sikusudie kujua kila kitu lakini ninataka kujifunza. Mbele ya kuwa mchungaji nilikuwa msimamizi wa kitengo cha kazi ya umeme ya kampuni nilikuwa nikitumikia na nina kumbuka kushiriki semina moja ya mafunzo ambayo yalihusiana kwenye kiingilio cha technologia mpya. Ninakumbuka kwa dhairi kartasi ya habari iliyobandikwa kwenye ukuta wa mbele w chumba cha kituo cha mikutano ambayo inasomeka, ‘’Yule anaye uliza ulizo anaweza kuzitokeza kuwwa mpumbavu kwa dakika tano lakini Yule ambaye hakuuliza ulizo anabaki mpumbavu kwa baki ya maisha yake yote’’. Je, nikweli!
Nilipoanza uchungaji nilikuwa nikiuliza wachungaji vigogo kutoka makanisa mengine ambao walikuwa wakifanya mambo makuu ikiwa ningekutana nao nakuwauliza maulizo juu ya yale waliyo yafanya. Niliona kuwa wachungaji wale walikuwa tu wenye shauku pia ya kukutana nami na kunisaidia. Ikiwa kila mara unakuwana nafasi ya kuongea na kiongozi anayejulikana sana usipoteze mda wako ukijaribu kumtumikisha awe mwanaume au mwanamke na ujuzi wako lakini waulize maulizo yanayofaa. Ikiwa unajaribu kuwatumikisha wataelewa haraka kuwa haujue yakutosha kama vile unavyofikiri unajua. Kwa ngambo nyingine watatumikishwa zaidi na haja yako ya kujifunza na maulizo unayo uliza.
 Kupakwa mafuta na zawadi za kiroho. Hapa ninajikumbusha kwenye upako wa Roho Mtakatifu na mchangamano wa zawadi za Roho. Mtu anaweza kuwa mwongeaji anayefaa kutoka vitu vionekanavyo kwa macho ya kidunia ikiwa anakosewa upako wa Roho Mtakatifu basi mahubiri yake itakuwa ni hakika ingine ya pili, bila kujali namna yalivyotayarishwa vizuri.
14
Kama tunavyo soma katika Agano Jipya inakuwa dhabirri sana namna alama za maishara na maajabu yalikuwa kwa kusaidia kanisa kukua. Paulo anasema katika Warumi 15:18-19, Maana sitathubutu kutaja neon asilolitenda Kristo kwa kazi yangu, Mataifa wapate kutii, kwa neon au kwa tendo, kwa nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu; hata ikiwa tangu Yerusalemu, na kando kando yake, mpaka Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu. Injili nyingi sana zinazopatikana katika sura za mwanzo za kitabu cha Matendo zinakuja juu yake kama matokeo ya waamini kusema katika lugha nyingine na makutno kushangazwa kwa yale wanayosikia. Mambo kama na hayo yalitendeka wakati Petro na Yohana waliponya mtu kwenye mlango mzuri wa Hekalu, makutano yalikuja yakikimbia kuona yaliyotendeka nah ii ilimupa Petro nafasi ya kuhubiri tena.
 Mwanendo wa mambo ya adili. Hayo ni, kukataa uasherati, kutoshindwa na tama, udanganyifu au vitendo vingine ambavyo kwa kawaida tuna hesabia kuwa kama dhambi. Tumaini ni kwamba hii ni wazi kabisa ambako sina la kueleza juu yake, lakini, kwa bahati mbaya, ni eneo ambalo lina ingiza wachungaji wengi katika matatizo mengi. Uzinzi n matumizi mabaya ya pesa za kanisa huenda ni dhambi mbili kubwa zinazopelekea wachungaji kuanguka.
Acha nichange jinsi nilivyo panga huduma yangu kwa ngambo ya uchumi. Kuanza nayo inaorodheshwa na NSW serkali katika Australia na sababu yake kwa sheria za ukubalifu kiserkali na maagizo. Pesa zote ambazo huduma inapokea inaenda katika akiba ya huduma mbalimbali – Huduma za Maendeleo ya Uongozi Unaounganishwa – na sio katika akiba yangu mwenyewe. Siweze andika hati ya fedha au kuchukua pesa kutoka kazi za huduma kwa binafsi yangu lakini ni na hitaji saini ya pili kutoka mmoja wa wanamemba wa Baraza. Tena, wanamemba watatu wa Baraza wanafungamana name makusudi ikiwa nina tayarisha malipo mwanamemba mwengine a Baraza, ambaye hafungamane name, ni huyo atasaini ukubalifu wa malipo. Siweze kuonekana nikiwatatiza washirika wangu kwa kusaini ukubalifu wa gharama y matumizi.
Katika kila safari ninachukua buku ndogo pamoja name na nina andika matumizi ambayo ninatumia na ikiwa ninapana kiwango kikubwa cha pesa kwa watu ninmuona nayepokea kwa kunijaziya resiti. Ninachukua pamoja name kiwanga cha kurasa za resiti wazi popote niendapo katika Afrika. Mtunza hazina ambaye pia si mmoja wa washirika wangu, anachunga hesabu ya kila tendo; ya kuingia inaonyeshwa kwenye Baraza la mwaka la Jumla (AGM) la huduma na kila mmoja atapewa nakal (copy). Baada ya AGM katibu (anatoa) maelezo ya kiuchumi sahihi kwenye serkali kwa ajili ya idhini.
Uchumi wote wa huduma za Maendeleo ya Uongozi (Leadership Development Ministries Inc. LDM) yanatumiwa katika njia ya pekee nay a wazi makusudi Shetani asiwe na nafaasi ya kusukuma tuhuma na kufanya huduma kuingia katika tabia mbaya.
 Uongozi binafsi pamoja na hali nzuri. Hii inaweka ndani tabia kama vile uongozi wa kipekee na hali nzuri. Inaweka ndani: kufanya yale unayosema unaweza, kupanga mda wako vipasavyo, kuwa mtu mkamilifu kuliko kuwa mdanganyifu.
Matumisi mazuri ya wakati ni ya muhimu ikiwa unataka kufanikiwa kama kiongozi. Nilisoma hivi karibu nakala moja katika Rwandair Express katika Gazeti la kuruka angani katika ndege juu ya Nelson Mandela. Ili anagazia kuwa alikuwa akiamka daima pa sa 10:30 kila alfajiri bila kujali sharti alizokuwa nazo usiku mbele. Ilionyesha pia kuwa hakujaribu kamwe kuacha watu waendelee kungoja sababbu alikuwa akijisikia kutokufika kwa wakati kwenye ahadi ya kuonana wakati maalum ilikuwa ni tusi kwa mtu aliyekuwa akienda kukutana naye. Matumizi mazuri ya wakati ni ya muhimu kwa kiongozi.
‘Maongozi binafsi pamoja na hali nzuri’ pia inaweka ndani uwezo wa kuona nafasi katika hati yoyote inayotokea kuliko maisha ya John Wesley. Alipoenda Newcastle (kwenye Tyne) kuhubiri alikuwa akikabiliana na ulevi, mapigano na kulaani lakini jibu lake ilikuwa kusiwe na wakukata tama lakini washangilie, ‘’Mungu Asifiwe’’ anasema, ‘’Mji huu ni tayari kwa uhamusho’’. Historia inaonyesha kuwa haki lakini ilimubidi kuwa na uwezo wa kuona kuw mji ulikuwa tayari kwa injili na kutoshindwa na upizani na matatizo aliyo yaona.
15
Tuliona juu kwamba moja ya tabia za kiongozi, kama ukiwa kiongozi wa kizalikio au kiongozi mwelekevu, inahitajika kukuza uongozi binafsi unaofaa. Uongozi binafsi ni walazima kwa kila mtu anayehitaji kuwa kufanikiwa katika maisha. Nilifanya wiki moja mara moja tu pa Busia, Kenya na kujitembeza kupitia Shula la Misingi Lililo kumbwa na upepo mara mbili kwa siku. Nili vutiwa sana na neon la ujumbe (mission) wao ambalo lilikuwa ‘’kutia kwa taratibu utii katika wanafunzi wetu na kuwafanya kujitegemea wenyewe kwa kufanikisha maisha’’. Hakuna mtu awezaye kuwa kiongozi anayefanikiwa bila maongozi binafsi; uwe na uhakika kuwa unayakuza haya.
Tuliona awali kuwa ukaguzi moja wa ma kanisa ya Baptist katika ungereza uliona kuwa wakati nguvu muhimu ya mchungaji ilikuwa ni ‘usimamizi’ – ambao ninaelewa kuwa na maana ya kuwa akiwa ni mwanaume au mwanamke alikuwa amezipanga na angafaanya mambo kuteneeeka - au ‘maono’, nipo kanisa likawa likionekana kukua zaidi. Kwangu mimi, nguvu hizi mbili zina kuja chini ya anwani ya uongozi binafsi pmoja na hli nzuri’.
Kadiri huduma yako inavyokua unahitaji kuhakikisha kuwa unandeleza uwezo wako wa asili, karama za kiroho, tabia za mambo ya adili na maongozi ya kipekee makusudi kila moja ya ‘miguu’ hii iwe na nguvu za kutosha kwa kiti cha mbao kuchukua uzito wangu kinahitaji kuwa na miguu inne thabiti. Ikiwa mbili ni thabiti na mbili ni dhaifu, kitu kitaporomoka nitakapo kiikalia na nitaanguka chini. Hata kama ina miguu mitatu thabiti na moja uliyo dhaifu zaidi hahitachua vipasavyo uzito wangu. Yote inne inahitaji kuwa na nguvu za kutosha kwa kunihimili. Walakini, ikiwa nilitumia kiti kwa kuwekea kitabu kidogo, wakati nilikuwa nikiketi mahali pengine, halafu hata kiti chenye mguu moja zaifu inawezekana kingechukua uzito wa kitabu. Lakini, ikiwa nilitaka kiti kichukue toni kuliko uzito wangu wa kg 80, ningehitaji kuimarisha kila mguu makusudi yote yawe na hizo nguvu za ziada kwa kuchukua vipasavyo shehena hiyo kubwa.
Fundisho hili linatumiwa kwa huduma. Ikiwa una shughuli kubwa ya uwezo wa asili, upako mkuu na una tabia ya mambo ya adili lakini una maongozi ya upekee yaliyo chinibasi unaweza kuchukua huduma ndogo. Watu wataangalia kadiri ulivyo, mara unafika chelewa kwenye kikao au pengine mara nyingi unasahau kufanya yale muliyosema ungepaswa kufanya sababu upo mcha Mungu aliye mwelekevu zaidi na hodari. Walakini, kadiri huduma inakua itakumbana na uwezekano wa kuporomoka kwa sababu ya huo upungufu wa kipekee. Niliwajua watu hodari kabisa waliyoshindwa katika huduma sababu walikuwa wadhaifu aidha katika tabia ya mambo ya adili au kukosa maongozi binafsi. Yanayo kabili ni pia kweli. Watu wa naweza kuwa wenye mambo ya adili zaidi na kuwa na tabia ya kipekee lakini hawana zawadi kubwa yoyote ile. Watu hawa wanaweza kushika huduma ndogo sababu wapo “watu wazuri” lakini watakua kwa shida kwa kuwa na huduma zinazofaa kwa ajili ya huo ukosefu wa uwezo.
Kadiri huduma yako inakua unahitaji kuakikisha kuwa anakuza uwezo wako wa asili, zawadi ya roho, tabia ya mambo ya adili na maongozi ya kipekee makusudi kila moja ya “miguu” hii hiwe na nguvu za kutosha kwa kuchukua shehena inayohitajika ya huduma. Yaliyokuwa yanatosha kwa kuongoza kundi ndogo vipasavyo inahitaji kukuzwa kwa kuongoza kanisa kubwa au kundi la makanisa.
Wachungaji katika Afrika vijijini kuna mara wanasoma kuwa hawaweze kuvuta matajiri sababu wale walio ndani ya kanisa ni wamaskini na mchungaji ni maskini. (kwa “mataziri” mara nyingi wanajihusisha kwa wale wanaojiweza kiuchumi; ambayo tunaweza kuita “daraja ya kati (wastani) katika inchi za mangaribi). Jibu langu kwa fikira zao ni kuwaimiza wajiendeleze wenyewe. Katika Australia, na katika inchi za mangaribi kwa jumla, sifikiri kuwa watu wengi wanatarajia mchungaji kuwa tajiri, kwa kifupi, huenda wangelalamika kuwa kitu kimoja kilikuwa hakiendeki ikiwa angekuwa tajiri. Walakini, kwa kawaida matajiri wanasitawi sababu wana uwez wa asili pamoja na maongozi ya upekee na hali nzuri hakika. Wanayemtafuta ni mchungaji ambaye wanaweza kueshimu. Wanataka mchungaji anaye kuza uwezo wake wa asili, aliye na upako wa kiroho juu ya maisha yake na aliye na maongozi ya upekee pamoja na hali nzuri hakika. Wanakuwa wasio ridhika na wachungaji ambao ni wasuifaa na watatazamia penginepo.
16
Acha niwapeni mfano hai unao nihusu mimi kulingana na hayo yaliyo juu. Nilipokuwa mchungaji nilikuwa nastaajabu kwa vile watu wengi walio na daraja kuu katika philosophy (PhDs) walikuwa wamevutiwa na kanisa nilikuwa nikiongoza; ingawaje hawakuwa wanamemba wa dhehebu nilimokuwa. Juu ya hayo, nilikuwa nikishangaa na maneno mengi muhimu walikuwa wakiyatoa juu ya mahubiri yangu na uongozi ingawaje nilikuwa na daraja la shahada tu. Nina amini sababu yah ii kwamba nilijipanga vipasavyo kwa kujikuza mwenyewa nilipotoka kwenye chuo kikuu cha theologia. Nilitaka kukua na hivyo nika chukua uamuzi wa kusoma na kujifunza maneno yaliyo kuwa yakiambatana na huduma. Tokeo linajitangaza lenyewe.
Ninajua kuwa katika Afrika, na katika sehemu zingine za dunia, watu wanaonekana kuwa wanajihusisha sana na vyeo, tofauti zaidi na tulivyo Australia. Nina amini kuwa ni tatizo lililopo katika asili ya kiafrika ambalo kanisa linapashwa kuelewa. Walakini, ikiwa mchungaji angejikuja mwenyewe kwa nganzi njingine ya ujuzi ndipo anaweza kuvutia ngazi ingine ya watu katika kanisa lake maana yake kiwango kikubwa cha matokeo katika kanisa. Taratibu, kadiri mchungaji anakua na kujikuza mwenyewe, ni hivyo kanisa litakua na kuvutia watu walio na uwezo anaotaka kufikia bila kuzarau maskini. Kwa kawaida ufunguo ni uongozi. Wachungaji, jikuje wenyewe mukishirikiana na Mungu.
1.5. Uwe Pekeyako
Mungu alikupa utu wa kipekee pamoja na mchanganyiko wa zawadi za roho ambazo anatarajia wewe kuzitumia kwa ajili ya utukufu wake. Lazima tukuze yale tuliyo nayo na kuwa watu kama vile Mungu anavyotaka sisi kuwa kuliko kujaribu kuwa mtu mwebgine ule. Ndiyo, tungejifunza kwa wengine na kuchagua yale tunayofikiri inatuelekea sisi lakini mwishowe lazima tuwe watu kama vile Mungu alivyo tuumba sisi kuwa na sio mwigo wa mtu mwengine ule.
Nina weza kukumbuka nilipitia katika shindano hili miaka ya kutosha iliyopita. Nikuwa nikihudumia katika Afrika ya kati nay a mashariki kwa miaka michache nilipo alikwa kuzungumza katika Baraza lililofanyika kampala, Uganda, pamoja na wazungumzaji wengine wa kimataifa kutoka Afrika ya kusini na taifa zinazo Ungana, Marekani. Ninakumbuka vizuri nilijiuliza uliza nini nita fanya na nilijaribu kubadirisha kabisa yale niliyokuwa nikifanya na kutumia mtindo sawa ule wa Benny Hinn; nilipokuwa nikiangalia huduma yake kwenye TV. Mwishowe, nilisadiki kuwa Mungu alinipa utu wa kipekee pamoja na nguvu Fulani na mchanganiko halisi wa zawadi za roho, na kujaribu kuwa mtu mwengine ule inaweza kuwa tusi kwa Mungu kwani ninaweza kuwa nikimuambia kuwa alifanya kosa na kuwa nilihitaji kuwa mtu mwengine ule kabla ya pale ningetumiwa. Uwe pekeyako. Ndiyo, jifunze kadiri uwezavyo kwa wengine lakini baadaye lazima uwe pekeyako kwa kutumia yale Mungu aliyokupa.
Wazo hili “lakuwa pekeyako” litakuwa na maana ya kuwa una weza kuwa na mtindo tofauti wa uongozi kwa mtu mwengine ule. Mtindo wetu unahimizwa na utu wetu. Walakini, kama ninavyo angalia kwenye biblia ninaona kuwa Mungu anatumia watu pamoja na mifano ya utu. Musa aliyekuwa na utu unaofanana huzuri, alikuwa mmoja katika viongozi katika Agano la kale wakati, petro, ambaye alikuwa anatumainiwa sana, alikuwa ni mmoja aliyevutia sana wa viongozi wakuu zaidi katika kanisa la kwanza. Abrahamu, aliyekuwa mtulivu, na Paulo ambaye alikuwa mwepesi kwa hasira, walikuwa pia viongozi wenye nguvu nyingi na walikuwa na ushawishi mwingi juu ya vizazi vijao.
Kila utu unazo nguvu zake na kila unayo mazaifu yake lakini kuwa na utu wa pekee haikuzui kutumiwa vipasavyo na Mungu. Walakini, jaribu kutenda kama mtu aliye na utu tofauti na pamoja na zawadi za kiroho tofauti ni maelezo ya kufanyiza kwa ajili ya hasara. Tunayo hitaji kufanya ni kukamilisha nguvu za utu wetu na kupunguza mazaifu yao.
17
Sura ya 2
Uongozi kwa Kutumikia Njia ya Yesu.
2.1. Kinngilio
Wakristo wengi wangekubali kuwa Yesu anatuandaa pamoja na mtindo wa jinsi tutaishi maisha ya Ukristo lakini kuna mara tuna puza mtindo wa uongozi wa Yesu. Kuna sababu nyingi kwa haya lakini moja ya sehemu muhimu ni kwamba taratibu ya Yesu ya uongozi ni tofauti kabisa nay ale tunayoyaona kandokando yetu katika dunia. Tunaweza kujumlisha mtindo wa Yesu wa Uongozi kwa kusema kuwa alikuja kufanya mapenzi ya Baba yake ya kutumikia kuliko kutumikiwa. Mtindo wa Yesu wa uongozi kwa mamlaka ya mtu mwenyewe na sifa. Angalia shairi zifuatazo:
 Marko 10:45, “kwa maana Mwana wa Adamu naye hakuja kutumikiwa, bali kutumika, na kutoa nafsi yake iwz fidia ya wengi’.
 Luka 22: 27 “Maana aliye mkubwa ni yupi? Siye Yule aketiye chakulani? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye”.
Yesu hakuja kwa ajili ya, wala hakutafuta, sifa na mamlaka ya kidunia. Aliweka hayo yote kando na akajitwika “hali halisi ya mtumishi”. Ona Flp 2:7. Ikiwa ni jinsi hii Bwana wetu aliishi basi sisi tuliyo wana na binti zake tungefuata nyayo zake.
2.2. Usijifanye Bwna kwa watu wengine bali tumikia
Watu wamoja wanafikiri kuwa uongozi wenye nguvu maana yake kuwa Bwana wa wengine wanaokuzunguuka; kutoa amri na kutarajia wao kukutumikia. Wanaona uongozi kama mahali pa sifa na mamlaka ambako wanakuwa wafalme na watu cheni yao ni watumishi wao. Wanaono wengine kama vile wanakuwa hapo kwa kuwatumikia na kuongeza vyeo vyao. Wanatembea kandokando kama ikiwa wapo juu yaw engine na wanaonyesha hali inayosema, “hauwezze hata kusema name isipokuwa ninajishusha kukupa ruhusa”. Kuna nyakati nilisikia watu wakisema juu ya viongozi wengine kama walio wenye nguvu (thabiti) lakini ninayoyaishi yanadokeza kwamaba hawa wanaoitwa “viongozi wenye nguvu” kweli wana “jifanya Bwana juu ya watu” kuliko kuwatumikia. Wakati hii inaweza kuwa mtindo wa wengi katika ulimwengu na haikuwa njia ya Yesu na haingekuwa njia yetu ya kufanya kazi. Angalia shairi zifuatazo:
 Luka 22:24-27, “Yakatokea mashindano kati yao, kwamba ni nani anayehesabiwa kuwa mkubwa.25 Akawambia, wafalme wa Mataifa huwatawala, na wenye mamlaka juu yao huitwa wenye fadhili, 26 lakini kwenu ninyi sivyo; bali aliye mdogo; na mweye kuongoza kama Yule atumikaye.27 Maana aliye mkubwa ni yupi? Lakini mimi kati yenu ni kama atumikaye”.
Katika ukurasa sambamba katika Yohana 13:3-17 tunaona Yesu akitia mafundisho yake katika matendo kwa kuosha miguu ya wanafunzi wake. Hii ilikuwa inakadiriwa kuwa kazi ya unyonge na ilikuwa ikifanywa daima na mtumishi. Mtuhasiyekuwa na cheo chochote katika shirika angekadiriwa namna hiyo tendo la kazi chini ya heshima na daraja zao katika maisha; lakini Yesu alifanya hivyo kama mfano wa vile uongozi unavyo maanisha katika Ufalme wa Mungu. Nina kumbuka kwenda kwenye kazi isiyokuwa ya kawaida kwenye Millmead Centre (kanisa la Baptist la Guilford) katika ungereza kulikuweko Bwana Chiff Richard, ambaye alishiriki kanisa mara moja, alirudia kuimba. Kadiri wa geni walikuwa wakitembea kwenye jukwaa ikaonekana kama hakukuweko viti vyakutosha na kwa hiyo Cliff Richard akashuka ilikwaani haraka na akarudi akichukua viti vya ziada kwa ajili yaw engine kukaa. Hakukuwa na maana ya kuwa “Mimi ni mkuu na kuchukulia wengine viti ni chini ya cheo change katika maisha”, ni haja tu ya kutumikia kama vile mwanamemba wa mwili wa Kristo.
Kwa mwaka wangu wa kwanza wa wakati wote ukijifunza theologia, kanisa nilimokuwa nikishiriki lilinipa kazi Jumamosi asubui makusudi nipate angalau pesa kidogo kwa kulipa hati zangu za shule. Ilikuwa kanisa kubwa pamoja na shule la watoto wa dogo na kituo cha shule la utangulizi pamoja na vyao vingi. Kazi yangu ilikuwa kusafisha kanisa na kusafisha vyoo. Haya
18
yalikuwa mafunzo makubwa ikiwa ningetumia mtindo wa Yesu wa uongozi kwa kutumikia. Nina kumbuka asubui moja nilipomaliza kuporopa na kupanguza sakafu ya mlangoni, kundi la watu, waliokuwa wakitembea inje, waliingia ndani wakitembea kwenye sakafu ninayosafisha na viatu vyao vyenye matope. Hi ilikuwa nafasi ingine ya kukua katika kufanana na Yesu.
 Marko 10:41-44. Hata wale kumi waliposikia wakaanza kuwakasirikia Yakobo na Yohana. 42 Yesu akawaita, akawaambia, Mwajua ya kuwa wale wanaohesabiwa kuwa wakuu wa Mataifa huwatawala kwa nguvu, na wakubwa wao huwatumikisha. 43 Lakini haitakuwa hivyo kwenu, atakuwa mtumishi wenu, 44 na mtu anayetaka kuwa wa kwanza wanu, atakuwa mtumwa wa wote. Mafundisho haya ya Yesu yanafuata mahitaji ya Yakobo na Yohana, ya moja wao kuketi kuume kwake na mwengine kushoto kwake.hayo yalilinganishwa kuwa hali za mamlaka na sifa hapo zamani na inawezekana ilifikia hata wengi wa viongozi wa siku za Yesu kwa kutafuta nafasi kama na hiyo ya sifa.
Yesu anasema ukubwa katika Ufalme wa Mungu ni tofauti na ukubwa wa dunia. Hakuna ubaya wowote kutaka kuwa mkubwa katika Ufalme wa Mungu, ikiwa kweli ni kitu kizuri. Yesu anasema kwamba ikiwwa una hii haja kuu basi utakuwa mkubwa kwa kuwa kwanza mtumishi. Kama nilivyotaja katika utangulizi, Yesu alikuja kufanya mapenzi ya Babaye akiwa mtumishi wa wengine kuliko kuwa akitumikiwa.
Kama tunavyosoma katika Agano Jipya tunaona kwamba wa mitume wanaendelea kufundisha kitu hicho hicho. Soma yafuatayo:
 Katika wafilipi 2:5-8, Paulo anasema kuwa tungekuwa na nia moja kama Yesu na kutumikia wengine. Iweni nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwemo pia ndani ya Kristo Yesu;6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; 7 bali alijifanya kuwa hana utukufu akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu; 8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba!
 Wagalatia 5:13, Maana ninyi, ndugu, mliitwa mpate uhuru; lakini uhuru wenu usiwe sababu ya kuufuata mwili, bali tumikianeni kwa upendo. Jua kuwa tunahimizwa kutumia uhuru wetu kwa kutumikia wengine, na sio kuchochea sifa yetu wenyewe.
 1 Petro 4:10, kila mmoja kwa kadiri alivyoipokea karama, itumieni kwa kuhudumiana; kama mawakili wema wa neema mbalimbali za Mungu. Tunatumia pia karama zetu kwa kutumikia wengine na sio kuongeza sifa zetu binafsi na utukufu. Tunapoombea watu na wakipona au kufunguliwa kutoka mapepo, hatuna cha kujisifia. Imani, kwa asili yake kabisa, linaondoa msingi wowote ule kwa kujisifu au sifa. Soma Rum 3:27, ku wapi, basi, kujisifu? Kumefungiwa nje. Kwa sheria ya namna gani? Kwa sheria ya matendo? La! Bali kwa sheria ya imani. Ni Mungu aliyeponya wagonjwa sio sisi; yote tuliyofanya ilikuwa ni kuomba Yesu awaponye.
 1Petro 5:1-3, Nawasihi wazee walio kwenu, mimi niliye mzee, mwenzi wao, na shahidi wa mateso ya Kristo, na mshirika wa utukufu utakaofunuliwa baadaye; 2 lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia si kwa kulazimishwa, bali kwahiari kama Mungu atakavyo; si kwa kutaka fedha ya aibu, bali kwa moyo. 3 Wala si kama wajifanyao mabwana juu ya mitaa yao, bali kwa kujifanya vielelezo kwa lile kundi. Tena tunaona wazo hili la vile kiongozi wa kanisa anavyo jihusisha na watu walio chini ya usimamizi wake na sio kujifanya bwana juu yao na kuwatawala. Hoja ya mchungaji kama nah ii itakuwa ya kuhudumia wengine kwa ajili ya wema wa Ufalme na sio kujitajirisha. Maali pengine, Paulo anatuambia kwamba mtenda kazi anastahili ujira wake; maana yake mchungaji anastahili kulipwa na kanisa, lakini hiyo siyo inayomusukuma mbele. Hangechochewa na tama.
Ninaona kuwa niyakuhimiza kwani Paulo anaendelea kusema katika shairi la 6 kwamba kadiri tunavyo jinyenyekeza wanyewa na kuhudumia wengine kwa ajili ya wema wa wote, Mungu atatukweza. Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake. Paulo anafundisha fundisho hilo na analitumia kwa Yesu katika Wafilipi 2:9-11. Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia jina lile lipitalo kila jina; 10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwr, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi; 11 na kila ulimi ukiri ya
19
kuwa Yesu Kristo ni Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba. Hili ni fundisho muhimu la kuzingatia.
Ninafikiri wazo hili la kutumia hali mojawapo ya uongozi kwa kutikia wengine ni ngumu kabisa kwa watu kuiweka katika matendo wanapotoka katika asili ambako rushwa ni juu. Uongozi kwa kutumikia ni wakigeni kufuatana na mazingira alimokomaliya. Rushwa inaongoza kwa kutoa viongozi waliyo hapo kwa sifa yao wenyewe na kuchuma mali kuliko kutumia uwezo wao kwa wema wa wote. Ahina hii ya jamii haitowi mfano wa uongozi wa “mtindo wa Yesu” na wale wanaoishi ndani yake wanahitaji kupitisha mda wa zaidi wakifikiri juu ya jinsi Yesu alikuwa akitenda.
2.3. Kutumikia wengine haina maana ya kuwa tuna ruhusu watu kutusukuma kandokando na tunakuwa.
Hatupashwe kufasiri “uongozi kwa kumika” kumaanisha kuwa tuna ruhusu wengine kutusukuma pande zote na kuwa watoto wao bandia; kutumika tu yale wanayo hamuru. Hivyo sivyo jinsi Yesu alikuwa akitenda wala sivyo tupasavyo kutenda. Kumbuka, yale tuliyo yasema mwanzoni, “daraka muhimu la viongozi ni kuchukua watu mahali papya na nafasi nzuri zaidi”. Hatuweze kufanya hivi ikiwa tuna yiruhusu wenyewe kuamuriwa hayo na wengine.
Miaka yangu katika huduma ya uchungaji inahakikisha kuwa mara nyingi wanamemba ndani ya kanisa wanaojinsikia kuwa ni daraka lao kuamwisha yale yanayotokea ndani ya kanisa. Hii ni kweli kabisa wakati kanisa linatawaliwa na mfano wa kusanyiko la watu la kanisa la serkali. Pia kuna wengine wanao jaribu kufanya uchungaji katika njia nyingi kwa ajili ya kufikia yale wanayoyataka. Yesu hakuruhusu kamwe watu kumshurutisha kufanya kitu ambacho alijua hakikuwa haki wala hakuruhusu wengine wala kumuvuta kwa hila. Uongozi kwa kutumika haina maana ya kwamba tuna ruhusu ahina hizi za watu kuwa na nzia zao katika kanisa. Uongozi kwa kutumika maana yake tunaahidi kufanya yaliyo haki kwa kanisa; tuna ahidi kufanya wema kwa watu wote. Kuruhusu huku kuamuru na kuvuta watu kwa hila kuwa katika njia zao sio kutumikia mwili kwa wema ya wote.
2.4. Uongozi kutumikia maana yake tunatumika juu ya hali ya ushindi/ushindi
Wazo la kutumika juu ya suluhisho la ushindi/ushindi ni la maana ikiwa tutafuata mfano wa Yesu na kutenda kazi juu ya mafundisho ya “ uongozi kwa kutumikia ”. kwa ushindi/ushindi nina maanisha kwamba wewe kama kiongozi chuma kutoka maamuzi na watu unaoongoza pia wanachuma; pande zote mbili zinashinda. Maamuzi ya ushindi/ushindi yanafaidisha makundi yote mawili. Katika wafilipi 2:1-14 Paulo anahimiza kanisa pa Filipi kufuata mfano wa Yesu ambaye “alijifanya mwenyewe kutokuwa si kitu, akatwaa namna ya mtumwa”. Lakini Paulo ameahidi kabisa kwenye mafundisho ya ushindi/ushindi –ona shairi 4:kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali kila mtu aangalie mambo yaw engine. Anasema kuwa tungeangalia nyuma ya faida yetu wenyewe lakini pia tunge jitilia sharti juu ya hali njema ya watu wengine; hii ni ushindi/ushindi, ambako kila upande ukifaidika.
Stephen Covey, katika kitabu chake cha kuuza nzuri zaidi, tabia 7 za watu wakuu zaidi wanaofaa, anaeleza kuwa moja ya tabia za watu wakuu zaidi wanaofaa ni kufikiri ‘ushindi/ushindi’. Mafundisho haya inatumiwa kwenye CEO ya shirika kubwa kama ilivyo kwenye mume na baba. Hakuna anayetaka kupoteza kama tokeo la maamuzi yaliyofanywa na wengine; ina tokeza tu uchungu na kuendelea katika matokeo mabaya.
Ninakumbuka tukio ambalo lilitokea katika shule la Biblia mke wangu nani tulishiriki zaidi ya miaka 30 iliyopita maelezo hayo dhahiri faida hali ya ushindi/ushindi. Mmoja kati ya kundi la wakuu alikuwa ameweka utepe wa gramafoni na mtambo wa kutoa sauti mbele ya pale nilikuwa nikiketi, mwanafunzi (F) kutoka nchi hisiyo zungumza kingereza alitaka kufunga utepe wake kwenye gramafoni kwa shika mafundisho na kuyafuata wakati atakuwa huru. Kutoka pale nilikuwa nikiketi nilifikiri kwamba ilikuwa haiwezekane kwa vyovyote vile na kuwa angeambia wanafunzi mara moja kuwa haiweze ifanyike. Hakufanya hivyo, bali alisema, “Munapenda nifanye nini?” Alifanya pendekezo ambalo lilitatua tatizo lake bila kuhatirisha yale aliyokuwa akiyafanya. Ilikuwa ni hali ya
20
ushindi/ushindi halisi. Alifikia yale aliyokuwa ametaka Yule mwanafunzi mke na mwanafunzi mwanaume; kitu ambacho kilichangia kuboresha udungu katika shule la Biblia.
Mchango mwengine ni hali ushindi/kupoteza. Covey anaandika, “katika mtindo wa uongozi, ushindi/kupoteza ni njia ya kinguvu: ‘nimepata njia yangu; haukupata yako’.Ushindi/kupoteza. Watu wanahitajika kutumia mwelekeo, uwezo, hati ya kuthibitisha, mali au utu wa kupata njia yako”.5Jambo liletalo huzuni ni kwamba watu wengi wamepatikana katika njia hii ya kufikiri wote maisha yao.viongozi wanaotenda kazi juu ya mchezo wa ushindi/kupotezamara nyingi unaona kuwa hao walio chini yao wanakosa motisha na hawatimize matokeo makuu. Hakuna anayetaka kupoteza nyakati zote. Watu walio chini ya mtindo wa ushindi/kupoteza wa uongozi hawawezeshwe kutimiza zaidi ya vingine vile wangekuwa navyo. Kama vile matokeo mazao yanashuka chini na tokeo la mwisho sio ile ambayo ingekuwa ikiwa kiongozi alitenda kazi juu ya mafundisho ya ushindi/ushindi. Mara nyingi watu wanaondoka na wanenda mahali pengine wakati kiongozi aliye juu yao anatenda kazi juu ya Ushindi/kupoteza.
Sasa kuna kupoteza/ushindi. Hapa ni pale ninapoteza lakini wewe una ushindi. Usikubali ahina hii ya mafikiri ambayo hii ni ile iliyo na maana ya kuwa mtumishi; juu ahipo kupoteza/ushindi mara nyingi inatokea wakati upande umoja unanguvu zaidi na ungine ni zaifu wale kwenye upande moja ana kiburi ndogo kama na hiyo ambayo hawa amini kuwa wanastahili kufaidika kutokana na ushirika. Hali hii inaweza tokea katika ndoa wakati mume mmoja anajiona mwenyewe kama ‘mpatanishi’ atakaye fanya kila kitu kwa ajili ya amani. Hii haistahili. Ikiwa lengo la kiongozi ni kuwezesha watu kukomaa na kufaulu katika maisha ndipo hali ya kupoteza/ushindi si nzuri. Sio vema kwa kiongozi kufanya shauri ya kupoteza makusudi mtu mwengine apate ushindi; wala ni akiba ya kweli.
Mwishowe tuna mchanganyiko wa kupoteza/kupoteza. Juu yah ii shurti hizi zinazo amuriwa, Covey ana andika, “wakati watu wawli ushindi/kupoteza wanaenda pamoja hayo ni, wakati wote wawili ni imara, wakaidi, kutafuta faida yao wenyewe matokeo yatakuwa kupoteza/kupoteza. Wote wawili watapoteza. Wate wawili watakuwa wenye kulipiza kisasi na kutaka ‘kurudisha’ ana ‘kuwa sawasawa’ upofu kwenye hali ambayo ina ua kwa kusudi ni kijiua, huka kujilipiza kisasi n upanga ukatao kuwili”.
Anaendelea kusema, “Ninajua ndoa iliyo achana ambamo mume alikuwa ana amuriwa na jaji kuuzisha jumla ya mali aliyo nayo na kumurudishia aliyekuwa mke wake zaidi ya nusu. Kwa kukubali, aliuzisha gari ya thamani ya zaidi ya $10.000 kwa $50 na $25 kwa mkewe. Mke alipokataa, msimamizi wa baraza la hukumu alichunguza hali hiyo na akagundua kama mume alikuwa akiendelea katika njia ile ile kama desturi kwa jumla ya mali zote.Watu wamoja wanakuwa wanajiunga kabisa na adui, akishikilia kabisa pamoja na mwenendo wa mtu mwengine kuwa wamekuwa vipofu kwa kila kitu isipokuwa nia zao kwa huyo mtu kupoteza, hata ikiwa inamaana ya kujipoteza wenyewe”.6 Inaonekana wazi kuwa mwenendo huu sio nzuri kwa ndoa, kanisa, wala hali ingine ile ambamo kiongozi anajikuta mwenyewe.
Nina jua kuwa mara nyingi hali inajitokeza ambako uamuzi unaweza kuchukuliwa papo hapo na ambako hakuonekane kuwa suluhisho wazi ushindi/ushindi. Chini ya taratibu hizi kiongozi atachukua uamuzi ambao anajisikia kuwa kwa faida nzuri ya wote na kutumaini kuwa alifanya yaliyo kweli. Walakini, hali kama na hizi ni chache, na kawaida tunawakati wakufika kwenye matengenezo ya ushindi/ushindi. Mchungaji, mume wala baba, anayeendelea kutazamia kwenye hali za ushindi/ushindi ana jamaa lake linafikia yanayowezekana kwao na kufanikiwa katika maisha.
5 Covey, The 7 Habits of Highly Effective People, 207
6 Covey, The 7 Habits of Highly Effective People, 210
21
2.5. Mtindo wa uongozi wa Yesu unahitaji kujiweka chini kwa wote.
Amri ya kuwa mtiifu inapatikana katika Agano Jipya. Nikitu ambacho kinge eleza tabia ya kila mmoja ndani ya Mwili wa Kristo; wawe ni viongozi wa shirika, Mchungaji au mwanamemba wa kanisa. Angalia shairi zifuatazo:
 Yakobo 3:17, Lakini hekima itokayo juu, kwanza ni safi, tena ni ya amani, ya upole, tayari kusikiliza maneno ya watu, imejaa rehema na matunda meme, haina fitina, haina unafiki.
 Warumi 13:1, Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu. Lazima tutii serkali. Fahamu kwamba hatuamurishwe kuwatii juu wanaweza kutuomba kufanya kitu ambacho hakiambatane na ombi za kibiblia. Walakini, lazima tuwatii. Hivi karibuni tutazungumzia utofauti ulioko.
 Waefeso 5:21, Hali mna…nyekeana katika kicho cha Kristo. Aulo anaomba waamini kunyenyekelea waamini wengine.
Sehemu ya tatizo letu na shairi hizi, na zingine ambazo zinasema juu ya unyenyekevu, ni kwamba mara nyingi tunaelewa vibaya maana ya unyenyekevu. Watu wengi wanafikiri kuwa kunyenyekea mbele ya mwengine maana yake tunapaswa kuwaeshimu bila hata kusita. Shairi kama vile waefeso 5:22, ambayo ina ambia mke kujitiisha kwa mume wake katika vitu vyote, mara nyingi zinatafsiriwa kuwa mke lazima amueshimu mume wake katika vitu vyote. Hii sio kweli. Kunyenyekea sio sawa kama kueshimu.
Acha tuangalie kwanza waefeso 5:21-22 Biblia zetu zinagabua shairi za 21-22 mara mbili lakini hii ni pungufu sababu ina potoa yale Paulo anayoyasema. Nina amini kama ingekuwa imesaidia kabisa ikiwa shairi za 21 na 22 zilikuwa zinaunganika kwa kuunda shairi moja. Sababu yah ii ni kwamba wagiriki wana tendo mojaa tu ambalo linatumiwa kwa amri zote mbili; hayo ni, tendo ambalo linaambia waamini kujitiisha kila moja na mwengine. Ni tendo moja ambalo linasema wanawake kutii waume zao. Na siohata tendo moja ambalo linatumiwa mara mbili – mara moja tu katika shairi la 21 na mara moja tu katika shairi la 22 – kuna tendo moja tu.
Kwa bahati mbaya, tu nasoma shairi la 21, basi ni wazi inatumainiwa kuwa ‘kutii’ sio sawa kama ‘eshimu’, sababu sija sikia kamwe mtu akifundisha kuwa mwamini katika kanisa ataeshimu vitu vyote ambavyo mwamini mwengine anavyomuambia kuvifanya. Hakuna fundisho ndani ya Agano Jipya linalo nifundisha kuwa mimi, kama mwanamemba wa mwili wa Kristo, mazma nieshimu waamini wengine wote. Siweze; lakini ninawa jibika kuwatii.
Pamoja na sababu hii, utiifu maana yake nini? Acha niwakumbushe kuwa Waefeso 5:21 inasema, Hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Unyenuekevu maana yake tunaweka kando haki zetu na mapendeleo na kuhudumia wengine kwa wema ya watu wote. Ninapenda neon lifuatalo lililochukuliwa kutoka kwa Snodgrass juu ya shairi hili, “Yale Paulo anayo katika akili ni kwamba wakristo watupe kujiangalia wenyewe na watu mike kwa ajili ya wema wa wengine”.7 Nyuma katika Waefeso 6:1-5, tulisoma kuwa watoto laity waeshimu wazazi wao na watumwa laity waeshimu ma bwana zao wa kazi lakini hatuombwe kueshimiana kati yetu, isipokuwa tu kuwanyenyekea; hayo ni, tunatupakula kujifikiri wenyewe na kutia kando haki zetu makusudi tupate kutumika kwa ajili ya wema ya wangine.
Wakati mchungaji wa umri mkubwa anapojinyenyekeza kwa kiongozi kijana haina maana ya kama ata mueshimu kiongozi kijana na kufanya yale anayoyaomba lakini kuliko hayo mchungaji anaweka kand kila haja ya sifa na uwezo na anatumika kwa ajili ya wema wa kiongozi kijana makusudi yeye pamoja na kanisa waweze kujengwa. Hii ni mbalimbali kabisa na ‘kujifanya bwana juu ya watu’ sababu ninapojifanya ‘bwana juu ya wengine’ ninajipenda mwenyewe katika cheo change na sifa na sijipe sharti kwa lazima ya kukua kwa wengine. Ninapojifanya bwana juu yaw engine niona jishughulisha kwanza kwa ajili yangu mwenyewa na mara nyingi nitamalizia kwenye ushindi/kupoteza kama matokeo kuliko ushindi/ushindi. Wakati kiongozi anapochukua hali ya utiifu
7 Snodgrass, Ephesians, 311
22
sawa Yesu, anakuwa mtu anayejipa sharti kwa kuwezesha watu wake makusudi watimize vipasavyo zaidi kuliko vingine wangekuwa navyo. Siyo hii ambayo kiongozi anafanya?
Nini kinachotokea kwa hali ya mchungaji mkubwa kwa wale walio chini yake, pia inatokea katika kupindua. Viongozi vijana na wengine wenye vyeo vya uongozi ndani ya kanisa lazima watii mchungaji wao mkuu.katika 1 Petro 5:5 Petro anaambia vijana kuwa wawatii wale walio na daraka ya uchungaji juu yao. Tafsiri ya NASB ni nzuri; “enyi vijana, vivyo hivyo, jitiisheni kwa wazee wanu”. NIV inaonekana kukosewa jambo ambalo Petro analoliweka anapotafsiri kigriki kama, “vivyo hivyo ninyi vijana, watiini wazee”. Tangu neon la kigriki linapotafsiwa ‘mzee’ au ‘mchungaji’ katika 1 Petro 5:1, ni vizuri zaidi kuipatia maana moja na shairi la 5; hayo ni, kuwa inarejelea kwa mtu moja aliye na usimamizi kuliko mtu moja aliye mzee wa mwili.
Acha nitoe maelezo zaidi juu ya wazo hili la vijana wawatii wale walio na daraka ya uchungaji inaonekana kuwa zaidi ya tatizo katika inchi zimoja za dunia kuliko katika zingine; inawezekana ina kitu Fulani cha kufanya pamoja na mtindo wa uongozi wa taifa ambao ulipata njia yake katika kanisa. Niliona na kusikia viongozi vijana wengi ambao walijisikia kuwa wana wito wa kuchunga kanisa lakini ambao hawakuwa na sababu katika njia ya utiifu. Wana wake kando kwa kudhoofisha mchungaji mkubwa makusudi watu wanaweza kuwafuata. Walipokuwa watu wengi kwa upande wao wangeondoka na kuchukua hao watu pammoja nao na kuanzisha kanisa lao wenyewe. Walakini, matokeo wanatengana na kanisa la asili wanakuhusu utambaaji wa uchanga na uaribifu.
Historia inaonyesha kuwa hawa wavijana wasio watiifu wanavuna yale waayoyapanda kwa sababu kwa kawaida mtu moja anapandishwa katika kanisa lao na kuwadhoofisha; tayari kuanzisha mpasuko mwingine. Katika wagalatia 6:7 Paulo anatupatia mafundisho muhimu ya kiroho; ‘Tunavuna yale tuliyo yapanda’. Msidanganyike, Mungu hadhihakiwi; kwa kuwa chochote apandacho mtu ndicho atakacho vuna. Tokeo la mwicho kwa mtindo huu wa mwenendo ni kwamba kuna kanisa ndogo nyingi lakini makanisa machache kati ya hizo ni kubwa la kutosha kwa kununua uwaja, kusimamisha jingo nzuri na kulipa wachungaji. Shabaa ya kuwa hivyo ni kwamba wana pofikia kwenye ngazi Fulani mtu mwengine watamaa ya cheo anainuka na kuwadhoofisha; akichukua nusu ya jamii ya watu waabuduo wao na kuondoka nao bila mapato ya kutosha kwa kuendelesha kukua kwao.
Nilianza mazungumuzo haya pamoja na hitaji kwa wazee wa chungaji kuwa wanyenyekevu na kujitahidi kwa hali ya ushindi/ushindi sababu ni nafikiri hii ni funguo Ikiwa mchungaji anajipatia sharti ya ‘kuwezesha watu wake makusudi watimize zaidi kuliko vingine wangekuwa navyo’; kuliko sifa yake mwenyewe na uwezo, basi ina elekea kuwa kiongoji kijana hatajisikia kuhitaji kuchukua mambo katika mikono yake mwenyewe na kuyaweka inje kwa kuanzisha kanisa lake mwenyewe. Badala ya hayo, atakuwa amepatikana kwenye mtindo wa Yesu wa ‘uongozi kwa kutumikia’ na kutenda kazi njia hiyo mwenyewe.
Brian Houston, Mzee Mchungaji wa kanisa la Hillsong-Australia ni mfano mkuu wa mafundisho haya. Hillsong ni kanisa kubwa zaidi katika Australia. Ninakumbuka nilisikia Brian akiambia wachungaji kuwa ilikuwa ya muhimu kwamba wa wajenge watu walio chini yaohata ikiwa hawa watu wanakuwa maarufu zaidi kuliko wao. Alitumia mfano wa Darlene Zschech, kiongozi wake wa maabudu, na kuchangia jinsi alivyo fikia kusema kwenye Conference katika USA na alikuwa amesimama pamoja na Darlen wakati mwanamke moja alipomkaribia akiwa na Camera. Brian kwa mzaa alisema kama alifikiri hivyo mwanamke alikuja kumwambia mara ngapi ujumbe wake ulimubariki na angechukua picha yake lakini hakufanya hivyo. Ali muuliza ikiwa anaweza kumupiga picha pamoja na Darlene. Moja ya shabaa zinazofanya kanisa la Hillong kuwa kubwa hivyo ni kwamba viongozi chini ya Brian wamejifunga kwake na kwenye maono yake sababu wanajua kama Brian pia amejipa sharti kuwa kuwajenga.
Acha nipotoke na niseme kuwa nilijua kiwango cha watu wengi ambao wanasadiki kama waliitwa kuchunga kanisa na kuwa wote wana karama na akili ambazo zinatosha kwa kufanya hivyo. Kwa bahati mbaya, ni wamoja wamoja tu wanaofikiri hivyo. Wamoja wa watu hawa walisadiki kweli kama waliitwa kwamba wachunge hadi wapate kanisa litakalo wakubali kama mchungaji wao lakini kwa bahati mbaya ina tokea tu katika mzozo. Nina amini kwamba ni mwili ambao una hitaji
23
kuhakikisha kuwa Mungu aliita mutu kuhudumu na kuwa walipewa karama zote zinazofaa. Nilipoomba kwa dhehebu langu ukubalifu wa kusoma kama mchungaji, waliandika makanisa mawili ya mwisho ambamo nilikuwa nikishiriki ma barua kwa kuona ikiwa watu wanajua ya kuwa Mungu alinibariki katika njia hii.
2.6. Mpende watu wenu na muombe juu yao.
John Maxwell ana andika ‘’lazima ungepata kuwapenda kabla ya kuweza kuwaongoza’’8. Ikiwa watu wanajua kwamba unawapenda na kuwa unawapenda upendo unaotoka katika moyo, nadhani hawana budi kukufuata. Wachungaji wamoja wanashurutisha kusudi juu ya sifa zao wenyewe ambazo wanapatia kipao mbele kuwa watu ni wa baadaye, karibuni kero kwao, kwa kutimiza ksudi zao. Watu hawapendi kutumiwa na kuna wakati wamoja kwanza watafuata mchungaji kama na huyo sababu wana kubaliana na maono yake,matokeo ya mwisho ni kuwa mara nyingi wana sononeka na kuhasirika na kwenda mahali pengine. Utofauti wangu kwa usemi wa Makwell ni: ‘’La zima upende watu wako na sio kuwaona tu kama njia ya kutimiza makusudi yako mwenyewe’’.
Katika 1 petro 4:8 tunasoma, ‘’Zaidi ya yote iweni na juhudi nyingi katika kupendana; kwa sababu upendano husitiri wingi wa dhambi’’. Sisi wote tuna nguvu na sisi wote tuna mazaifu. Mafanikio mangi kati yetu yalikuza nguvu zao na kupunguza mazaifu yao. Ikiwa watu wako wanajua kuwa unawapenda watakusamehe juu ya wingi wa makosa yako. Haya ni yamuhimu kujua. Hakika inaiweka raïsi kuongoza.
8 Maxwell, Developing the Leader within You, 59
24
Sura ya 3.
Mafundisho toka kutoka 18
3.1. Uongozi hafifu unaleta matatizo
Jambo linalo tajwa juu yetu katika kutoka 18 linonyesha jinsi uongozi ulivyo wa muhimu ikiwa tunaenda kutimiza mambo tunayopewa na Mungu wetu. Mungu alimuhita Musa kuongoza waisraeli kutoka katka utumwa na kwenda katka inchi ya Ahadi lakini kwa wakati ule Yethro alikuja kuwaona; tunakuta kwamba maendeleo yao yalisimama vipasavyo ona kutoka 18:13. Asubuhi yake Musa akaketi ili awapishie hukumu watu; na hao watu wakasilala kumzunguka Musa tangu asubuhi hata jioni. Sio tu walipo simama kwa wao moja wakati Musa alipotatua matatizo lakini walikumbana na hatari halisi ambayo Musa ange stahimili kutoka ‘kudhoofika’; ambako kungekuwa na matokeo ya kutisha kwa wakati ujao. Kutoka 18:17-18, Mkwewe Musa akamwambia, ‘’Jambo hili ufanyalo si jema. 18 Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia; maana jambo hili ni zito kwako; huwezi wewe kulitenda peke yake’’.
Yethro ametambua kuwa Musa ana tatizo na uongozi wake na anamupa shauri ya jinsi ya kuyashinda. Kama tulivyosoma awali katika kutoka 18 tunaona kuwa jibu ilikuwa kubadirisha muundo wa utaratibu wake, wakilisha mamlaka, fundisha wengine zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuifanya. Musa alikuwa akitenda pamoja na ‘huduma moja muhimu’ mtindo wa uongozi nah ii ilikuwa chanzo cha tatizo. Alihitaji kukuza uongozi wake ikiwa alienda kufanikiwa katika kuchukua kabisa kazi ambayo Mungu alimupa.
Jua kuwa Yethro hakumupa Musa ‘shauri la kiroho’. Hakumuambia kuomba zaidi au kutaka huduma kubwa ya Roho Mtakatifu, wala hakumuambia kuhudumu zaidi katika ma alama na muimiza; kwani hii haikuwa uzaifu wa Musa. Alikuwa mtu aliyetumika katika uwezo wa Mungu zaidi ya watu ambao wamewai kuishi. Tatizo lake halikusababushwa na ukosefu wa upako lakini ilikuwa ni tokeo la uongozi afifu; ni hii alihitaji kubadili kwa leo wachungaji wengi wanaweza kuhitaji kuomba zaidi au kuendelea katika karama za Roho katika njia kubwa lakini hii haikuwa ndiyo tatizo la Musa. Kuwa kiongozi Mkristo kunatuhitaji kuwa na nguvu katika pande zote mbili sehemu ya kiroho na sehemu ya asili, na inayofuata inahusika na uongozi.
Tunahitaji kujua kuwa Musa alikuwa na uwezo wa kutimiza kazi kubwa kwenye hatua hii kwa hiyo Mungu alimutumia vipasavyo kwa kupambana na Faraho, anaongoza waisraeli nje ya Misri, aliwapeleka kupitia Bahari Nyekundu na katika ya jangwa. Watu waliyo na upako mkubwa kweye maisha yao na wanao endelea katika uwezo wa Roho Mtakatifu mara nyingi wapo na uwezo wa kuweka nyota kubwa katika huduma. Watu wanavutiwa kwanza kwao sababu ya yale wanayoona Mungu akiyafanya kupitia wao, lakini ikiwa wanapungukiwa na welekevu wa uongozi unaofaa, hawaweze kuwa na uwezo wa kuendesha huduma pamoja na kiasi kimoja cha kufanikiwa.
Hii haina maana ya kwamba uongozi ni muhimu zaidi kuliko zawadi ya kiroho au kuwa inagomboa hitaji kwa mwombaji, mbali na hiyo, lakini haimaanishe kuwa tunahitaji kukuza welekevu wa uongozi wetu vile kwa maisha yetu ya kiroho.
3.2. Matatizo pamoja na ‘huduma ya mtu moja mtindo wa uongozi’
Musa alikuwa akifanya ‘huduma ya mtu moja’ mtindo wa uongozi ambamo alikuwa moja ambaye alikuwa akifanya huduma zote. Kila mara watu walipokuwa na matatizo walikuja kumuona Musa na angejaribu kutatua matatizo yao. Mtindo huu, ambao unatumiwa mara nyingi na wachungaji leo, una vizuizi vingi vifuatavyo:
 Inazuia maendeleo katika hali ya Israeli ilizuia maendeleo yao kwenda mbele kwenda kwa Inchi ya Ahadi kwani walipitisha muda wao mwingi sasa wakisimama hadi pale Musa alifanya huduma. Katika hali ya makanisa ya mahali inapunguza kukua sababu mchungaji anaweza kufanya tu mengi zaidi.
25
 Ina lazimisha ulegevu mwingi juu ya kiongozi na mara nyingi matokeo ndani yake ‘kujitenga’ na kuacha huduma. Kumbuka shauri la Yethro kwa Musa katika kutoka 18:17-18, “Mkwewe Musa akamwambia, Jambo hili ufanyalo si jema. Huna budi utadhoofika wewe, na hawa watu walio pamoja nawe pia”. Kujaribu kuwa mmoja anayefanya huduma zote inaweza kuongoza kwa uraisi kwenye sikitiko, kuishiwa nguvu kiroho na kimwili; hasa ikiwa upo mwenye bidii ya kufanya vyema yote yapasayo na huduma ina hanza kukua.
 Watu hawatarizika. Hii itaweza kuonekana kuwa ya kigeni kuelewa kwa kiongozi asiyejua. Anaweza kutoa hoja, “ndio, ninaweeza kufahamu kuwa huduma ya mtu moja inaweza kunicheofisha kabisa lakini haikosi ni ya kufaa zaidi kwa watu” hii sivyo ilivyo. Sikilizeni shauri la Yethro katika kutoka 18:18 na 23, “Wewe na watu hawa walio pamoja nawe mutajidhoofisha wenyewe…kwamba utafanya jambo hili, na Mungu akikuagiza hivyo, basi utaweza kusimama wewe, na watu hawa wote nao watakwenda mahali pao kwa amani”. Juo kuwa huduma ya mtu moja sio nzuri kwa watu vile vile; ina wadhoofisha na hawafanikiwe kwenda popote.
 Ni mbalimbali na mafundisho ya Agano Jipya. Waefeso 4 :11-12 inatuambia kuwa shabaa ya Kristo kuweka viongozi ndani ya kanisa haikuwa makusudi wapate kutumika huduma zote lakani zaidi kuandaa watakatifu makusudi watakatifu wapate kuhusishwa ndani ya huduma. “ Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii, na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu ; 12 kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe ”.
 Watu wanapenda zaidi kulaumu mchungaji. Mchungaji anapofanya huduma zote mwenyewe mara nyingi watu wanamulaumu sababu hakujibu mahitaji yao ingawaje anaweza kuwa akifanya kitu kizuri. Watu wanapohusishwa katika huduma mara nyingi wanaona kanisa kuwa ‘kanisa letu’ kuliko ‘kanisa la mchungaji’ na kama tokeo, wanajaribu kupunguza malaumu ; hakuna atakaye kulaumiwa hadharai waowenyewe.
Pamoja na yaliyo juu moyoni acha niwapeni sababu za kwa nini wachungaji mara nyingi wanatumia mtindo wa huduma ya mtu moja
 Hawajui lolote zaidi kwa nini Musa aliruhusa hali hii kutokea ? kwa nini alikuwa ni yeye aliyekuwa akitoa hukumu zote ? N inaposoma kutoka ninafikiria kuwa alikuwa akitenda hivyo sababu alifikiri hivyo ilikiwa kitu kizuri kufanya. Musa, pamoja na tabia yake ya huzuni ambayo ilikuwa na upendeleo kwa kuwa akitoa zabihu mwenyewe. Aliona kuwa hiyo ilikuwa wajibu wake na kwamba alihitaji kutoa zabihu mwenyewa kwa kutumikia watu wake. Haya yaweza kuwa ya muhimu zaidi lakini so busara zaidi. Inadokeza pia kuwa Musa, pamoja na mafundisho yake yote katika uongozi. Jibu lake kwenye maswali ya Yethro inatuambia kwamba alikuwa amekosewa mafundisho ya msingi. Chuo cha mafunzo ya thedogia kwa kawaida kimeanguka katika jamii hii. Wanaweza kutumia muda mwingiwakifundisha wanafunzi wao jua ya theologie, mashauri na elimu ya maadili lakini wanatoa mda mdogo kwenye mafundisho ya inahitaji kuwekwa ndani. Wachungaji pamoja na viongozi wengine, iweni na hakika kuwa munaweka kando kujifunza kadiri muwezavyo juu ya uongozi. Munaitwa kuwa kiongozi kwa hiyo jiandae mwenyewe kwa ajili ya kazi.
 Kwa desturi itakokea ijapokuwa unachukua hatua za kuifadirisha.Yethro alipo uliza Musa kwa nini alikuwa ni yeye mwenyewe aliyekuwa akitenda kama muamuzi alijibu, ‘’kwa sababu watu wananijilia kutafuta mapenzi ya Mungu’’ . (kutoka 18 :15) nina uhakika kwamba Musa hakuambia watu wanapashwa kumujilia pamoja na maneno yao ; waliyafanya tu. Hii ni asili ya mwanadamu. Ikiwa watu kanisani wanataka kuona mtu fulani juu ya tatizo, wazo lao la kwanza ni kumuona mchungaji. Kwa kawaida hii ni kweli ikiwa ni mtu mwenye akili nzuri. Watu wanapenda kuwa endea viongozi wenye akili pamoja na matatizo yao kuliko kwa mshirika wake.
 Wachungaji wamoja wanataka kusimamia kil akitu na hawatake kuwakilisha madaraka. Niliwai kukutana na wachungaji wamoja ambao wanazingatia mtindo wa ‘huduma ya mtu moja’ sababu hawapende wengine kuchukua uamuzi. Wanataka kusimamia kil akitu ambacho kinasemeka na kufanyika na wanataka kuhakisha kuwa maelezo yote ya mwisho ni njia wanayotaka kitu hicho. Hawatake kuwakikisha madaraka na kuruhusu wengine kutoa maamuzi. Kiongozi kama na huyo anatenda kama kizuizi ambacho kinazuia kanisa kukua.
26
Ikiwa kiongozi huyo alifundishwa kuhusu uongozi lakini hajuwi yupi anayeweza muwakilisha katika usimamizi akiwa na madaraka ya kutosha, ndipo kwa kawaida ina onyesha kwamba kiongozi ana tatizo la ndani. Kama ninavyo angalia nyuma kwenye miaka iliyopita kuwa nilikuwa ninajihusisha na maisha ya kanisa niliona wachungaji wengi ambao walikuwa na huu uzaifu. Tungewaita ‘watawala wachupavu’.
Acha niwape mfano. Miaka mingi iliyopita mke wangu nami tulienda kwenye kanisa ambalo, kufuatana na hali, lingepashwa kukua kwa kasi lakini halikukua. Mchungaji alisisitiza kuwa hakuna kundi ndani ya kanisa linaloweza kufanya kikao asiposhiriki na alikuwa mwenyekiti. Kusudi lake ilikuwa ni kuendelea kuongoza makusudi hakuna uamuzi uliochukuliwa ambao haukuwa kwa faida nzuri ya kanisa kama alivyokuwa akiyaona. Nina uhakika kwamba alikuwa na nia njema zaidi lakini aliharibu yaliyohanza, aliseta bidii yoyote ambayo yeyote ule angekuwa nayo na kuzuia kukua kabisa. Haitaki kusema ilitokeza kitendo kikubwa cha manunguniko na mgawanyiko ndani ya kanisa na hatimaye mchungaji aliondoka na akaenda katika kanisa lingine.
Walakini, historia hapo juu lina mwisho unao furahisha ambamo mchungaji mpya alikuja ambaye aliweka tumaini katika mafundisho ya uongozi wa kundi na kanisa likakua kimiujiza. Nina weza kukumbuka mmoja wa viongozi akiniambia kwamba hawakutaka kuwa mbali na kukosa huduma ya mahabudu munamo wakati huu sababu vitu vingi vya kuvutia vilikuwa vikitokea.
Tungejua pia kuwa zimoja ‘huduma za mtu moja’ zinaonekana kuendelea vizuri mwanzoni ; hasa ikiwa kiongozi ana karama kabisa. Musa ni mfano mkuu wa haya. Aliongoza watu kutoka utumwani Misri, walivuka bahari nyekundu na kuelekea jangwani. Ilikuwa ni jambo la, “ mbali zaidi, Nzuri zaidi ! ” lakini huzuni ni kwamba haikukawia kwa mda mrefu sababu alikuwa amevumilia katika jangwa, akijihusisha na matatizo ya watu tangu asubui hadi jioni, hangeweza kutoka. Mwanzoni alikuwa amefanikiwa sababu watu walikuwa wamevutiwa na karama zake nyingi na kwa haja moja ya kupona.
Walakini, tisho la faraho kwa waheni lilipo toweka, watu walihitaji matatizo yao yapate kushughulikiwa, kuliko kuya puza kwa muda kitambo kama walivyofanya walipokuwa wakitoroka Misri, karama za kiroho za Musa zilikuwa hazitoshi kwa kubadirisha miundo yake ya uongozi. Karama zake zilimuchukua mbali kabisa lakini hazikutosha kwa kutimiza kazi ya kuongoza Israeli katika inchi ya Ahadi. Niliona wachungaji, wamoja ambao nitataja baadaye, ambao walikuwa na karama kweli na ambao waliwezesha watu kuwafuata kwa mwanzo. Huzuni, ukosefu wao wa wlekevu wa uongozi hatimaye ilizusha tatizo kama na hili, watu walianza kuondoka na kwenda penginepo.
3.3. Badili miundo yako ikiwa ni lazima
Kama viongozi, tunahitaji kubadi miundo ya shirika zetu tukiondoa vizuizi vya kukua. Shauri la Yethro lilimukwamua Musa kutoka mzigo uliyokuwa ikimlemea wa kujaribu kufanya huduma zote mwenyewe na alimupa wakati na nguvu ya kutoka kwenye kazi nyingi za uongozi. Suluhisho la Ythro ilikuwa ni kubadili miundi ya uongozi ambayo kwayo Musa angeweka wakuu juu ya maelfu, mamia, hansini na makumi kwa kutumika kama waamuzi wanapokumbana na maneno yaliyo makubwa na kuhifadhi usimamizi mwingi. Ona kutoka 18 :21-22, zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu ; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi ; 22 nao wawaamue watu hawa siku zote ; kusha kila neno lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neno dogo wataliamua wenyewe ; basi kwako wewe utapata nafasi zaidi, nao watauchukua huo mzigo pamoja nawe.
Miundo mizuri haisibitishe kuwa huduma yako ita kua lakini inahippatia nafasi nzuri zaidi ya kufanya hivyo. Miundo mibaya itazuia kabisa kukua.
27
Katika Matendo 6 :1-5 tunapata kujua habari ya jinsi kanisa la kwanza lilivyo balidili muundo wa shirika lao kwa ajili ya kuzuia tatizo la mgawanyiko uliyekuweko lakini si wazi kulikuweko kutopatana katika kanisa sababu wayahudi wa kiyanani walikuwa wakinungunika kwa sababu wajane wao walisahauliwa kwa ngao wa chakula na huenda wakienda na njaa. Ona jinsi wa mitume walivyoshulikia hadi hiyo. “ Hata siku zile wanafunzi walipokuwa wakiongezeka hesabu yao, palikuwa na manunguniko ya wayahudi wa kiyunani juu ya waebrania kwa sababu wajane wao walisahauliwa katika huduma ya kila siku. 2 Wale Thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, Haipendezi sisi kuliacha neo la Mungu na kuhudumu mezani. 3 Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili, 4 na sisi tutadumu katika kuomba na kulihudumia lile neno ”
Jibu kwa tatizo hili lilikuwa ni kubadili miundo ya shirika ya kanisa ya kwanza. Inaonekana kuwa mitume walihusika na kuhubiri na maombi na vile vile kukusanya na kugabua chakula kwa wajane na kwa wengine wenye mahitaji. Bila shaka walizidiwa kutumia kil akitu vizuri na hivyo walikuwa wamepewa na Mungu hekima ya kubadili miundo yao. Walikuwa na kanisa kwa jumla wakachagua watu saba wenye kujawa na Roho kwa kuangalia mgao wa chakula ya hawajiweze na wanaopungukiwa wakati wao waliendelea katika kuomba na huduma ya Neno. Tatizo hili katika kanisa la kwanza lilikuwa na uwezekano wa kulipasua kupitia misingi ya ujamaa lakini shida ilizuiwa sababu ya badiriko kwenye muundo wa shirika.
Ni ya muhimu kuwa na miundo mizuri ya shirika katika makanisa ya mahali ikiwa watafurahiya kukua kwa jumla na uthabiti. Ndiyo, tunahitaji kufundisha watu wetu kuwa na upendo saidi na utunzaji lakini hii haitoshi kamwe ; tunahitaji kubadili miundo yetu vile vile.
Acha niseme pia tunahitaji kuendelea kubadili miundo yetu kadiri kanisa lunavyo badirika. Yale ambayo pengine yalitumika vizuri miaka kumi iliyopita haiweze kufaa sasa. Hali zinabadirika na kanisa linajitaji kubadirika makusudi lipate kuendelea kukua.
3.4. Chagua watu wazuri
Mara moja unapokuwa na miundo mizuri mahali hapo unahitaji kuchagua watu wazuri kwa kuwajazia. Umuhimu wa kuchagua mtu mzuri kwa huduma ya namna yake haiweze kukazwa zaidi. Kanisa au kwa huduma itasimama au kuanguka juu ya nguvu ya kiongozi wake. Walakini, usipane cheo cha uongozi kwa mtu tu sababu anajitoa kwa hiari yake kufanya jambo ; hakikisha kuwa wanafaa.
Acha nivute uangalifu wenu kwenye vifungo vitatu vya Maandiko.
 Shauri la Yathro kwa Musa katika kutoka 18 : 21, “ Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu ”.
 Pendekezo la mtume kwenye kanisa la kwanza katika Matendo 6 :3, “ Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili ”.
 Mafunzo ya Paulo kwa Timotheo juu ya tabia za kiongozi wa kanisa katika 1Timotheo 3 :1-10, Ni neno la kuaminiwa ; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema. Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha ; si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu ; bali awe mpole ; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha ; mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu ; (yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kanisa la Mungu ?) Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya ibilisi. Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje ; ili asianguke katika lawama na mtego wa ibilisi. Vivyo hivyo mashemasi na wawe wastahivu ; si wenye kauli mbili, si watu wakutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu ; Wakiishika siri ya imani katika dhaùiri safi. Hawa pia na wajaribiwe kwanza ; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.
28
Muhtasari, tunaweza kusema kuwa watu ambao wanachaguliwa kwenye vyeo vya uongozi wanahitaji kuwa :
 Watu wa Roho wanao ogopa Mungu na wanaojawa na Roho Mtakatifu.
 Waliyo na tabia ya kimungu.
 Ni watu wenye uwezo waliyo na karama za Roho za kufaa.
 Kuwa ni sifa njema miongoni mwa watu ; pande zote ndani na inje ya kanisa.
 Kuwa na hekima upewayo na Mungu.
Acha tukague yaliyo juu kwa maelezo zaidi
Watu wa Roho wanao ogopa Mungu na wanaojawa na Roho Mtakatifu.
Haya yanaonekana kuwa wazi zaidi kwamba mmoja hangeihanza lakini, bahati mbaya, watu wamoja wanachaguliwa kwenye vyeo katika kanisa au katika shirika ambao hawaonekane kuwa na hali yoyote ile katika maisha yao ya kiroho. Mara nyingi zaidi watu wanachaguliwa kwa sababu wana uzoefu wakufaa katika mambo ya dunia lakini ambao hawafahamu mafundisho ya kiroho. Tunahitaji watu wanao amini kuwa uongozi ni zaidi ya kutumia ufundi uliothibitika kutoka mambo ya dunia; kuna kimo cha kiroho ambacho lazima kiwe kwanza katika mafikiri yetu. Nina amini kuwa neon la Mungu kwa Zerubabeli linatumiwa kwa wote wanaojishughulisha na huduma ya kanisa. Zekaria 4:6, Akajibu akaniambia, akisema, hili ndilo neon la BWANA kwa Zerubabeli, kusema, si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa Roho yangu, asema BWANA wa majeshi.
Viongozi wangekuwa watu wanao ogopa Mungu. Wanapashwa kuishi maisha yao wakijua kuwa siku moja watasimama mbele za Mungu na kupana hesabu ya kila kitu walicho kisema na kukifanya. Kitu kinacho nivutia zaidi kuliko kitu kingine kile ni ukweli wa Mthayo 25: 23 na mfano wa talanta, “Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.” Ninataka kusimama mbele za Mungu na kusikiya yeye akisema maneno yale, “Vema, mtumwa mwema na mwaminifu. Ulikuwa mwaminifu kwa yale niliyokuitia uyafanye” Si kwamba nifikiye yale Billy Graham alitimiza na sita hukumiwa kwa yale aliyoyafanya; kwangu la kufanya tu ni kufanya yale Mungu aliyo niitia kufanya. Tuna hitaji viongozi wanao ogopa Mungu na kuishi na thamani za milele katika moyo.
Waliyo na tabia ya kimungu
Ni yamuhimu viongozi kuwa na tabia ya kimungu. Yethro alishauri Musa kuchagua watu ambao walikuwa waaminifu na asiye tamani mapato ya aibu wakati Paulo alipana orodha ndefu ya nguvu ambazo kiongozi wa kanisa angeonyesha. Tabia ni yalazima sana. Ni ya muhimu kujua ni muda gani Paulo alioutoa kwa msimamo wa tabia ya mtu; kwa kifupi, alitumia muda mwingi zaidi juu yah ii kuliko anaofanya juu ya karama za mtu.
Kuna eneo tatu muhimu ambazo zinamfanya wachungaji kujikwaa na kuanguka. Katika kingereza tunaesabia kwao kama GGs; Gold, Girles and Glory, yaaani Dhahabu, wasichana na Utukufu. Nilitaja haya katika sura ya 1 tuliposema juu ya haja ya kukuza tabia yetu ya adili lakini acha ni yazungumziye tena.
 Dhahabu inatumiwa kwa matumizi mabaya ya uchumi. Ni yenye maana kuona wote wawili Yethro katika kutoka 18:21 na Paulo katika 1Timotheo 3:3 wanataja hii. Viongozi wawe “mtu mwaminifu asiyetamani mapato ya aibu; asiye mpenda fedha, na asiye kimbilia mapato ya aibu”. Una weza kuwa na upendo wa fedha hata ukiwa maskini. Moja ya faida za kutoa sehemu ya kumi na kuomba ina saidia kutoweka huru kutoka katika kuongozwa na fedha. Ikiwa tunapana asilimia kumi kwa Mungu kwa nia na kwa moyo kunjufu inaonyesha kuwa tunauongozi juu ya fedha kuliko hezo kuwa na uongozi juu yetu. Matumizi mabaya ya uchumi inaonekana kuwa tatizo zaidi kwa viongozi wa kanisa la Afrika kuliko ilivyo katika inchi za Magaribi.
29
Ni ya maana kuwa makanisa na mashika ya kikristo zinasimamisha taratibu zinazo hakikisha kuwa matumizi yao ya fedha inashinda shutumu. Ni juu ya hiyo nilizungumzia awali jinsi gani nilivyo anza huduma yangu.
 Wasichana ni uasherati; kwa kawaida pamoja na jinsia tofauti ijapokuwa hivi karibuni kuna wakati unatendeka kwa watu wa jinsia moja. Huduma nyingi kubwa zimeisha angamia na dhambi ya uzinifu. Kadiri nionavyo haya yanapiga for a katika inchi za Magaribi kuliko katika Afrika lakini wenzi wangu wamoja wa Afrika wanaamini kuwa ni pia tatizo katika bara lao.
 Utukufu unatumiwa kwa wachungaji na viongozi wa makanisa ambao wanajisifu juu ya huduma zao, wakitenda kama ikiwa yote yanayofikiwa ni sababu ya jinsi walivyo wakuu. Wanasahau kuwa kila kitu tunachofikia kinatoka kwa Mungu.
Achat nitaje pia kwa uchungu juu hii ni dhambi ingine ambayo inafanya wachungaji kuwa wasiyofaa. Ona waebrania 12:15, Mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisiye likachipuka na kuwasumbua, na watu wengi wakatiwe unajisi kwa hilo. Wachungaji na wake zao ni sababu kwa neon ‘mzizi mchungu’ wakunasa na kuwaharibu. Iweni kwenye zamu yenu watu wanapo walaumu bila sababu; sameha, samehe na bila sababu katika sura inayofuata).
Upungufu katika eneo la tabia au sifa itaumiza zaidi kuliko kitu kingine kile. Ni juu ya hiyo tunahitaji viongozi wanao muogopa Mungu.
Watu hodari pamoja na karama za kiroho zinazafaa
Viongozi wanahitajika kuwa watu hodari; wanapaswa kuwa na uwezo wa kuongoza kazi ambayo walikabiziwa. Lazima wawe watu ambao wanaweza kugeuza maono kuwa ukweli. Kuna umuhimu mdogo katika kumuweka mtu kwenye cheo cha uongozi ikiwa ni wasiofaaaa; haidhuru kwa jinsi wanaweza kuwa wacha Mungu.
Acha niulize ulizo, ‘jinsi gani tunbajua kuwa mtu atathibitisha kuwa hodari?” jibu langu ni, “tuna angalia kwa yale waliyo yafanya wakati uliopita, juu alama nzuri zaidi ya wakati ujao ni mwenendo wao uliopita”. Je, waliongoza vizuri kazi walizozipewa awali? Ikiwa ndiyo, basi kuna uwezekano wakuongoza usimamizi unaoambatana na cheo inayofuata vizuri. Yesu alisema kitu kimoja sawa na hicho katika mfano wa wakili asiye na haki: “Aliye mwaminifu katika lililo dogo sana, huwa mwaminifu katika lililo kubwa pia; na aliye dhalimu katika lililo dogo, huwa dhalimu katika lililo kubwa pia”. (Luka 16:10)
Acha ni changia nanyi yale ninayoyaishi. Mungu aliponiita kwenye huduma ya uchungaji ya muda wote nilikuwa msimamizi kwa huduma ya kuongoza kundi la vijana kanisani wenye umri wa miaka 9 hadi 12. Kundi langu lilikuwemo wato wazima 13 na tulikuwa na karibuni vijana 70-80 waliokuwa wakishiriki ibada la jioni. Pamoja na hayo, pia nilikuwa nikufundisha somo la Juma Pili. Tulipokuwa tukiagana na kanisa la Canada, ambako tuliishi miaka mitano na walikuwa wakienda ulaya kwenye chuo cha Biblia muda wa miezi 6, mchungaji alisema kitu kimoja ambacho sitakisahau kamwe. Alihimiza imani yao kuwa tuliitwa kwenye huduma na kwamba tuna karama zinazotosha na uwezo wa kufaulu sababu tulionyesha haya kwa vile tulivyotumika ndani ya kanisa.
Kadhalika aliendelea kusema kwamba aliwai kuona wanafunzi wengi katika ma semina waliotaka kuwa wasemaji mashuhuri katika baraza na kuchunga ma kanisa ma kubwa lakini ambao hawakufundisha darasa la juma pili wala kujishughulisha katika maisha ya siku kwa siku ya kanisa lao la mahali katika njia yoyote ile. Watu hawa wana mipangilio mikubwa lakini maisha yao ya zamani haikuonyesha kuwa walikuwa na uwezo wa kufaulu kwenye cheo hiki ; kwa kifupi, tabia zao za zamani zilionyesha kuwa wote walikuwa wakisema na bila kutenda. Waliyo hitaji kufanya ilikuwa ni kurudi kwenye tabia za msingi na kuonyesha kuwa walikuwa hodari kwenye cheo hicho cha chini na basi, wanapo jithibitisha wenyewe pale, wanachukua cheo cha uongozi kinacho fuata. Walipo faulu kwenye ngaji hiyo ndipo walikuwa tayari kwa ile inayofuata.
Singetuma mtu kuanzisha kanisa au kuchunga liloko hadi pale wangelionyesha kuwa walikuwa na nguvu kwa kuongoza huduma katika kanisa la mahali. Niliona watu wengi pia wanashindwa
30
sababu walitumwa nje mapema sana bila hata alama ya uthibitisho nyuma yao. Inawezekana walijua vitu vizuri vya kusema na wanaweza kuwa na sauti ya kusadikisha lakini hawakuonyesha kuwa walikuwa na uwezo wa kuongoza huduma ya kundi.
Iweni waangalifu na watu wanaotaka cheo mashuhuri katika kanisa lakini ambao hawakubali kuanza kutumikia kwenye cheo cha chini. Nilikutana na watu wengi ambao wana uhakuka ya kwamba Mungu aliwaita kuwa na huduma inayo enea popote lakini wasiotaka wala hawaweze kuonoza huduma katika kanisa.
Kuwa na ushuhuda mzuri miongoni mwa watu ndani na nje ya kanisa
Katika 1 timotheo 3 :7 tunasoma kuwa kiongozi wa kanisa “ imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje”. Imempasa kuwa mtu anayeheshimiwa na watu kama wakiwa ndani au nje ya kanisa mara nyungi Paulo anataja haya na ni yakupendeza. Kwa mfano, katika shairi la 2 tunasoma kuwa msimamizi / mchungaji imempasa kuwa ‘mwenye kiasi na busara’ na katika shairi la 4 kwamba watoto wake watamuheshimu nje katika ustahivu. Vivyo hivyo mashemasi na wawe ‘wastahivu wa heshima’ (shairi la 8) na vivyo wanawake na wawe ‘wastahivu wa heshima’ (shairi la 11). Kuwa mstahivu wa heshima ni kitu ambacho kingetambulisha kila kiongozi ndani ya kanisa.
Tunapo weka watu kwenye vyeo vya uhongozi tunahitaji kuuliza maulizo, ‘je, hawa watu wana ushuhuda nzuri miongoni mwa watu ndani na nje ya kanisa ? Watu hawa ni wastahivu wa heshima ? ” Hii ni ya maana, kwani ikiwa si wastahivu, wanaweza kuongoza kanisa katika ugomvi. Lakini ni zaidi ya hayo ; watu hawatafuata kiongozi wasio mpenda ; ni kama vivi hivi kama hayo.
Jinsi mtu anavyoonekana katika mahali pake pa kazi ni ya muhimu sana na inatuambia kazi kubwa juu ya mtu. Je, wana ushuhuda kwa kuwa wavivu au kuwa watumishi wema ? Wanajulikana kama mtu aliye mwanamemba nzuri wa kundi na mwepesi kutumika pamoja na au ni watu ambao watu lazima wawe waangalifu juu yao sababu wanapatwa na hasira haraka sana ? Katika maneno mengine, “ je, wana ushuhuda nzuri kwenye kazi ; je watu wanawaheshimu ? Ninajua kuwa dhehebu zimoja za magaribi, kwanza wanakubali mtu kufundishwa kama mchungaji, kwa kawaida wanapata kumbukumbu kutoka kwa mtu ambaye alitumika naye kwa kuhakikisha ikiwa alikuwa na “ ushuhuda mzuri na watu wa nje ”. huu ni ushawishi wenye busara sana na unaweza kuokoa kanisa kwenye wingi wa maumivu ya moyo katika siku zijazo. Kumbuka, alama nzuri zaidi ya kazi kwa wakati ujao ni mwenendo wao uliopita.
Nilikuwa ninashirikiana na chuo cha Biblia pa Ujeremani siku nyingi, mwanzo kama mwanafunzi na baadaye kama mwalimu na nilikuwa na heshima nyingi kwa mwanaume aliyekuwa msimamizi kwa wakati ule. Ninaweza kukumbuka nilikuwa na mazungumuzo naye juu ya mwanafunzi aliyefikiri kuwa aliitwa kuwa mchungaji wa ujana kwa muda wote katika inchi yake ya asili. Msimamizi alitambua kwamba unajifunza zaidi juu ya mtu kwa kuchunguza taratibu jinsi wanavyotumika kazi zao ipasavyo kuliko unavyofanya kwa yale wanayosema ndani ya chumba cha mwalimu. Kwa kuchunguza mtu taratibu kadiri wa navyotumika unaweza kuhakikisha ikiwa ni waaminifu, wanatumika vizuri na wengine, ana uwezekano wa kuwa kiongozi, anazuia mzozo vizuri na majaribu mengine ambayo ni ya muhimu kwa kuthibitisha ikiwa mtu ana ‘stahili hesshime’ na ikiwa wanaonyesha tabia za uongozi.
Kuwa na hekima unayopewa na Mungu
Bublia inatuambia kwamba hekima unayopewa na Mungu nit oleo muhimu ikiwa tutakuwa viongozi wakuu. Kwa mfano:
 Yosefu alipewa hekima na hii ilikuwa moja ya mambo ambayo ilimuwezesha kuwa mtawala juu ya Misri. (ona Matendo 6:10)
 Luka anatuambia kwamba Yesu alikua katika hekima kama mtoto. Ona Luka 2:52. Alipoanza huduma yake watu kutoka mzi wao wa asili walishangaa na hekima yake na kustaajabu jinsi alivyoipokea. Ona Mathayo 13:54
31
 Hekima ilikuwa inatakiwa kwa wale ambao walichaguliwa kuhudumu mezani katika Matendo 6:3
Yale yaliyokuwa yakitumiwa nyakati za biblia ni nzuri pia kwa leo ninayoyaishi yanaonyesha kuwa wachungaji wamoja wanafanya maamuzi ya upumbavu ambayo inatokea kwenye matokeo mabaya; kitu ambacho kingeepukwa ikiwa tu wangekuwa na busara dogo. Yakobo anatuambia kwamba ikiwa tunakosa hekima tungeomba Mungu na atatupatia nayo. Ona Yakobo 1:5, Lakini mtu wa kwenu akipungukiwa na hekima, na aombe dua kwa Mungu, awapaye wote, kwa ukarimu, kwala hakemei; naye atapewa.
3.5. Usiweke watu ‘Ndiyo’
‘Mtu ndiyo’ ni mtu ambaye kwa kawaida anakubali yale kiongozi anayoyasema na anayotumika na kamwe haseme kitu chochote kilicho tofauti na kile kiongozi anachotoka kusikia. Hii haifae kwa yeyote ule; pamoja na kiongozi. Acha nifanye maelezo juu ya hii
 Ya kwanza ni kwamba unataka watu ambao wanajitolea kwenye Theology, maono na philosophy ya kanisa. Kwa mfano. Ikiwa unafikiri kuwa karama zote za Roho zinapatikana leo, hautake mtu kwenye kundi lako la uhongozi ambaye anasiki kuwa wote walikuwa wameondoka wamitume walipokufa na kuwa kanisa halingetarajia yeyote wao kuwa ikitumika leo. Mbali na hayo, ikiwa unaamini kuwa kanisa linge onyesha ukweli wakati usiyofaa wa Injili katika namna ya wakati ule ule, pamoja na mziki na maabudu ya wakati ule ule, basi hautake mtu ambaye anajitolea vipasavyo kwenye taratibu za asili ya maisha ya kanisa na maabudu. Ikiwa watu hawa wapo kwenye kundi la uongozi na kushika kwa nguvu sana kwenye nia zao na kutaka kuakikisha kuwa mawazo yao yamesamanika, halafu utakuwa na mzozo wa bure na inawezekana wataishi kadogo katika njia ya kukua kanisa.
 Walakini, unapotaka watu ambao wanajitolea kwenye theology, maono na philosophy ya kanisa, unataka wao kujisikia huru kwa kutoa maelezo yanayofaa kwa kujenga. Kwa mfano, “Mchungaji, si fikiri kuwa wazo hili ni njia nzuri zaidi kwa kutimiza maono yetu sababu ya XYZ” au “Mchungaji, nina masharti juu ya yale tunayotumika sababu watu wamoja wanaweza kuitafsiri kwa kumaanisha kuwa tunatumia vibaya pesa za kanisa. Ningependa kupendekeza kuwa tunafanya kitu kama ABC” kwa tumaini, mazungumzo yanayofaa katika hewa ya upendo ingefuata kwa kuruhusu uamuzi unaofaa zaidi kufanyika.
Hautake mahali ambako viongozi wanaojitolea kwenye timu lenu haujisikie raha kusema kuwa hawakubaliane na kitu munacho kusudia. Nilijua wachungaji ambao walibuni mahali ambako yeyote anayesema kitu tofauti kwa yale wanayopendekeza inaonekana kama kuwa si mwaminifu kwenye maono ya kanisa. Baadaye tutazungumzia hitaji kwa kiongozi kusikiliza shauri na kulikagua lakini watu kwenye kundi watatoa tu maelezo ya kujenga ikiwa wanajisikia kiongozi ni wazi kwa kupokea mapendekezo yao bila kuwafanya kujisikia kuwa si waaminifu.
Tony Blair aliandika, “Nilipenda…(yaani wamoja wa ‘watu’ wakimzunguuka)… kabisa sababu ninajua wangeniambia yale waliyofikiri. Hiyo siyo kusema walikuwa wasiyotii… lakini walisema yanayotoka moyoni niliyapokea, na yalivuta shauri linalosaidia na hata matumaini kutokana na hiyo”9
3.6 kanuni za juu kwa wale wenye daraka kubwa
Tuna hitaji kutambua kuwa eneo la usimamizi tunnalomupa mtu, kanunu ya juu ambayo tunaahamurisha kwao. Tunahamurisha mbali zaidi kutoka mchungaji katika mipaka ya wema na nguvu kuliko tunayofanya kutoka parking msaaiidizi kwa gari. Tuna hitaaji zaidi sana kutoka kwa kiongozi wa dhehebu kuliko yale tunayoyafanya kwa mtu anayeongoza kundi dogo la kundi la nyumbani. Kadiri ukubwa wa eneo la usimamizi ulivyo ndivyo zaidi mtu angefanya na kristo katika daraaka zaa huduma tunahitaaji kufahamu haya.
9 Blair, A Journey, 114
32
Walakini, tusingelingoja mkristo kukuza uzima wa kiroho mwingi kabla ya kuwashirikisyha katika maissha ya kanisa. Haapo inabidi kuwa kimoja kwao cha kufaanya katika huduma za watoto au timu ya ukaribishaji au timu ya maabudu wala timu ya matumizi ya jumla karibu ya kutoka kwao.
Walakini, tunapokuwa tukitaafuta mtu wa kuongoza moja ya timu hizi zza huduma ingetupasa kuchagua mtu aliye na kiasi kikuu cha tabia ya umungu kuliko tunavyotarajia kwenye wanamemba wa timu mojawapo. Kadhalika, tunapochagua mtu kuwa mchungaji tunatarajia hata kiasi cha juu cha maisha ya kiroho pamoja na tabia nzuri inayofaa kuliko tunayofanya kwa wengine ndani ya kanisa.
Nina amini kwamba kadiri kiasi cha ukuu wa usimamizi ambao tunampa mtu ndani ya kanisa au dhehebu, kadiri tabia ya juu ambayo tunahitaji kwao na jinsi kiasi kikuu cha maongozi tungefanya juu yao ikiwa ni kwa niaba yao isiyofaa. Ingetupasa kukubali wakristo wapya mahali walipo na kuwashirikisha katika maisha ya kanisa, ni kwa ajili ya hiyo Mungu anatukubali, uhodari na uongozi kama watu wanavyochukua daraka za uongozi.
3.7. Msiwape watu usimamizi mwingi mno haraka zaidi
Paulo anatupatia shauri nzuri katika 1Timotheo 3:6 kuhusu mchungaji na viongozi kwa jumla. Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi. Fundisho hili linaelekea kwenye kila eneo la uongozi. Wakati tungeshirikisha wakristo wapya katika huduma ya kanisa karibu ya kuokoka kwao lazima tuwe waangalifu tusiwape usimamizi mwingi mno haraka zaidi. Wanahitaji kupata kiwango fulanicha maisha ya kiroho kabla ya kuweza kuongoza cheo cha uongozi na kushughulikia matatizo yanayojitokeza. Kadiri kiwango kikuu cha usimamizi kilivyo ndivyo kadiri kiwango kikuu cha ukamilifu kinahitajika.
Namna ile inatumiwa kwa watu toka makanisa mengine, zaidi sana wale toka ndani ya eneo lenu. Iweni waangalifu. Kwa nini wanaacha kanisa na kuja kwenu? Pengine walikuwa wakitendewa vibaya katika kanisa linguine na itakuwa faida kwako lakini pengine wapo watafutao faida zao binafsi ambao wanaozusha matatizo kote waendako. Chukua mda wa kukagua. Watu chupavu watafurahia mahitaji yako kwa kukagua na watakueshimu hiyo, jihadae katika njia inayofaa.
3.8. Wakilisha huduma na upane mamlaka yanayofaa.
Sasa kwamba Musa alikuwa na muundu nzuri na watu wazuri kwa kujazia daraka mbalimbali, ilimubidi kuwakilisha huduma kwao na kuwapa mamlaka yanayostahili kwa kuendesha huduma hiyo. Hii ni karibuni na sehemu ya shauri ambalo Yethro alimupa Musa na moja ambayo wachungaji wamoja kuwa nguvu zaidi kuyaweka katika matendo kumbuka shauri la Yethro, zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia, na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi; 22 nao wawaamue watu hawa siku zote; kasha, kila neon lililo kubwa watakuletea wewe, lakini kila neon dogo wataliamua wenyewe.
Shairi zinazofuata zinaonyesha kuwa Musa alifuata maagizo ya Yethro na aliwakilisha huduma kwa watu aliyowachagua. Pamoja na usimamizi wakuhukumu aliwapa pia mamlaka ya kuchukua maamuzi wao wenyewe; hawange weza kuzungumza kila uamuzi naye na kutazamia ukubalifu wake mbele ya kuendelea. Kufanya yanayofuata ingefanya hali kuwa mbaya zaidi kwa wote waliohusika. Musa alikuwa akiwakilisha mamlaka yakufaa kwa wale ambao aliwapa usimamizi. Musa aliendelea kujishughulisha na mambo magumu na alikuwa na usimamizi mwingi, lakini mambo madogo aliachia ‘timu lake’.
Fikiri juu ya hali yako. Ni katika sehemu gani unahitaji kuwakilisha mamlaka? Ni katika utunzaji wa wachungaji, uongozi wa maabudu, huduma za ujana wala usimamizi? Muna jaribu kuweka kando jumaa ya kujifunza biblia na kuendelesha kikao cha maombi makusudi mupate kushikilia uzuifu kwa yale yanayofundishwa wakati unapoweza kuwa na muundo wa chembechembe ya nyumbani pamoja na wengine kuongoza makundi mbalimbali?
33
Nilikuwa nikiuliza ulizo, “Nini kinachotokea ikiwa munapatikana katika kanisa ndogo ambamo watu ni maskini na hawana uzoefu wa uongozi katika shughuli za dunia? Ikiwa hauna watu waliyotangulia kuwa na ujuzi wa uongozi itakuwa je? Shauri langu ilikuwa ni kuanza na kitu kilicho kidogo. Pengine ikiwa unaongoza kikao cha maombi kila jumaa unaweza kuwakilisha maabudu ya kufungua kwa mtu mmoja. Kutana na mtu huyo na kumuambia yale yanayohitajika, labda nyimbo tatu pamoja na maombi ya kufungua na utangulizi. Unamuambia jinsi ya kuchagua nyimbo lakini sema naye kabla ya kikao kwa kuakikisha kuwa anafaa. Baada ya kikao utakuwa pamoja naye kwa kuzungumzia yale aliyoyafanya. Umuambie aliyoyafanya vizuri nay ale angerekebisha na jinsi ya kurekebisha. Ni muhimu kuambia mtu aliyoyafanya vizuri sababu mtu haweze kujua kuwa yale aliyoyafanya yalikuwa zuri; anaweza kuifanya kwa bahati au hakukuwa na uhakika ikiwa alikuwa akifanya kitu kizuri.
Mtu anapo onyesha kuwa anaweza kufanya kazi zuri kwa maabudu ya kufungua sasa wakilisha mamlaka mengi kwao. Endelea hivyo hadi pale utakapo akikisha kwamba unaweza kugabizi usimamizi zaidi kwake wa kikao cha maombi kwa jumla.
3.9. Ambia watu yanayohitajika kwao; maelezo ya kazi
Tunapo wakilisha huduma tunahitaji kuambia watu yanayohitajika kwao. Ona kutoka 18:24-26, Basi Musa akasikiza neon la mkwewe, akayefanya yote aliyokuwa amemwambia. 25 Musa akawachagua watu wenye uwezo katika Israeli yote, akawaweka wawe vichwa juu ya watu, wakuu wa maelfu, na wakuu wa mia na wakuu wa hamsini, na wakuu wa kumi. 26 Nao wakawaamua watu siku zote; mashauri magumu wakamletea Musa, lakini kila neon dogo wakaliamua wenyewe. Viongozi waliambiwa yale yaliyokuwa yamehitajika; wangetendea kazi maneno mepesi bali yale yaliyo magumu hatimaye yachukueni kwa Musa ayatendee kazi. Hatuambiwe maagizo yote ambayo Musa aliwapa viongozi lakini moja inahakikisha kuwa ndani muna wazo moja la kuwa lini kiongozi wa 10 angetuma neon gumu kwa kiongozi wake wa 50.
Kumbuka pia kutoka 18:20, Nawe utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kuifanya. Hapa tunasoma kuwa Musa hakufundisha watu amri za Mungu tu lakini aliwaonyesha jinsi ya kuendesha kazi ambayo inawapasa kuifanya. Watu waliyochaguliwa kama viongozi hawakujua tu yale watakayoyafanya lakini walionyeshwa vile vile jinsi ya kuyafanya. Tutazungumza juu ya umuhimu wa kufundisha viongozi vyetu baadaya lakini hapa nina taka kutilia mkazo hitaji la kuambia watu yale watakayoyafanya na yanayohitajika kwao. Inawapasa kujua mamlaka gani wanayo na maamuzi gani wanayoweza kuyafanya bila kuyafikisha kwa wakuu wao. Ninayoyaisha katika shughuli za dunia yanaonyesha kama watu katika ngazi mbalimbali za usimamizi wana vyeo tofauti vya mamlaka. Tutazungumza juu ya jambo hili vizuri zaidi baadaye tutakapo sema juu ya kuchukua maamuzi ndani ya mipaka mingi mno.
Acha turudi nyuma kwenye wazo la kuwaambia watu yale inayohitajika kwao. Acha tukubali kama mulipangilia kufanya muundo wa chembechembe ya nyumbani kuliko kuchanganya maombi ya kila jumaa na mafundisho ya biblia. Wale wanao changuliwa kuongoza kundi ingewapasa kupewa taarifa kuhusu yale yanayotarajiwa kwao. Kwa mfano,
 Je, hapo kuna wakati moja wa kuanza na kumaliza au kila kundi linaruhusiwa kuchugua wakati na siku inayo wapendeza?
 Je, hapo kuna kanuni zinazoandikwa ambazo zitafuatwa au wapo huru kabisa kukubali mambo?
 Je, inawabidi kuzungumza juu ya jambo moja kila kikao au wapo huru kuzungumza chochote wanachotoka?
 Kuna kitu kingine kinachotarajiwa kwao? Inawabidi kutayarisha utunzaji wa mchungaji kwa kila mwanamemba? Je, inawabidi kutii kila ripoti ua yaliyotokea kila jumaa?
Huduma inaonekana zaidi kuendeka kwa amani wakati watu wanajua yale yanayotarajiwa kwao.
34
3.10. Wapeni viongozi wenu uhuru wa kutoa maamuzi ndani ya mipaka mingi mno munayoyaweka.
Unapo wakilisha kazi unahitaji kumpa mtu mamlaka ya kuchukua maamuzi ndani ya mipaka mingi ambayo muliyoiweka. Inawapasa kuchunga usimamizi mwingi wa kazi kwa kuakikisha kama vitu vinafanyika kulingana na maono yako na philosophia lakini inakubidi kuwezesha watu kuchukua maamuzi ingawa ikiwa siyo njia kamilifu ambayo mungeifanya.
Ikiwa unawapa watu usimimizi lakini hauwapi mamlaka yanayofaa kwa kutoa maamuzi ndani ya mipaka mingi, vitu vitakuwa visivyovumilika kwa wale walio chini yako. Mvutano utakuwa mwingi na labda wataacha na kwenda penginepo.
Kumbuka historia lifuatalo. Mtu moja alichangia nami jinsi alivyokuwa amezuiwa pamoja na kuzuia utawala ambao mmoja wa wachungaji wanaoshirikiana wa kanisa alilokuwa akishiriki aliyotumia juu ya kila kitu. Alieleza namna alivyokuwa ikiweka kanisa la maabudu ya asubui na alikuwa ameweka kila kitu katika mahali pake, mchungaji alipokuja kwake na kumuambia kuwa meza ndogo kwenye jukwaa ilikuwa mahali pabaya. Ndipo kiongozi alizogeza meza karibuni 30cm upande wa kuume, aliangalia kwenye meza na akasema, “Hapana, inahitaji kurudi karibuni 15cm”. Tena alisogeza meza, aliangalia tena na kusema, “Sivizuri kabisa, inahitaji kuwa hapa”. Tena aliisogeza mahali pake pa asili. Kwa kadiri ionekanavyo, hii ilikuwa mfano mmoja na kila kitu aombacho alifanya. Ninaamini amuta shangaa kupata habari ya kama hawa watu wawili waliishiwa hatimaye walitoka na kwenda katika kanisa lingine katika mahali.
Mfano huo hapo juu ni mkuu sababu unaonyesha kuwa tatizo la kuwakilisha mamlaka lilikuwa na machache yakufanya kwa pale meza ilikuwa inatiliwa; ilikuwa kila kitu, hata ikiwa ilibidi kurudisha meza pale ilipoanzia.
Ni nini ambacho kingefanyika? Nina amini mchungaji angekutana pamoja na kamati lake la uongozi lililo anza kazi, na pengine pamoja na wanamemba wa kundi ikiwa inafaa, na pamoja kuamua jinsi nyumba ingepangwa kwa ajili ya huduma ya maabudu. (Katika hali hii, ninaamini kama nyumba ilitumiwa kwa vitu vingine katika wiki, kwa hiyo, ilibidi kila kitu kifungwe na kuwekwa kando baada ya kila huduma na kasha kupangwa tena juma pili ijayo). Angeamua upande gani watu wangekaa na vitu vingepangwa namna gani; nusu mviringo kwa upande mmoja wa marefu ya kanisa kwa jinsi ya kushuka katikati au misafa mitatu ambayo ina viti mnane pana kwa mbili upande mmoja wa marefu ya kanisa au vyote vile vilivyo faa kwa jengo. Wangeamua pia jinsi wanavyotaka eneo zingine kupangwa. Ninaamini kwamba mchungaji angekuja kwenye shauri na wazo katika akili lakini angehusisha pia timu lililo anza kazi kwenye maamuzi ya mwisho.Kufanya kiongozi wa kundu na kundi lake kushiriki katika hatua ya kuchukua uamuzi ingewasaidia kujisikia kuwa walikuwa sehemu ya huduma; kuliko mzuzu katika mchezo wa sataranji.
Mchungaji angefanya hayo hapo juu angetoka ndani ya kundi, na mtu ambaye alichagua kuwa kiongozi, kupanga jengo kila wiki na hapana kukatiza. Nina amini haikuzuru kitu hata kidogo ikiwa meza ilikuwa 30cm upande moja. Ikiwa mchungaji alifikiri kuwa kiongozi aliyesimikwa alikuwa akifanya kitu kibaya ambacho kinahitaji kurekebisha angesema na kiongozi peke yake kuliko kumusahisha hadharani ya watu.
Mtu mwengine aliniambia tukio lingine kama na hilo baada ya mwezi moja niliposikia hayo yaliyo juu. Walichangia jinsi walivyo hamia katika eneo jipya na wakaanza kushiriki kanisa ambalo lilikuwa na agizo mpya kabisa na mchungaji aliye muelekevu sana. Labda mtu huyu alikuwa ni kiongozi mkuu wa maabudu akiwa vilevile muhubiri mzuri na mchungaji muangalifu. Kama tokeo la hili, kanisa lilianza kuvuta watu wapya na idadi iliongezeka kadiri ilivyofikia huwa pana zaidi kuliko hesabu ya kitaifa. Walakini, hakuwa kiongozi mzuri na kusisitiza kila kitu kifanyike vizuri kadiri apandavyo. Alikuwa pia mtimilifu na hakuna aliyeweza kufanya kazi yoyote kwenye cheo chake kikuu. Labda, baada ya viti kupangwa kwa ibada la asubuhi angekuja pamoja na kupanga kila upya na kukaza viti tena kwa sababu havikuwa katika matakwa yake.
35
Hali ilifikia kuwa mbaya kabisa kadiri timu lililochaguliwa liliweka viti mapinda kwa makusudi tu ya kumusumbua. Niliambiwa kuwa tangu hapo kanisa lilipungua karibuni watu 20 na anafanya jitiada za kuendelea kuwa kiongozi. Ikiwa huyu mwanauma mwelekevu alikubali kuwapa watu mamlaka ya kuchukua maamuzi bila kuwa amesimamiya kila kitu, nina uhakika kanisa lingeendelea kukua taratibu.
Sitashughulika na jambo hili sasa lakini ni ya muhimu kukumbuka ku: “sifu hazarani bali toa makosa faragani”. Katika 1 Wathesalonika 5:11, Paulo anatuambia, Basi? Farijianeni na kujengana kila mtu na mwenzake vile vile kama mnavyofanya. Kwa mfano, ikiwa kuna mtu aliyetumika kazi nzito kwa kuandaa tukio fulani basi uwasifu hazarani kwa wakati unayofaa au ikiwa kundi la watu lilitumika kazi nzito kwa kutayarisha jengo kwa kazi maalum ndipo uwe hakika umewasifu hazarani. Tumia hekima na usifanye hii mno, juu haupendi kuifanya itokee kuwa mzaa, lakini, kwa jumla, ni vizuri kusifu hazarani. Walakini, usitoe makosa ya mtu au ya kundi la watu hazarani sababu hayo inawafedhehesha na hii sio vema kamwe. Wazo la kutoa makosa ni kusaidia mtu kufanya kazi nzuri zaidi au kuwa mtu zuri na hii ni tendo bora faragani na sio kwa kuzaraulika hazarani.
3.11 Weka mipaka
Nilitaja juu kwamba unapo wakilisha kazi unahitajika kupea mtu mamlaka ya kuchukua maamuzi katika mipaka kazaa ambayo uliyoweka. Acha sasa tuzungumzie jambo la kuweka mipaka kazaa. Mipaka hii inawekwa kwa sehemu nyingi lakini niruhusu kutaja tano tu.
 Maelezo ya kazi ya kila mtu. Hii ina saidia kudhihirisha yale mtu anayokusudiwa kufanya. Ina saidia kudhihirisha kazi zao na eneo za mamlaka.
 Taarifa ya Imani. Makanisa mengi yana Taarifa ya Imani inayoandikwa na inaimiza mwenendo katika njia nyingi. Kwa mfano, kanisa ambalo linaamini tu katika kubatiza waamini halitakubali kiongozi wa kundi la nyumbani kuongoza huduma ya ubatizo wa moto; kwa rafiki ambaye angali anazaliwa wakati wa kusanyiko lao la nyumbani. Vile vile, makanisa yanayo amini kwamba zawadi za Roho zimeenda zake hawaweze kukubali watu kusema kwa lugha wanapo kusanyika katika kundi la nyumbani. Kujua nini taarifa ya imani inasaidia watu kufanya katika mipaka kazaa inayokubalika.
 Thamani za kanisa na philosophia. Mara kwa mara haya ni ya sio andikwa lakini ni ya muhimu sana. Acha tuangalie kwenye dhambi kama mfano.
 Makanisa mamoja yanajua kuwa dhambi ni mbaya lakini wanachagua kutofundisha juu ya dhambi wanataka kuzingatia kwenye wema wa Mungu na hawatake kuchukiza wasioamini wanaotafuta ukweli.
 Wengine, kama vile mimi mwenyewe, wanafundisha kwamba dhambi ni mbaya na niharibifu lakini wanataka kuzingatia kwenye wema na uwezo wa Mungu kwa kutubadirisha. Wangesema kuwa kuendelea kuvuta uangalifu wa watu kwenye dhambi hakutoe mabadiriko lakini kunatufanya kutaka kutenda dhambi zaidi. Ona warumi 7. Tunayo hitaji kufanya ni kuanza kuambia watu watubu dhambi lakini ndipo waende kuzingatia kwenye kazi ya kubadirika ndani ya Roho Mtakatifu na neema ya Mungu; kitu ambacho kinaongoza kwenye ‘wingi wa maisha’ (Yohana 10:10)
 Kuna wengine wanaamini kuwa tokea dhambi kuwa aibu kwa kila mtu (Mit 14:34) kanisa lingejiona lenyewe kama likihubiri juu ya dhambi za taifa makusudi watu wapate kuepukana na hukumu ya Mungu.
Ikiwa ulishikilia kwenye mtazamo ninao ufanya, haungetoka kiongozi wa kundi la nyumbani kuwa mtu anayeona kuwa kusudi zao ni kuendelea kuhubiri juu ya dhambi za shirika letu. Hii ingekuwa kinyume ya ufahamu wako kibiblia toka warumi na tofauti na vile unaamini watu wanabadirika. Kwa upande mwengine, ikiwa uliamini yale ninayoyafanya, hali ya pili, haungetaka viongozi wenu wa makundi ya nyumbani kuendelea kupuuza dhambi na kutosema juu ya dhambi.
36
Zaidi watu wanavyo fahamu thamani na philosophia ya kanisa, zaidi watafahamu mipaka unayotaka kuweka. Haya yanapotokea unaweza kuwapa uhuru zaidi na zaidi kuchukua maamuzi wakijua kuwa watakuwa kwenye mstari pamoja na mwelekeo ambao kanisa linachukua.
 Makusudi na Maono. Ninaiona inafaa kukuza makusudi na shabaa kwa mwaka; yote mbili kwa kanisa kwa jumla na kwa kila shirika ndani ya kanisa. Viongozi wanapojua makusudi haya na maono inawasaidia kwa kuchukua maamuzi katika mipaka kazaa ambayo uliyoiweka. Kwa mfano, acha tukubali kuwa uliweka kusudi la kujenga kanisa kubwa kwa kukaribisha watu wa zaidi wa nao kusanyika sasa. Ikiwa viongozi wenu wanajua haya, ni rahisi kwao kuanzisha mwelekeo huu kwa yale wanayoyafanya kuliko kudai kuwa kanisa halingekuwa na jengo lake pekee lakini wanakusanyika ma nyumbani.
Acha nipotoke kwa muda na kusema juu ya yale tungefanya ikiwa wewe, kama mchungaji, unasikia mmoja wa viongozi wako wa kundi la nyumbani akifundisha kuwa kanisa halingenunua kiwandja na kujenga sababu Agano Jipya inafundisha kwamba kanisa ilikuwa ikikusanyika manyumbani tu na hawakumiliki majengo. Wakati wa safari yangu moja Afrika nilikuwa nikiuliza huliza hili kila mara. Mmoja wa wachungaji alijibu, ‘Ningemuambia anione mimi na kuuliza yale anayoomba radhi na kubadili yale alikuwa akifanya au ningemutenga’’.
Kuna kazi kubwa ya haki kati yale mchungaji aliyoyasema lakini singeenda kwa haraka ndani na kumutisha pamoja na kumutenga na kumutoa inje. Kumbuka kwamba mchungaji alisema kuwa mchungaji wa kundi la nyumbani angemuona faragani. Hii ni vizuri; kumbuka msemwa, ‘’kusifu hazarani, toa makosa faragani’’. Mbali zaidi, ikiwa kiongozi wa kundi la nyumbani aliamua kufundisha kuwa kanisa halingesimamisha jengo mpya bali wakikusanyika tu manyumbani, na anajua kwamba hii ilikuwa tofauti kwenye makusudi na maono ya kanisa, ndipo ningemukalisha chini kutoka kwenye cheo cha kiongozi wa kundi la nyumbani. Amuweze kuwa na kiongozi anayedai kwa makusudi kitu ambacho ni kinyume kabisa kwenye makusudi na maono ya kanisa.
Walakini, singekuwa haraka pia kwa kumuondoa kwenye daraka lake. Kuna vitu vichache ambavyo ningejaribu kugundua ninapo kutana naye faragani. Kwa mfano:
 Ningejaribu kuona kabisa ikiwa yale niliyo yasikia yalikuwa ya kweli. Matetezi mara kwa mara yanaweza kuwa si kweli. Watu wamoja, hata waamini, wanapenda kusikia maneno yasiyofaa na kuisukumiza kwa wengine, kuigeuza ingali mbele zaidi katika njia. Ningejaribu na kutoa jibu kwa kuuliza mtu Yule ulizo kama vile, “Bob, au jina lolote lile analo, unajisikiaje juu ya kusudi la kanisa la kununua uwanja makusudi tupate kusimamisha jengo kubwa kwa ajili ya maabudu yetu ya Juma pili? Ningesema wazi kuwa niliambiwa kuwa alikuwa akifundisha kwamba atungefanya hivo isipokuwa nilijisikia kuwa hakuwa ananiambia yale aliyokuwa akiwazia hakika.
Nilikuwa nikizungumza hivi karibuni na marafiki wamoja walio niambia juu ya mwanamke wanayemjua aliyegeuka toka kanisa na kuacha kwenda wakati mchungaji alipo muita ndani ya ofisi yake na kumukalisha chini toka wasifa wa uongozi kufuatana na habari aliyosikia. Ikiwa yale aliyo yasikia yalikuwa kweli ndipo mwanamke angeazibiwa, lakini bahati mbaya haikuwa kweli; ilikuwa tu maneno ya ukorofi na hakika mwanamke alikuwa bila hatia yoyote ya kitendo kiovu. Ikiwa mchungaji angechukua mda wa kuchunguza yale aliyosikia, kuliko kuyachukua kama ukweli, matokeo yangekuwa tofauti kwa wote walio usika.
 Ikiwa kiongozi wa kundi la nyumbani alikubali kuwa alikuwa akifundisha kuwa kanisa alinge simamisha jengo mpya ninge muuliza kwa nini alikuwa akifanya hivyo wakati kanisa lina kusudi la kujenga jengo kubwa. Inawezekana kuwa hakuelewa maana hasa ya yale aliyokuwa akifanya na alikuwa na nia ya kugeuza sasa yale aliyo onyesha kwake. Labda alikuwa na usikizi mbaya wa yale kanisa la Agano Jipya lilifanya na alikuwa akienda kugeuka mara moja ulipochangia naye kwa nini kanisa lilitaka kupumbazika katika mwelekeo lililo chagua.
37
 Walakini, ikiwa anakakamia katika kudai kuwa kanisa lisisimamishe jengo mpya basi hamuna budi kumuweka chini toka cheo chake cha uongozi.
 Kwa nini tunafanya vitu jinsi tunavyofanya. Hatua nyingine katika kuweka mipaka ni kutumika na ulizo la “ kwa nini tunafanya vitu jinsi tunavyofanya ” ni zaidi ya “ nini tunafanya ” lakini “ kwa nini tunakifanya ”. zaidi watu wetu wanaelewa “ kwa nini ” zaidi tunaweza kuwa na uhakika ya kuwa watachukua maamuzi yenye busara katika mipaka kazaa walioipewa. Kuambia watu “ nini cha kufanya ” bila kuwaambia ‘kwa nini tunakifanya’ ni vizuri ikiwa kila kitu kinaendeka vizuri katika njia ipasayo, lakini ikiwa hali ina badirika na mtu atachukua uamuzi kama kwa nini tutafanya baadaye, ni vizuri zaidi wapee kipaumbele moja ya kufaa ikiwa wanaelewa kwa nini tunafanya vitu jinsi tunavyofanya. Ninakumbuka nilizungumzia haya na kundi la wachungaji wa Afrika na walitumia chaguo lao la muziki kama mfano. Niliwaambia kuwa wachungaji ndani ya kanisa zao wanahitaji kujua kwanini wanaimba nyimbo ambazo wamissionari walizozileta kwa nyakati fulani na kwa nini wanaimba nyimbo za kiafrika kwa taratibu tofauti ya kiafrika juu ya zingine.(wana nyakati halisi wanapoimba nyimbo za missionari na nyakati zingine wana jipa moyo katika kuimba muziki wa kiafrika). Nilitaja kwamba ikiwa wachungaji katika kanisa zao wanajua kwa nini wanaimba tu nyimbo za kiafrika kwa nyakati fulani halafu wangepunguza kuimba “ muziki mbaya kwa wakati mbaya ”. mazungumzo yanayofuata, au ukosefu wa hayo, inaonyesha kuwa hakika hawakujua kwa nini walifanya yale waliyoyafanya.
Ni ya muhimu kuuliza kila mara, “ kwa nini tunafanya vitu namna hii ? ” unapojua kwa nini unafanya vitu ni rahisi kuijulisha watu wako. Ni rahisi kuweka mipaka makusudi wapate kuwezeshwa kufanya vitu vikubwa.
Moja ya sehemu za funguo katika haya yote ni “ kuongea, kuongea na halafu ongea tena zaidi ”. hii haiwezi kuwa mkazo zaidi. Ni ya muhimu kuchangia maono yako na watu ; wapi unaona kanisa kwa muda wamwaka moja, miaka mbili, na kadhalika. Lakini ni muhimu kuwa umechangia zaidi kuliko ‘nini tunayotaka kufanya’ ; lazima uchangie pia ‘kwa nini tunaenda kuifanya jinsi hii’ watu watakapoelewa ‘kwa nini’ watajisikia kabisa kuchukua maamuzi ambayo ni ya lazima na katika mipaka kazaa ambayo uliyo iweka.
3.12. Hifadhi shughuli nyingi
Kama mchungaji na kiongozi lazima huhifadhi shughuli nyingi ingawaje inakubidi kuwakilisha huduma na kusahau juu yake una shughuli ya kuhakikisha kuwa inakamilika kulingana na maono na philosophia ya kanisa. Ona Kutoka 18 :19-20, ingawaje Musa alikuwa atawakilisha huduma ya kuhukumu mambo madago alikuwa angali tu na shughuli nyingi na kushughulikia mambo yale yalio makubwa zaidi. Pamoja na hayo alikuwa na shughuli ya kufundisha amri na sheria kwa wale waamuzi wapya waliowekwa ; alikuwa akiwaonyesha jinsi ya kuishi na wajibu wao ulikuwa nini. Kuwakilisha shughuli pamoja na uwezo unaofaa lakini akihifadhi uchunguzi mwingi makusudi huduma au mradi viendeke vipasavyo, ni thibitisho kwa uongozi zuri.
Nina amini kwamba moja ya funguo ya kuwa na uwezo wa kuwakilisha shughuli pamoja na uwezo unaofaa wakati unahifadhi shughuli nyingi’ ina kuhusu mwenyewe pamoja na ‘picha kubwa’ kwa mfano, “ shabaa za huduma hii ni gani na je, tuna zitimiza ? ” Makanisa mengi vilevile yana orodha ya mambo ambayo hayana makusudi sahihi na tayari vitu vinaendelea sawa na kawaida yake, au baya zaidi ingali, inashuka na kakamka.
Acha niwapeni mfano wa jinsi nilikuwa nikiendesha kazi kwa masiku ya kazi yangu ya kidunia ufundi wa umeme. Kabla sija oa nilikuwa kiongozi wa timu ya uchunguzi wa umeme na mwandishi wa ramani na moja ya shughuli zangu ilikuwa kurekebisha nguvu ya kuzunguuka juu ya kupunguza yale yanayo geuka kutoka kawaida yake. Nilikuwa nikitumika sehemu hii mimi mwenyewe. Mara moja baada ya kuoa tulienda canada na huko nilichukua nafasi kama Msimamizi wa uchungaji wa idara la umeme (kazi ya kutengeneza mtambo na machine). Sasa nilikuwa na timu ambayo ilikuwa inasimamia uchunguzi wa njia za kuzunguuka na niliona kweli kuwa vigumu kutojitia kwa mambo madogo ambayo yalikuwa bila maana. Nilijivuna mwenyewe kwa kuwa vizuri zaidi kwa yale nilikuwa nikiyatenda na kulikuwako nyakati hilipokuwa imara ningeona nzia ndogo
38
bora ya kutumika kitu fulani lakini nilikuwa nikijiuliza mimi mwenyewe. ‘Je, haikuzuru kitu chochote ?’ Ikiwa ‘haikuzuru’ basi niliwaache waendelee bila kusema lolote lakini ikiwa niliona itahatarisha kazi ndipo ninge izungumzia pamoja nao.
Nijiifunza haraka kuzungumza mambo mengi ya kurekabisha pamoja nao, kama vile mambo mengi katika njia hivo kama kuakikisha walikuwa ndani ya “ mipaka ambayo nilikusudia na kwamba ‘picha kubwa’ zilizotolewa zilikuwa zuri. Niliporidhika kuwa haya yaliyotolewa yalikuwa kweli niliacha maelezo kwao. Haku kuwa wakilisha kuwa wabuni na kuchukua maamuzi ya siku kwa siku waliokuwa wakiitaji kuchukua bila mimi kuangalia kwenye mabega yao kila wakati, lakini nilichukua ushunguzi mwingi katika mikono yangu. Ili niwezesha kuburudika na kujisikia kuwa na tumaini ya kuwa mradi laiti ufikie mwisho wenye mafanikiyo.
Nilipo ingia katika huduma na nilianza kuchunga kanisa nilitumia desturi sawa hii. Kama nilivyo taja juu, kwa mwisho wa kila mwaka laiti niombe kila kiongozi wa timu kukuza makusudi na malengo kwa mwaka ujao, inayowapa mwelekeo wa kuendelea. Ningezungumza makusudi haya pamoja nao kwa kuakikisha kuwa walifaa katika maono na philosophia ya kanisa na kuwa walikuwa wenye haki na wanaofaa. Hayo yalipokuwa kwenye mahali ningewaacha kuendelea katika huduma tumainifu ambayo walikuwa wakiendelesha katika mwelekeo nzuri.
Pia nilitenga ma usiku ya Jumatatu kando kwa kutumia wakati pamoja na viongozi wangu ; kuzungumzia huduma zao pamoja nao, kuwaimiza, kutoa mashauri inapahitajika, kutoa utonzo wa uchungaji na kuwa huduma ilikuwa ikiendelea katika mwelekeo nzuri. Sikujihusisha mwenyewe na mambo ya siku kwa siku mwenyewe ila nilijisikia kuwa mwendo ulikuwa ukianza kuendelea ambao ungekuwa na mwisho wenye matokeo mabaya. Acha nieleze zaidi juu ya eneo inne muhimu ambazo nilishughulikia. Zilikuwa :
 Utunzo wa uchungaji. Unapaswa kupenda watu wako ikiwa unaenda kuwaongoza vipasavyo kwa muda murefu. Kikao chako peke yako na mmoja kwa mmoja vitakuwezesha kuwatolea utozizo wa uchungaji. Watu wanapokumbana na matatizo binafsi, pengine manyumbani kwao au hata kwa kazi zao, umuhimu wao ni sawa vile unapunguka.ikiwa hii haikushughulikiwa, inaweza kutokeza matatizo makubwa pamoja na hayo watu wanaacha huduma. Lazima tupende watu wetu na sio tu kuwaona kama njia ya kutimiza makusudi yetu wenyewe. Njia ambamo tuna watolea utunzo wa uchungaji ina waandaa kwa mtindo wa jinsi ya kutoa utunzo na msaada kwa wale walimo ndani ya timu yao. Ona Wagalatia 6 :2, Mchukuliane mizigo na kuitimiza hivyo sheria ya kristo.
 Zungumza juu ya kila matatizo unayo patikana sasa. Kikao chako pekeyako na mmoja kwa mmoja kinakuwezesha kuwauliza namna gani huduma inaendelea na kuzungumza kila matatizo wanayo weza kuwa nayo. Watu mara kwa mara hawatiki kuzungumza mambo hayo hazarani sababu hawapendi kupana wazo la kuwa wasio na maarifa na hawawezi kuweza. Walakini, wanapokuwa na mmoja ambaye wanayempenda na kuheshimu, na pamoja ambaye wanaye ona pasipo mashaka, kawaida watakuwa wazi na kuzungumuza mambo kama na hayo yawezekana wanawezakuwa wanakumbana na matatizo mengi lakini mazingira yasiotisha ya mmoja kwa mmoja yanawapa salama ya kuwa wazi na kuyazungumza.
 Zungumza juu ya azimio zao Na maono ya baadaye. Hii inakupa nafasi ya kuzungumza Yale wanayo azimia kufanya baadaye. Labda hawakufanya chochote katika eneo hili Na kwa hiyo hii inakupa nafasi ya kuizingumzia.Ikiwa walieleza azimio ndipo unaweza akikisha ikiwa inafaa. Kwa kanisa. Unapojua picha kubwa’ ni kweli unaweza kuwa na hakika ya kuwapa uhuru wa kueleza kinaganaga kama wanavyoona sawasawa.
 Wapeni mamlaka. Kukutana na mtu kwa mtu kuna kupa nafasi ya kuimiza na kuwezesha kila mtu makusudi aweze kufikia kutimiza zaidi ya vile alivyo fanya. Sababu yangu yakuchagua ma usiku ya siku ya juma tatu ilikuwa kwamba baraza lilikuwa likikutana katika usiku ule mara moja kwa mwezi. Ili ifanya kuwa ya muhimu kwangu kwa kuchagua jioni hiyo kwa kuwatuesha kila moja peke yake manyumbani kwao pindi za majuma tatu zingine.
39
Kilicho nihakikishia kuwa nitamuona kila mmoja ni matayarisho niliyoyafanya mbele ya wakati. Viongozi wangu wote walikuwa na makazi binafsi na hawakuwa watumishi wa muda wote kwa kanisa ndilo kusudi lililotuma tukifanya vikao vyetu usiku. Nilifanya vilevile ma ahadi za kuwaona mbele ya wakati. Hii ilikuwa na faida nyingi ikiwemo kumpa kiongozi wakati wakutumika juu ya kila kitu alichokijua kilikuwa kimebaki na ambacho angekifanya kabla ya kufika kwangu.
Nina amini kuwa ya maana wachungaji kutoa mda wakieleza na kusimamia kwa viongozi wao. Ni rahisi sana kwao kutoa nguvu zao zote kwa ajili ya matatizo ya watu wanaohitaji muda wao kama alivyofanya Musa na kutojali wale waliyo na vyeo vya uongozi. Walakini, kwa kufanya hivi inatubidi kupangilia mda wetu vizuri na kuorodhesha kazi muhimu katika juma letu. (Tuta zungumzia mpangilio wa wakati katika vipindi vijayo lakini acha niseme kuwa ni ya maana kupangilia siku yako, jumaa na mwaka makusudi utekeleze vitu ambavyo ni vya muhimu. Bila utaratibu huu unaweza kuwa una amurishwa na kazi za haraka ambazo mara kwa mara sizo za muhimu lakini inayosongamana nje na iliyopo).
3.13. Fundisha viongozi wako makusudi waweze kutumika huduma vizuri
Kumbuka shauri la Yethro katika Kutoka 18:20. Utawafundisha zile amri na sheria, nawe utawaonyesha njia ambayo inawapasa kuiendea, na kazi ambayo inawapasa kufanya. Tunaona hapa kuwa mchungaji hangewakilisha mamlaka na kusahau juu ya mamlaka hayo, wala mara moja angeomba kupewa sababu mbele ya wakati. Lazima ajishughulishe na kuwafundisha viongozi wake wanao ripoti kwake kwa kuwafundisha mafundisho, kwa kuwaonyesha jinsi ya kuishi na jinsi ya kuongoza huduma zao na kuwasaidia kufundisha wale wanao ripoti kwao. Kwa kifupi atawafundisha makusudi wao, na kanisa kwa jumla, waweze kuwa bora katika maisha na katika huduma.
Donald Washewiez, katika kijitabu, The Facts of CEO life, anasema juu ya umuhimu wa kiongozi kwa kuakikisha kuwa watu wamefundishwa makusudi wafikie yanayo wezekana kwao. Ana andika, “Nina amini kiasili watu wanataka kufanya kazi zuri. Wajibu wangu ni kuwaonyesha wazi hayo yana maana gani. Nihayo kiongozi anafanya.” 10 Nina hakika ana haki. CEO ya shirika kubwa haionyeshe kila mfanyakazi kwa upekee jinsi ya kufanya kazi zao vizuri lakini anawajibika kuakikisha kuwa inatokea.
Mambo kama na hayo yanatokea kanisani. Mchungaji angekuwa na uwezo wakufundisha watu katika sehemu zimoja lakini hatakuwa na ustadi wa kujaza kila eneo. Yanayofuata yakiwepo, anahitaji kuleta watu waliyo hodari sehemu hiyo kwa kufundisha watu wake. Ingawaje Nina nguvu katika sehemu nyingi ni lazima nilete msaada wa inje kwa kufundisha kundi la maabudu na wale waliyo na zawadi za kipekee. Walakini, mara nyingi ina saidia kuleta watu wa inje kukuhuzuria unapo fundisha kundi lako katika sahemu ambamo upo hodari,sauti tofauti, njia tofauti, inaweza kufanya maajabu maranyingi.
Kumbuka katika Kutoka 18:20 kwaba Yethro ana weka pamoja “kufundisha” na “kuonyesha.” Mafundisho ya darasani hayatoshi, tuna hitaji kuwa “juu ya kazi” mafundisho vile vile (“on the job training” “OJT”). Ni hivyo Yesu alivyo fundisha wanafuzi wake kuchukua huku na huko agizo kubwa. Fahamu yafutayo:
 Kwaza, waliangalia aliokuwa akifanya
 Alikuwa akiwafundisha kadiri walikuwa wakienda pamoja. Ona Marko 8:31
 Aliwatuma inje kuyafanya wao wenyewe. Katika Luka 9:1ff alituma wale kumi na wa wili (ona pia Math 10:5-16). Luka 10:1ff alituma makumi saba. Kumbuka kwamba alikuwa akiwafundisha mbele ya kuondoka. Hakuwa anawatuma inje bila mwelekeo wowote.
10 The facts CEO life, Continental Airways Inflight Magazine, June 2004 45.
40
 Alikagua waliyoyafanya walipo rudi. Ona Luka 10:17ff. kumbuka jinsi wakati wa mkaguo munakuwa ndani wanafunzi ‘wakieleza kuwa hata mashetani waliwatii katika jina la Yesu’.
 Kawaida walikuwa wakiyafanya peke yao.
Hiki ni kielelezo kikubwa kwa kufuata pamoja na watu unao taka kufundisha. Kwa mfano, ikiwa unataka kufundisha kiongozi wa kundi la nyumbani basi endelea kama ifuatavyo:
 Kutana nao katika kundi lako la nyumbani. Au lingine ikiwa hiyo ni yakufaa zaidi, na uwaache wafuate yanayotendeka (Hatua ya 1).
 Kutana nao inje ya kundi lako la nyumbani na uwaambie kwa nini unafanya vitu vimoja na jinsi ya kutayarisha na kuongoza kundi. (Hatua ya 2)
 Uwaruhusu kuongoza kundi usiku moja ukiwa ukihuzuria (Hatua ya 3)
 Kutana nao baadaye kwa kuchunguza, toa mapendekezo na uwaimize (Hatua ya 4)
 Unapofikiri wanakuwa tayari, uwape wao wenyewe kundi ndogo kwa kuongoza lakini kutana kwa kawaida pamoja nao kwa muda kwa kuimiza na kutoa mapendekezo (Hatua ya 5)
 Uwaongoze kuanza hatua kwa hatua ya mafundisho pamoja na mtu mwengine (Hatua ya 6)
 Hakikisha kuwa unafuata kikao pamoja na hawa viongozi mara kwa mara kwa kuwaimiza na kuwasaidia kuendelesha zaidi (Hatua ya 7).
Ikiwa una kanisa kubwa na una hitaji viongozi watano zaidi wa kundi la nyumbani unaweza kuuliza viongozi waliyoko wa kundi kutaja watu ndani ya kundi lao ambao wanafikiri wapo tayari kufundishwa kama viongozi wapya. Mara moja munapo kubaliana juu ya makandindeti wanaofaa, na wanapo kubali kufundishwa, utawapêleka wote pamoja na muwape darasa za kufundisha wanazo zihitaji. Hii ni sawa na hatua ya 2 hapo juu. Hatua ya tayari ilichukuliwa inje tangu walipokuwa sehemu ya kundi na tayari walionyesha yanayo wezekana kwao. Hatua ya 3 na ya 4 itakuwa ingali itaongozwa inje na viongozi binafsi wa kundi la nyumbani hadi pale waajiriwa wapya watakapo kuwa tayari kupewa kundi la nyumbani lao wenyewe.
Mwishowe, kadiri kanisa linavyo kua. Ungetia mkono katika kazi za makundi ya nyumbani, hitimisha na mafundisho ya viongozi, kwa mtu mwengine. Kumbuka, wewe kama mchungaji, ungali utashikilia usimamizi mwingina uwe umejihusisha katika ‘picha kubwa’ kama inavyohusu kwa huduma ya kundi la nyumbani.
41
Sura ya 4
Maarifa Mengine kutoka Musa
4.1. Usiogope watu hodari katika uongozi wako
Niligusia kidogo juu ya jambo hili katika sura ya 1 lakini ninataka kukazia zaidi juu yalo sababu ni ya muhimu sana. Hii ni sehemu ambamo tunaweza kujifunza kazi kubwa tukiangalia kwenye Musa na jinsi alivyojibu kwa watu hodari chini yake. Kwa bahati mbaya, wachungaji wamoja wanajisikia kukosa amani na kuwa na hofu ikiwa mtu mwengine katika kanisa lao au chama anaonyesha ustadi zaidi katika sehemu moja kuliko wanavyofanya. Wanataka kuamini kuwa wako waubiri wazuri zaidi, nabii wazuri zaidi, washauri wazuri zaidi, watenda miujiza wazuri zaidi na kujisikia woga au kuwa na hofu ikiwa mtu mwengine anaonyesha uwezekano mkubwa katika moja ya sehemu hizi. Wanataka kila mmoja kuja kwenye mashauri kwao, au basi wanawaruhusu kwa kuwapa anwani kwa mtu mwengine, na anafadhaika ikiwa watu wanaanza kuenda kwa mtu mwengine katika kanisa. Wnataka kila mtu kuamini kuwa ni manabii wenye upako zaidi ndani ya kanisa na wanajisikia hofu ikiwa watu wanapendelea kwenda kwa kiongozi mwengine kwa ajili ya neno la unabii.
Siku moja nilikutana na nabii hodari sana ambaye alijenga kanisa bila kitu na alianzisha makanisa mengine kwa mafanikio katika uongozi wake. Walakini, kulikuweko bila shaka matatizo katika kazi yake na wamoja wa watu wake muhimu waliniambia kuwa haweze husimamisha yeyote anayeonekana kuwa hodari zaidi kuliko yeye katika sehemu yeyote ile. Ikiwa mtu fulani alianza kuendesha huduma muhimu angemutoa inje kwa kumukomesha na kuwadhihaki. Moja ya kanisa kubwa zaidi katika mji ambamo nilisikia habari hii ilikuwa ikiongozwa na mtu ambaye alikuwa mchungaji wa kanisa dada chini ya uongozi wa huyo mtume. Sababu adhaika na akaanza kukomesha na kudhihaki mchungaji. Siya kusema, hali ilikuwa isiyowezekana kwa mchungaji kuvumilia na kutopenda aliondoka kazini na akaanzisha kanisa lake mwenyewe. Ilikuwa kama ahibu sababu mtume alikuwa na upako mkubwa juu ya maisha yake na alikuwa hodari sana katika njia nyingi. Hange endelea zaidi na zaidi kwa kutekeleza mambo makubwa ikiwa aliendelesha watu hodari katika kundi lake kuliko kuwakomesha.
Ikiwa unasonga watu hodari utapata hasara sababu ya hiyo. Usiwe na hofu juu ya watu hodari chini ya uongozi wako. Uwape moyo kwa yale wanayo kwa yale wanayoyafanya kama mchungaji hauhitajike kuwa muhubiri mashuhuri au mshauri mzuri zaidi au mtenda mwiujiza mzuri zaidi, lakini unaitiwa kuwa kiongozi anaye kuza watu makusudi kazi ya Kristo ikue. Kuwa kiongozi mkuu ndiyo unayohitaji kuzingatia.
Musa ni mfano mkubwa wa kiongozi ambaye hakuogopa watu hodari chini yake lakini alitaka wengi wa kundi lake kadiri iwezekanavyo kutumia zawadi zao za kiroho kwa wingi zaidi. Katika Hesabu 11:24-29 tuna soma,
Musa akatoka, akawaambia watu maneno ya BWANA, akawakutanisha watu sabini miongoni mwa wazee wa watu, aka waweka kuizunguka Hema. 25Ndipo BWANA akashuka ndani ya wingu, akanena naye, akatwaa sehemu ya roho iliyokuwa juu ya Musa, akaitia juu ya wale waze sabini; ikawa roho hiyo ilipowashukia, wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena. 26Lakini watu wawili walisalia kambini, jina la mmoja aliitwa Eldadi, na jina la wa pili aliitwa Medadi, na roho ile ikawashukia; nao walikuwa miongoni mwao walioandika, lakini walikuwa hawakutoka kwenda hemani, nao wakatabiri kambini. 27Mtu mmoja kijana akapiga mbio, akaenda akamwambia Musa, akasema, Ekdadi na Medadi wanatoa unabii kambini. 28 Yoshua mwana wa Nuni, mtumishi wa Musa tangu ujana wake, akajibu akasema, Ee bwana wangu Musa, uwakataze. 29Musa akamwambia, Je! Umekuwa na wivu kwa ajili yangu, ingekuwa heri kama watu wote wa BWANA wangekuwa manabii na kama BWANA angewatia roho yake.
42
Katika kifungo hapo juu, Roho alikuja juu ya wazee sabini waliofuatwa na Eldadi na Medadi na wakaanza kutabiri. Yoshua alionekana kuhusika kuwa hii inaweza kuzoofisha mamlaka ya Musa tangu wengine walipoanza kutabiri na alitaka Musa awakataze. Lakini Musa hakuwa na hofu na hii kwani alijua kuwa Mungu alimuita kuongoza watu wa Israeli katika inchi ya Ahadi na kuwa alihitaji watu hodari wote ambao angepata ikiwa alikuwa akienda kutimiza kazi yake kwa mafanikio. Alitaka wale walio chini yake kuwa hodari kadiri wawezavyo sababu alijua kwamba hii ingefanya kazi yake kuwa kubwa na nyepesi.
Bill Hybels, Mwanzilishi na Mchungaji Mkuu wa Willow Greek Community Church, moja ya makanisa makubwa na yenyemvuto katika USA, ni mfano wa siku hizi wa kiongozi ambaye hana hofu na watu wenye ujuzi zaidi chini yake lakini kwa kawaida anaye enda nje kutafuta watu kama hao kuwa sehemu ya kundi lake. Ana andika, “Ninatafuta wenye daraja ya ujuzi inayoinukia zaidi ambao naweza kupata. Nina omba Mungu kunisaidia kupata mmoja ambaye zawadi hizo za kiroho zilizoendelea miaka na miaka. Tulipokuwa tukitafuta mmoja wa kujiunga katika kundi letu la mafunzo, ninaomba Mungu kutusaidia kupata mtu aliye na zawadi hodari mno za kufundisha, naam aliye hodari kabisa kuliko mimi… nikiwa ninatafuta kiongozi wa makazi, ninatafuta aliye na zawadi za usimamizi nyingi mno na mkondo wa nyota unao andika habari vizuri. Miaka iliyopita nilitambua kuwa ikiwa sikuanza kuzunguuka pekeyangu pamoja na watu wamoja waliopo ningekuwa nimeangamia kwa change-moto za kuongoza willow. Sasa ninapo angalia kandokando ya meza wakati wa mikutano yetu ya kundi za uongozi ninaona wengi ni wenye elimu kuu na wenye ujuzi. Ni mimi tu ninaye kosewa uthibitisho!11 Sababu moja wapo za Willow Creek Community Church kukua sana ni kwamba Bill Hybels alivuta kundi kubwa pamoja. Aliwainua kuliko kuwazuia wakati ilipoonekana kuwa wanaweza kuwa na ujuzi zaidi kuliko yeye katika sehemu fulani ya huduma.
4.2. Sikiliza kwa kushauri na uikague
Moja ya vitu tunavyo jifunza kwenye Kutoka 18 ni umuhimu wa kuwa wazi kwa kupokea shauri. Usifikiri kuwa unajua yote na kuwa hakuna awezaye kukufundisha kitu chochote. Usiwe mwenye kiburi kuwa hauta wasikiliza wengine wanapokuwa na kitu cha kukuambia. Hii ni hasara. Uwe mtu asiyekuwa wazi tu kwa kupokea shauri lakini aliye pia na nia ya kujifunza, nia ya kuongeza ujuzi na nia ya kukua. Ongeza tabia hii. Soma Methali 13:10, kiburi huleta mashindano tu; Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.
Musa alikuwa mtu ambaye alikuwa akisiliza mashauri na kukubali sehemu ambazo zilikuwa za muhimu na kukataa yale yasiyofaa. Hesabu 12:3 ni vesi inayofaa juu inatuambia kuwa Musa alikuwa mnyenyekevu sana na hiyo ni shabaa moja wapo lililo mfanya kuwa na nguvu za tabia ya kusikiliza, kushauri na kuchukua uamuzi unaofaa. Ona Hesabu 12:3, “Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi”.
Daudi ni mfano mwengine wa kiongozi mkuu ambaye alikuwa na alikuwa akipokea shauri toka kwa wale waliyo mzunguka. Tunaona hayo katika 2 Samweli 19:1-8 Yoabu alipomfikia baada ya kuuawa kwa mwanaye Absloma. Daudi aliruhusu sikitiko lake mwenyewe kupotoa uamuzi wake na kama matokeo alifanya uamuzi mbaya ambao ungekuwa na matokeo mabaya zaidi. Walakini, alikuwa na nguvu ya tabia ya kumusikiliza Yoabu, kukubali kuwa alifanya kosa, na kubadirisha matendo yake ya kawaida. Ona 2 Samweli 19:5-7, basi Yoabu akaingia nyumbani kwa mfalme, akasema, wewe leo umefedhehesha nyuso za watumishi wako wote, waliokua leo roho yako, na roho za wanao, na za binti zako, na roho za wakezo, na roho za Masuria wako, kwa kuwa unawapenda wakuchukiao, na unawachukia wakupendao. Maana umetangaza leo ya kuwa wakuu na watumishi wako si kitu kwako,
11 Bill Hibels Courageous Leadership (Zondervan. Grand Rapids 2002) 83-84.
43
maana leo nimetambua hivi, kama Abusalomu angahishi, na sisi soto tungalikufa leo, ingalikuwa uyema machoni pako. Basi sasa, ondoka, utoke nje, ukasema na watumishi wako maneno ya kuwatuliza roho zao, maana mimi nakuapia kwa BWANA, usipotoka, hatabaki hata mtu mmoja pamoja nawe usiku huu, na mambo haya yatakuwa mabaya kwako kuliko mabaya yote yaliyo kupata tokea ujana wako sasa.
Niliona mukutano wa watu wanao ojiwa kwenye TV ya Austalia12 hivi karibuni na bwana Richard Branson, mwanzilishi na CEO ya Virgin Airlines, ambapo alitaja kuwa alichukuwa mda mwingi akisikiliza kundi lake na kuandika maelezo yao makusudi apate kuwakagua. Aliyekuwa akiwaoji ndipo akawaonyesha sinema yake fupi akizungumuza pamoja na wamoja wa ngazi za wafuasi wake,na kuandika wanayoyasema. Sio ya kushangaza kuwa bwana Richard mbele alisema katika azimio kuwa kundi lake lilikuwa tiifu kwake.
Walakini, tunapo hitaji kusikiliza watu na kukagua yale wanayo yasema, hatupashwe kuchukua maamuzi juu ya msingi ya yale itakayo tufanya kuwa wenyekupendwa na watu wote pamoja na walio kandokando yetu. Zaidi, tu napashwa kufanya uchaguzi wetu juu ya msingi ya ile iliyo haki. Tutazungumuza haya kwa maelezo zaidi mbele.
4.3 Tazamia lawama
Somo lingine muhimu ambalo tunalo lisoma kutoka maisha ya Musa ni kwamba tungetazamia lawama ikiwa tunakuwa viongozi. Angalia yafuatayo:
 Kutoka 15:24, ndipo watu wakamnung’unikia Musa, wakisema, tunywe nini?
 Kutoka 16:2, na mkutano mzima wa wana wa Israeli ukawa nung’unikia Musa na Haruni, huko barani.
 Kutoka 17:2-3, kwa hiyo hao watu wakateta na Musa, wa kasema, tupe maji tunywe. Musa akawaambia, kwani kuteta na mimi? Mbona mnamjaribu BWANA? Watu wakawa na kiu huko; nao wakamnung’unikia Musa, wakisema, Mbona umetupandisha kutoka Misri, kutuua sisi na watoto wetu na wanyama wetu kwa kiu?
 Hesabu 14:1-4 Mkutano wote wakapaza sauti zao wakalia, watu akatoka machozi usiku ule. Kisha wana wa Israeli wote wakamnung’unikia Musa na Haruni; mkutano wote wakawaambia, Ingekuwa heri kama tungalikufa katika nchi ya Misri, au ingekuwa heri kama tungalikufa katika jangwa hile. Mbona BWANA anatuleta mpaka nchi hii ili tuanguke kwa upanga? Wake zetu na watoto watakuwa mateka; Je! Si afadhali turudi Misri ? wakaambiana, tumweke mtu mmoja awe akida tukarudi Misri.
 Hesabu 16 :1-2 , Basi Kora, mwana wa Ishari, mwana wa Kohati, mwana wa Lawi, akatwaa watu, pamoja na Dathani na Abiramu, wana wa Eliabu, na Oni, mwana wa Pelethi, waliokuwa wana wa Reubeni ; nao, pamoja na watu kadha wa kadha waw ana wa Israeli, watu mia mbili na hamsini, wakuu wa mkutano, watu wenye sifa, wakainuka mbele ya Musa. Pamoja nao wanaume wa Israeli 250, ambao walijulikana vizuri kuwa viongozi ambao walisimikwa kuwa wanamemba wa baraza.
Katika matukio yaliyopo hapo juu tunaona kuwa Musa hakufanya kilicho kibaya, alikuwa akifanya yale Mungu aliyomuitia kufanya, lakinini matatizo yalipotokea watu walimuamakia na kunungunika juu yake. Kila wakati Mungu alithibitisha uongozi wa Musa kwa kuonyesha uwezo wake kupitia maishara, ma alama na miujiza lakini waliendelea kunungunika. Nina ona Hesabu 14 :4 kuwa yote mbili inatiisha na kweli kimajonzi. Musa aliongoza wa Israeli jangwani, waliishi ishara baada ya ishara, lakini walitaka kujiondolea Musa na kurudi utmwani. Bahati mbaya hii ni asili ya mwanadamu na anaye chukua kazi ya uongozi anaweza kutazamia lawama katika hali moja au nyingine ; mengi ya hayo yatakuwa yasiyo
12 ABC Sydney,”Talking heads” 13 Sepember 2010
44
na msingi. Tunayoyaishi yanadokeza kuwa kadiri kazi ya uongozi ilivyo kubwa kadiri lazama itakuwa kubwa.
Acha nihadithie tukio langu binafsi. Nilipo kubaliwa katika huduma na ilikuwa karibu ya kuanza mafunzo yangu ya theologia nilipokea ufunuo mkubwa kutoka Maandiko. Nilikuwa nikisoma Yohana 11, kufufuka kwa Lazaro, nilipofika kwenye vesi ya 37, Baliwengine wao wakasema, Je ; Huyu aliyemfumbua macho yule kipofu, hakuweza kumfanya na huyu asife. Hapa tunaona Mwana mkamilifu wa Mungu akilaumiwa na watu wamoja kwa kitu ambacho hakuwa anakisimamia. Fikiri juu ya hii kwa muda. Aliponya wagonjwa wao na alifungua macho ya vipofu lakini waliendelea kunungunika na walikuwa wakilaumu. Ndipo Roho Mtakatifu alisema kwangu, Ikiwa walilaumu Yesu unaweza kuwa na uhakika kuwa watakulaumu. Kiongozi mzuri anajua hii kuwa ni kweli.
4.4. Jinsi ya kuzuia lawama
Fanya yaliyo kweli
Jibu letu kwa lawama ni lamuhimu. Siku zote tunapashwa kuwa watu wanaofanya yale tunayojua ni kweli na tusichukue njia rahisi kwa ajili tu ya kupendeza wale wanao nung’unika. Ikiwa unataka watu wakupende na unachukua maamuzi yanayosimamia kwenye mafikiri haya, utajiingiza mwenyewe katika tatizo. Siku zote fanya yale unayojua Mungu amekuitia kuifanya. Ikiwa hauna uhakika na uamuzi halisi basi tafuta ushauri kutoka kwa watu wa Mungu wenye busara lakini usiendelee kutumika kwenye msingi wa kuchunga uwe umependwa na watu wote. Paulo anatoa ushauri mkuu katika 1 Wathesalonike 2 :4-6, Bali kama vile tulivyopata kibali kwa Mungu tuwekewe amana injili, ndivyo tunenavyo ; si kama wapendezao wanadamu ; bali wampendezao Mungu anayetupima mioyo yetu 5 Maana hatukuwa na maneno ya kujipendeza wakati wowote, kama mjuavyo, wala maneno ya juujuu ya kuficha choyo ; Mungu ni shahidi. 6Hatukutafuta utukufu kwa wanadamu, wala kwenu, wala kwa wengine tulipokuwa tukiwalemea kama mitume wa kristo.
Kuchukua maamuzi yanayosimamia juu ya kupendeza watu ni hasara. Ikiwa unajaribu kupendeza makundi mbalimbali kwa ajili ya kupendwa na watu wote unaweza kufikiya kutokumpendeza hata mtu na kila mtu kukabiliana nawe. Kumbuka historia la huzuni lifuatalo. Kufuatana na idadi ya mambo ugonjwa unaendelea ndani ya kanisa ambalo nilijua matokeo yake ikawa mafarakano mengi katika dhehebu ; kila mmoja alitaka kanisa liende katika njia tofauti. Kwa bahati mbaya, mchungaji alitaka kupendeza kila mtu na aliambia kila kundi ambalo walitaka kusikia ; liliwaakikishia kuwa yale waliyoyataka yangetokea. Ndipo sasa akawaambia kwamba wangependa kila mtu na, sababu ya hii, kila kitu kingekuwa kizuri. Matokeo ilikuwa ya kumalizia katika hasara sababu yale ambayo moja ya mafarakano ilikuwa ikitaka ilikuwa wao kwa wao wenyewe kwa yale wengine walitaka. Ilikuwa haiwezekani kwake kufanya yale kundi lilikuwa likitazamia na alikuwa angali akifanya tu yale kundi B lilikuwa likitaka. Sitaki kusema kila kundi lilijisikia kusalitiwa wakati mchungaji hakuweza kufanya yale aliyo waagiza na, kama tokeo, watu wengi walianza kuondoka kanisani. Hatimaye, mchungaji pia aliondoka na kwa miaka miwili kanisa, ambalo mbele lilikuwa na nguvu sana, lilifunga milango.
Kwangu mimi, moja ya mifano mbaya sana inapatikana katika Kutoka 32:21-25 ambako Haroni aliwasikiliza watu na akafanya yale waliyoyataka ingawaje alipaswa kujua kama ilikuwa mbaya: ''Musa akamwambia Haruni watu hawa wamekufanya nini hata ukalete dhambi hii kuu juu yao? 22 Haruni akasema, hasira ya bwana wangu isiwake, wewe unajua watu hawa, ya kuwa wamejielekeza kwa mabaya. 23Maana waliniambia, katufanyie miungu, itakayokwenda mbele yetu, kwa maana mtu huyo Musa, aliyetutoa katika nchi ya Misri, hatujui yaliyompata. 24Nikawaambia, mtu yeyote aliye na dhahabu na aivunje, basi wakanipa, nami nikaitupa ndani ya moto, akatoka ndama huyu. 25Basi Musa alipoona yakuwa watu hawa wameasi, maana Haruni amewaacha waasi, ili wawe dhihaka kati ya adui zao''. Huu ni
45
mfano wa uongozi hafifu. Alifanya yale watu waliyoyataka hamkini sababu alitaka apendwe na watu wote. Hakukiri hata kwa Musa kama alifanya ndama wa ng'ombe; hakuna mtu aliyepaswa kuamini kama alitupa dhahabu motoni na kukatokea ndama wa ng'ombe. Usiwe mgoigoi. Usifanye kitu tu sababu kitakufanya kupendwa na watu wote wakati unajua kama ni kibaya. Usikose kutumikisha utawala na kutiisha watu sababu una woga ya yale watu watafikiri juu yako. Kutofuzu kuongoza na kufanya yaliyo haki ni kufanyiza maafa.
Wakati watu wanapo tulaumu tunahitaji kuelewa kuwa kila mara hawatunung’unikie bali wanamnung’unikia Mungu. Hii ilikuwa hasa kesi ya Musa. Hawakutaka kumtumainia Mungu na kuendelea mbele katika nchi ya ahadi kwa imani kwa iyo wakamgeukia Musa ambaye alikuwa wakili wa Mungu anayeonekana. Hawakumkasirikia Musa bali walimkaasirikia Mungu ; kweli Musa alifikia kuwa mmoja ambaye juu yake walionyesha hasira yao. Ona Hesabu 16 :12-14, kisha Musa akatuma kuwaita Dathani na Abiramu wana wa Eliabu ; nao wakasema, “ Hatuji sisi, 13Je ! Ni jambo dogo, wewe kutuleta kutoka nchi iliyojawa na maziwa na asali, ili kutuua jangwani, lakini pamoja na haya wajikuza mwenyewe uwe mkuu juu yetu kabisa ? 14 kisha, hukutuleta katika nchi iliyojawa na maziwa na asali, wala hukutupa urithi wa mashamba, na mashamba ya mizabibu ; je ! Unataka kuwatoboa macho watu hawa ? Hatujui ”. Musa hakuwatoa toka nchi yenye kujawa maziwa na asali kwa kuwaua jangwani ; walitoa hayo juu yao wenyewe kwa ajili ya kutokutii kwao. Ndiyo sababu yao ya kutofurahia maisha katika nchi ya Ahadi ilikuwa ni kwa sababu ya uasi wao wenyewe ; ilikuwa ni kosa yao na sio Musa. Walakini, sababu Musa alikuwa kiongozi mteule wa Mungu alikuwa mmoja ambaye walishambulia. Kila mtu anayeongoza huduma ndani ya kanisa anahitaji kuelewa haya.
Dhihirisha ni wapi lawama zinapotokea
Ni ya muhimu kudhirisha ni nani anayekulaumu na ahadi yake kwenye kanisa ni gani. Ninaona inafaa kuchora ramani ya ‘’Lawama ya Mchungaji’’ na uweke watu kwenye ramani hiyo tangu 100 ukishuka kwenye 0 ; 100 wakiwa watu wanao mlaumu mchungaji zaidi na 0 wakiwa wale wanao mlaumu kidogo. Ndipo uchore ramani ingine ya ‘’Ahadi kwenye kanisa’’ na uweke watu kwenye ramani hiyo tangu 100 ukishuka kwenye 0 ; 100 wakiwa watu ambao wanajihusisha zaidi katika huduma ya kanisa na wanao jitolea kwa kuisaidia na mali zao wakati 0 ni wale wenye ahadi ndogo kwenye kanisa katika muda wa huduma na mali. Ninayoyaishi yanadokeza kuwa wale walio kwenye kilele cha ‘’lawama ya mchungaji’’ mara kwa mara yanakuwa kwenye msingi wa ‘’Ahadi kwenye ramani ya kanisa’’, hao ni, wale wanaolaumu mchungaji zaidi ni wale wanao ahadi ndogo kwenye kanisa.
Jinsi ya kuzuia watu wenye lawama ambao hawajitoe kwenye kanisa
Ikiwa unaona watu wanao kulaumu ni wale ambao hawajitowe kabisa kwenye kanisa, basi unapambana na watu walio sawa na wale waliokuwa wa kimlaumu Yesu katika Yohana 11 :37, si kitu yale unayoyafanya, watu hawa hawatakuwa na furaha kamwe na, ukuwaruhusu, watajichukulia kazi kubwa ya wakati wako na nguvu. Fanya kama vile Yesu alivyo fanya, puuza manung’uniko yao yote na endelea kufanya yale uliyoitwa kufanya. Katika miaka yangu ya mwanzo katika huduma nilijaribu kusaidiya watu hawa lakini niliona kuwa hawakuwa wanaridhika kamwe na yale niliokuwa nikifanya na hawakukua kamwe kama tokeo la jitihada zangu. Watu hawa ni ‘mimi’ ninafaa na wanajihusisha tu na yale wanayoweza kupata toka kanisa na hawaangaikie yale ambayo wanaweza pana. Chochote kile unacho wapa kamwe hakitatosha. Usipoteze mda wako ukijaribu kufurahisha watu hawa. Havitafanya kazi na haiweze kuwabadirisha. Uwe na adabu kwa watu hawa unapokutana nao lakini usifikiri unaweza kuwafurahisha kwa kuwapa yale wanayoyaomba.
Watu hawa wanalaumu watu katika kila hali ya maisha, na wewe, kama mchungaji wao, kuna shabaa nyingine sahihi kwa asili yao ya lawama. Kuwapa watu hawa kazi kubwa ya wakati wako na juhudi sio kwenda kuwa anayefaa kwa yeyote ule ; hakika sio kwako, kanisa,
46
wala hata wao. Wanahitaji kufikia kwenye hatua ambako wanashikilia madaraka kwa kazi zao na kusimamisha kulaumu makusudi waweze kuanza kukua. Watabadirika tu wakati hii inatokea. Ninayoyaishi yanadokeza kuwa watu hawa kwa kawaida wanaenda toka kanisa kwa lingine na hata kutangaza kuwa watakatifu sana kwa nyakati. Kuna mara watajaribu kubembeleza mchungaji kwa manajili ya kupata mda wake zaidi ; ‘’Hakuna anaye nisikia vile vile wewe’’ kujaribu kupendeza hawa watu haiwezekane na isiyozaa matunda. Uwaombee Mungu akawabadirishe na kuwapa nia ya kukua.
Acha nitaje kuwa wamoja wa watu hawa wanaweza hata kuonekana kuwa rafiki za mchungaji kwa uso wake lakini anamulaumu nyuma ya mgongo wake na kujaribu kudhoofisha mamlaka yake anapokuwa akizungumza na watu wengine. Pia jihadhari na wale wanaolaumu watu mbele zako sababu inawezekana watakulaumu wewe kwa wengine wanapokuwa wakiwaongelea.
Kuzuia lawama wakati watu wanapojitolea kwenye kanisa
Walakini, ikiwa lawama zinakuja kwenye watu ambao wanajitoa kikamilifu kwenye maisha na huduma ya kanisa na wasio na asili ya kulaumu watu. Basi unahitaji kuzingatia kabisa yalee wanayoyasema. Kunaweza kuwa na ukweli fulani ndani yake na unaweza kuhitaji kuitendea kazi, inaweza kuwa njia ya Mungu ya kujaribu kupata usikizi wako. Unaweza kuwa umekosa. Inaweza kuwa hali kama na ile ya 2 Samweli 19 :1-8 ambayo alipambana na Daudi. Daudi alikuwa na kosa kwani aliruhusu huzuni yake zidi ya Abosalomu kutawala matendo yake. Wakati mtu sawa Yoabu ambaye alionyesha miaka na miaka kama alikuwa mtiifu kwa Daudi, ghafula akawa mjuzi, basi Daudi angekuwa mpumbavu kwa kutojali shauri lake.
Ikiwa unajikuta ghafula mwenyewe katika hali ambamo watu wanaojitoa kanisani wanakuwa wajuzi zaidi yako ndipo bila shaka angalia yale unayoyafanya. Unaweza kubadili mipangilio yako. Usiogope kutafuta ushauri kwenye wacha Mungu ambao unawaeshimu chini ya tukio hizi ; hasa ikiwa unajisikia kuchoka au kushindwa.ona tena Methali 15 :22, Pasipo mashauri makusudi hubatilika ; Bali kwa wingi wa mashauri huthibithika.
Ikiwa unaendelea kupambana na kazi kubwa ya lawama kutoka kwa wale wanaojitoa kwenye kanisa na wasio na asili ya kulaumu watu, basi hii ni tatizo kweli. Ushauri wangu ungekuwa wakuwa na maongezi muhimu pamoja na kiongozi mcha Mungu mwenye busara ambaye unatumaini. Inawezekana ya kuwa ulibadili njia yako ya kufikiri ghafula na hii inatokeza tatizo. Nilisikia habari za kanisa ambalo lilikua kwa uthabiti na inawezekana lilikuwa kanisa kubwa katika eneo lake, na ikiwa kwa kawaida kulikuweko lawama toka kwa wale ambao hawakuwa wanajitoa kwa kanisa, Baraza pamoja na viongozi muhimu wengine walikuwa wenye juhudi kweli na wenye kujitoa kwa mchungaji mdogo na maono yake.Walakini, kitu kimoja kilitokea katika uongozi. Bahati mbaya, wengi wa watu hawa, wakiwemo na idadi kwenye Baraza walijisikia kutokuwa na chaguo lingine isipokuwa kuacha kanisa na kwenda penginepo. Tokeo la mwisho lilikuwa na matokeo yasiyofaa kwa wote waliohusika.
Inawezekana pia kuwa unaweza kuwa katika kanisa mbaya na kuwa utu wako na elimu yako haipatane na kanisa au eneo ambamo unapatikana. Ikiwa hii ndiyo kesi, ushauri ungekuwa kufikia kuamia kwenye kanisa lingine ambalo linapatana zaidi na wewe, hii ni sehemu ya kuwa kiongozi. Kiongozi anaitwa kutokeza mabadiriko na kuweka kanisa mahali papya na pazuri ; upinzani ni usiyoepukika. Yesu na Musa walikumbana na upinzani na nihivyo itakavyo kuwa hata kwako.
Inawezekana kuwa haupatane na huduma ya uchungaji. Nilikutana na watu wadogo kama hao na somo zuri zaidi la tendo kwao ilikuwa ni kurudi kwenye kazi ya kawaida au kuchukua aina nyingine tofauti kabisa ya huduma ambayo ilikuwa inakuhusu zaidi. Maamuzi haya hayangechukuliwa haraka au mwangani lakini yanahitajika kusema kwa minajili ya wote
47
wanaohusika. Hakikisha kuwa unatafuta mshauri mcha Mungu mwenye busara kabla ya kuchukua tendo lolote kama na hili.
4.5. Jibu letu kwa lawama isiyo na haki
Usihichukue mwenyewe
Ni ya lazima sana kutokuchukua lawama isiyo na haki mwenyewe. Usihichukue kama vile matukano yako binafsi. Usipatwe na hasira. Usianze kushakia uwezo wako au mwito wako kwenye huduma. Watu wanaokulaumu asili yao ni hivo na haina kitu cha kufanya hata ukiwa na haki wala umekosa au hata ukiwa mwenye kuweza wala hapana. Ni hivo tu walivyo; asili yao ni ya kulaumu.
Acha niwape mfano wa hii kama unavyoelekea kwenye kitabu,The Shack (banda). Sisi wawili mke wangu Carol na mimi tunafikiri hiki ni kitabu kikubwa sababu kinawapa wasomi wake njia mpya na inayosaidia kuelewa ugumu wa utatu na ajabu ya neema ya Mungu kwetu sisi wenye dhambi. Walakini, mke wangu alikutana na mwanamke aliye mjuzi kwa asili na akaanza kulaumu kitabu bila kujua Carol kweli alikipenda. Mwanamke huyu inawezekana alipewa DVD inayochambua hicho kitabu na akaieleza katika mwangaza usiofaa. Kwa mda Carol aliuliza huyo mwanamke ikiwa alisoma hicho kitabu yeye mwenyewe au alisegamia tu kwa yale aliyoyasikia mwengine akisema. Alikubali kuwa hajawai kukiona hicho kitabu na hakika hajakisoma; yote aliyoyafanya ilikuwa ni kukubali lawama isiyo na haki kama kweli. Kwa nini alikuwa akifanya hivi? Yote ninayoweza anasema ni hiyo inayoonekana kuwa asili yake. Ni mjuzi sana wa kanisa katika Australia na havinishitushe kwani jibu maalum kwa kila kitu ni kuwa mjuzi na kuamini maneno yasiyofaa. Ikiwa unasikia maelezo yasiyofaa juu ya muhubiri au kitabu, usiamini hadi utakapo ichunguza mwenyewe. Ndiyo unaweza kuwa ukimsikiliza mtu mjuzi. Ni hii ninayo maanisha ninaposema watu wamoja ni wajuzi kwa asili, kwa iyo usichukue lawama zao kwako wewe mwenyewe.
Sasa turudi kwenye Musa, kuna watu wadogo katika historia ambao walikuwa wenye akili ya kutosha zaidi kuliko alivyo kuwa. Ni mmoja wa viongozi wakubwa katika biblia. Ni aliyeshuhudiwa kuwa mwanaume mtakatifu zaidi ambaye hajawai kuishi kwa kuwa ni mtu pekee ambaye Mungu alizungumuza naye uso kwa uso. Ona Hesabu 12:7-8. Mbali zaidi, alikuwa akitumika na upako wa Roho Mtakatifu kuliko viongozi wengine wangeliota ndoto tu, hata sasa, kwa kutojali haya yote, alikuwa akiendelea kulaumiwa. Ni hii ni ile kiongozi anaweza tazamia. Ikiwa unachukua lawama isiyo na haki kama matushi binafsi, au kama mashutumu juu ya uwezo wako wa kuongoza huduma, unaenda kuwa na maisha magumu kabisa kama kiongozi. Ninashakia ikiwa mtu kama na huyo angeendelea katika uongozi muda murefu.
Acha Mungu akutetee
Hesabu 12:1-3 ni mfano mzuri wa jinsi ya kuzuia lawama isiyo na haki. Katika kifungo hiki tunasoma jinsi Aroni na Miriamu walivyokuwa wakimlaumu Musa, lakini kama tunavyosoma, tunaona kuwa Musa alikuwa katika kweli na Aroni alionekana kupatwa na wivu, kama vesi 2-3 zinavyoonyesha. “Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? BWANA akasikia maneno yao. 3Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi ”
Yaliyotokea baadaye yanaandikwa katika vesi za 4-9, “ Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje. 5BWANA katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili. 6kisha akawaambia, “ sikilizeni naye akaenda zake ”. kumbuka kuwa Musa hakujaribu kujitetea mwenyewe lakini aliachia Mungu hayo.
48
Warumi 12 :19-20 inatumiwa katika hali hii. “Wapenzi, msijilipize kisasi, bali hipisheni ghadhabu ya Mungu; maana imeandikwa, kisasi ni juu yangu mimi; mimi nitalipa, anena Bwana. 20Lakini, adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivyo, utampalia makaa ya moto kichwani pake”. Wakati mtu fulani akitendea jambo mbaya. Hatuta mrudishia ubaya au kutafuta kujilipizia kisasi; hiyo ni kazi ya Mungu. Yeyote anaye kwenda katika kazi ya kikristo ya kila aina angetazamia lawama isiyo ya haki kuinuka zidi zao. Hii ilitokea kwa Yesu na itatokea kwetu. Haya yanapotokea hatungetoka nje na kujitetea sisi wenyewe lakini afadhali ihachie Mungu apate kututetea.
Fikiri yafuatayo kutoka kwenye kitabu nilichokisoma hivi karibuni cha R.T Kendall 13 kwenye dibaji, usijitetee mwenyewe unapolaumiwa. Ana sihi sana wasomi wake tusimuibe Mungu yale anayoyafanya vizuri zaidi, kazi ya kutetea wanaotendewa vibaya. Moja ya kitu Mungu anachokifanya vema kabisa, anasema, ni kusafisha jina la mtu ambaye alikuwa ameshitakiwa bila sababu, walimzingizia au kuumiza katika njia yoyote ile. Anaifanya katika njia ambazo zinafanya moyo kusita. “usijaribu kusaidia Mungu nje” aliandika Kendall, “usijaribu kamwe – kamwe –usijaribu kusafisha jina lako mwenyewe. Hiyo ni kazi ya Mungu”. Alifanya hivi kwa Musa na atavifanya kwetu. Ona pia 1 Petro 5:6, Basi nyenyekeeni chini ya mkono wa Mungu ulio hodari, ili awakweze kwa wakati wake.
Endelea kufanya yale Mungu aliyokuitia kufanya
Moja ya matatizo ya lawama isiyo haki ni kwamba tunajisikia kuwa tungejitetea wenyewe. Walakini, kama tulivyotaja juu, hatutafanya hivyo lakini tutayaachia Mungu. Wajibu wako ni kuendelea kufanya yale Mungu aliyokuitia kufanya. Usiwe na mwendo wa nyoka na kupoteza wakati unaofaa na nguvu kwa kujaribu kusafisha jina lako. Shetani angependa wewe kufanya hivyo kwani atakufadhaisha kwa kufanya huduma. Katika Yohana 11:37-39, Yesu anatutayarishia mtindo zuri wakufuata. Jibu lake kwa wale wa kandokando yake waliokuwa wakimlaumu kwa kutokuzuia kifo cha Lazaro, ilikuwa ni kuendelea na huduma ambayo Mungu alimupa kuliko kujaribu kueleza matendo yake kama kwa nini hakuja mapema. Ni hivyo tungepashwa kutenda.
Billy Graham pia ni mfano mkubwa wa kufanana na Kristo katika msimamo wake. Billy amekuwa mtu aliyetwigwa lawama niyingi zisizo na msingi kuliko watu wote ninao wajua na mengi ya hayo yalikuwa yakitokea katika waamini wa kanisa la Biblia. Ilikuwa ni vigumu sana na ilionekana kwa nyakati kuwa ya kuchukiza sana. Hakika ilikuwa bila msingi. Ndiyo Graham kiwazi aliyapuza na alikataa kujitetea mwenyewe wala kulaumu wale waliokuwa wakimshambalia; aliendelea tu na kazi ambayo Mungu alimuita kufanya; kuhubiri injili. Nimesoma hivi karibuni nakala moja ambamo Billy Graham alishuhudia ukristo kuwa na viongozi wa kanisa wanaoeshimiwa zaidi katika karne ya makumi mbili. Graham hakwenda hupande kamwe toka kazi aliyoitwa kufanya na kama tokeo Mungu alimuthitisha haki na akamuinua.
Usiwe na hasira na kulipiza kisasi
Nilitaja hii juu lakini inahitaji kurudiliwa sababu hata kiongozi mcha Mungu anaweza kuanguka kwenye mtego huu. Hakika Musa alimaliza. Katika Hesabu 20:2-12 tunasoma jinsi watu walivyokuwa wakinung’unika na kulaumu Musa bila msingi. Ona vesi ya 4, Mbona mmewaleta kusanyiko la Bwana hata jangwa hili ili tufe huku,sisi na wanyama wetu ? Mungu anaamuru musa kusema kwa mwamba lakini kwa mvujo na hasira Musa ameupiga mwamba, sikieni sasa enyi waasi, je? Tuwatokezee maji katika mwamba huu ? Hesabu 20:10) hatujuwi kwa nini Musa alipotoka kwa kutohesimu na kuwaka hasira juu ya watu lakini tunaweza kuielewa. Manung’uniko yao ya kawaida na lawama lazima yalikuwa magumu
13 RT Kendall, Out of the Comfort Zone, (London, Hodder and Stought 2005) 140
49
zaaidi kishinda ; haasa tunapokumbuka kuwa wange kuwa katika nchi ya ahadi wakishangilia uzuri wake wakati ule. Ilikuwa ni watu kukosewa imani ambayo ilitokeza kwenye shida yao lakini walichukua kukaripia Musa kuliko kukubali jukumu juu ya matendo yao.
Ina onekana kuwa uchovu wa mwili nisehemu iliyochangia kwa huzuni ya Musa ya ghafula. Tunapo kuwa na mchoko ina weza kupotoa mwelekeo wetu na tunaweza kuchukua maamuzi na kuchukua hatua ambazo hatungazifanya tulipokuwa katika mwili na tayari kwa huzuni. Sheria inatowa mwaliko siku ya sabato kuwa ya pumziko na hili ni fundisho zuri kwetu sisi wanaoishi chini ya Agano Jipya.inasaidia kwa kushinda lawama vilivyo. Acha nami pia niongeze kuwa ni shauri zuri kutokuweka aumuzi maalum unapojisikia kugonjwa au kuchoka sana. Sehemu hizi zote mbili zinaweza kupotoa maamuzi yako na imani
Omba na tarajia Roho Mtakatifu kubadili hali
Maombi Ni chombo cha ajabu ambacho kinaruhusu Mungu kuleta mabadiliko katika hali fulani. Ombea wale wanaokulaumu. Unaweza kushangaa kwa yale Mungu atakayo yafanya.
4.6 Uwe Na uhakika viongozi wako wajuwa na roho Mtakatifu
Musa alivyokuwa akiwatendea wa Israeli kama inavyopendekezwa na Yethro yalikuwaa yenye kufanikisha sana na iliwezeshwa watu kuendelea mbele kuenda kwenye nchi ya ahadi. Walakini, tuliona katika Mwanzo 11 kuwa manung’uniko ya kila siku ya watu yalikuwa mengi zaidi kwa Musa na akamuambia Mungu “mimi siwezi kuwachukua watu hawa wote peke yangu kwakuwa ni mzigo mzito sana wa kunishinda. 15na kama ukinitenda hivi nakuomba uniulie mbali kwamba nimepata fadhili mbele ya macho yako nani nisiyaona haya mashaka yangu “ Hesabu11:14-15 jibu la Mungu ni la kupendaza, Kisha BWANA akamuambia Musa “nikusanyie watu sabini miongoni mwa wazee wa Israeli ambao wewe wawajua kuwa ndio wazee wa watu hawa wasi mame huko pamoja nawe , 17nami nita shuka niseme nawe huko, nani nitatwaa sehemu ya roho iliyo juu yako na kuiweka juu yao ;nao watachukua mzigo wa watu hawa pamoja nawe , ili usiuchukue wewe peke yako.” (Hes.11:16-17).mbele katika vesi ya 25 tunasoma kuwa “Ikawa, roho hiyo ilipowashukiya,wakatabiri, lakini hawakufanya hivyo tena.”
Hii ina niambia kuwa kadiri iliyo muhimu kuwa na muundo wa shirika ambao utahahidhisha kukua na kadiri iliyo ya maana kuwa na wacha Mungu, viongozi hodari kama sehemu ya kundi lenu, ni ya muhimu kuwa viongozi hawa ni wenye kujawa na Roho Mtakatifu, juu bila hii, utaona kuwa itanfanya kazi yote kuwa mzito na kuchelewesha kukua kwa kanisa.
Katika Matendo 6:2-3 tunaona fundisho hili likitiliwa katika matendo na mitume walipo azimu kuwa kanisa lichague wanaume saba kuhudumu mezani wakigabua chakula kila siku, wale thenashara wakawaita jamii ya wanafunzi, wakasema, haipendezi sisi kuliacha neno la Mungu na kuhudumu mezani. Basi ndugu, chagueni watu saba miongoni mwenu, walioshuhudiwa kuwa wema, wenye kujawa na Roho, na hekima, ili tuwaweke juu ya jambo hili, na sisi tutadumu katika kuomba na kuliudumia lile neno. Neno hili likapendeza machoni pa mkutano wote, wakamchagua Stefano, mtu aliyejaa imani na Roho Mtakatifu, na Filipo, na Prokoro, na Nikanori, na Timoni, na Parmena, na Nikolao mwongofu wa Antiokia, ambao wakawaweka mbele ya mitume, na walipokwisha kuomba wakaweka mikono yao juu yao. Kumbuka ilitakiwa kuwa wewe wenye kujawa Roho hiyo ni kuwa,lazima wangekuwa watu wakutumika na uwezo na zawadi za Roho.
Nina taka kuanza kila kikao cha kazi za kanisa na maombi na maabudu kuliko maobi mafupi ya kufungua juu hii inadhihirisha ukuu wa roho kwa vile tunavyovifanya. Hatufanye kazi kama mfano wa maamuzi tu lakini tunajaribu kugundua mapenzi ya Mungu katika kikao. Hii inafaa sana kwa makanisa, kama vile Wabaptist na Marafiki wa kinjili, wanao tumika chini mtindo
50
wa serkali ya jamii ya watu waabuduo. Ni muhimu kukazia kuwa makanisa haya hayaazimu kutumika chini ya utaratibu wa kidemocratia ambako kila mtu ana haki ya kusema yale wanayofikiri. Kanisa si democratia bali theocratic na christocratic, hayo ni, inatawaliwa na Mungu na Kristo. Mtindo wa jamii ya watu waabuduo inasimamia kwenye fundisho la Biblia kuwa kila mwamini ana roho ya Kristo na kadhalika kanisa, linapojiunga pamoja, linaweza kuakikisha yale Mungu anayoyasema. Kusudi la kanisa kukusanyika ni kudhihirisha roho wa Kristo kuliko kuacha kila mtu kusema yale anayotaka kusema. Kuanza kazi ya kikao sawa na hicho na muda murefu wa maabudu na maombi inatusaidia kufahamu fundisho lake.
51
Sura ya 5
Kufanikiwa kunaleta mabadiriko
5.1. Yampasa kiongozi kufanya mabadiriko.
Awali nilitaja kuwa moja rafiki yangu alienda uongozi kama: “kazi muhimu ya viongozi ni kuchukua watu kwenye nafasi mpya na bora zaidi.” Kwa ajili ya kufanya hivi yampasa kuwa na uwezo wa kufanya mabadiriko kwenye wakati unaofaa na katika njia inayofaa. Uwezo huu wa kufanya mabadiriko ni ile inayo tafautisha kiongozi na msimamizi. Msimamizi anaweza kushikilia programme moja kwa moja katika njia inayofaa na anaweza hata kuifanya kuwa inayofaa zaidi lakini anaendelea kuiendesha katika uelekeo ule ule. Viongozi wana uwezo wa kufanya mabadiriko kwenye wakaki unaofaa na katika njia inayofaa, makusudi shiriki lifikie kunako welekeo mwingine, moja ambayo ina faida na ya kufaa kwa matukio.
Makanisa na shirika za madini ingine hawaachiliwi na mafundisho haya na inawapasa kuongozwa na watu wenye uwezo wa uongozi na sio tu uwezo wa usimamizi ikiwa watazidi kuishi na kukua katika muda murefu. Shirika zote lazima ziwe zikibadirika wakati kwa wakati, sijuwe yoyote ile iliyo tofauti. Kabla ya computers kuweko kila ofisi ilikuwa haikosi chombo cha kuandika kwa chapa wakati ule shirika kubwa kubwa zilikuwa na chumba kinachojaa vyombo vya kuandika kwa chapa kinachojaa na karani wa kupiga vyombo vya kuandika kwa chapa wanaotokeza hati za maandiko. Vyombo vya kuandika kwa chapa havipo tena katika ulimwengu wa sasa vilibadirishwa na computers kwa matokeo ya kuwa kampuni ambazo zilikuwa zikitengeneza na kuudha vyombo vya kuandika kwa chapa lazima vibadirike au zisikuweko tena. Elimu inatuambia kuwa wa dinosaurs hawa kuzingatia shurti za mabadiriko katika ulimwengu kandokando yao na huku wakawa iliyozimika. Matokeo kama na hayo yanafikia kila shirika ambalo linakataa mabadiriko.
5.2 Badili taratibu lakini hapana maneno.
Acha niyaweke wazi toka mwazo yale nisiyotetea kuwa tubadili maneno ya biblia makusudi iwe ikubalike zaidi kwa watu wa kisasa. Hapana, mafundisho ya Yesu na Mitume ni yenye kufaa sasa kama yalivyokuwa katika karne ya kwanza na hayakubadirika. Yanayobadirika ni taratibu tunazotumia kwa kunena manano hayo. Aina ya muziki tunaotumia, jinsi tunavyotumia ulimi wetu, mahali na wakati tunapokusanyika kwa kuabudu na jinsi tunavyo vaa ni moja wapo wa mambo ya msingi ambayo lazima yaendelee kubadirika makusudi kanisa lipate kutoa injili vipasavyo katika njia inayofaa.
Inapendeza kujua kuwa wakati Royo Mtakatifu alipowaongoza mitume kuandika vitabu vya Agano Jipya, walichagua Koine (kigiriki cha kawaida) kuliko kile kinacho kwatuka cha wasomi. Kigiriki Koine ilikuwa ni lugha ya mchanganyiko wa watu na kwa iyo kanisa la zamani lilichagua kutoa injili katika njia ya elimu inayofaa tangu mwanzo. Wangeweza kuchagua kuandika katika kiebrania wakitoa hoja kuwa ndio lugha Mungu aliyotumia kwa kuwapa wa Israeli Amri kumi na kwa hiyo ilikuwa ni lugha takatifu. Wangeweza kuchagua hata kigiriki cha wasomi kwa msingi wa kuwa kizuri zaidi na kwa hiyo chombo kinachostaili zaidi kwa kujulisha kindani ukweli wa kiroho.lakini hawakufanya hivyo, walichagua lugha ya watu. Wakati wasiyoamini waliposikia injili au walipoenda kwenye kusanyiko la maabudu hawakuwa wanapambana na kitu ambacho kilikuwa tofauti na asili ya vile walivyokuwa wamejua katika maisha yao ya kila siku.
Nina amini mafundisho hayo yanaweza kutumiwa leo. Shabaa moja la kukua kwa makanisa ya kituo cha maisha ya wakristo (Hillsong) pa Australia ni kuwa walifikiria kubadiri musiki wao, maabudu yao, mitindo ya mavazi na yanayofanana na hayo makusudi walisha kuwa
52
wakati huu. Maneno wanayo hubiri ni maneno ya Biblia, na hii ni kwa wakati mdogo, lakini inatolewa katika njia ambayo inafaa kiasili kwenye jamii za watu wanao wazuguuka.
Kwa bahati mbaya, kundi zimoja za kanisa kwa utashi wao wakuwa wenye kufaa, wanabadili maneno kwanza. Kwa mfano, wengi katika nchi za Magaribi wanaona wazo la Jehanum kuwa lisilokubaliwa na kwa hiyo makanisa hayo yanafundisha kuwa hakuna Jehanum. Wanaeleza sana miujiza ndani ya biblia kwa ajili ya kuifanya ikubalike zaidi kwenye dhamira za akili. Wana weka makuani na ma askofu wanaojamiana wao kwa wao au wanashindwa kuazibu mchungaji aliyezini. Wana achia mbali wazo lakuwa biblia ni neno la Mungu pasipo kosa na ni mamlaka yetu ya juu zaidi katika mambo yote ya imani na desturi. Wanafikiri vibaya zaidi kuwa kubadili maneno ya biblia itawafanya kuwa wanaofaa zaidi. Kaguo la kukua kwa kanisa linaonyesha kuwa yaliyo mbalimbali kabisa ni kweli. Ni maneno ya biblia ambayo iliyo yakufaa na tunaachana nayo kwenye kifo chetu.
Tuna hitaji kujua kuwa maneno ya injili kila mara yalikuwa yakigombana na asili ya kidunia na tungebadili maneno yetu makusudi watu wapate kutukubali upesi zaidi. Walakini, inatupasa kubadirisha taratibu zile tunazotumia kwa kutoa injili ya “Kristo aliyesulubiwa” kuliko taratibu zetu zinazofaa za asili. Ona 1 Wakorintho 1:23-24, bali sisi tunamhubiri Kristo, aliyesulibiwa; kwa Wayahudi ni kikwazo, na kwa Wayunani ni upuzi; 24 bali kwao waitwao, Wayahudi kwa Wayunani, ni Kristo, nguvu ya Mungu, na hekima ya Mungu. Linganisha hii na 1 Wakorintho 10:32-33, Msiwakoseshe Wayahudi wala Wayunani wala kanisa la Mungu, 33vile vile kama mimi niwapendavyo watu wote katika mambo yote, nisitake faida yangu mwenyewe, ila faida yao walio wengi, wapate kuokolewa.
Tunahitaji kufanya nguvu zote kwa kuakikisha kuwa taratibu zetu zinazofaa na mwenendo usio wa kibiblia havizuie kukua kwa kanisa
5.3. Kwa nini inatupasa kubadirika.
Kuna sababu tatu muhimu zinazopelekea kanisa kubadilika
 Eneo kandokando yao inabadirika,
 Kitu kimoja nikisichofaa katika kanisa,
 Kila kitu kinaenda vizuri lakini mabadiriko lazima yaweko kwa kuakikisha kuwa kukua kunaendelea.
Acha tuangalie kwenye kila moja ya pointi hizi kwa maelezo zaidi.
 Kwanza, kanisa linahitaji kuwa lenye kufaa kwa jamii yake lakini ikiwa jamii inabadirika ndipo kanisa linahitaji kubadirika sambamba nayo. Kwa mfano, kanisa linalopatikana katika eneo la utendaji wa wasomi litakuwa tofauti kwa lile linalo patikana katika wilaya ya kabila maskini na ikiwa eneo la kanisa linabadirika kutoka moja kwa lingine basi kanisa linapaswa kubadirika pamoja nalo. Taratibu zinazotumiwa katika eneo la kabila maskini zitakuwa tofauti na ambazo ingetumiwa katika eneo tendaji la matajiri.
Kuna mara nchi mzima itabadirika. Babangu alinizungumzia mara moja kwamba munamo karne ya 1920 hadi 1930 watu waeshima walikuwa wakishiriki kanisa Jumapili jioni huko Australia hata ikiwa walikuwa hawajazaliwa mara ya pili. Hii iliwezesha kanisa za injili kupata nafasi ya kuhubiri injili kwa idadi kubwa la watu wasiookoka ; kitu kimoja ambacho kinatokea kwa waongofu wengi. Walakini, munamo karne ya 1950 hadi 1960 hii ilibadirika na watu wasioamini waliacha kuja kanisani kwa msingi wa taratibu. Wamoja walitupilia mabadiriko chini kwa shindo la vita vya 2 vya ulimwengu kwenye mafikiri ya watu wakati wengine walitazamia kuanzisha television na raha ya kukaa nyumbani wakitizama sinema zuri ; hasa wakati wa kibaridi cha usiku. Kwa sababu yoyote ile, hali inabaki kuwa mazoea ya jamii iliyo badirika, na kanisa vile vile ilibidi libadirike. Bahati mbaya, kanisa nyingi hazikufanya hivyo na zinaendelea kuzingatia kawaida yao ya ibada za injili Juma pili jioni
53
juu ya watu wasiyo wa jamii ambao walikuwa hawaje tena. Kufanyiza makanisa kubadirisha fikira zao makusudi waende nje katika jamii kwa kuchangia na wasioamini ilikuwa vigumu sana kwa wengi kukubali.
 Kiongozi pia anahitaji kufanya mabadiliko kwa ajili ya vitu visivyofaa vinavyojitokeza kanisani. Pengine shughuli zimoja kanisani zinatendeka katika njia inayoleta fedheha kwa kanisa au pengine ni isiyofaa tu na anajitwalia kiwango kikubwa mno cha malipo ya ufundi na pesa ambazo zingetumika penginepo. Inayofuata ni matatizo kweli pamoja na makanisa ya Magharibi ambayo yameanzishwa kwa muda. Kujaribu kutangua shughuli ambayo imetendeka kwa miaka mingi kuna mara inaonekana kama vile ukufuru lakini mara nyingi ni vizuri ikiwa kanisa linaendelea mbele na linahubiri jamii lake vipasavyo.
 Mara kwa mara mageuzi yana hitaji kuanzishwa sababu kila kitu kinatendeka vizuri. Hii ni hali iliyo kuweko katika Matendo 6 ambako wale kumi na wawili iliwabidi kugeuza muundo wa shirika lao kwa kuchagua watu saba kwa kuhusika na mgao wa chakula kila siku. Yawezekana kanisa la mahali linakua kwa kasi kadiri inafikia kuwa vigumu kwa watu wote kuenea katika jengo kwa wakati moja. Katika hali hii inambidi kiongozi kuamua ni taratibu gani la tendo la kuchukua na ndipo anashawishi watu kumfuata katika uamuzi huo. Ana idadi ya chaguo. Anaweza kuongeza huduma nyigine, kupanua jengo, kuanzisha kusanyiko la pili katika jengo lingine au kusimika makanisa mengine dada inje la hilo kanisa linatutangulia.
Kila anachokusudia kukifanya ni mageuzi na inamubidi kutokeza mageuzi. Kiongozi akikusudia kutofanya lolote, kwa sababu anaogopa yale watu wanaweza kusema au kufanya au sababu matatizo yanaonekana kuwa mengi, hapo hali yawezekana kuwa mbaya zaidi. Hata ikiwa mageuzi yanahitajika kwa sababu bayana lazima ataendelea kufanya kitu kama sivyo vitu vitapinduka kando na kuharibika.
Acha niwapeni mfano wa pointi iliyo tangulia. Nina jua kanisa moja katika mji wa nchi ya Australia ambalo lilikuwa linapanua kwa haraka kupitia kukua kwa wongofu na huenda ilikuwa kanisa kubwa zaidi katika dhehebu lake nje ya mji mkuu. Ilikuwa na uhusiano wa juu zaidi wa watu waliokuwa wakikusanyika kulingana na watu wa eneo lake wa kanisa lolote katika taifa lao. Ikiwa na ibada mbili siku ya Juma pili moja asubui na ingine jioni. Kanisa lilikuwa likijaa katika ibada zote mbili, viti vilijaa kwenye sehemu za kanisa kwa marefu na kuzunguuka pande zote kwa kukaribisha watu wote. Hapo kulikuweko na mabishano mengi kuhusu nini waweza kufanya lakini mwishowe kanisa ambalo lilikuwa linasimamiwa na aina ya jamii ya watu waabudua wanaongozwa kiserkali, likaamua kutofanya kitu. Munamo miaka michache kanisa lilichakaa kimaajabu na mara nyingi ilikuwa ikijaa sehemu moja
Kwa nini haya yalitokea ? kulikuweko na idadi ya mambo.
 Watu wamoja waliacha kuja ikiwa hawakuja haraka na kuchelewa kidogo sababu walijua wasingekuwa na uwezo wa kupata kiti bila kufanya kelele.
 Watu hawa mara nyingi waliacha lote kushiriki sababu ilikuwa rahisi kukaa nyumbani kuliko kusukumana kwa kupata kiti.
 Ilipoteza bidii yake ya kuhubiri sababu watu walijua kuwa ikiwa wataalika rafiki zao hawatapata kiti pamoja.
 Hii ilituma inapoteza msisimko wake juu ya kuona watu wapya wanaokolewa na kuongezeka kanisani.
 Mara lilipoteza msisimko wake juu ya kutangaza injili na kukua ikaanza kuangalia ndani na kuchekwa na wengine kanisani na juu ya kanisa kwa jumla
 Mara hii ilitokea hesabu yake ikashuka zaidi.
54
Ninakumbuka nilizungumza na mtu muhimu kanisani miaka miwili baada ya azimio kuchukuliwa la kutokufanya kitu na alionekana kuwa mwenye kusikitika kwa vile kanisa lilivyo chakaa. Alisema kuwa alifikiri matatizo ya kupunguka kwa hesabu ilianza wakati walipochukua uamuzi potevu wa kutokuwa na ibada lingine au kupanua jengo. Aligundua jinsi matoleo yalivyoanza kupunguka na wahuzuriaji kupungua kwa mambo mengine, pamoja na ukame ambao ulikuwa unashika taifa kwa wakati ule, lakini kwa kuangalia nyuma alitambua kuwa ilikuwa ni uamuzi wa kutokufanya kitu hiyo ilikuwa ndiyo sababu ya matatizo.
5.4. Inampasa kiongozi kuwa wazi kwa mabadiriko
Kukua kunahitaji mabadiliko na inampasa kiongozi kuwa wazi kwa mabadiriko ikiwa kanisa liko linakua. Ninapenda usemi unaosema kwamba, “ watu wamoja wanakufa kwa umri wa 30 lakini wanazikwa kwa umri wa 70 ”. hiyo ni kwamba, watu wamoja wanapoteza nia ya kubadirika wakati wangali na umri wa 30 na bila mabadiriko hakuwezi kuwa kukua. Bila kukua hakuwezi kuwa nguvu na msisimko katika maisha. Watu hawa wanajifunga wenyewe kutoka kitu ambacho kinge wahitaji kuingia katika mabadiriko na kwa hiyo wanapungukiwa juu ya yote Mungu anayo kwa ajili yao katika kipindi kinachofuata cha maisha yao, tayari wamekufa ingawaje wangali hai.
Kuna usemi mwingine ambao niliyouona kuwa wa kweli, “ waasi wa serikali wanakuwa wenye kupinga maendeleo ”. hii ina maana ya kuwa watu ambao walikuwa wenye bidii kwa ajili ya mabadiriko walipokuwa wangali vijana mara walipinga badiriko lote kama vile walisha zeeka, hasa inapohusu kubadirisha juu ya yale wanayofikiri katika ujana wao. Hiki ni kitu ambacho wachungaji wanahitaji kujihadhari nacho. Musiki ni mfano zuri wa hii. Wachungaji wanaweza kupinga jaribio lolote la kuingiza musiki wa kisasa katika ibada la maabudu ya kawaida hataikiwi walishauriwa kitu hicho hicho walipokuwa wangali na umri wa kati ya miaka kumi na shirini.
Ninapenda haya maneno toka Mwenyekiti wa kundi la kampuni William A. Hewitt, ” Kuwa kiongozi unapaswa kuhifadhi yote kupitia maisha yako tabia ya kuwa mpokeaji wa mawazo mapya ”.14 uwe na uhakika kuwa unajiweka mwenyewe katika hali ya kupokea mawazo mapya. Ujiweke wazi mwenyewe kwa watu wanaofanya vitu vikuu kwa Mungu, sikiliza kwa yale wanayo yakusema, tazama kwa yale wanayoyafanya, fikiri kupitia yale unayoyaona, chagua au fanyiza ile ambayo ni ya lazima.
5.5. Watu wanapinga mageuzi hayo yanafikia tu kukiweko na uwezekano
Watu wanapinga mageuzi na wanayapinga kwa sababu nyingi. Mtu mmoja alisema kuwa wanadamu ni viumbe wenye tabia na kitu chochote ambacho ni tafauti kwa yale waliyoyazoelea ni yenye kupinga kwa sababu hii. Si kitu kama ni kwa ajili ya wema wao au sio. Wanaendelea kuipinga. Hawafanye hivo tu sababu wanaikataa lakini mara nyingi watajiweka wenyewe katika mageuzi makubwa katika mafuatano ya mambo. Rafiki yangu alikuwa akitumika kwenye kampuni ambayo ilikuwa karibu ya kupangilia taratibu ya ofisi yake lakini mbele yao kuanza msimamizi wake alimuonya kuwa watu wamoja wangetoka kwenye kampuni kama matokeo ya mageuzi. Rafiki yangu alionyesha shaka kuwa watu wangefanya hayo lakini karibuni nyuma walipo maliza mageuzi watu wamoja waliondoka kwa ajili ya sababu hiyo.
Watu hawapingi mageuzi sababu wanakuwa wabuni wa tabia lakini sababu wanaongopa yale mageuzi yanaweza kumaanisha kwao. Itakuwa zuri kwao au mbaya zaidi ? Watu wanaogopa wasichokijua na ni juu ya hii ni muhimu kwa kiongozi wa kanisa kueleza faida za mabadiriko na kwa nini wanayafanya wakati kanisa nililokuwa nikishiriki miaka michache iliyo pita walikusudia kuongeza ibada ingine asubuhi kwa kuzuia tatizo la msongamano ; uongozi
14 Maxwell Developing the Leader within You 51
55
ulitumia karibuni miezi mitatu wakieleza kwa nini walikuwa wakipendekeza ibada la pili na faida zitakuwa nini. Kama tokeo la hii, mpito ulikuwa wenye kurizisha. Ghafula walitangaza juma pili kuwa kuanzia Jumaa lijalo, hapo kutakuwa ibada mbili asubuhi, kila moja ikianza wakati tofauti, na kuwa watu wana uhuru wakuamua katika jumaa ni ibada lipi wanalotaka kulishiriki, nina uhakika mabadiriko hayangekuwa kadiri yalivyokuwa yamefanikiwa.
Walakini, kawaida mabadiriko yana ukubwa uliyo kinyume kabisa kwa iyo sababu watu kwa desturi wanakataa mabadiriko. Hii ina maana ya kuwa kiongozi lazima ahakikishe kwamba hakuanzisha mabadiriko kwa ajili ya mabadiriko tu. Mabadiriko lazima yafikiriwe na inapaswa ionekane kuwa itakuwa na faida kwa kanisa kabla ya uongozi kuyaanzisha. Mageuzi mengi zaidi bila hata matokeo moja yenye faida itakuwa ni kutia kanisa katika hatari sababu ya ukubwa uliyo kinyume kabisa ambao kila mara unaisindikiza. Tunapochukua tena maneno ya William A. Hewill, “ tabia ya uongozi utakayopana itafuatana na uwezo wako wa kukagua mawazo mapya, kutofautisha mabadiriko kwa ajili ya mabadiriko kutoka mabadiriko kwa ajili ya watu ”.15
Acha tukubali kuwa kuna mpango ndani ya kanisa ambao haufanane kutumika na uongozi unakadiriwa kwamba wanapaswa kuamua lakufanya kwa ajili ya mpango huo. Lazima tufikiri gharama zote mbili ya kuacha au kuibadirisha kimchezo na gharama ya kutofanya kitu chochote. Mara nyingi mipangilio ya kanisa inaweza kuhitaji kukombolewa au kubadirishwa kikamilifu sababu walipoteza nguvu zao na wanatumia muda mwingi mno na nguvu. Mara kwa mara wanazuia mpango mzuri kuanzishwa mahali pake. Ikiwa azimio limesimamishwa watu wamoja wataumia na kujisikia kukataliwa na inawezekana wanaondoka kanisa hata ikiwa hali inazuiwa na uelekevu mkubwa zaidi wa uongozi. Mara nyingi hii ni bei tunayolipa kwa ajili ya kuona kukua bayana ndani ya kanisa zetu.
Acha nirudi kwenye kanisa lile la nchi ambayo ilikusudia kutokufanya kitu chochote juu ya tatizo lake la msongamano. Hitaji la kubadirika na kufanya kitu kilichotofauti ilikuwa ni kupambana kamili ikiwa kanisa lilikuwa likiendelea kukua. Walakini, walibadirika na kuanzisha ibada zingine. Nina uhakika kwamba hesabu ndogo ya watu wangekataa mageuzi na kuondoka kanisa. Hii ni busara inayopendeza katika asili ya mwanadamu. Walikataa mabadiriko lakini kwa kufanya hivyo walijitia wao wenyewe katika mabadiriko makubwa ; mmoja aliondoka na kwenda kutafuta kanisa mpya.
Mabadiriko yatatokea lakini uongozi wa kanisa unahitaji hekima kwa kujua nini cha kubadirisha na nini chakutokubaridisha. Wanahitaji pia hekima kwa kujua wakati gan i wa mabadiriko. Kukamilisha mda inaweza kuwa muhimu zaidi kama mabadiriko yenyewe.
5.6. Watu wanapaswa kukutumaini kabla ya pale watakapo kufuata na kukubali mabadiriko
Kufanya mabadiriko katika shirika la kujitakia kama vile kanisa, watu wanapaswa kutumaini kiongozi. Wanahitaji kujua kuwa uko mtu wa haki hasiyefanya haya mabadiriko kwa manufaa yake lakini anafanya yale anayofikiri kuwa bora zaidi kwa kanisa lote. Wanahitaji kujua kuwa una wapenda na wanajitolea kwao na wana faida yao moyoni. Kama tulivyotaja awali, “ Lazima uwapende kabla ya kuweza kuwaongoza ”.
Nina weza kukumbuka nilisoma waraka juu ya kukua kwa kanisa miaka iliyopita ambamo nilikuta kuwa makanisa mengi hayakukua hadi pale mchungaji alipokuwa pale miaka tano au sita. Tumaini la waraka lilikuwa la kuhimiza wachungaji kukua makanisani mwao kwa muda murefu na sio kutoka mapema mno. Mafikiri yangu mwenyewe kama vile kwa nini makanisa haya yalianza kuishi kukua kikamilifu nyuma ya kipindi hicho cha wakati na sio mbele, hiyo
15 Maxwell Developing the Leader within You 51
56
ndiyo iliyokuwa miaka ya kutetea iliyopea watu nafasi ya kuweza kujua mchungaji na kwa hiyo walimutumaini kufanya mageuzi.
Nina amini kuwa ni kinyume cha kukua kuwa na wachungaji wanaobadili makanisa baada ya kila miaka mitatu ; muna hitaji muda zaidi kuliko huo kwa kupata tumaini la watu na kuona kanisa linakua kikamilifu. Nina kumbuka tukuwa na mchugaji moja miaka ilio pita ambaye, kipindi alipokuwa na mazugumuzo na mke wangu nami peke yangu,alisema kuwa ange stafu munamo miaka ingine kumi na nilinjisikia kuwa angekuwa mchugaji kwa miaka ingine mitatu tu. Nilipo fikiri juu ya hiyo nilifikiria kuwa alikuwa “ msimamizi ” aina ya mchungaji kwa hili hiyo alishikilia kanisa akiliongoza lakini hakukuwa kamwe kukua halisi katika makanisa aliokuwa akiyasimamia,hakika sio tu wale ninao wajua. Labda sababu yake ya kukaa miaka mitatu tu ilikuwa alijua hakuwa na kitu cha kuwatolea watu njuma ya wakati huo. Kuliko kupangilia kuondoka angejitaidi ‘kujiendelaza mwenyewe’ makusudi afikilie kuwa kiongozi anayetokeza mageuzi,yanayo wezesha kanisa kukua.
Nina jua wachungaji walikwenda kwenye makanisa wakiwa na mipangilio mikubwa lakini ilifikia kufika sababu watu hawakuwa nyuma ya maono yao.tatizo leo ilikuwa maradufu :
 Kwanza, hawakuelewa uongozi. Uongozi ni kufanya watu waweze kukufuata, sio tu kukuza makusudi na kutoa oda.
 Pili, hawakupangilia kukuza tumaini kwanza pamoja na watu wao. Tumaini lilikuwa haba, ikiwa lote imefikia ghafula, inachukua muda, labda miaka mingi. Ikiwa kanisa lilipasishwa wachungaji kwa haraka, kila mmoja akienda kwenye kanisa kubwa upesi iwezekanavyo kama cheo kilivyo tolewa kwake, ndipo inaweza kuchukua miaka mingi kwao kuona kuwa munajitoleo kwao kuliko kuwatumia kama ubao wa kujisaidia kuruka kwenye kanisa kubwa lenye wingi wa neema.
Tumaini lina tuhitaji kukuza uhusiano na watu, hasa viongozi muhimu. Haya yanapotokea na watu wanapoona kuwa uko mtu wa tabia bora anayewapenda, watakutumaini na kuwa na nia ya kukufuata. Ndipo unaweza kuonyesha maono na kufanya mageuzi bila tatizo kabisa. Ufunguo ni kukuza hayo mawasiliano.
5.7 Watu wanakubali mageuzi kwa hali tofauti
Siku zangu za kazi ya kutengeneza mtambo na machine nilijifunza kuwa wakati mazao ya ufundi yanapo tolewa kwenye soko ukubalifu wake mara kwa mara unafuata tao la kengele. ‘waanzilishi wa mambo mapya’, wanao wakilisha asilimia ndogo ya soko, wataitumia mara mojo. Karibu nyuma ya hayo ‘waliokubali mapema’ wataanza kuinunua. Hawa watu ni wengi kuliko waanzilishi wa mambo mapya lakini hasilimia za soko ziliopo ni ndogo. Nyuma ya hii kunakuja ‘waliokubali wa kati’ ambamo kati yao uwingi wa watu unapatikana, halafu ‘waliokubali nyuma’ na mwishowe ‘wazembe’. Kinachopendeza, hidadi ya watu wanao tumia bizaa ina anza kushuka wakati wamoja wa wale waliokubali wa kati ndipo wanaanza kuitumia. Shabaa ya hiyo ni kuwa wakati waliokubali nyuma na wazembe bado hawaja toka na kwenda ngambo, waanzilishi wa mambo mapya na wanaokubali mapema waliacha kuitumia na wameenda katika hatua inayofuata ya kuendesha mbele elimu na habari ya ufundi.
Tangu ukubalifu wa bizaa unapotegemea kwa vile watu wanafikiri na jinsi wanavyo kubali mageuzi, tunaona kuwa watu wamoja watachagua haraka wazo mpya wakati wengine wana chukua mda mrefu zaidi mbele ya kuikubali. Tunajifunza nini kutokana na haya ?
 Ikiwa una kusudia kuendelea mbele na wazo mapema zaidi basi watu, isipokuwa walio wachache kabisa, papo hapo watatupia mbali wazo hilo.
57
 Ikiwa unachunga kidogo lakini ingali tu mapema mno, muna hatari ya kupasuka sababu kubwa watu wanakubali wazo lakini pia idadi kubwa inakataa.
 Walakini, usifikiri kuwa kila mtu atakubali mabadiriko mbele ya wewe kufanya hayo mabadiriko. Hii inaweza kuwa hatari, sababu wakati munapokuwa mukichunga wazembe waikubali, waanzilishi wa mambo mapya, wanaokubali mapema nawa kati watakuwa wasio vumilia kuwa wanafanana kuondoka kanisa na kwenda munamo lingine analoliona linasonga mbele. Viongozi wengi muhimu kwa kawaida wanatoka katika kundi hili na hauwezi kuwafanya kuondoka kwa wingi. Ikawa mungali munaendelea kuona watu kama wanakataa mageuzi na kungoja kila mmoja kukubali wazo ,watu hawa huenda wasijiunge nanyi kamwe.
Una hitaji asilimia ngapi ya wanao kubali wazo kabla ya kujaribu kuanzisha mageuzi ? hayo yanafuatana na jinsi watu wanajisikia uchu mwingi juu ya mageuzi. Sio tu hulizo la wangapi wanao kubali mageuzi lakini pia ni wangapi wanaokataa mageuzi na nguvu gani wanazo wale wanaokabiliana nayo wanavyo jisikia juu yake mara kwa mara kuna kundi la watu, pana siku waliyo imara sana, wasio na msimamo mkali kwa njia moja au nyingine, na kujionyesha wana kutumainia, watafurai kwenda pamoja na yule unayependekeza. Unahitaji washawishi kamili, aghalabu karibuni 20%, kwa kuwa upande wa mageuzi kikamilifu. Basi ni jambo la kulinganisha ni wangapi wanao kataa wazo na kujaribu kuakikisha ushawishi gani watakuwa nao juu ya kundi wasio kuwa na mtazamo imara kwa njia moja au nyingine. Endelea mbele na mageuzi wakati wewe na wapinzani wako muhimu munafikiri inakuwa wakati muhafaka wakusonga mbele.
Kumbuka, watu wamoja siku zote watalaumu mchungaji bila kujali yale anayo yafanya, kwa hiyo usidhani kila mtu kuwa nyuma yako na kwa upande wa wale unao azimu. Ufunuo ni kuelewa ni nani aliye katika kibali. Ikiwa ni uongozi wa msingi na karibuni watu wote wanao jitolea ndipo itakuwa labda wakati muhafaka wa kusonga mbele lakini ikiwa wengi wa watu wanao jitolea wangali na mashurti basi unaweza kutumia muda zaidi ukieleza na/au kubadili wazo. Usisahau kuwa watu wana hitaji muda kwa kukiri wazo, kwa hiyo usiwakusudiye kufanya uamuzi mkubwa bila wakati maalum kwa kuitumia na kuikubali.
Unajua watu nyuma ya mageuzi wanapokuwa wakitumia maneno, ‘sisi’, ‘yetu’, ‘yangu’, kuliko ‘wao’, ‘ninyi’, ‘wale’, … kwa mfano, acha tukubali kuwa unakusudia kupanua jengo lako kwa kukaribisha watu wa ziada. Unataka watu wawe ‘wakisema,’Tunaenda kupanua ’ kuliko ‘wanataka sisi tupanue’. wakati watu wanasema sisi kuliko ‘wao’ , au ‘yangu’, kuliko ‘yenu’ munajua walikiri mageuzi na wapo tayari kuendelea nayo.
5.8. Watu siku zote ‘wanachagua’ njia moja au nyingine.
Nilikuwa mchungaji wa Baptist kwa muda fulani na kwa hiyo nina uzoefu wa kielelezo cha jamii ya watu wa utawala wa kanisa ambako kikao cha kazi ya kanisa kinahitaji kutoa idhini kwenye maamuzi mengi kwa kuchukua taratibu ya uchaguzi. Wabaptist na Marafiki ni mifano ya hii aina ya utawala. Namna zingine za utawala wa kanisa inachukua taratibu ya machaguzi munamo mkutano wao wa Baraza lakini sio pamoja na jamii la watu waabuduo, wakati wengine wanajivuna wenyewe kwa kutokuchagua kamwe.
Kitu kimoja nilicho gundua kupitia miaka yangu katika makanisa zenye namna nyingi za utawala ni hayo siku zote watu watachagua njia moja au nyingine. Katika ma kanisa za Baptist/marafiki wanachagua kwa mikono yao wakati taratibu ya uchaguzi inachukuliwa lakini watu wanachagua pia katika makanisa mengine ; kawaida kwa miguu yao. Kwa hii nina maanisha kuwa ikiwa awakubaliane na kitu kimoja, na hawana taratibu la mkutano ambamo wataeleza mawazo yao, watachagua kwa miguu yao bila kushikilia yaliyo kusudiwa. Hawatahudhuria tu bila magumu.
58
Niliwasikia wachungaji wengi katika makanisa ambazo hajichukue taratibu za machaguzi wakinung’unika kuwa watu hawapo nyuma ya maono yao na maazimio. Hawaelewi kwamba watu siku zote watachagua kwa madhumuni yao na kwa hali hii walichagua kwa miguu yao bila kushikilia ni nini mchungaji alicho kitia mbele.
Hanipo nina shauri makanisa yafuate mfano wa jamii ya waabuduo kwani nina pinga desturi kama na hiyo lakini ninayoyasema ni kwamba wachungaji wanahitaji kuelewa mafundisho ya mageuzi yanayofaa makusudi watu wanapochagua, wala katika kikao kawaida cha kazi au kwa miguu yao, watasindikiza azimio za mchungaji. Kukataa kwangu hasa kwa ‘mfano wa jamii ya waabuduo’ ni kwamba ni kubwa kwa maelezo, na kikweli hapo kuna ushawishi unaotosha katika Agano Jipya kwa kuisindikiza, lakini kwa mazoezi mara nyingi ina dhoofika kwa namna ya democratia ambako kila mtu anafikiri ana haki ya kusema kila kitu wanacho kitaka. Kama tokeo, kinyume kabisa, nia ndogo, waoga kanisani mara nyingi wana songwa na kila jaribio la kuendea. Mara nyingi hicho sicho kisa cha ‘kusikiliza Roho Mtakatifu ili tupate kuthibitisha roho ya Kristo’ lakini njia ya kuendea ambako watu wana weza kuwa na uhakika kuwa wana ingia kanisa kufanya wanalolitaka. Walakini, mnapaswa kusema kuwa nilikuwa katika makanisa mamoja makubwa ya Baptist ambazo zilikuwa zimepita kiasi cha “ kupea kila mtu nafasi ya kusema kila wakitakacho juu ya kila jambo ”, kwenye jamii ya watu linalotafuta roho wa kristo.
Changamoto kwa wale wanaotumika chini ya mfano dhehebu ni kusikilia roho ya Agano Jipya makusudi kanisa lisianguke katika matope katika kusumulia kila habari yote ya kazi lakini msikilizeni Roho Mtakatifu na mtende kwa huyo. Matendo 13 :1-3 ni mfano mkubwa wa vile kusanyiko la kanisa linaweza kuwa. Ni dhahiri kuwa makanisa makubwa ya Baptist yaliyo na maelfu makumi ya wanamemba walipita kiasi cha ‘’kupea kila mtu nafasi ya kusema kila wakitakacho juu ya kila jambo’’, kwa hiyo ni visivyowezekana kwa vyovyote wakati kanisa ni kubwa mno.
5.9. Musichague isipokuwa muna uhakika wa matokeo
Hii inatumiwa hasa kwa makanisa ambayo yana aina ya kidhehebu ya utawala lakini fundisho linatumiwa pia kwa makanisa mengine, hata yale yaliyo na ‘aina ya kwa chini’ aina ya utawala. Nina pendekeza kuwa musipeleke kitu chochote kwenye uchaguzi hadi mtakapo hakikisha matokeo. Ikiwa munamashaka, basi muna hitaji kuwasiliana zaidi pamoja na watu wanaohusika hadi mnapo tumaini kuwa muna jibu ambalo litaenda kukubaliwa na walio wengi zaidi. Kushindwa kufanya hivi matokeo yatakuwa tu uharibifu hali ya pata /poteza.
Tuna hitaji kuwa watu wanao jitolea kwenye hali ya pata/pata. Hayo ni, pande zote mbili pata kama vile tokeo la uamuzi. Bahati mbaya, kuchangua juu ya jambo kunapelekea kwa kutokeza hali ya pata/poteza kwa wale walioenda upande wa uchaguzi wa walio wengi walipata, wakati wale walio chagua kushindana nao, walipoteza. Watu hawapendi kupoteza, hasa wakati inapotokea kwenye msingi wa kawaida. Hali ya pata /poteza ina elekea kutokeza mzozo wa kudumu ambao sio zuri kamwe kwa kanisa au kwa shirika lolote lile.
Nina amani kuna vitu vya kujifunza kutokana na hii:
 Endesha uchaguzi kwa kadiri iliyo ndogo iwezekanavyo. Muchague tu kwa yale yaliyo muhimu kabisa. Zaidi munavyo chagua zaidi hali za pata/poteza munatokeza mzozo zaidi ambao munaotaka kutokeza.
 Ikiwa mutachagua, musiufanye hadi mtakapokuwa na uhakika ya kuwa utapita na uwingi mkubwa, na yanasababisha madhara madogo sana. Nina penda kuona kuchagua kama njia kawaida ya kuhakikisha yale tuliyo yakubaliana. Kumbuka, kuwa watu wamoja sikuzote watakabiliana nawe na mazaifu mara yatajitokeza kwa baraza kwa yeyote ule, lakini muwape watu wakati wa kukiri mageuzi.
59
Fundisho hili pia linatumiwa kwa makanisa yasiyo na utawala wa kidhehebu. Kumbuka, watu sikuzote wanachagua njia moja au nyingine, kwa hiyo usianzishe mageuzi makubwa hadi utakapojua kuwa watu wakutosha wali ‘chagua’ katika fikira zao juu ya mageuzi na wata yasaidia.
5.10. Ufunguo mkubwa kwa kufaanikisha mageuzi: “shawishi washawishi muhimu kukusaidia kwanza”.
moja ya funguo muhimu zaidi ambayo nilifunza kila mara kuhusu kufanikisha mageuzi kama mchungaji ilikuwa ni kushawishi washawishi muhimu upande wako kwanza. Nilisoma kitabu kimoja miaka mingi iliyopita ambacho kilinisaidia kuelewa sababu zilizo nyuma ya hii. Nililinganisha kanisa ndogo na kabila na nikaeleza hali tatu ambazo naweza tu kukumbuka mbili; sultani wa kabila (mfalme) na tabibu. Sultani wa kabila (mfalme) ni mtu aliye kiongozi wa kabila na anayetarajiwa kuwa na utawala wa kabila. Tabibu haonekane na kabila kama kiongozi lakini mmoja anaye imarisha matatizo yao wakati kuna kitu kinachoenda kombo.
Katika kanisa ndogo sultani wa kabila kwa kawaida ni mtu muhimu wa kazi ambaye Alisha fanya siku nyingi kanisani na ni mshawishi mkuu. Kwa kawaida anachukua cheo cha mtu wa kwanza wa kazi kama vile ‘mwenyekiti wa baraza la wazee/mashemasi’, ‘katibu wa kanisa na kama hao. Mchungaji katika mfano anaonekana kama tabibu, mmoja anaye angalia nyuma yao na kuimarisha matatizo yao. Pana siku mpango huu kwa kawaida sio wazi wakati mwengine ni wazi. Nina kumbuka mahojiano niliyokuwa nayo na kamati ya uchungaji wa kanisa kubwa dada, walio niambia kuwa ikiwa nilikubali cheo cha Mchungaji wa kwanza walitaka niwe nina tumia wakati wangu kwa kuhudumia katika jamii wakati wanapoendesha kanisa. Sio kusema, sikukubali cheo.
Simama na uwaze juu ya kanisa lako mwenyewe. Je! Ina sultani wa kikabila ambaye anaongoza kazi kubwa ya ushawishi pamoja na watu? Yuyo mtu ni nani?
Mchezo huu haukuwake katika kanisa kubwa juu ni kubwa zaidi kwa kila mtu wa kazi kuongoza aina hiyo ya ushawishi. Mchungaji wa kwanza wa aina hii ya kanisa anaonekana kama wote wawili sultani wa kikabila na tabibu. Kadhalika, hali ya sultani wa kikabila kawaida anapatikana kanisani ambayo ilianzishwa na mchungaji aliyoko wala ana fanana kuwa pale ikiwa mchungaji alikuwa kwenye kanisa kwa muda murefu, kwa hali kama na hizi usiwezeshe mfanya kazi kupata huu ushawishi. Hii inaweza pia kuwa moja ya sababu zinazo pelekea makanisa mengi makubwa kutokukua hadi pale mchungaji atakapo kuwa pale kwa miaka tano au sita. Sio tu aliwafanya watu wake waanze kumutumaini ambalo laweza kulingana na upungufu wa ushawishi wa sultani wa kikabila.
Moja ya faida za kuanzisha kanisa mpya ni kwamba hauta rithi Sultani wa kabila. Muda mwingi unaokaa kanisani, zaidi ushawishi wako unavyo ongezeka. Ni wakati tu unapoondoka ndipo mfanya kazi wako muhimu anaweza toka kwenye cheo cha sultani wa kabila, juu atakuwa na heshima ya watu wakati mchungaji mpya anapopata tena heshima hiyo. Hali ina changanya ikiwa mchungaji mpya anaishi miaka michache na Sultani wa kabila angali na cheo chake cha uongozi.
Kuna siku kuna sababu zuri zaidi kwa nini mfanya kazi muhimu anayepandishwa kwenye cheo cha ushawishi. Ma kanisa mamoja zilikuwa na wachungaji ambao walikuwa wachanga, walifanya maamuzi ya upumbavu au tu hawakuwa watu ambao watu walitaka kuwafuata. Mfanya kazi muhimu, upande mwengine mara nyingi anaonyesha kuwa anajitolea kwa kanisa na anajihusisha kwa wema wa kanisa na matokeo ya kuwa watu wanataka zaidi kumfuata.
60
Katika kanisa ndogo una puza uhusiana wa huyu sultani wa kabila/tabibu kwa hasara yako. Kwa nyakati zimoja unaweza kabili mtu huyu na kujaribu kuwa sultani wa kabila wewe mwenyewe, lakini ikiwa unafanya, una hitaji kuthibitisha kuwa umejenga tumaini la kutosha na watu makusudi watakuwa upande wako katika makabiliano yanayofuata, kuliko pamoja na mfanya kazi muhimu. Kwa kawaida ni vizuri zaidi sultani wa kabila kuwa upande wako makusudi aanze kudokeza mawazo yenu kwa wengine na kufanyiza agenda ambayo ni kukuhifadhi pamoja na wako.
Ufunguo kwa kufikia haya ni kukuza uhusiano naye. Mkutane kwa msingi kawaida lakini acha iwe ya kawaida. Zungumzie maono yenu ya wakati ujao, mawazo yenu juu ya huduma na sikiliza kwa yale anayo yakusema. Usizani kuwa kila kitu unachokisema ni kizuri sana na kila kitu anachokisema ni mbali zaidi na uwezo wake mwenyewe. Nipo mwamini imara ambaye tuna hitaji kusikiliza kwa mashauri ya watu wengine sababu mazao ya mwisho ya kundi la watu kwa desturi ni bora kuliko ile ya mtu moja. Mazungumzo haya, yanapo kamata hewa ya upendo na tumaini, inakupa nafasi ya kujibu maulizo haya na kusafisha maono yako binafsi.
Munapo kuwa katika makubaliano juu ya mageuzi yanayokusudiwa hapo ni wakati wa kuianzisha kwa mkuu wa kundi la viongozi wa kanisa, kama ma shemasi, baraza, au jina lolote wanalolipewa na dhehebu lenu. Ikiwa unadokeza mageuzi, na sultani wa kabila hakubaliane nayo, bahati zako za kupata watu wengine nyuma yako ni ndogo. Hata ikiwa una wapata kuchagua juu ya mageuzi ita kufanyia wema mdogo isipokuwa wanakiri mageuzi. Ikiwa ni wakati tu wanakiona kama kitu ambacho ‘’sisi’’ tunaenda kufanya, kile kitafaulu. Ikiwa wanasema juu ya kitu kile kama azimio ‘’lenu’’ basi inaonekana sana kuwa hawata weka uzito wao nyuma ya hecho.
5.11. Mfano unaofaa kupata watu upande wako.
Nilipo maliza tu kufundisha yaliyo juu kwa kundi moja la wachungaji katika Afrika ya kati wakati mmoja wao alipo simama na kusema, ‘’Nimeona sasa mahali nilipo kosea’’. Ndipo akaendelea kueleza jinsi alivyo jaribu kuanzisha makundi madogo ndani ya kanisa lake, ambalo lilikuwa limeundwa kwa mfano wa utawala wa kidhehebu, lakini nambari yake watu wawili, sultani wa kabila, alikuwa amekabiliana nayo. Alipo ileta kwenye kikao cha wazee, mtu wake aliwashawishi kuchagua wakikabiliana nayo. Ndipo akaileta kwenye kikao cha kazi za mwezi za kanisa lakini muda huu Baraza la wazee lote lilishawishi kanisa kutoendelea nayo. Sio kusema, ilizusha hali isiyofaa ndani ya kanisa na ilikuwa kizuizi kwa mafanikio.
Huu ni mfano unaofaa wa mchungaji kutosikia neno la sultani wa kabila. Mchungaji angetumia mda zaidi pamoja na mchawishi wake mkuu kwa kumpata upande wake na nyuma ya wazo, kwani bila msahada wake matokeo yalikuwa yamebashiriwa. Sio tu mchungaji hakupata azimio lake kukubaliwa lakini kushinda kwake tu kulitumika kwa kuongeza uwezo wa sultani wa kabila na kuifanya hata zito zaidi kwa kuwezesha kitu chochote kupita siku zijazo. Wachungaji wamoja wanaweza kusema, ‘’sina wakati wa kuchunga, nina maono na inapaswa kufanyika mara moja juu mioyo inaenda jehanum kila siku tunakawisha’’. Ina sikika vema lakini jambo linabaki bili kuwa na msahada wa sultani wa kabila kanisha halitapokea maono, itachelewa tu.
Kumbuka, isipokuwa watu wanakufuata, haupo kiongozi lakini tu mtu aliye na mipango mikubwa.
Pamoja na yaliyo juu moyoni, acha niseme jinsi mchungaji anaweza endelea kuwa na kanisa linalopokea maono yake kwa furaha kwa makundi madogo. Kwanza, sultani wa kabila na kanisa kwa jumla wanapaswa kukutumaini. Wanapaswa kusadiki kuwa una moyo wa kupenda kanisa, na moyo wa kuwapenda, kwa roho kawaida anza kukutana na mfanya kazi wako muhimu na kuza huu uhusiano, kwani bila hiyo bahati zako za kufaulu ni ndogo.
61
Fanya utafiti wako juu ya makundi madogo na kwa nini una fikiri wangekuwa wenye kufaa kwa kanisa lako. Ndipo, wakati wa vikao vyako vya kawaida pamoja na sultani wako wa kabila, taja kuwa ulikuwa ukifikiri juu ya makundi madogo na kwa nini unafikiri wangekuwa wamejua sana juu ya kanisa. Umuulize anayofikiri. Isipokuwa alikuwa akifikiri juu hiyo yeye mwenyewe, ni asili ya mwanadamu kuwa atapinga wazo wakati linapo tolewa kwa mara ya kwanza kwake. Ana weza kusema, ‘’Inasikika vema kwa makanisa mengine lakini haiweze kutumika pale sababu ya X Y Z’’. Usitoe hoja lakini umupe bahati ya kufikiri juu ya wazo. Ndipo ufanye kazi ya nyumbani moja wewe mwenyewe makusudi upate jibu kwa hayo machukio.
Wakati wa kikao chenu cha baadaye cha kawaida inua jambo la makundi madogo tena na changia jinsi ulivyo fikiri juu yale aliyoyasema. Taja jinsi ulivyosema kwa mchungaji katika kanisa lingine juu ya hiyo kwa kuthibitisha ulitenda na jinsi alifikiri kuwa haitakuwa tatizo ikiwa ulitenda ABC. Muyazungumze mbele lakini musisukume kwa sharti hadi pale mutakapoona kuwa Alisha anza kukiri wazo. Hatimaye atasema, au akubali, kuwa ni wakati wa kuanzisha makundi madogo ndani ya kanisa.
Mara moja hii yanapotokea basi ni wakati kwako kwa kupangilia, pamoja na mchango wake, jinsi gani utaanzisha wazo kwa hatua ya baadaye ya uongozi, kawaida Baraza la wazee au kadiri yoyote dhehebu lenu linavyo ihita. Wakati huu kiingilio cha wazo ni kawaida zaidi. Una kiinua kwenye kikao na pasha sultani wa kabila katika njia ingine kwa kuonyesha wengine kwamba yupo nyuma ya wazo. Kuna vitu vitatu unavyo hitaji kufanya:
 Changia maono kwa makundi madogo. Pana maelezo juu ya jinsi watakavyo fanya kazi, lakini hakikisha kuwa unachangia nao faida ambazo makundi madogo yataletea kanisa
 Pana mda kwa watu kuizungumzia na inua machukio
 Jibu machukio yao katika njia inayofaa
Kumbuka, watu wanakubali mageuzi namna tofauti kwa iyo uwape muda wa kufikiri juu ya wazo. Ningeshangaa ikiwa wote walikubaliana na tayari kwa kukubali wazo munamo kikao cha kwanza. Ikiwa hapo kunaonekana kuwa makubaliano mamoja ya jumla basi unaweza kutaja kuwa mutaizungunzia baadaye katika kikao kinachofuata na ndipo uangalie ukubalifu wa wazo. Nini yataka kuwa zaidi ni ile ya mtu moja au wawili wanaokabiliana na maono. Katika jambo hilo panga kukutanisha watu hawa moja moja peke yake na si desturi na zungumza jambo hilo nao. Usijaribu kuchunga wakati kwa kuona wapinzani wote kwa wakati moja kama watafanya kizuizi zidi yako na hawatafungua na muchangie jinsi wanavyo ona kweli. Unapaswa kusema nao moja kwa moja. Leta sultani wa kabila kama ukiona inafaa. Ikiwa watu wanakabiliana nayo lakini bado hawaja sadiki kuna faida, hapo inaweza tu kuwa jambo la kuwapa wakati wa kufikiri juu yake na chunga kikao kinacho fuata. Unapoona kuwa kila moja yupo katika makubaliano kwa jumla na alikiri wazo, ndipo uangalie ukubalifu kutoka kwao kwa kuendelea na kutenda kazi ya azimio.
Sasa kuwa una viongozi wako muhimu kwa upande ni wakati wa kuihanzisha kwenye kanisa. Majilio yako yatafuatana na njia ya uongozi wa kanisa lako. Ikiwa ina namna ya utawala wa jamii ya waabuduo, mahali ya mwili wa kanisa unakubali maamuzi haya kwanza, hapo unahitaji kuileta kwenye Baraza la Mwezi au vyovyote vile dhehebu lako linavyo ihita. Unafuata mtindo sawa sawa na vile ulivyofanya na Baraza la wazee. Hayo ni, changia maono na makundi madogo, pana maelezo juu ya vile yatakavyotumika pamoja na mkazo kwa faida yatakayoleta kwa kanisa. Patia watu mda wa kuzungumzia na kuinua vizuizi. Jibu vizuizi vyao kwa namna inayofaa. Katika jambo la makundi madogo, nina weza kupitisha jumaa kazaa zinazotengwa kwa mikutano nikihubiri juu ya namna kanisa la kwanza lilikuwa likikusanyika pamoja katika Hekalu wote kwa jumla lakini pia walikuwa wakikusanyika katika nyumba za watu vile vile. Uwaonyeshe kuwa ni kibiblia. Saidia kwa kuondoa mashaka yote
62
na woga ambao waweza kuwa nao, makusudi wakati itakapoingizwa ndani ya kikao cha kazi cha Mwezi si kitu ambacho ni kigeni kabisa kwao.
Patia watu wakati wa kukubali wazo na usiende mbio kwenye uchaguzi ikiwa 60% wanakubali lakini 40% wanakataa basi hauna umoja na yawezekana yaweza kuwa hasara kuwa na watu wengi mno wanao kabiliana na wazo. Usifikiri kuwa utachunga hadi pale kila mtu atakapokubali lakini jaribu kupata kiwango cha juu cha walio wengi ambacho kinawezekana kwa kutozuia maendeleo, ingiza sultani wa kabila na wazee katika maonyesho makusudi kila mtu ajue kuwa wanakubaliana na wazo hilo.
Ikiwa muna namna ya utawala wa kanisa ambao hauhitaji ninyi kupata ukubalifu toka kwenye kundi la kanisa kabla ya kuingiza wazo la makundi madogo, au uamuzi mwengine, hapa ni rahisi kidogo, walakini na haja ya kupata watu upande na kuwafanya wakufuate. Naweza kuwa ningali nafundisha juu ya jambo. Lazima nichangia maono pamoja na faida zake na kuwapa muda wa kukubali mageuzi. Watu wataenda kuchagua kufuatana na namna ya utawala wenu. Ikiwa ni mfano wa jamii ya watu waabuduo basi mchaguzi ni wa kawaida ambao unachukua nafasi katika mkutano unao amriwa. ikiwa muna mfano wa ‘toka juu chini’ na uchaguzi usiyo wa kawaida mahali pote katika utaratibu, watu watakuwa wakichagua; lakini wakati huu itakuwa ni kwa miguu yao au kwa lawama zao.
Acha nieleze kadiri kanisa nililokuwa nikishiriki kikamilifu lilivyo fikia mageuzi ya kutoka kwenye ibada moja asubui hadi kwa mbili. Ilikuwa na namna ya uongozi wa ‘toka juu chini’ na haikufanyisha kamwe kikao cha kanisa ambamo watu wanaomba kuchagua juu ya mageuzi inayokusudiwa. Uongozi ulikusudia kuwa wazo la ibada nyingi asubuhi ilikuwa ni jibu kwenye tatizo la msongamano. Walichangia mawazo yao munamo huduma za kanisa, wakieleza maono na kuwapa watu moyo kuwa hawataenda mbio kwenye uamuzi wa ghafla. Kadiri watu walivyokuwa wakiuliza maulizo na masikitiko kwa hiyo uongozi ulisema mambo. Nyuma ya miezi kazaa, ilipokuwa wazi kuwa washawishi wakuu walikuwa na shauri moja, walitoa orodha ya maswali kwa kukadirisha msahada na kuuliza watu huduma gani wanayofikiri inaweza kuwafaa vema zaidi. Tarehe ilichaguliwa kwa kufanya mpito. Kwa kupunguza wonga mbele uongozi ulikusudia kufanya huduma zote mbili tofauti kwa muda wa wakati makusudi watu wapate kuhudhuria zote mbili mbele ya kufanya uchaguzi wao wa mwisho. Mpito wote ulipita bila shida kabisa na kukua kukatokea na watu walichagua na miguu yao kwa kukubali mageuzi kwa furaha.
5.12 Tumia busara katika mwendo unapofanya mageuzi
Yeyote ambaye wakati wowote alipanda na kuchukuliwa na aina ya baisikeli inayo sukumwa anajua kuwa ni rahisi kuanza kwenye hatua upande wa nje kuliko kwenye mlima na ni vyepesi kuendesha ukikanyangia pendal ukipanda mlima wakati tayari unaendelea kuliko pale ungaliki ukianza kutoka kwenye ilikuwa ikisimama chini ya m lima. Tunajua pia kuwa ikiwa tupo tukisukuma gari lenye magurudumu mawili, ni vyepesi kupandisha mzigo mzito juu yake mara tunapokuwa tukienda, kuliko ilivyo kuanza kupeleka mzigo mzito. Mwendo unafanya tofauti zote.
Makanisa na orotha zao za mambo yaliyo kusudiwa kutendwa ina mwendo ambao tunapaswa kuelewa. Kumbuka kanisa nililolitaja awali ambalo lilianza kukua lakini kwa hatua ambayo haingeweza kudumu sababu ya ukosefu wa mahali pa kukaa na ndipo ikaanza kupunguka. Tatizo ilikuwa kwamba ilipoteza mwendo wake na kwa hii ikaonekana kutowezekana kukamata tena kukua iliyokuwa nayo kwanza kupata kuona viti vinapatikana mara moja. Mara moja mwendo unapopotea ni vigumu kabisa kuupata tena, ni vigumu kabisa kuliko kuuacha ukienda munamo nafasi ya kwanza.
Uwe na uhakika kuwa kanisa lenu linaanza kukua kabla ya kujaribu kuongeza mwendo. Usijaribu kufanya mengi mno kwa mara moja kwani, kama gari ya gurudumu mbili na mzigo
63
mzito; unaweza kuwa na uwezo wa kuiendesha au acha iwe ikienda na vifaa ulivyo navyo. Watu watakuwa na uchovu na kuacha au kupoteza upya wao na shauku ya kazi. Usijaribu kufanya mengi haraka sana, bana kwenye kiwango kidogo cha vitu vinavyofaa na uvifanye vizuri. Kadiri unavyoanza kuendelea, wengine watajiunga nawe na hivo utakuwa na vifaa vingi na kuwa na uwezo wa kupanua. Mfano wa gari la magurudumu mawili, yale musingeweza kusukuma mukiwa watu wawili munaweza kuisukuma vyepesi mukiwa watu watano. Tena, iweni makini, ni kazi ngapi za mpya munazo anza kwa wakati moja au ukubwa gani kazi mpya inao. Hakikisha kuwa unaweza kuisukuma kwanza, bila kuchosha wasukumaji, na ndipo inapanua kadiri watu wanapokaa nyuma kusukuma.
Ikiwa kuna msukumo mwingi mno gari ya magurudumu mawili kulingana na uzito juu yake, vimoja vitaanguka sababu wataona kuwa hawahitajike. Kadiri kanisa ilivyo kubwa, na zaidi ya vifaza au mazao unayo, wingi orodha ya mambo uanayo kadiriwa kutendeka unayoweza na yange tendeka. Watu waelekevu wanataka kutumiwa na ikiwa hakuna nafasi kwao katika kanisa lenu mara nyingi wataenda kwenye kanisa ambalo linafunguka kwao.
64
Sura ya 6
Mafundisho ya kugomboa wakati
6.1. Utangulizi
Sura hii itazungumzia jinsi ya kutumia wakati wako vipasavyo, juu bila huu welekevu pengine hautafikia kutimiza kazi kubwa. Ni vyepesi kupoteza wakati, sio kwa sababu uko mzahifu kweli, lakini sababu hauitumie katika njia inayo toa matunda. Kiongozi ana ombi nyingi juu ya wakati wao na kufaa kwao kwa kawaida kutathibitishwa na urembo gani wanao kwa kutumia wakati. Kila mtu ana saa 24 kwa siku; awe ni Raïsi wa umoja wa mataifa au mwombaji maskini zaidi. Hatuwezi nunua wakati wa kuzidi, tunaweza tu kuitumia kwa kuzaa matunda zaidi.
Nina jitanguliza juu ya makusudi ya kitabu hiki kuwa hauko mzahifu. Nina amini kuwa mchungaji ambaye analipwa kwa wakati wote na kanisa lake inampasa kutumika kwa vyovyote kama saa nyingi kama viongozi watu wa kazi muhimu wanavyopitisha katika kazi zao za kawaida na kwa huduma yao. Kujitanguliza kuwa haupo mzahifu, ufunguo kwa mafanikio makuu ni kutumika na MALIDADI kuliko na NGUVU.
Ninapenda yale Tony Blair aliyoandika juu ya kugomboa wakati, “moja ya funguo za kutumika kazi ya waziri wa kwanza au Raïsi ni kugomboa wakati wako. Umuhimu wake ni mkuu. Unionyeshe kiongozi anayefaa na nitakuonyesha daftari iliyotengenezwa vibaya. Haya hayana chakufanya na esabu ya masaa yaliyotumikwa - Niliwakaribia viongozi ambao walitumika masaa ya kuchekesha zaidi, masaa kumi na nane kwa siku saa za kupita kiasi cha kufanyika kila mara – lakini kama saa inatumiwa kwa kufaa’’16. Yale yanayotumiwa kwa waziri wa kwanza wa Raïsi ina tumiwa pia kwa mchungaji au kiongozi wa dhehebu
6.2 Umbalimbali kati ya muhimu na haraka
Hatua ya kwanza kwa kutumika malidadi ni kuthibitisha ni nini iliyo ya muhimu kwako? Uliitwa kufanya nini? Uliitwa kufanya nini kama mzazi, mume au mke, mchungaji, mwanainchi nk? Hakuna mwisho kwenye ombi ambazo ziko juu yako lakini utume wako ni gani hapa duniani? Ni nini kilicho cha muhimu kama kukabiliana na yaliyo haraka? ‘Haraka’ ni kazi zinazotusonga na zina omba uangalifu wetu. Kwa mfano, simu inalia na tunajisikia kulazimishwa kujibu au kuna mtu anayetaka kuongea nasi hata ikiwa haiwezi kuwa ya muhimu kabisa. Kwa upande mwengine, tunaweza kusema kuwa watoto wetu ni wa muhimu zaidi na kuwa tunapenda wao wakomae kwa kuwa wacha Mungu, lakini hatutumie wakati wa lazima nao kwa ajili ya haya kutokea. Tunaweza kuwa wenye kazi nyingi mno kwa kutumika vitu vya haraka, kinacho kishindo cha muda murefu kidogo, kuwa tuna wakati mdogo unaobaki kwa kutumia kwa yale tunayojua kuwa muhimu kweli.
Yesu alitupatia mfano mzuri katika kupambanua kati ya haraka na ya muhimu. Ona Yohana 17:4, Mimi nimekutukuza duniani, hali nimeimaliza kazi ile uliyonipa niifanye. Maelezo gani ya ajabu; alifanya yale Baba aliyomutuma kufanya. Jinsi gani haya yangekuwa kweli wakati kulikuweko na watu wengi ambao hawakupona, na wengi ambao bado hawajamuamini? Nyuma ya kupaa kwake alikuwa tu na wafuasi 120 lakini tayari alikuwa na uwezo wa kusema kuwa alimaliza kazi aliyopewa na Baba. Huko kulikuweko na ombi nyingi juu ya wakati wake, na vitu vingi vizuri mno ambavyo vingemvuta mawazo kutoka utume wake, lakini alifanya yale yaliyokuwa ya muhimu kuliko yale yaliyo kuwa ya haraka. Iwapo Yesu alikuja kutimiza kazi mbili kubwa. Ya kwanza ilikuwa kushughulika na tatizo la dhambi makusudi mwanaume na; mwanamke wapate kusamehewa na wawe na maisha mapya; ya pili ilikuwa ni kufunza kundi la watu kuchukua habari ya injili kwa miisho ya nchi.
Njia moja inayo dhihirisha yaliyo muhimu kwako ni kufikiri kuwa upo karibu kuja na jamaa yako, marafiki wamoja wa karibu kuja na jamaa yako, marafiki wamoja wa karibu, na pengine wenzi
16 Blair 107
65
wako wamoja wa kazi waliwai kuitwa kwenye chumba chako kukuona yawezekana kwa wakati wa mwisho. Kama jamaa lako na marafiki wanavyosema kwako nini watakayosema juu yako? Je, wataonyesha upendo wao kwako kuwa ulitumia wakati nao katika hali za kuthibitisha maisha yao, na kuwasaidia kupitia hiyo? Je, watakushukuru kwa kuwaonyesha ukweli wa Yesu kwa njia unayo ishi? Je, watoto wako wote watatawa hapo au wamoja hawatakuwepo sababu walikukataa kufuatana na unafiki ambao waliokuwa wakiona katika maisha yako. Mshangao wa pamoja kutoka kwa wazazi wazee ni kwamba hawakutumia mda wa kutosha pamoja na watoto wao wakati walipo kuwa wakikua.
Kama munavyo lala kwenye kitanda munafahamu kuwa mpo karibu ya kwenda kuwa pamoja na Bwana na kuwa kwa siku ya hukumu mutapana hesabu ya jinsi mulivyo tumia wakati wenu, ni mulichokifanya na nina hamu kufanya. Je, munajua kuwa mulifanya yale Mungu aliyowaitia kufanya? Je, utasikia akisema ‘’kazi njema, vema na mtumishi mwaminifu’’ kutoka kwa Babako aliye mbinguni? Inasemeka kuwa hakuna mtu, wakati anaenda kufa, anayetaka kutumia wakati zaidi katika ofisi. Huu ni ukweli tulivu, hivyo watu wengi wanatumia wakati mwingi zaidi kwa kujaribu kupata utajiri na mamlaka tu kwa kutimiza baadaye juu ya hayo haikuithamanisha, sio hapo wangeweza kutia hali zao za kuwa kwanza.
Acha niwapeni taratibu kazaa za hali ya kuwa kwanza. Ni zifuatazo:
 Mungu
 Watoto
 Mke
 Huduma
Kwa wengi wetu ni vigumu kupambanua kati ya Mungu na huduma sababu tunafikiri kwamba tunamuweka Mungu kuwa wa kwanza tunapokuwa tukitumika na nguvu katika huduma. Hii sio lazima hivyo. Acha niwapeni mifano mimoja ambayo itawasaidia vipasavyo kwa kuelewa umbalimbali.
Ninajua mchungaji aliye anzisha kanisa katika Afrika ya Mashariki ambayo ilikua kwenye kiwango kizuri. Ilifikia hatua ambayo ilikuwa na uwezo wa kumulipa mshahara makusudi apate kuangalia nyuma ya mahitaji ya jamaa yake bila shida. Walakini, alianza kusikia sauti ya Mungu ikimuita kuagana na kanisa na kupanda kanisa lipya katika eneo lingine bila msingi wa kuanza nao. Kwa wale wa Australia nina hitaji kuwambia kuwa huko hakuna matunzo ya bure au masomo ya bure wala faida zisizo na kazi katika nchi hii, hapo hakuna kitu. Kueshimu Mungu katika hali hii inaweza kubebesha asili nzito juu yake mwenyewe na maisha yake. Aliomba ushauri toka watu kwenye harmashauri ya kitaifa ya dhehebu na walikubaliana kwamba ulikuwa ni mwito mgumu lakini ikiwa alikuwa na uhakika wa kuwa hii ndiyo Mungu alikuwa akisema basi lazima kuwa mtiifu na kwenda. (Alikuwa ni mmoja). Hatimaye, alikiri kuwa huyu alikuwa Mungu na hivyo alihamisha jamaa lake lote katika jimbo lingine na akaanza tena. Hii ni kutia Mungu kuwa wa kwanza.
Acha tuone sasa kwa kutia nia yako mbele ya huduma. Mchungaji anayeoa lazima atunze mke wake na kukuza uhusiano wake naye. Ni vibaya kutokumujali kwa msingi wa kuwa analemewa sana kwa kufanya huduma; kuhuzuria kusanyiko zote za maombi ya usiku, kushauri watu, na kuombea wengine. Hata anapokuwa nyumbani, kuna nyakati mchungaji ni mwenye kuchoka sana kwa kutumia wakati pamoja na mke wake, na kumusikiliza kadiri anavyo changia mahitaji yake pamoja naye. Haya yanapotokea mke anafanana kuwa mpya kanisani na asiyejitolea kabisa kwa kanisa au kwenye huduma. Niliwai kusikia wachungaji wanao dai kuwa wake zao hawapo nyuma yao katika huduma na kuwa hawana shauku nayo. Hali hii sio tu kuwa inakuwa vigumu kabisa kuchunga kanisa lakini inaweka asili isiowezekana juu ya uhusiano wa ndoa; pana siku yaweza kutokeza mwisho wake kwenye kuachana.
Moja ya vitu ambavyo ninaenda kudokeza katika sura hii ni kwamba ufikiri kugawa wakati wa kutumia pamoja na mke wako; muwe na siku, mwende kutumia soda na mukae na muongee, au chochote ninyi wawili nunachokifurahia. Acha tukubali kuwa mulikaa kando Jumanne asubuhi pa saa 9:30, kuwa na tarehe na mke wako makusudi muweze kuwa pamoja na mufurahiane kila mtu
66
na mwenziwe. Acha tukubali kuwa kabla ya wewe kuondoka tu unapokea simu ikiita kutoka kwa mwanamemba wa kanisa akisubiri kukuona upesi sababu ya shida inayojitokeza. Kupitia ninayoyaishi ninashauri kuwa kuna vitu vidogo sana ambavyo ni vya muhimu kabisa, kuwa hawangesubiri masaa mawili kabla uwatendee kazi. Kuweka mke wako mbele ya huduma ina maana kuwa unaambia huyu mtu kuwa hauweze kuwaona mara hiyo sababu una shughuli lakini utakuwa huru munamo saa 11:30, wala wakati wowote muda wako pamoja na mke wako utakuwa umekwisha. Pengine unaweza kuwa na neno ndogo la maombi kwenye simu na mtu yule, toa mashauri mamoja ya haraka, na ndipo uendelee kutumia huu mda wakufaa pamoja na mke wako. Usitangue wakati pamoja na mke wako hivyo unaweza kukutana na huyo mtu.
Hapo kunaweza kuwa hali zimoja ambazo zinahitaji uhudumu wako maramoja. Ikiwa mtoto aligongwa na gari na alipelekwa hospitalini na hatumainiwe kuishi, basi hii ni moja wapo wa kesi hizo. Katika hali kama na hiyo lazima nichangie habari na mke wangu na huenda sote wawili tuende hospitalini maramoja.walakini, katika miaka yangu yote kama mchungaji, nilipo gawa wakati wakuwa na mke wangu pamoja na watoto, sijawai kamwe kuwa na hali ambayo isingesubiri masaa mawili au zaidi kabla nifikie hapo. Tuna hitaji kutia wake zetu na watoto mbele ya huduma. Ikiwa unajifunza kutumika malidadi utagundua kuwa unaweza kuwa na huduma inayofaa na ungali unatumia mda mzuri na mke wako na watoto. (Yaliyo juu yanatakika pia kwa mchungaji mwanamke; lazima akuze uhusiano na mume wake na kuangalia nyuma ya mahitaji yake).
6.3 Azimia vitu muhimu kwanza katika maisha yako
Nina amini kuwa ni ya maana kutambua mambo muhimu na ndipo uyapangilie katika jumaa lako. Ikiwa hauweze kufanya hivi utakuta kuwa yatasukumiwa upande moja na kutopata usikizi wako. Tatizo la mambo muhimu ni kwamba wara nyingi hawapo haraka. Kupata wakati huo pamoja na mke wako makusudi mupate kuongea na kufurahia kila moja na mwenziwe sio haraka na inaonekana kupuziwa lakini, ikiwa unaendelea kufanya hivi, unaweza kuona uhusiano wa ndoa yako utakuwa mara dufu. Huzuni, mara nyingi inakuwa chelewa mno kwa ngazi hii hautafanya kitu kinachofaa juu ya kisa hicho.
Tuangalie mfano unaofuata kwa kuangazia zaidi umuhimu wa kuazimia mambo muhimu kwanza na ndipo ujenge vitu vingine kandokando ya yale.
Mwalimu moja alisimama mbele ya somo lake la philosophia na alikuwa na vitu vimoja mbele yake. Somo lilipo anza, kimya kimya, alitwaa gudulia la kioo kubwa mno na iliyo tupu na akaanza kuijaza kwa mipira midogo kupiga kwa fimbo za vingoe. Ndipo aliuliza wanafunzi ikiwa guduria limejaa. Wakakubali kuwa ndiyo imejaa. Kwa hiyo mwaalimu akatwaa sasa bweta la changarawe na kuzimwangia ndani ya guduria, alitikisa guduria upesi. Changarawe yalikuwa yakijifigirisha mahali ambako palikuwa wazi kati ya mipira midogo. Ndipo tena aliuliza wanafunzi ikiwa guduria limejaa. Wakakubali ndiyo limejaa. Baadaye mwaalimu alichukua bweta la mchanga nakulimwanga ndani ya guduria. Naam, mchanga ulifukia kila kitu chochote. Alihuliza mara tena ikiwa guduria lilikuwa limejaa. Wanafunzi walijibu wote pamoja “ndiyo”. Sasa mwaalimu alitokeza kopo la kahawa zuri toka chini ya meza na akamwanga yote ndani ya guduria, ilijaza vipasavyo mahali ambapo palikuwa wazi kati ya mchanga. Wanafunzi walicheka. ‘’sasa’’ mwaalimu alisema, kama cheko linatulia, ‘’Ninataka mujue kuwa guduria hii inatoa alama ya maisha yako.
Mipira midogo ni vitu muhimu – Mungu, mke wako, jamaa yako, afya yako, mambo unayotamani – vitu ambavyo ikiwa kila kitu chochote kilipotea na vimebaki tu, maisha yako yangekuwa yangali yanajaa. Changarawe ni vitu vingine ambavyo ni kama kazi yako, nyumba yako, gari lako. Mchanga ni kila kitu tena – vitu vidogo. Ikiwa unatia mchanga katika guduria kwanza’’, aliendelea, ‘’hakuna chumba juu ya matatizo au mipira midogo. Yale yale yanaenda juu ya maisha. Ikiwa unatumia wakati wako wote na nguvu juu ya vitu vidogo, kamwe hautakuwa na chumba juu ya vitu ambavyo ni muhimu kwako. Uwe mwangalifu kwa vitu ambavyo ni vya kupima kwenye furaha yenu. Cheza na watoto wako. Chukua muda wa kupata maelezo ya tabibu. Chukua mke wako nje kwenye chakula kikubwa cha kutwa. Kwa kawaida kutakuweko na kazi ya kusafisha nyumba au kusukua gari.
67
Tunza mipira midogo kwanza, vitu ambavyo ni vya kawaida. Weka vipao mbele. Inayobaki ni mchanga tu’’.mmoja wa wanafunzi alipandisha mkono wake na akauliza kahawa inalinganishwa na nini ? Mwaalimu alicheka. “ nina furahi uliuliza ”, alisema. “ inaenda tu kukuonyesha kuwa haidhuru namna gani maisha yako yanaweza onekana kujaa, kwa kawaida kungaliki na chumba kwa kahawa zuri pamoja na rafiki ”.
Huu ni mfano wa kumeta meta wa jinsi tunaweza faulu zaidi ikiwa tunapambanua kati ya yaliyo muhimu na isiyo ya muhimu na pana kipao mbele kwa ya kwanza. Ikiwa mwaalimu alimwanga mchanga ndani ya guduria kwanza na kisha changalawe, angepata kuona kuwa hakuwa na nafasi ya kutosha kabisa kwa mipira midogo. Basi angefanya uamuzi kama ni nini cha kuongeza kwenye mipira midogo na nini cha kutoa nje. Kila alicho kikusudia hangekuwa na uwezo wa kuvieneza vyote katika guduria. ‘mipira midogo’ mimoja muhimu hayangepata uangalifu wake juma hiyo.
‘Mipira midogo’ inawakilisha nini kwako ? Labda:
 Uhusiano wako na Mungu
 Uhusiano wako na mke wako
 Uhusiano wako na watoto wako
 Afya yako
 Kukua kwako mwenyewe na maendeleo.
Chukua wakati sasa wakuesabu yaliyo muhimu kwako kama mtu, mume au mke, mzazi, mchungaji. Mipira midogo muhimu katika maisha yako ni nini? Fanya moja juu ya maisha yako mwenyewe na ingine kwa huduma yako.
6.4 Toa kanuni yako ya jumaa kwanza
Mara moja yule aliye kusudia ‘mipira midogo’ ni nini, sasa unahitaji kugawa wakati kwa hayo munamo jumaa. Ninapendekeza kuwa ugawe siku yako kwa vipande vitatu; asubuhi, alasiri na mangharibi. Sasa weka katika ‘mipira mdogo’ mfano wa mashughuli makusudi vitu vya muhimu kawaida vinaenda kufanyika. Ninajua kuwa kutakuweko na jumaa ambazo hii haiweze kufaulu, kama vile jumaa wakati ulipotoka nyumbani juu ya mafunzo lakini ni ya muhimu kuakikisha kuwa kwenye juma la kawaida, na hii ni kawaida kwa wengi wetu, vitu muhimu vinawekwa kwanza. Tutaangalia katika kutia ‘changarawe’ na ‘mchanga’ baadaye, lakini kwa ngaji hii weka ndani ‘mipira midogo’, hapo ni, hivyo vitu muhimu ambavyo vingepewa kipao mbele katika jumaa lako.
Nilipo kuwa nikichunga kanisa niliweka kando vipande vya wakati kila jumaa juu ya shughuli zifuatazo na katika njia hii nilikuwa na uwezo wa kupea kipao mbele yale nilifikiri kuwa ya muhimu.
 Ijumaa usiku iliwekwa kando kama usiku wa Jamaa. Hatukupangilia kusanyiko lolote kwenye usiku ule wala kupanga kuona yeyote ule. Tulipokaa chini kwenye chakula kikuu cha alasiri pamoja na jamaa tulifunga simu makusudi simu isituvute mawazo wanapotuita. Basi tulipitisha magharibi pamoja tukicheza michezo au vitu vingine ambavyo tulivipangilia awali tunavyojua watoto wata vifurahia.
Tulifanya pia kila chakula cha magharibi kisicho cha kawaida tulikaa tukijogelea meza na tulizima television. Hamuweze kuwa na aina ya wakati wa maana pamoja ikiwa television inawaka; hata ikiwa ni program ya kikristo. Tulizima pia simu na machine za kujibu wazi. (Acha niseme kuwa hii ilikuwa mbele ya simu za mkononi. Sasa lazima uzime simu yako ya mkononi). Kanisa la kwanza liliishi na kukua bila kuwa na simu ya mkononi kwa wakati wote. Kabla ya kula tulikamatana mikono nami niliomba kwa ajili ya chakula na mambo mengine mamoja. Kamwe sikuomba zaidi ya second 20-25 kama watoto wanavyo udhi vingine; unaweza funga imani kubwa kwa pamoja katika maombi mafupi.
68
Nyuma ya kumaliza kula kila mtu alichangia habari mbili fupi: kitu ambacho kiliwafikia mchana. Tulikuwa na kanuni ambayo hakuna mtu hangeikatiza wakati mtu mwengine alikuwa akisema wala kuchambua au kufanya elezo lote lile la kukanusha juu yale mtu aliyochangia.
Watu wanaojua jamaa yetu wanastaajabu kwa vile tunavyo karibiana lakini tulitia msingi juu ya hii kadiri watoto wanavyokua wakitoa wakati zuri pamoja.
 Nilitwaa siku moja nikaiweka kando ya huduma. Kawaida hii ilikuwa Juma tatu lakini baadaye niligeuza Alhamisi sababu ilikuwa inafaa zaidi. Huduma inaweza kuomba kabisa kuwa wachungaji wajisikie kuwa lazima watumike kila siku lakini si vizuri kwa afya yetu na hayazae matunda kwa muda murefu. Biblia inatuambia kuwa tutatumika tu siku sita kwa jumaa.
Kawaida nilipangilia kufanya kitu fulani pamoja na mke wangu Carol kwa siku. Tunaweza kuwa tulienda kwenye matembezi au kuondoka na kuchangia kahawa. Kutumia huu muda pamoja na mke wangu ulikuza uhusiano wetu na ilionekana tunafanya kila kitu chochote kuwa rahisi. Hata sasa tuna simamisha mwendo wa saa 10 :30 am kila asubuhi na kukaa kwenye sehemu ya nyuma ya baraza ya nyumba pamoja ; tukinywa kahawa ya cappuccino na kuongea.
 Nilitumia Juma tatu usiku kila jumaa pamoja na viongozi, mojawapo kama kundi au kama mojawapo. Hii iliniwezesha kutoa maono kwao na kuelewa ni wapi walipokuwa kama watu. Ili nisahidia kuwatolea tunzo la uchungaji linapo hitajika na kuwapa mafunzo yanayo faa na mifano.
 Nilitumia Jumanne asubuhi nikitayarisha mahubiri na Ijumaa asubuhi kuyaandika yote. Ninajua wachungaji wanao jishughulisha zaidi na shughuli zisizo za muhimu ambazo mara nyingi wanatafuta wenyewe bila kutayarisha mahubiri Jumamosi usiku na wana anza kutayarisha munamo saa kumi hiyo magharibi. Kwangu mimi kama mchungaji, utayarisho wa mahubiri ni moja ya ‘mipira midogo’ ambayo ninatia kwa mara ya kwanza katika guduria.
 Jumatano usiku ilitumiwa kwa mafunzo na kuchukua nje kundi la Mlipuko wa Injili. Ninaona Injili kuwa ya muhimu na ingepewa kipao mbele. Ikiwa tunatia mchanga katika guduria kwanza sasa tutaona kuwa hatuweze kuwa na wakati wa hii kazi ya muhimu.
Hivi ndivyo vitu muhimu ambavyo nilikuwa nikiweka kwa mara ya kwanza katika jumaa yangu. Nyuma ya hayo kila kitu chochote nilikiweka pembezoni mwa hayo. Sikuwa na cha kunikera kwa mwisho wa jumaa ikiwa nilitoa wakati wakufaa na nguvu kwa kutumika vitu ambavyo vilikuwa vya muhimu ; kama vile wakati na mke wangu na jamaa au kufundisha viongozi wa kanisa. Nijua nitafanya hivyo sababu niliwapangilia nafasi ya kwanza.
Pia niliweka kando kujiendeleza mwenyewe mara moja nilipo maliza chuo cha Biblia. Nina kumbuka nilikuwa nikishauriwa kufanya hii na mchungaji wa kwanza wa kanisa kubwa. Alieleza jinsi alivyo enda kutoa ushauri kwa mchungaji ambaye alikuwa ameacha huduma sababu ya mchomo wa nje na mambo mengine yanayo ambatana na hayo. Alichangia namna alivyoona rafu ya vitabu na nikatambua kwamba huyu mtu hakununua vitabu vingine vipya tangu alipotoka kwenye chuo cha Biblia. Katika maneno mengine alisimamisha kukua na matokeo aliyokuwa nayo ni ya kutokuwa na kitu kipya cha kutoa kwa wengine
Ikiwa unaishi katika nchi inayo endelea hauwezi kuwa na fedha au wakati wa kununua vitabu na kukuza mafikiri yako juu ya mambo mamoja kama nilivyofanya lakini kuna njia zingine za kujiendeleza mwenyewe. Nina jua mwaalimu moja wa biblia wa kimataifa na msemaji katika baraza aliye niambia kuwa alikuwa akijaribu kusoma katika biblia mara moja kwa mwaka kwa mwanzo wa mwaka angechagua jambo ambalo alitaka kujifunza zaidi juu yalo – kwa mfano, ‘maombi’ – na ndipo angeandika mashairi ambayo inashughulika na jambo hili. Kadiri anavyo soma anawaza juu ya shairi hizi nakuona ni maarifa gani mapya atakayo gudua.
69
6.5 Tayarisha mwaka wako
Hatua inayo fuata ni kupangilia mwaka wako na hii inahitaji matayarisho ya mwaka. Juu bila hii vingi vya vitu muhimu ambavyo ungekuwa ukifanya yatakuwa yamesongwa nje na vitu vya kawaida na vya haraka. Tazama kwenye makusudi yako na sasa anza kugawa wakati kwa ajili yake. Inawezekana kuwa unapofanya hii utagudua kuwa una makusudi mengi zaidi kwa ajili ya hali yako na kuwa utachosha watu wako nje ikiwa utajaribu kuyatimiza yote. Rekebisha makusudi yako kwa kuamua ni ipi yaliyo ya muhimu zaidi kwa maono yako na uyagawe. Ni maombi iliyo ya muhimu ? Ikiwa unafikiri ni ya muhimu basi weka kando siku zimoja za maombi kwako wewe mwenyewe pekeyako na hivo kwa kanisa. Waza juu ya shughuli zingine na onyesha mafaa yake ukisimamia juu ya jinsi yalivyo yamuhimu kwa maono/kusudi lako. Ikiwa haufanye hivi, inaonekana kabisa kuwa kamwe hauta karibia pembezoni na kumaliza hayo makusudi.
Nina kumbuka nilikuwa katika kamati ya uongozi wa Masomo ya Biblia katika Ulaya muda wa miezi sita na Msimamizi aliambia wanafunzi kwa mwanzo wa mwaka kuwa watatembelea eneo la kutalii maarufu la kuvutia katika jimbo na wangeifurahiya kabisa. Walakini, hakuna tarehe iliyo harifiwa na ilikuwa kwa kawaida kitu ambacho tutaenda kufanya siku zijazo. Karibu ya katikati ya kipindi na mwisho nilimuhuliza wakati gani tutaenda matembezini mahali pa kutalii. Kama nilivyo jua wanafunzi wataifurahia. Nina uhakika munajua jibu ilikuwa gani, “ Tulienda nje ya wakati, hakuna nafasi ya siku zinazobaki kwa hii ”. yote hayo yalihitaji kuwa na kalenda ya matukiyo juu ya kukubaliwa kwa mwanzo wa mwaka wa masomo, na kwa ajili ya kuifatilia. Huyu mtu aliniahidi pia kunipeleka kwenye utalii wa historia la kanisa la maana linalo chaguliwa katika jimbo lakini hatimaye avikufanyika sababu singe weza kamwe kumukaza kuthibitisha tarehe. Ikiwa unataka vitu muhimu kutokea basi unahitaji kutoa wakati wa kuendelesha kalenda ya matukio ya kanisa mwakani.
Toa wakati moja kwa kuomba mbele ya hivi makusudi upate kusikia ‘maneno yoyote ya ukweli’ ambayo Bwana anaweza kujaribu kukupatia.
6.6 Ujipatiye wakati wa kutosha kwa kupata ema sana
Acha nieleze kwa mfano yale ninayo maanisha na mfano ufuatao. Nilipokwenda kuchunga kanisa katika mji wa nchi Austrlia nilialikwa kujiunga na ndugu Mkubwa wa serkali wa mahali, ambako nilikuwa nikitumikia. Nilikuta kuwa wengine walikuwa hawataki kuchukua nyazifa za uongozi na kwa iyo haraka sana nikawa katibu au msimamizi kwa wakati ule nilikuwa pale. Ndugu kawaida alikuwa anaweka matukiyo ya ‘makanisa yanayo changamana’ na angeamua, kadiri wakati unavyokaribia, ni nani wange alika kuwa mgeni msemaji. Desturi ilikuwa ni kuchukua aumuzi mwezi moja au miwili kabla ya tukio na ndipo katibu angetoa kawaida aliko tupu. Bahati mbaya, sababu tulizitoa nyuma zaidi, wasemaji wazuri wote kawaida walikuwa hawana wakati na ikawa wakati wa hatua kwa hatua ya kupata mtu ambaye alikuwa huru munamo tarehe hiyo. Sio kusema, kwa kawaida hawakuwa watu wazuri kwa tukio.
Ili nichukua tu tukio mbili kama katibu kwa kutimiliza kuwa nilikuwa ninatumia kiwango kikubwa mno cha wakati usiyofaa nikijaribu kupata msemaji anayefaa sababu ya huu ukosefu wa matayarisho mbele ya wakati. Ndipo nilitambua kuwa tulipo anza kuzungumzia mipango vitu vinavyofaa kwa tukio la mwaka huu ambavyo tulikusudia juu ya msemaji kwa mwaka ufuatao, kujiwekea juu mwaka katika kuendesha mbele. Tokeo la huu mpangilio wa mbele ya wakati ulikuwa kuwa kwa kawaida ina nichukua tu mwito moja wa simu na barua ya kufuatilia kwa kupata iwezekanavyo msemaji zuri zaidi kuliko 20 kwa 30 ambayo ningefanya kwa kupata moja wa chini. Mpango wa mwaka unaofanyika vinavyofaa mbele ya wakati, utakuwezesha kufikiliza yaliyo muhimu na itakupatia wakati zaidi wa kutumia ukifanya yale yaliyo muhimu, ikiwemo wakati pamoja mke wako na jamaa.
Mfano huu unaonyesha umuhimu wa mpango kwani unapunguza shida na unakuwezesha kufikia matokeo mazuri. Kumbuka nilisema awali, “ kutumika MALIDADI, sio lazima NGUVU ”.
70
6.7 Endeleza mpango wa jumaa ulio dhairi
Ikiwa ulifuata hatua hizi sasa utakuwa tayari na ‘kanuni ya mpango wa jumaa’ na kalenda inayo enea ya mpangilio wa mwaka wa kanisa. Sasa amua lini mutaenda kuanza kutumika kwa kila shughuli. Mara nyingi mutawakilisha usimamizi wa shughuli za siku kwa siku ya tukio la peke yake kwa mtu mwengine lakini una hitaji kutumia wakati ukichangia maono na watu hawa na kuakikisha kuwa mpangilio wao upo ndani ya mipaka ya yale munayo tarajia.
Sasa gawa wakati juu ya ‘mpango wako wa jumaa’ kwa jumaa hiyo kwa mfano, unaweza kusudia kutembelea kundi la uongozi juu ya mradi huu Alhamisi lakini toa wakati kidogo Jumanne kwa kupangilia juu ya kikao hiki. Andika haya katika ukurasa wa jumaa. Sasa andika vitu vingine ambavyo unapaswa kushughulikia katika jumaa na uyaweke kwenye daftari kwa upande katika jumaa. Ruhusu wakati juu ya vizuizi ambavyo unajua kawaida vitakuja. Ukurasa wangu wa mpangilio wa jumaa ulikuwa kwenye kartasi ya A4 ambayo niligabua kwa siku saba, kila siku na vipande vitatu; asubuhi, alasiri na magharibi. Nyuma niliandika kila kitu ambacho nilijua ninapaswa kukifanya na nikavipa nambari nikianzia kwa 1. Mbele ya ukurasa niligabua hizo nambari kwenye sehemu katika siku. Sasa 1 ilikuwa na mpango kwa jumaa ambao ungeniwezesha kutumika kwa uhodari zaidi na kupunguza masumbufu.
Nina jua kuwa kuna programmes zuri sana za computer ambazo zinakuwezesha kupanga siku yako na jumaa lakini wachungaji wengi katika nchi zinazo endelea hawana ruhusa ya kukaribia computers; huko pendekezo langu ni kuwa mutumie ukurasa wa karatasi.
6.8 Tayarisha orodha ya vile ‘utakavyo Fanya’ kwa siku
Utakumbuka kuwa kutayarisha orodha ya vile’utakavyo Fanya’ ni kitu cha mwisho unacho kifanya. Ikiwa unafanya hii kwanza unaweza kugundua kuwa unafaa zaidi kwa kufanya vitu vitendeke lakini, kwa huzuni, unaweza kuweka ngazi wako juu ya ukuta na kuwe unafaa sana kwa kuupanda, na kutambua tu, kuwa uli utiya juu ya ukuta mbaya unapofika kwenye mwisho.
Orodhesha yale utakayo yafanya kwa siku na andika kila ahadi imara za kuonana kwa wakati maalum. Ndipo uvipange kwa kufuatana na umuhimu na N° 1 ikiwa ya muhimu zaidi. Gawa pia ni saa ngapi utakazo tumia kwa kila kitu kimoja. Kwa mfano, ‘Andika barua kwa Fred’ kitakuwa ni kitu ambacho utakacho kifanya katika kikao kimoja lakini “Anza kwenye kitabu cha mafunzo ya uongozi wa Baraza” kinaweza kuwa ni kitu ambacho utatolea tu masaa mawili zaidi na kuacha yanayo salia kwa jumaa lijalo. Ninajua kuwa waandishi watakuambia kuandika baadaye kwa kila kitu kimoja kwenye orodha yako ya vile ‘Utakavyo Fanya’ orodhesha kiwango cha wakati uliogawa kwa hiyo. Nina weza kukubali kuwa siya fanya kamwe hivi lakini kwenye kazi itaweza kumalizika kwa kipindi kifupi cha wakati, nilifanya andiko kwa ufahamu juu ya wakati gani ninaotaka kutoa kwa kuifanya. Labda hili ni eneo ambamo naweza kuza hali. Faida ya kugawa wakati kwa kila kitu ni kukuwezesha kuwa pasipo huruma kwa wakati. Kuna usemi usemao, “Wakati ulio twaliwa kwa kutimiza kazi yoyote utapanuka kwa kujaza wakati ulioko”. Hii ni kweli kabisa na kitu ambacho tunahitaji kuwa macho nacho.
Mara moja ulipo ipea kazi yako kipao mbele, basi anza kwenye kitu cha 1, kitimize na ndipo usogee kwenye kitu cha 2, na vivyo hivyo ukishuka na orodha. Kuna wakati hautamaliza kila kitu kwenye orodha lakini usiwe na wasiwasi juu ya hayo. Kwa mwisho wa siku utatayarisha orodha mpya kwa siku inayofuata na unaweza kuona kuwa yale uliyoweka mbele yalibadirika. Nini kilichokuwa kinafuata kwenye orodha pengine kimeshuka chini ya msafa na vitu vingine vinaweza kuwa muhimu zaidi.
Haya ni maelekezo ambayo yanaweza kujifunzwa. Kwa asili mimi siyo mtu anayefanya mambo kwa utaratibu lakini nilijiongoza mwenyewe kutumia wakati kwa busara. Faida kuu ya mpango wa kugomboa wakati kwangu ni kwamba inanizuia kutoka taabu; nikijiuliza ikiwa nitapata kufanya kila kitu kwa wakati au kama nitasahau kitu kilicho muhimu. Kuwa na mpango wa siku yangu, jumaa na mwaka unapunguza taabu na unaniwezesha kutumika kwa utulivu kupitia yale ninayo ya kufanya. Tokeo la mwisho ni kwamba nimetimiza yaliyo muhimu zaidi kuliko vingine vingekuwa.
71
6.9 Kupata faida ya mwisho kutoka vikao
Acha niendelee na tuzungumzie jambo lingine, kupata faida ya mwisho kutoka vikao. Vikao vinaweza kuwa chombo mojawapo muhimu kwa kuakikisha kuwa maono yako inafanyika au kupoteza wakati mwingi. Kuna hesabu ya mambo ambayo una hitaji kusikia moyoni ikiwa yatakuwa ya kwanza.
Matayarisho ya mkutano
Ikiwa unataka kupata faida nyingi kabisa kutoka mkutano unapaswa kuupangilia. Lazima ujiulize maswali mawili:
 Mkutano huu una kusudi gani?
 Ni tokeo gani unalotumaini kufikia ?
Ikiwa ulijibu majibu yanayo ridhisha kwa hayo maswali yaliyo juu, uwe na uhakika kuwa inatayarishwa kwa ajili ya mkutano au kikao ambayo inaambatana na inakusudia haya. Ikiwa hauna angenda unaweza kutangatanga ukizungumzia mambo bila shabaha ambayo ni isiyofaa.
Inafaa sana kushauri watu mbele ya wakati wa agenda na kuwapa vifaa vinavyofaa kwa kusoma na kufikiri juu yake. Ikiwa watu watakuwa na uvumilivu au pana ripoti inayoendelea, wanafaa pia wawe walijulishwa mbele ya wakati kwa kuakikisha kuwa ilitayarishwa sawa kwa mazungumzo mengine inaweza kuendelea na, hata sasa, hitimisho linalo fanikisha haliweze likafikiwa.
Nilishuhudia mchezo huu halisi wakati moja uliopita wakati mwenzi wangu mu Afrika, alikuwa kwenye Almashauri ya Taifa ya dhehebu lake, alisema kukutana nami nyuma ya chakula cha asubuhi/kikao cha utendaji ambacho alikuwa atahuzuria. Kikao kilikusudiwa kumaliza saa mbili lakini kwa mwisho wa wakati ule kikao kilikuwa hakija kuwa bado karibu ya kuisha. Ndipo aliomba radhi mwenyewe na akaja kuniambia kuwa anaweza kuwa basi saa ingine moja au pengine mbili. Masaa matatu baadaye, kikao kilifika kwenye mwisho na tulikuwa na uwezo wa kusema. Alikiri kosa juu ya urefu wa kikao na aliniambia kuwa kulikuwa kazi kubwa kwa ajili ya shughuli mpya ambayo watu hawakuharifiwa mbele ya wakati. Kama tokeo la hii iliwachukua wakati mrefu wa kufikiri kwa mambo mwenyewe. Bahati mbaya, hii ndiyo inayotokea wakati watu hawapewi andiko kwanza makusudi wapate kufikiri juu ya mashughuli na kupata mambo yanayostahili mbele yao kuchukua uamuzi.
Ikiwa inawezekana kuna kitu kimoja kwenye agenda ambacho kina angalia mbele na kina sema juu ya maono. Vikao vingi mno vinashughulikia tu maamuzi ya ‘siku kwa siku’ na kuacha sura ya maono ya agenda. Ikiwa una pandisha barua bila kuita watu kufanya uamuzi papo hapo, una wapa nafasi ya kubadili yale unayo yasema ; kuwawezesha kumiliki uamuzi kwa wakati unaotaka kitu fulani juu yake.
Chunga andiko la yale yaliyo kusudiwa na nani anaye isimamia.
Hakikisha kuwa umeandika maneno machache ya kikao. Zaidi andika maamuzi yote ambayo yalifikiwa. Mara moja unapo fikia uamuzi usiendelee kwenye kitu cha shughuli inayofuata hadi pale utakapopana nafasi kwa mtu mmoja katika kikao kuakikisha kuwa uamuzi umechukuliwa. Uwape pia mwanzo wa wakati. Kwa kawaida uwe na “Tendo lililotendeka na Tarehe”. Mpango wa vitu katika taarifa au uiweke maramoja nyuma ya kuandikwa kwa mazungumzo. Kwa mfano, ikiwa mulikusudia kujenga kitu kimoja hapo mpango wa ‘Tendo lililotendeka na Tarehe’ lazima iwe na kitu kimoja kama vile, “Joseph Blow kwa kupata kumbukumbu tatu kwa kikao kijao”. Ni nayoyaishi yalionyesha kuwa hata ikiwa mtu anapewa kuchukua usimamizi juu ya uamizi hakuna kitu kinachofanana kutendeka.
Hii ni huenda sehemu ya shauri moja tu ya muhimu zaidi ninayoweza kupana kufuatana na “kupata faida ya juu kutoka vikao”. Ninaweza kukumbuka nyuma ya kumaliza masomo yangu ya
72
theologia na kusoma taarifa za shauri za Baraza za kanisa kwa kupata wazo ya vile vilivyo tokea. Nilifahamu kuwa kwa mwanzo wa mwaka uliopita walikubali kufanya miundo mimoja midogo ya mageuzi kwenye jengo lakini hakuna aliyepewa usimamizi wa kuyatekeleza. Ninaposoma taarifa za Baraza linalofuata nilitambua kuwa mambo yaliinuliwa tena chini ya “kuinuka kwa shughuli” na kuwa kila mtu alijisikia kuwa mabadiriko yalikuwa yenye kufaa. Ile ilitokea katika kikao cha pili na cha baadaye. Ikiwa ninakumbuka vizuri, ilichukua zaidi ya miezi sita kufanya haya mabadiriko madogo ya kadiri. Kama kungekuwa na mtu aliyekabiziwa usimamizi wa kutekeleza mageuzi na kupewa kupangilia wakati wa kuifanya, ingefanyika haraka iwezekanavyo. Hakuna anayependa kuulizwa kwenye kikao kijao kwa nini hawakufanya vitu vimoja ingawa kuna shabaa zuri ya kutotenda neno. Matazamio ya kufadhaishwa katika njia hii mara nyingi inasababisha watu kutenda yale waliyo ombwa kutenda.
Niliona karatasi kubwa ya kutangaza habari ya kubandikia ukutani ya viboko na vinywa vyao pana vinavyofunguka ambayo ina someka, “Wakati yote yanasemwa na kutendeka, mengi kwa kawaida inasemeka kuliko kutendeka”. Hii ni kwa shari kweli, hasa kwa vikao, lakini ikiwa ulipanga mbele ya wakati na kuakikisha kuwa mtu mmoja anachukua usimamizi wa kutekeleza maamuzi ambayo yalifanyika, mutaona mengi yanatendeka kuliko vile mulivyokuwa mukitarajia.
Endesha kikao cha kufanikiwa
Kama mwenyekiti ni kazi yako kuongoza kikao kwenye hitimisho linalofanikiwa bila kukiacha kuyumba yumba bila shabaa. Zamani katika somo hili juu tulizungumza jinsi kanisa linaweza shawishi watu wenye kusitawi. Munaweza kukumbuka yale niliyo andika, “walakini, watu matajiri ni wenye kusitawi sababbu wana nguvu za asili na malezi ya kipekee na hali zuri hakika. Wanacho kitazamia ni mchungaji ambaye waweza kueshimu. Wanataka mchungaji aliye kuza nguvu yake ya asili, aliye na upako wa kiroho juu ya maisha yake na aliye na malezi ya kipekee na mwenye hali zuri hakika. Wana kuwa wasioridhika na wachungaji wasio na maarifa na watatizama penginepo”. Kuendesha kikao cha kufanikiwa ambacho hakiyumbe yumbe kwa nafasi yoyote na kupoteza wakati wa watu itasaidia kuchunga watu wanaositawi waliokuja kwenye kanisa lenu.
6.10 Hitimisho ya maneno
Fikiri usemi ufuatao toka mwandishi aliye hifadhi jina lake. Ina fanya muhtasari wa uongozi vizuri.
Viongozi wabaya: watu wanasema wanawachukia
Viongozi wazuri: watu wanasema wanawapenda
Viongozi wakuu: watu wanasema, “Tulikifanya sisi wenyewe”
Kuitwa na Mungu kuwa kiongozi katika Mwili wa Kristo ni faida kubwa. Mungu akubariki kama unavyo jipanga kuwa kiongozi ambaye Mungu alikuita wewe kuwa.
73
Bibliography
Beasley-Murray, Paul and Wilkinson, Alan. Turning the Tide. London: Bible Society, 1981
Blair, Tony. A Journey. London: Hutchinson, 2010
Covey, Stephen. The 7 Habits of Highly Effective People. Melbourne: The Business Library, 1996
Maxwell, John. Developing the Leader Within You. Nashville: Thomas Nelson, 1993
Snodgrass, Klyne. The NIV Application Commentary: Ephesians. Grand Rapids: Zondervan, 1996

No comments:

Post a Comment