Friday 5 December 2014

MBINU ZA MAZIDISHO YA KIROHO



MBINU ZA MAZIDISHO.

UTANGULIZI.
Biblia imerekodi habari za kuumbwa Kwa ulimwengu na mwanadamu wa kwanza (Adamu na Hawa). Amri ya kwanza iliyotolewa na Mungu kwa viumbe hawa wapya ilikuwa ni kujizidisha.
“Mungu akaumba mtu kwa mfano wake.Kwa mfano wa Mungu alimwumba mwanamme na mwanamke aliwaumba, Mungu akawabarikia,Mungu akawaambia zaeni mkaongezeke mkaijaze nchi na kuitisha”……Mwanzo 1:27-28
Tendo hili la uzazi halikutakiwa liwe la kimwili pekee, uzidisho wa kimwili (ongozeko) tu bali pia lilitakiwa kuwa tendo la kiroho yaani uzidisho wa kiroho
Maadamu Adamu na Hawa wanajizidisha kimwili wangeijaza dunia na viumbe vingine  kama wao. Watu wenye kumjua Mungu na wenye kutembea katika ushirika na Mungu. Wangekuwa pia wazazi wa kiroho wenye kuzaa watu wenye kiroho ( wenye  uhsiano na Mungu). Wangezaa kiroho na kimwili pia.
Kuanguka kwa mwanadamu wa kwanza dhambini kuliathiri tendo hili la uzazi na kujizidisha Mwanzo sura ya 3.
Dhambi ilileta matokeo ya kifo cha kimwili ambacho kilirudisha nyuma uzidisho wa kimwili. Pia   ilisababisha  kifo cha kiroho ambacho ni kutengana kati ya Mungu  na mwanadamu mwenye dhambi.  Mwanzo 2:11. Hili   pia  liliathiri tendo la kujizidisha kiroho.
Kwa sababu Mungu alimpenda sana mwanadamu aliandaa mpango maalumu wa kumuokoa mwanadamu kutokana na janga hili la kifo cha kiroho (spiritual death) .
Mungu alimtuma Yesu kristo kufa kwaajili ya  dhambi za wanadamu wote.Yesu alilipa adhabu  ya dhambi dhetu kwa kupitia kifo chake pale msalabani.Kisha aliishinda mauti kwa kufufuka kwake tena kutoka kwa wafu.  Soma Injili ya  Yohana  sura ya 20.
Hivyo basi kila mmoj wetu ni lazima achague kukubali mpango wa Mungu wa wokovu kwa kumkubali na kumpokea Yewsu Kristo kama Bwana na mwokozi wa maisha yake na kutubu dhambi zake.
Ukiwa mwamini katika Kristo Yesu umesamehewa dhambi zako umeokolewa kutokana na kifo cha kiroho (mauti ya kiroho) japo kuwa mwili wako siku moja utakufa  lakini utaendelea kuishi  kiroho na utapokea mwili mpya   utakao ishi milele mbinguni. Soma   Wakoritho  wa kwanza sura ya 15.

Kuokoka ni kuzaliwa kiroho. Unaumbwa upya kiroho.
Hata imkeuwa mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipy.a Yakale  yamepita tzama yamekuwa mapya. 2 Wakorinto 5:17
Mwanzo wa uumbaji wa mwanadamu wa kwanza agizo la Mung kwao  lilikuwa ni Kujizidisha.Agizo la kwanza  kwa waamini ni sawa na lile Mungu alilomwagiza Adamu Kujizidisha kiroho.
Tunatakiwa kujizidisha kiroho na kuijaza dunia kwa kuwaleta watu kwa Yesu Kristo kama sisi tulivyoletwa na kuwafanya kuwa na ushirika  na Mungu.
Wakati Yesu alipowaita watu kumfuata ilikuwa ni wito wa mazidisho.ya kiroho. Luka 5:10
Agizo lake la mwisho kwa waamini lilikuwa ni kujizidisha kiroho.Matendo 1:8
Ili kukabiliana na changamoto yakuwafikia maelfu ya watu wanaokufa katika dhambi bila kuipokea Injili kila mwamini anapawa kuwa mzazi ( mwenye kujizidisha) .  na kujifunza kanuni za mazidisho .
Kozi hii inafundisha mbinu za ki-Biblia ,uzazi na mazidihs ya kiroho ambazo zitakuwezesha  wewe kujizidisha katika kutii Agizo la Mungu. Utajifunza jinsi ya kujidizisha kiroho kama wewe binafsi  na kushirikiana na waamini wengine  katika kanisa la mahali pamoja na makaisa mengine.
Kama ukifanyia kazi kanuni za ki-Bibia zilizofundishwa katika kozi hii utajisikia kuwajibika na kuwaleta maelfu ya watu waliofunzwa na kuandaliwa kwa kazi ya mazidisho. Ukifuata kanuni za ki-Biblia utapata matokeo ya ki-Biblia.
MALENGO YA KOZI.
Baada ya kumaliza kujifunza kozi hii utaweza:
·       Kujizidisha kiroho kwa kufanyia kazi  mbinu na kanuni za mazidisho.
·       Kutoa muhtasari wa kanuni za mazidisho zilizofundishwa katika Agano jipya.
·       Kueleza jinsi kila mwamini anavyoweza kjizidisha kiroho ili kuweza kuleta maelfu ya watu kwa Kristo Yesu.
·       Kufanya nyumba yako kuwa kituo cha mazidisho.
·       Kuainisha sababu zinazo kwamisha mazidisho ya kiroho.
·       Kuanzisha kituo cha mazidisho ya kiroho.





SURA YA KWANZA
WAVUVI WA WATU.
Malengo ya mada.
·       Baada ya kumaliza mada hii utaweza:
·       Kuandika mstari wa ufunguo toka kichwani mwako.
·       Kutambua agizo la kwanza na la mwisho la Bwana Yesu kwa wanafunzi wake.
·       Kufafanua maana ya mazidisho.
·       Kueleza maana ya mazidhisho ya kiroho
·       Kueleza maana ya mbinu
·       Kueleza maana ya methodolojia.
·       Kueleza maana ya methodolojia ya mazidisho kiroho.
·       Kutoa mhtasari wa kanuni za asili za uvuvi zinazotumika katika uvuvi wa kiroho.
Mstari wa ufungo.
“Yesu akawaambia, njoni mnifuate, name  nitawafanya kuwa wavuvi wa watu”. Marko 1:17
Wakati Yesu alipoanza huduma yake ya hadharani  hapa duniani aliwaita watu kadhaa ili kuwa wanafunzi wake wa awali.
Agizo(amri) lake la kwanza lilikuwa ni kujizidisha  kiroho. Kama wangemfuata, yeye  angewafanya wavuvi wa watu.Wangeza kwa kuvua kiroho wanawake na wanaume kama wao.
Ujumbe wa mwisho wa Yesu kwa wanafunzi wake ulikuwa ni wito kwa uzazi na mazidisho ya kiroho.
“Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho mtakatifu; nanyi mtakuwa ni mashahidi wangu katika yerusalemu na katika Uyahudi wote na Samaria na hata mwisho wan nchi. Akiisha kusema hayo;walipokuwa wakitazama akainuliwa wingu likampkea kutoka machoni pao   Matendo ya Mitume 1:8-9

Ni  jinsi gani wanafunzi wangeweza kutimiza hili agizo kuu walilopewa na Yesu?
Namna  gani kundi hili la watu wangejizidisha na kuufikia ulimwengu wote ?

MBINU ZA MAZIDISHO.
Yesu alifunua mbinu maalumu ambazo zingewawezesha wanafunzi wake kutimiza agizo kuu. “Kuzaa Kiroho” Mojawapo na muhimu ya mbinu hizi  zilitolewa kama sehemu ya Agizo kuu katika Matendo ya Mtume 1:8.
Wanafunzi wangejizidisha kupitia  kuvikwa nguvu na Roho Mtakatifu.Mbinu zingine zilifunuliwa pale wanafunzi walipoanza kujizidisha na kuufikia ulimwengu kwa Injili.  Mbinu hizi zimeandikwa katika kitabu cha Matendo ya mitume. Na nyaraka katika Agano jipya.
Kozi hii inaelezea na kutoa ufafanuzi wa hizi mbinu za  mazidisho. Kozi hii inakufundisha wewe jinsi ya kutumia mbinu hizi ili kuweza kujizidisha kiroho na kuweza kutimiza Agizo kuu la Mungu.
Lakini kabla ya yote unapaswa kuelewa maana ya kujizidisha.
Kuzidisha ni kuongezeka mara nyingi  kiidadi kwa  kujizidisha.Kitu kinapojizidisha huzaa zaidi na zaidi katika ufanano uleule.Mazidisho ni matokeo ya kuzidisha.
Mfano 3×3 = 9 wakati 3+3 =6.  4×3 maana yake ni kwamba  namba 4 zinatakiwa kuwa tatu, yaani 4, 4, 4 ambako huleta jawabu la 12. Hivyo kuzidisha huleta jawabu kubwa kuliko kuongeza. Jambo la msingi hapa ni kwamba namba moja hujirudia katika mfanano ule.
Katika ulimwengu wa asili wanawake na wanaume wanazaliana wenyewe  kwa kuwa na watoto. Wanajizidisha kimwili.
Mazidisho ya kiroho yanatokana na kuzaliana kiroho. Mwamini huzaa kiroho kwa kuwashirikisha  Injili watu wengine wasiomjua Mungu (wasiookoka)  kwa kushuhudia na kuhubiri na kuwaongoza hao aliowashuhudia au kuwahubiri kuwa waamini na kuwawezesha kuwa wanafunzi wa Yesu.
Biblia inadhihirisha mbinu za ki Mungu kwaajili ya mazidisho ya  kiroho.
Mbinu ni mpango uliowekwa kwajili ya kufanikisha lengo fulani mahususi. Au ni hatua zinazowezesha jambo fulani kufanyika kwa ufanisi kama ilivyokusudiwa.
Methodolojia ni Mkusanyiko wa mbinu mbalimbali  zinazowezesha au kufanya kazi kwa pamoja ili kufanikisha jambo fulani lililokusudiwa.
Methodolojia ya mazidisho  ni mkusanyiko wa mbinu mbalimbali zinazowawezesha waamini kufikia lengo la uzazi wa kiroho kwa njia ya kujizidisha.
Lengo halibadilikji.  Tunatakiwa kuzaa kiroho na kuufikia ulimwengu wote kwa Injili  ya Yesu Kristo.  Kuna mbinu mbalimbali ambazo kwazo lengo hili laweza kifikiwa .  Mbinu hizi kwa pamoja huitwa methodolojia ya mazidisho.
Wakati Mwamini anafanyia  kazi mbinu za ki Mungu za mazidisho matokeo yake huwa ni uzao wa kiroho.Yaani waamini wapya huzaliwa kiroho katika mji wa mimba ambao ni kanisa.
WITO KWA MATENDO
Watu ambao  Yesu aliwaita kwanza kuwa wanafunzi wake  walikuwa ni wavuvi.Walikuwa ni watu wenye kazi. Hawakukamata  samaki kwa wakati mmoja. Walitumia nguvu kubwa kuvua na  kupata samaki wengi wa kila aina.
Wakati Yesu alipowaita kuwa wavuvi wa watu alidhihirisha mpango  wenye kufanana na ile kazi yao ya uvuvi  kwaajili ya mazidisho ya kiroho. Wanafunzi wake walitakiwa kuvua watu toka kila taifa, tamaduni, lugha na makabila yote. Nyavu zao za kiroho zingejazwa.
Yesu aliwaita watu kwaajili ya  kazi .Alisema angewafanya kuwa wavuvi wa watu.Hawangekuwa  watazamaji  tu  katika mpango wa Mungu.Wangekuwa washiriki   wakuu kwa kuwa wavuvi  wa roho za watu.Wito wa Yesu bado ni sawa. Haujabadilika.Tunapaswa kuwa wavuvi wawatu.  Kama si wavuvi basi si wanafunzi.
WAVUVI WA WATU
Kwanini Yesu alitumia mfano wa uvuvi kuwaita wanafunzi   wake ?
Kwanza ulikuwa ni mfano ambao wangeuelewa  kwa urahisi.Hawa watu waliishi  kwa shughuli ya uvuvi. Kazi ya uvuvi ilikuwa ni kitu ambacho walitumia  nguvu zao nyingi na muda wao mwingi. Wakati Yesu alipowaita kuwa wavuvi walielewa  kwamba wangewavua  samaki (watu) katika ulimwengu wa kiroho.
Walielewa pia mahitaji ya wito huo.  Uvuvi wa kiroho ungehitaji kujitoa kikamilifu.  Kutoa muda na nguvu.
Pili Yesu alitumia mfano wa uvuvi kuwaita wanafunzi wake kwa sababu kuna kanuni za uvuvi wa asili  zinazoweza kutumika katika uvuvi wa watu (uvuvi wa kiroho).
Baadhi ya kanuni hizo ni:
1.    Unapaswa kwenda mahali samaki walipo.Kama unataka kupata samaki unapaswa kwenda samaki walipo.  Samaki huishi majini.  Huwezi kuwapata samaki kwakuwasubiri ukiwa juu ya mlima au ukiwa jangwani.  Mvuvi wa watu unapaswa kwenda mahali ambako watu ambao hawajaokoka wanapatikana au kuishi.  Watu ambao hawajaokoka wanapatikana katikia maeneo mbalimblai huwezi kuwasubiri katika mejengo ya kanisa ndipouwavue. Nenda mahali wanakopatikana,  mfano sokoni,mashuleni, hospitalini, magerezani,maofisini majumbani na mahali pengine popote wanakopatikana na kisha wavue

2. Lazima uchunguze  mazingira.  Katika uvuvi wa asili mvuvi anapovua huzingatia mazingira, huchunguza kina cha maji, aina ya maji, ili kujua kama ni maji ya chunvi au la, namna upepo unavyopiga. Mambo haya yote kwa kawaida hutoa tathimini ya  aina ya mtego na mbinu  unazopaswa kutumia Kuvua.  Hizi pia ni mbinu utakazotumia katika uvuvi wa watu.  Kweli hizo hapo juu ni sawa kabisa katika mambo ya kiroho.  Nilazima uchunguze  mazingira ambamo watu wanaishi.  Nini mahitaji yao?  (Tambua mahitaji yao) Nini kinaendelea katika maisha yao?   Hii itakusaidia wewe  kujua mbinu utakazotumia  katika kuwavua watu hawa.
Yesu alipokutana na mwanamke kisimani katika Ijili  ya Yohana 4 alichunguza mazingira aliyomkuta  yule mwanamke .  Alikuwa anatafuta maji ya kawaida.  Yesu alitumia hitaji hili la mwanamke  kumsaidia kutambua hitaji lake la kiroho. Mbinu aliyotumia   ilimleta mwanamke katika ufalme wa Mungu.
 Kama huchunguzi mazingira katika uvuvi  wa kiroho (watu) utajikuta mwenyewe unavua juu ya mlima.  Kwa sababu hujui watu wanakopatikana na jinsi ya kuwafikia.
3      .Tumia mbinu mbalimbali. Mvuvi bora hutumia mbinu mbalimbali katika kuwakamata  samaki.  Hutumia vitu mbalimbali ili kuwavutia samaki. Hutumia zana mbalimbali za uvuvi . Aina mbalimbali za samaki huvutiwa na mbinu mbalimbali za uvuvi.  Ndiyo maaana mvuvi bora hutumia mbinu mbalimbali. Mvuvi aweza kujifunza baadhi ya mbinu hizo katika vitabu vinavyohusu uvuvi. Anajifunza mbinu zingine kutokana na uzoefu na uchunguzi wa kina. Mbinu anazotumia hubadilika lakini lengo daima linabaki kuwa lilelile. Kukamata samaki.
Kama unataka kuwa mvuvi bora wa watu unapaswa kutumia mbinu mbalimbali. Watu  wanatofautiana hivyo hata vitu vinavyowavutia vinatofautiana. Wengine huvutiwa na mahubiri au mafundisho aukufarijiwa wakati wa matatizo. N.k. Mbinu za uvuvi wa kiroho zinatofautiana lakini lengo daima ni lilelile. Kupata roho zilizopotea na kuzileta kwa Yesu Kristo.
4. Unapaswa kutoa nje na kurudisha tena. Haijalishi mbinu unayotumia, unapswa kuitupa nyavu majini na kuitoa tena.  Katika uvuvi wa kawaida  jinsi unavyotega mitego yako majini ni jambo muhimu sana. Unatakiwa kutega mitego yako kwa umakini sana . Pia unapaswa kuwa makini katika kuwatoa samaki kwenye mitego baada ya kuwakamata.
Katika ulimwengu wa rohotumeahidiwa kwamba tukilitoa Neno la Mungu halitaturudia bure. Litafanikisha  lengo katika maisha ya watu Isaya 55:11.
Unapotumia Neno la Mungu utakuwa katika shabaha kila wakati  na hatimae litawakamata wanawake na wanaume nakuwaleta katika ufame wa Mungu.
5. Tambua majira na nyakati.Majira ma  nyakati huathiri sana shughuli ya uvuvi katika ulimwengu wa asili. Baadhi ya samaki huhama na hawawezi kupatikana katika  baadhi ya kanda wakati wa majira fulani.  Samak wakubwa hukamatwa mapema mchana wanapokuja katika eneo la juu la uso wa maji ili kupata chakula.  Kama utavua katika majira yasiyo sahihi au muda usio sahihi huwezi kuwakamata samaki wengi. Wakati ni muhimu sana katika uvuvi wa kiroho pia.
Utajifunza baadae jinsi ilivyo muhimu kuvua  maeneo yenye samaki wengi wakati samaki wanauma kiroho.
6.  Lazima uwe mvumilivu.Katika ulimwengu wa asili mvuvi hutakiwa kuwa mvumilivu.Ni lazima asubiri samaki waingie kwenye mtego aliotega na kukamatwa.  Hii pia ni kweli katika ulimwengu wa roho.
Kwahiyo ndugu vumilieni hata kuja kwake Bwana. Tazama mkulima hungoja mazao yake ya nchi  yaliyoyathamani, huvumilia kwaajili yake hata yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho  Yakobo 5:7.
KUZAA KIROHO
Katika ulimwengu wa asili samaki hupelekea kutokea kwa samaki wengine wengi kwa njia ya kuzaliana. Uvuvi katika ulimwengu wa asili husababisha mazidisho ya samaki .
Uvuvi katika ulimwengu wa  roho husababisha mazidisho  ya watu katika ufalme wa Mungu. Uzazi wa kawaida husabisha mazidisho ya watu walio hai. Uzazi wa kiroho husababisha  pia mazidisho ya watu kiroho.
Hii haiji kutokana na programu  za kibinadamu.  Uzazi wa kiroho huja kupitia mtiririko wa maisha ya kiroho toka kwa Mungu. Katika maisha ya kawaida ya binadamu maisha ya kiumbe kipya  huanza  katika tumbo la uzazi la mwanamke(uterus) na seli hai moja . Seli hiyo  hujizidisha hadi mtu kamili anapokuwa amefanyika.  kisha mtoto huzaliwa.
Uzazi wa kiroho pia ni sawa na huo.Huanza na mtiririko wamaisha  ya ki-Mungu kwa mtu mmoja , hujizidisha katika tumbo la kiroho la uzazi  ambalo ni kanisa. Na kisha mtoto wa kiroho huzaliwa.
Katika mada inayofuata utajifunza  jinsi kuzaliana na kujizidisha kiroho kunavvoanza.
zoezi
1.    Andika mstari wa ufungo wa mada hii toka kichwani wako
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………

2.Agizo la kwanza  na la mwisho la Bwana Yesu kwa wanafunzi wake lilikuwa ni.
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
3.    Eleza maana ya mazidisho  ……………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………….


4.    Ninamna  gani waamini wanavyoweza kuzaa kiroho
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………

5.    Eleza maana ya mbinu.
.......................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................................…………………
6.    Eleza maana ya methodolojia
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………
7.      leza maaana ya  methodolojia ya mazidisho.
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………

8.     Toa muhtasari wa kanuni za uvuvi  katika ulimwengu wa asili zinazoweza  kutumika katika uvuvi wa watu.
………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………











MADA YA PILI
SIKU YA VITU VIDOGO
Baada ya kumaliza kujifunza mada hii utaweza.

·       Kuandika mstari wa ufunguo toka kichwani mwako.
·       Kuandika mhtasari wa kanuni za msingi za mazidisho.
·       Kueleza aina mbalimbali za  ukuaji wa kanisa.
·       Kuorodhesha marejeo ya maandiko yanayoonesha kwamba mazidisho ni ki-Biblia.
·       Kubaini sababu hasi zinazoweka msisitizo wa  kukua kwa kanisa kiidadi pekee.

Mstari wa ufunguo.
Maana ninani aliyedharau siku ya mambo madogo ? ”  (Zekaria 4:10)
Ukuaji wa mwili wa binadamu huanza na seli hai moja ambayo ni matokeo ya ushirika  kati ya mwanamme na mwanamke kupitia tendo la ndoa. Seli hiyo hujizidisha katika tumbo la uzazi la mwanamke  mpaka kiumbe kingine kimeumbika. Kiumbe hicho kinapokuwa kimepevuka  pia huwa kina uwezo wa kujizidisha.
Ukuaji wa kiroho huanza na ushirika wa karibu kati ya mtu mmoja na Bwana Yesu Kristo. Maisha ya kiroho hutiririka  katika roho na nafsi ya mtu aliyempokea Yesu kama Bwana na mwokozi wa maisha yake.
Aina hii ya uzima hulelewa katika mji wa mimba wa kiroho ambao ni kanisa, hukua mpaka mwanafunzi  mwingine amezaliwa .  Mwanafunzi huyo anakuwa na uwezo wa kuzaa kiroho kwa kuwaleta watu wengine kwa Yesu Kristo. Misha huanza na seli hai moja katika  wa kimwili au  ulimwengu wa kiroho.
Ndiyo maana Mungu alisema nani aliyedharau siku ya mambo madogo ? Zekaria 4:10.
Katika mada hii utaanza na mambo madogo.  Utajifunza kanuni za msingi za mazidisho na aina mbalimbali za ukuaji kiroho. Utajifunza jinsi Mungu anavyohusika na mazidisho ya kiroho na vigezo vinavyoonesha msisitizo potofu katika ukuaji wa kanisa kiidadi (numeric growth). Utaanza na mambo madogo ambayo kwayo ufunuo mkuu umejikita.

Kanuni za msingi za mazidisho.
Nilazima uelewe kanuni za msingi za mazidishoya kirohoili uweze kujifunza na kufanyia kazi .  Kanuni za ki-Biblia za mazidisho hazibadiliki lakini mbinu za uzidishaji zaweza kubadilika lakini lengo daima linabaki kuwa lilelile. Lengo na kanuni za mazidisho zinabaki kuwa sawa  lakini mikakati  ya kufikia lengo hilo hubadilika.
Lengo laMungu tangu mwanzo wa nyakati limekuwa ni :
,,,,”Yaani kuleta madaraka ya wakati mtimilifu, atavijumlissha vitu vyote katika Kristo,vitu vya mbinguni na vitu vya duniani pia naam, katika yeye huyo”Waefeso 1:10
Watu wake na hali ya kihistoria hubadilika  kati ya mataifa, Mungu hubadili mikakati yake ili kufanikisha lengo lake.
Mfano     Wakati mababa wa Israeli waliposhindwa kutekeleza wajibu wao wa kiroho  (kikuhani) Mungu aliinua makuhani. Wakati makuhani walioanza kuwa wadhalimu aliinua manabii kama viongozi wa kiroho.
Yesu alitumia mbinu mbalimbali katika huduma yake. Hakushugulika na watu wote kwa njia moja.  Mbinu zake zilibadilika lakini lengo lake lilibaki sawa daima. Kugusa na kubadilisha maisha ya watu. Hizi ni baadhi ya kanuni za msingi unazopaswa kuzielewa ‘ Siku ya  mambo madogo’ .  Kabla ya kuanz kujihusisha.
Mungu huhusika na mkutano.
Mungu daima amekuwa anahusika na ulimwengu mzima
Kwamaana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwana wa pekee ili kila mtu amwaminie asipotee bali awe na uzima wa milele” Yohana 3:16

,,, bali huvumilia kwenu maana hapendi mtu yeyote apotee bali wote waifikilie toba” 2 Petro 3:9.

Yesu alilielezea hili aliposema   Mwana wa adamu alikuja kutafuta na kuokoa kile kilichopotea” Luka 19:10

Mungu anahusika na mkutano . Anahusika na idadi.  Anahusika na  mazidisho ya waamini watakao zaa na kuieneza Injili. Unapoanza somo la mazidisho unapaswa kuanza  na mtazamo huo alio nao Mungu wa kuufkia ulimwengu wote kwa ujumbe wa Injili.
Ni Mungu anaetoa au kusababisha ukuaji. Mazidisho ya kiroho hayawezi kufikiwa bila Mungu kuhusika.  Ni Mngu anaesababisha ukuaji.

…”mwenye kukuza ni Mungu”  1. Wakorintho 3:
Mwamini nilazima atumie kanuni za ki Mungu.  Kuna kanuni katika Neno la Mungu zinazoshusika katika maisha ya kila siku  na huduma.Mungu hutenda kazi kupitia watu wanaojua kufanyia kazi kanuni hizo za kiungu.
Tangu mwanzo wa ulimwengu Mungu amekuwa akifanya kazi katika dunia hii kwa kupitia mwanadamu.  Aliwapa adamu na Hawa kazi ya kutunza bustani. Alimtuma Nuhu kuokoa maisha hapa duniani wakati wa gharika kuu. Mungu alimwinua Ibahimu kuunda taifa la Israeliambalo kupitia kwalo angejidhihirisha kwa  mwenyewe kwa mataifa yote ya dunia.  Mungu pia aliwatuma manabii, wafalme, na waamuzi kufanikisha mpango  wake katika Agano la kale.

Katika Agano jipya mtu Yohana mbatizaji alitayarisha njia ya Bwana Yesu.  Yesu alianza hudumayake na watu wa kawaida.  Na alipopaa kwenda Mbinguni aliacha hatima ya Injili katika mikono ya watu hawa wa kawaida.

Rekodi zote  za Biblia zinaonesha Mungu akishirikiana na mwanadamu  au mwanadamu akituia kanuni za ki Mungu kufanikisha lengo la Mungu.    Hii ni kweli katika mazidisho ya kioho .   Mungu hamtumii mtu yeyote kutangaza Injili . Huwatumia wanawake na wanaume wanaoelewa na kushiriki kaununi zake za mazidisho.
Paulo alielezakuhusu ushirikiano  “ Nilipanda na Apolo  akamwagilizia maji lakini ni Mungu anaekuza”  1 wakorintho 3:6.
Paulo alieleza umuhimu wa waamini kutimiliza wajibu wao katika mpango wa Mungu.  
“ Kwa kuwa kila atake liitiajinala Bwana  ataokolewa .
“Basi wamwitaje yeye wasiye mwamini?  Tena wamwinije yeye wasiyemsikia? Tena wamsikiaje pasipo mhubiri ?”   Warumi 10: 13-14
Yesu ndiyo lengo la mazidisho. Yesu alisema ;
Nami nikiinuliwa juu ya nchi nitawavuta  wote kwangu” Yohana 12:32
Yesu alikuwa akiionga hapa kuhusu kuinuliwa juu ya msalaba kufa kwaajili ya dhambi za ulimwengu. Kupitia kifo chake angewavuta watu wote kupitia nguvu ya Injili.  Unapohubiri Injili tambua kwamba tayari Yesu amekwisha inuliwa.  Anpokuwa ameinuliwa juu katika maisha yako n kanisa lako atu watavutwa na nguvu ya Injili.  Mazidisho ni lazima Yesu anapokuwa anpokuwa ameinuliwa juu.

Neno la Mungu  hubababisha ukuaji. Mathayo 13:1-9
Yes alieleza mfano katika  Mathayo 13:18-23 soma habari hii katika biblia yako. Katika mfano huu mbegu  huwakilisha Neo la Mungu. Mungu  ameahidi kwamba tunapopanda Neno lake halitarudi bure. 
“ Ndivyo litakavyo kuwa neno langu, litokalo  katika kinywa changu halitabnirudia bure. Bali litatimiza mapenzi yangu  nalo  litafanikiwa katika mambo  niliolituma  ISaya 55:11


,,,,Ninaliangalia neno langu  ili nipate kulitimiza”   Yeremia 1:12
Ni Neno la mungu ambalo huleta mabadiliko katika maisha ya watu.  Mabadiliko hupelekea ukuaji na mazidisho ambayo yamejikita katika Neno la Mungu.

Roho Mtakatifu huwezesha mazidisho.   Katika ujumbe wa mwisho wa Yesu kwa wanafunzi wake alisema,

“Lakini mtapokea nguvu akiisha kuwajilia juu yenu Roho mtakatifu; nanyi mtakuwa ni mashahidi wangu katika Yerusalemu na katika Uyahudi wote na Samaria na hata mwisho wan nchi” Matendo ya Mitume 1:8
Nguvu ya roho mtakatifu huwezeshamazidisho. Karama za Roho Matatifu huwezesha mazidisho. Tunda la Roho la roho mtakatifu hubababisha kuzaliwa kwa waamini wapya. 
Tuachunguzakazi ya Roho  Mtakatifu  katika mazidisho  katika  kozi hii baadae.

Mazidisho ni wajibu shirikishi.  Katika kanisa la kwanza  (kanisa la karne ya kwanza baada ya Kristo). Kazi ya kutangaza Injili haikuwa ya wachungaji, wainjhilisti, waalimu, manabii na mitume pekee. Kila mwamini wa agano jipya aliwajibika katika kueneza Injili.
Kama tunataka kuufikia ulimwengu wote kwa Injili ni lazima turudi katika  mpango wa agao jipya  wa kila mwamini katika mwili wa Kristo (kanisa)  kuwa mzazi wa kiroho.
 Hatuwezi kuufikia ulimweng,  kwa kuacha wajibu wa kueneza Injili mikononi mwa watu wachache tu. Kuna waamini wa kutosha ambao wangeweza kuufika ulimwengu wote kwa urahisi kwa Injili ya yesu Kristo. Kumekosekana watu  wenye unuo wa kutambua kuitikia fursa kwaajili ya mazidisho.
Agizo lililotolewa na Yesu kwa waamini “ Kwenda ulimwengui mwote na ujumbewa Injili. Hutakiwi kusubiri  amri ya kwanza kwa sabau amri imekwisha kutolewa .
AINA ZA UKUAJI
Biblia imeelezea aina nne za za ukuaji wa kanisa au mazidisho ya kanisa. Aina hizo ni :
1.    Ukuaji wa kijografia, Ukuaji huu ulitabiriwa na Yesu Matendo ya Mitume 1:8. Kanisa lilitakiwa kukua kijografia, yaani kuenea toka eneo moja mpaka eneo jingine, Toka mji mmoja mpaka mji mwingine, taifa moja hadi taifa jingine.
2.    Ukuaji wa kiidadi, Kanisa ingeongezeka kiidadi wakati linakuwa kijografia. Kuka kiidadi  kwa kanisa la kwanza kumeelezwa katika katika kitabu xcha Matendo ya mitume.
Mfano. Kanisa liliongezeka toka watu 12 hadi watu 120 matendo 1;15
Toka watu 3000 katika matendo 2:41 hadi watu 5000 katika Matendo 4:4.

3.    Ukuaji wa kimakundi (Ethic growth).  Kanisa la kwanza pia lilikuwa  kimakundi . Injili ilienea nje ya mipaka ya kiyahudi ilifika mpaka Samaria  na kwa matafifa yote. Injii ilienea katika makundi mbalimbali yenye tamaduni tofautitofauti . Toka utamadui wa kiyahudi mpaka utamaduni wa kisamaria.
4.    Ukuaji wa kiroho. Ukuaji wa kiidadi sio msisitizo pekee wa mazidisho ya kiroho. Kama utakavyojifunza baadae katika kozi hii. Ukuaji wac kiroho ni muhimu sana. Wanafunzi wa Yesu ni lazima wakue katika viwango vya ubora wa kiroho na kiidadi.
“Lakini  kueni katika neema na katika kumjua  Bwana wetu na mwkozi Yesu Kristo” .2 Petro 3:18
Shauku ya ungu ni kwamba:

Tuishike kweli katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, aliye kichwa Kristo”.   Waefeso 4:15.

MSISITIZO WA IDADI
Baadhi ya watu hudharau suala la ukuaji wa kiroho katika mazidisho ya kanisa na ukuaji wa kanisa kwa sababu wanaamini  kwamba kuweka msisitizo wa idadi si sahihi.




















MADA YA TATU
KIELELEZO CHA MAZIDISHO
Baada ya kumaliza mada hii utaweza;
Kuandika mstari wa ufunguo toka kichwani.
Kufafanua maana ya  mfano.
Kueleza  sababu kwanini Yesu alitumia mifano.
Kubaini kanuni za mazidisho katika mifano iliyofundishwa na Yesu.


Msitari wa ufunguo.


……………………………………….Marko 4:33

UTANDULIZI
Mada hii inalenga katika kananu za mazidisho zilizofundishwa na Yesu  katika huduma yake akiwa hapa duniani. Kielelezo ni habari inayotumia  mfano  kutoka katika mazingira asilia ya ulimwengu kuelezea ukweli wa kiroho.
Maana halisi ya neon kielelezo ni kuweka kando ya , kulinganisha.  Katika vielelezo Yesu   alilinganisha   mifano asilia  na kweli za kiroho. Kielelzo habari ya kiulimwengu yenye kweli za ki-Mbingu

Kwanibni vieelezo?
Wanafunzi walimuuliza  yesu kwanini  alitumia mifano kufundisha kweli za kiroho
“Na wanafunzi wakja wakamwambia, kwanini unaongea nao kwa mifano?”
Mathayo 13:10.
Yesu akajibu, kwa sababu ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme lakini si wao {kosa}

Mathayo 13:11
Kuelewa kweli zilizofundishwa kwa mifano kuliwezekana kwa wanafunzi kwa sababu walikuwa  na ufahamu wa kiroho. Waliokuwa hwana ufahamu wa kiroho walisikia mifano na wakashindwa kuielewa. Kweli za kirohgo zaweza kutambuliwa kwa ufahamu wa kiroho.
1Kor 2:14
Tmu mwenye ufahamu wa kiroho ni mtu Yule aliyezaliwa mara ya pili. Wale wqenye ufahamu wa kiroho huelewa  kanuni zilizofundishwa katika mifano. Mtu wa mwili kamwe hawzi kuelewa.
INJILI YA UFALME
Injili unayotakiwa kuihubiri kwa mataifa ni injili ya ufalme wa Mungu. Ujumbe wake unahusu kuzaliwa kwa Yesu, maisha na huduma yake.Inahusiaha kifo chake kwaajili ya wenye dhambi na ufufuo wake  toka kwa wafu. Unapawa kuwaeleza watu namna ya kuingia katika ufalme wa Mungu.

MFANO WA MAZIDISHO.
Yesu alitoa mifano mingi kuhusu ufslme wa Mungu. Mojawapo ya mifano hiyo ulihusu jinsi ufalme wake ungeenea duniani  kote. Mifano ifuatayo kuhusu  kuka kwa ufalme inadhihirisha nanuni za msingi za mazidisho. Tazama marejeo yotwe katika biblia yako.

·       Kondoo aliyepotea      Mathayo 18:12-14; Luka 15:4-7
·       Sarafu ilyopoteLuka  15:8-10
·      Mwana mpotevu: Luka  15:11-32
Mifsno hi inadhihirisha jinsi Mungu anavyohusika na waiopotea na uharaka wa  unaotakiwa kuufanya ili  kuwaleta katika ufalme wa Mungu. Haijalishi kwanini wamepotea. Kondo walikuwa wanatangatanga, sarafu ilipotea kwa uzembe. Mwana alipotea kutokana na uasi wake mwenyewe. Unatakiwa kufanya kila jitihada kuwatafuta waliopotea dhambini. Unatakiwa kuwaendea kule walipo na siokuwasubiri waje kwako.
Mungu hajihusishhi na jinsi gani watu walivyopotea bali jinsi wanavyoweza kupatikana.

Empty Banguet table   
   
Sherehe tupu  Luka 14:15-23
Mazidisho ayapaswi kusimama eti kwa aababu baadhi ya watu wanakataa kuitikia mwito wa Injili. Unatakiwa kuwatafuta watu walio na njaa ya kiroho na kuwaleta katika sherehe iliyoandaliwa na Bwana.

Mtini usiozaa matunda      Luka 13:6-9
Yesu alitoa mfano wa mtini usio zaa. Mtini ni kiwakilishi cha  taifa la Israeli. Mungu aliwainua Israeli kama taifa  ambalo kwalo angeudhihrisha ufalme wake kwa ulimwengu kwa kupitia taifa hili. Mungu alitarajia mtini Israeli kuza matunda kutoka kwa mataifa ya kipagani ya luimwengu kwa kuwashirikisha Injili. Lakini Israeli walibaki tasa na wasio na matunda.
Sasa Mungu ameliinua kanisa  kwaajili ya kusudi hili. Mungu anawalea waamini na kuwaanda kuwa wazalishaji  kama alivyofanya kwa taifa la Israeli. Kusudi lake ni lilelile. Tunatakiwa kuleta matunda toka kwa mataifa yaani kuwaleta watu kwa Yesu kw kuwahubiri Injili ya Ufalme wa Mungu. Mungu hapendezwi na mti  usio zaa matunda.

·       Talants: Mathayo  25:14-30; Luka 19:11-27
·       Msafiri : Marko 13:34-37
·       Mtumishi: Mathayo 24:43-51; Luka 12:39-46
·       Mtumishi anayetazama: Luke 12:36-38
·       Wakili mwaminifu: Mathayo 25:14-30



Mfao wa mtumishi unasisitiza uwakili wa hekima katika Injili ambao waamini wamekabidhiwa. Kila mwamini amepewa talanta au kipawa fulani cha kutumia katika kuieneza Injili. Unatakiwa kutumia talanta uliyopewa katika kuieneza Injli bila kujali talanta yako ni kubwa au ndogo kiasi gani. Kila mwamini anapaswa kujizidisha. Yesu atakaporudi tena atawatuza wale waliotumia vizuri talanta zao. 




Wale wasiozalisha wanaitwa kuwa sio waaminifu.
           Luka  (Matthew 16:27)


Yesu alitambua kuwango cha uzalishaji kanika hatua za mazidisho.
 Luka 12:48
……………………………………………………………………………………………..
Ufalme wa mungu huenezwa kwa hekima kwa kutumia vipawa  ya kiroho tulivyopewa na Mungu. Ukitumia kile Mungu alichokupa thawabu yako inaongezeka. Usipotumia utapoteza hata kile ulichonacho.




Mpanzi                                  Mathayo 13:3-8; Mark 4:3-8; Luka 8:5-8
Ufalme wa Mungu unaenezwa kwa kupanda mbegu ya neno la Mungu. Hakuwezi kuwa na mazidisho pasipo Neno la Mungu. Matunda hutegemea uzima ulio katika  mbegu (Neno la Mungu) na mwitikio wa udongo (mwitikio wa mtu kwa neon la Mungu). Kutakuwa natofauti ya mwitio kwa Neno lililopandwa.
Wajibu wako ni kupanda. Kwa kadli unavyopanda mbegu ya Neno la Mungu baadhi ya ardhi ikotayari na kutoa mavuno. Sehemu nyingie ya ardhi ni duni vivyo inatoa matunda kidogo. Hata yesuy alikabiliana na  tatizo la udongo usio na mwitikio katika huduma yake hapa duniani.
Marko5:56…………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………………..
Kwa kadli unafanya kazi ya kuuzidisha ufalme wa Mungu  kwa kuwaleta watu kwa yesu shetani atajaribu kuleta pingamizi. Atajaribu kupanda watu wanaoitwa magugu miongoni mwa mbegu njema ya Mungu.
Baadhi ya watu wanokiri na kuija kanisani si waaminifu  ni magugu yaliyopandw na shetani. Yesu hatakiwa wewe kutumia muda mwingi na nguvu nyingi kushughulika na magugu. Anataka uweke mkazo katika kupanda mbegu njema kazi ya kutenganisha ni yak wake mwenyewe.

Uvuvi
Yesu alilinganisha kukua kwa ufalme wa Mungu na nyavu kubwa iliyorushwa baharini. Kila aina ya samaki waliingia, lakini nyavu inapotolewa  majini kuletwa  nchi kavu samaki wavuri hutengwa na samaki wabaya.
Ufalme utawaleta wanaume na wanawake kutoka katika mataifa mbalimbali. Wengi wataingia. Baadhi watakuwa waaminifu  na baadhi sio.  Katika siku ya mwisho ya hukumu  Yesu ataporudi  wema na wabaya watatenganishwa . Hujaitwa kutenganisha umeitwa kuvua.

Punje ya haradali          Mathayo  13:31-32; Marok 4:31-32; Luka 13:19
Ufalme wa mungu uajizidisha kama punje ya haladari.Punje ya haladari huwa ndogo sana mwanzoni. Lakini hukua hata kufikia kuwa kama mti.  Ufalme wa Mungu duniani mara nyingi huwa na mwanzo mdogo.Yesu aliporudi Mbinguni baadfa ya hudumsa yake hapa duniani aliacha  kikundi kidogo cha waamini kuieneza Injli.Kikundi hicho kidogo cha waamini kilijizidisha na kuwa maelfu ya waamini  katika mataifa mbalimbali.




                                   Mathayo13:33; Luka 13:21
Ufalmw wa Mungu utajizidisha  na kuenea kupitia 








Mzabibu na matawi yake  Yohana 15:1-16
Mfano huu  unaeleza mahusiano yaliyopo kati ya Yesu na hatua za kuzaa matunda. Yeye ni mzabibu wa kiroho na sisi ni matawi yake.  Huwezi kuzaa matunda peke yako. Unakuwa na uwezo wa kuzaa matunda kwa kadri unavyokuw umeungamanishwa na Yesu. Yesu anataka kuondoa katika maisha yako kila kitu kinachoweza kukufanya usizae matunda ili uweze kuzaa matunda bora.


Mavuno  Mathayo 9:37-38,  Luka 10:2
Katika mfano huu shamba ni ulimwengu. Mavuno ni wanawake na wanaume waliotayari kuiitikia Injili ya ufalme. Mavuo makubwa ya kiroho yako tayari yakisubiri kuvunwa na  watendakazi  wa kiroho.

Kanuni nyingine za  Mazidisho.
Yesu alifundisha kanuni nyingine za mazidisho katika maelezo mafupi.

Nuru ya ulimwengu                        Mathayo  5:14-16; Luka 8:16
Ufalme wa Mungu utajizidisha wakati waamini  wanatokea kama nuru  katika mji ulio juu ya kilima  ambayo inaweza kuonekana  kutka maili nyingi. Tunatakiwa kuuangazia nuru  ya Ysu ulimwengu uliojaa giza.Ufalme wa Mungu utazidishwa kwa kadri watu wengi wanavyoijia nuru.

Chumvi ya dunia.Luka 13:4
Katika wakati wa Biblia chumvi ilipakwa katika nyama ili kuzuia isioze. Waamini ni chumvi inayotakiwa kupakwa kwa ulimwengu  kwa ujumbe wa uhifadhi yaani wokovu. Ufalme wa Mungu utazidishwa  wakati watu wanaokolewa kutoka kwenye uozo wa dhambi.



Hazina ya mbinguni          Matthew 6:19-21; Luke 12:15.
Waamini hawatakiwa kujishughulisha zaidi na kutafuta hazina za duiani kuliko kutafuta hazina ya Mbinguni. Tumeitwa kwaajili ya maizidisho ya kiroho. Kwadili unawashirikisha watu ujumbe wa Injili hazinayako Mbinguni itakuwa inazidishwa.

Mlango mpana                         Mathayo 7:14
Huwezi kuhukumu njia sahihi kwa kigezo cha idadi.Njia ya upotevuni inabeba watu wengi wakati njia ya kuelekea uzimani inabeba watu wachache.

Kazi nyingi   Mathayo 7:22
Kazi nyingi za ajabu zitafanywa na watu wengi  katika hali ya nje kutakuwa na mazidisho na ukuaji. Lakini kufanya kazi nyingi za ajabu si lazima  kuwe ni kufanya mapenzi ya Mungu  na kulitimiza kusudi. Kazi ya Mungu inatakiwa kufanywa na watu wa Mungu kwa njia ya Mungu.


Kidogo ni bora                      Mathayo 10:42; Mathayo  14:15-21
Kila kitu kinachofanywa kwa Jina la Yesu hata kama kinaoonekana kidogo ni cha thamani.Muujiza wa Yesu kulisha watu zaidi ya  5000 kwa  samaki  na mkate michache unaelezea jinsi Mungu anavyozidihsa kwa kutumia kidogo tulichonacho.

Kukua kunahitaji badiliko                                           Marko 2:21-22; 7:13
Makuzi mapya yanahitaji mabadiliko. Huwezi kuweka kitu kipya katika kitu cha kale chenye mfumo wa maisha ya dhambi. Uwezo mkuu wa nguvu za  Mungu huzuiwa  na waamini wanaoishi  maisha ya kale na hawaitaji mabadiliko.


Pata kwa kupoteza  Marko  8:34-37; 10:29-30
Pokea kwa kutoa  : Luke 6:38.
Kanuni za ulimwengu zinafundisha kwamba unapata kwa kupokea zaidi na zaidi . Yesu alifundisha kwamba unapata kila kitu unapokuwa umepoteza kila kitu. Kile kinachotokea kupota katika ulimwengu wa asili kinapatikana  katika ulimwengu wa Roho.

Kifo huleta uzima                                            Yohana 12 :24
Kupitia kifo cha Yesu watu wengi waepata uzima wa milele. Ili mbegu iweze kuzaa ni lazima ife.Kupitia kifo huja uzima . Ili kuwa mwamini mwenye kuzaa ni lazima ufe kwa mapenzi yako mwenyewe. Ni lazima ufe kwa dhambi. Nilazima uache njia yako na kufuata njia ya Yesu Krsito.

Kanisa katika mwamba                              Mathayo 16:18
Ufalme Wa Mungu umejengwa juu ya mwamba ambao ni  Yesu Kristo. Hakuna ukuaji bila Yesu kuhusika.  Yesu alisema “nitalijenga kanisa langu” Alisema hakuna mtu angeweza  kuja kwake bila kuvutwa na baba yake (Mungu).
 Yohana 6:44
Upinzani ungetarajiwa lakini  malango ya kuzimu hayangeushina  mpango wa Mungu wa ukuaji wa ufalme wake.

No comments:

Post a Comment